Kajala Masanja Akiri Kumtembezea Bakora Mwanaye

Muigizaji wa Bongo movie na Balozi wa Biko nchini Kajala Masanja maarufu Kama ‘Kay’ amefunguka na kuweka wazi kuwa kwenye malezi ya mwanaye wa pekee Paula haoni hatari kumpa kichapo pale inapobidi.

Kajala amezaa Mtoto mmoja Paula na mtayarishaji wa muziki mkongwe nchini P Funk majani na Bongo huyo Ana umri wa miaka kumi na Sita.

Katika interview aliyofanya na Global Publishers, Kajala amefunguka kuhusu malezi ya Mtoto Wake huyo na kusema:

Wengine hawawezi kujua ni jinsi gani ninaishi na Paula. Unajua mimi ni mama kijana, lakini lazima mtoto wangu anitii na aishi vile ninavyotaka au ninavyomuelekeza na akinizingua ninamfundisha adabu. Lakini pia kuna wakati tunaweza kuzungumza tukacheka na kutaniana.”

Kwenye mahojiano hayo Kajala alifunguka na kuweka wazi kuwa huwa anamchapa mwanaye pale inapobidi kufanya hivyo:

Nampiga tena siyo kitoto, anaponikosea mimi ni mkali sana. Siku zote nilifundishwa na mama yangu ‘akupigaye ndiye anayekufunza’. Paula anapokosea ninamfundisha na panapostahili kumchapa nafanya hivyo japokuwa siyo mara nyingi maana Paula ni mkubwa sasa, tunakaa tunazungumza na ananielewa vizuri na kuna kipindi tunakuwa marafiki sana.”

Lakini pia Kajala alifunguka kuhusu Changamoto za kulea Mtoto Kama Single mother kwani yeye na baby daddy wake waliachana kitambo sana:

Ni magumu kwa sababu sidhani kama kuna mama anapenda kulea mtoto bila baba ila kwa sababu imenilazimu kuwa hivyo, sina jinsi na uzuri Mungu kanipa nguvu ya kusimama kama mama ingawa huwa anakwenda kwa baba yake anapopata nafasi.”

Kajala Akana Tetesi Za Kuwa na Ujauzito Wa Pfunk

Muigizaji wa Bongo movie Kajala Masanja ‘Kay’ amefunguka na kukana tetesi zinazosikika Kwenye mitandao ya kijamii kuwa ana ujauzito wa PFunk.

Kajala na Pfunk walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi miaka mingi iiyopita na baadae walijaliwa kupata mtoto mmoja pamoja anayeitwa Paula lakini siku za hivi karibuni imedaiwa wamerudiana.

Ingawa kajala ameshakataa kuwa hana uhusiano na Pfunk Tena zaidi ya kuwa marafiki kwa hivi sasa ili washirikiane kulea mtoto wao Paula inasemekana amerudisha majeshi kwa P.

Kwa habari zinazoshika kasi Kwenye mitandao ya kijamii kwa hivi sasa ni kuwa Kajala ameshika ujauzito wa Pfunk.

Kwenye mahojiano na   Over Ze Weekend, Kajala amedai kuwa amekuwa akiona  mengi kwenye mitandao ya kijamii kuhusu ishu hiyo, jambo ambalo anashindwa kuelewa limetokea wapi.

Jamani kwa nini watu wakimuona mtu amenawiri kidogo wanasema kuhusu mambo ya ujauzito? Mimi na P (Funk) mbona wanatung’an’ganiza sana? Wanashindwa kuelewa kabisa yule ni mzazi mwenzangu?” Alihoji Kajala akisisitiza kuwa hana kibendi“.

Miezi Michache iliyopita Kajala aliweka wazi kuwa alikuwa na ujauzito lakini kwa bahati mbaya ukaharibika ingawa hakuweka wazi nani hasa alikuwa muhusika.

Kajala-Siwezi Kuacha Kuongea na Baba Wa Mtoto Wangu Kisa Namuogopa Mke Wake

Muigizaji wa Bongo movie Kajala Masanja amefunguka na kuweka wazi kuwa hawezi kuacha kuongea na Pfunk ambaye Baba wa mtoto wake Paula kwa sababu eti mke wake hapendi.

