Lulu Afungukia Tetesi Za Kubeba Mimba Ya Majizzo

Muigizji wa Filamu za Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amefunguka na kuanika ukweli wote kuhusu tetesi za yeye kuwa na ujauzito wa mchumba wake Majizzo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Kipindi cha Play List cha mtangazaji Lily Ommy wa Radio Times FM, Lulu amesema kuwa hana ujauzito kama watu walivyodhani, bali alinenepa mno kiasi cha watu kuhisi hivyo kutokana na unene wake kumfanya aonekane kama mjamzito.

Lulu Micheal

Unajua mimi nikinenepa ni asili ya mwili wangu, nina mguu mnene sana hivyo uliongezeka, mwili pia uliongezeka kwa kiasi kikubwa kwani niliongezeka kilo 20 hivyo kila mtu aliamini nina ujauzito, sikuwa na ujauzito”.

Lakini pia Lulu alifungukia Tetesi Za kufunga ndoa walipoenda China  kwa kusema kuwa yeye hajafunga ndoa nchini China kama watu wanavyodai, bali alikwenda kwa ajili ya matembezi tu.

Mimi sijafunga ndoa China kama watu wanavyodai na watu wanaongea kwa sababu sina kawaida ya kutangaza mahusiano yangu“.

 

Alichosema staa wa filamu Bongo,Lulu kuhusu ‘kuachana’ na mchumba wake

Stori za mitaani kuhusu uchumba wa Elizabeth Michael,ajulikanaye kwa jina Lulu,mkali wa filamu Tanzania,kukatika zimemkwaza na kumpandisha hasira sio mchezo.

Inaripotiwa kua sio mapenzi mubashara tena kati yake na mpenzi wake,baada ya wawili hao kutemana kama big G.

Elizabeth Michael na Majizo

Kwa mujibu wa taarifa hii,mambo sio kama kawaida kwani pendo limevunjika huku kila moja akiongea lake.

Madai kuwa staa huyo wa filamu na mpenzi wake kuonyeshana kisogo yalienea kwenye mitandao ya kijamii huku wadaku wa town wakiongeza makali na pilipili zaidi na kudai kuwa, Lulu karejea nyumbani kwao na ana mpango wa kuanzisha maisha yake upya.

Staa huyo amekereka kuhusu stori hii,haya ndio maneno yake kwa wanahabari wanaotaka kujua kulikoni.

“Sitaki kuongelea chochote…sitaki kuongelea chochote, pliz…unajua mimi siyo mtu wa magazeti kabisa na unanijua vizuri…” amesema Lulu.

Kumbe hapendi stori za magazeti?