” Nina Mimba ya Rayvanny” Reality TV staa wa Kenya akiri

Watoto ni baraka kutoka kwa mungu na kila mmoja huja na sahani yake. Basi, Rayvanny anawatarajia watoto wawili mwaka huu kutoka kwa mpenzi wake Fahyma na mwanamke mmoja kutoka Kenya aitwaye Mishi Dorah.

Kulingana na ubuyu mjini Rayvanny na Mishi Dorah walikutana Instagram na kulingana na Mishi wakati huo Rayvanny alikuwa anamtaka awe kama Video vixen wake.

Mishi Dorah

Lakini baada ya kujuana miezi kadhaa wawili hawa walianza kuingiana kimapenzi na hivyo ndivyo Mishi alivyopata mimba.

Mishi ambaye ana watoto wawili alisimulia Rayvanny alivyokuwa akimsihi amzalie na hivi sasa ametambua kuwa ana mimba ya muimbaji huyu ambaye amekuwa akimkana mitandaoni.

Kwa kweli hakuna anayejua kilichotokea kati ya wawili hawa na yupi anasema ukweli au uongo. Hata hivyo ikiwa Mishi ana mimba basi Rayvanny atabarikiwa na watoto wawili mwaka huu

Reality TV star wa Kenya Mishi Dorah adai kuwa Rayvanny alitaka kumpa mimba

Kilichotokea kati ya Mishi Dorah na Rayvanny hakiwezi julikana kwa kiukweli kwani wawili hao walikutana wakati ambapo hakuna yeyote alijua kuwa wana ‘mahusiano.’

Mishi Dorah

Hata hivyo, Rayvanny amekuwa akimkana mwanamke huyu kwa kusema kuwa anataka kumuharibia nyumba na jina lake. Lakini baada ya Ghafla kumhoji mwigizaji huyo wa Nairobi Diaries, Mishi Dorah alisema kuwa ni kweli aliweza kupatana na Rayvanny kimapenzi.

Mishi Dorah aliendelea kwa kusema kuwa hajapata hedhi zake kwa mwezi mmoja kuonyesha kuwa kunauwezekano wa mwanamke huyu kuwa na mimba ya Rayvanny kutokana na alivyosema. Kulingana na Mishi, Rayvanny alikuwa anataka sana wawili hao wapate mtoto wao wa kwanza kitu ambacho alihisi hawezi kuharikisha kwani hakutaka kuiharibu figure yake.

Lakini swali bado ni…Kati ya mwanamke huyu na Rayvanny nani anasema ukweli? Ebu itazame interview yake hapa.

https://youtu.be/wN6ppPh-TEI