Engine Amkingia Kifua Wolper Dhidi Ya Harmonize

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Engine amemkingia kifua aliyekuwa mpenzi wake Jacqueline Wolper dhidi ya Ex wake Harmonize baada ya sakata lao Siku mbili hizi.

Bifu la Wolper na Harmonize lilifika pabaya kiasi ya kwamba Harmonize alianika listi nzima ya wanaume ambao Wolper amebanjuka nao kitendo kilicho wakera watu wengi.

Engine ametumia ukurasa wake wa Instagram kumuandikia Wolper barista ya wazi huku akimuahidi kuwa hataweza kumdharau au kumchafua kamwe kwani yeye ni mshindi Kwenye macho yake.

God Never rust….My prophecy…..U will always be there because your a Winner Wolper.Nakuheshimu sana liwake jua inyeshe mvua…Katika vitu sitaweza kuja kufanya ni kumdharau mwanamke awaye yoyote maana hata kama mwanaume ni kichwa basi mwanamke ni shingo na kiwiliwili usiisahau ‘A’ kisa umeijua ‘B’ maana huwezi kuandika majina makubwa ya Kiswahili kama Mama na Baba bila kutumia A”.

Engine alikuwa Kwenye Mahusiano na Wolper na hata walitangaza kufunga ndoa na juzi Harmonize amethibitisha Mahusiano yao baada ya kumuweka Kwenye listi ya wanaume wa Wolper.

Mchumba Wa Wolper Amedai Alikuwa na Uhusiano na Wolper Wakati Yupo na Brown

Sadick Athanas Sanga ‘Engine’ ambaye ni mchumba wa muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Jacqueline Massawe ‘Wolper’ amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na mrembo huyo.

Wolper aliuanza mwaka kwa kutawala kwenye midomo ya watu na kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutangaza kuchumbiwa na mpenzi wake huyo, lakini kilichowafanya watrend zaidi ni habari za kudai kuwa mwanaume huyo alifanya kufuru kijijini kwa kina Wolper kwa kujaza magari ya kifahari.

Tangu habari hizi zimeanza kuenea kuna mambo Mengi ambayo yamekuwa yakizunguzumzwa kiasi ya kwamba ameamua kufunguka yote kwenye mahojiano yake na Millard Ayo TV:

Mimi nimeshamchumbia Wolper na nimeshatoa na mahari yaani kila kitu nimeshakamilisha na tulizungumza tukakubaliana kwa muda mrefu na hatimaye tukafika hatua hii. Nimekuwa na mahusiano na Wolper kwa siku kwaiyo alivyokuwa na mtu mwingine nilimpisha aendeleenam mambo yake lakini walivyoachana na mimi nikachukua nafasi na tunaelekea kufunga ndoa sasa”.

Mume huyo mtarajiwa wa Wolper amesisitiza kuwa hana mpango wa kuanika taarifa zote kuhusu mahusiano yao kwenye mitandao ya kijamii ila tu  amesisitiza kuwa ndoa yao ambayo itafungwa hivi karibuni haitahusisha michango ya watu bali kutakuwa na mialiko tu.

Lakini pia mchumba wa Wolper amesisitiza kuwa taarifa zilizosambaa kwenye mitandao kuwa ndoa yao ya ghafla sio kweli kabisa kwani penzi lao halijakuwa kama uyoga bali walianza siku nyingi na mipango mingi imehusika.