Wiki chache zilizopita Kumekuwa na Tetesi kuwa Kajala na Pfunk wamerudiana na Pfunk kumuacha mke wake ambaye amezaa naye mtoto mmoja na hivi sasa ana ujauzito mwingine.

Lakini pia wiki chache zilizopita mke wa Pfunk alilalamika na kusema Kajala anataka kumvunjia ndoa yake na hata kudaiwa alikuwa yuko tayari kufungasha virago vyake na kurudi kwa wazazi wake.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Kajala amefungukia tetesi hizo na kusema anataka Samira ambaye ni mke wa Pfunk ajue kuwa yeye anaonana na Pfunk kwa ajili ya mtoto tu hana uhusiano naye mwingine Lakini pia hawezi kuacha kuonana kwa ajili ya mtoto wao.

Mimi sijamwambia aache ndoa yake kwa ajili yangu siwezi hata kumwambia hivyo! Ila ninachotaka kumwambia ni kuwa mimi na Pfunk ni lazima tuongee kwa ajili ya mtoto, Nilikaa miaka kama minne na P tunapishana hatusalimiani wala hatuongei lakini baadae nikaona tu ni ujinga tunamuumiza tu mtoto kwa nini tusisalimiane au P asiwe karibu na mtoto wake kisa ameoa? Wangapi wameoa na wanaangalia watoto wao”.

Lakini Kajala ameweka wazi kuwa ile video iliyisambaa Kwenye mitandao ya kijamii iliyomuonyesha yeye na Pfunk wakibusiana mbele ya mtoto wao ilikuwa ni katika harakati tu za kumfurahisha mtoto wao.

Kajala Adaiwa Kumpindua Mke Wa Pfunk

Muigizaji wa Bongo movie Kajala Masanja amezidi kukamata headlines kutokana na skendo yake yakurudiana na Baba watoto wake prodyuza mkongwe Paul Matthysen maarufu kama Pfunk Majani.

Kajala na Pfunk walikuwa kwenye mahusiano miaka kama kumi iliyopita ambapo walifanikiwa kuzaa pamoja mtoto mmoja lakini baadae waliachana na Pfunk kuwa na Mahusiano ya muda mrefu na mwanamke anayeitwa Samira ambaye pia amezaa naye mtoto mmoja na sasa mjamzito Tena.

Habari za chini ya kapeti za kimbea kabisa zinasema kuwa Kajala kampindua Samira kwa Pfunk hadi sasa inasemekana Samira amehama kwa Pfunk na amerudi kuishi nyumbani kwao kwa wazazi wake.

Habari hiyo imevujishwa na mtu wa karibu wa Samira ambaye ameliambia gazeti la Ijumaa Wikienda mambo haya:

Unajua P Funk kila alipokuwa akielezwa kuhusu Kajala alikuwa hanyooshi maelezo ingawa machoni alionesha kumpenda Kajala.

Mkewe ambaye kwa sasa ni mjamzito, ameishi kwenye kipindi kigumu sana. Anashindwa kumuelewa P Funk kwani watu kibao wanampigia na kumuambia wamemuona mumewe akiwa na Kajala”.

mtu huyo wa karibu na Samira alidai kuwa, mara kadhaa P Funk amekuwa akielezwa kuhusu …usaliti wake kwa Kajala lakini alikuwa akijitetea kwa kutumia kigezo cha kumlea mtoto aliyezaa na Kajala (Paula).

Yani Samira alikuwa akimbana P Funk lakini mara kadhaa P (P Funk) alikuwa anasema hakuna lolote zaidi ya yeye kwenda kumcheki mtoto hususan anapokuwa shuleni,” alisema mtu huyo. Akizungumzia picha zilizovuja, rafiki huyo wa Samira alisema shosti wake alivumilia zile picha za awali zilizomuonesha P Funk akiwa supermarket na Kajala lakini zilivyokuja kuvuja video wiki hii, ameona isiwe tabu afungashe virago vyake.