“TID Sio Baba Wa Mtoto Wangu, Prezzo Ndiye Baba”- Shekha

Mwanamke anayejulikana Kama Shekha ambaye Wiki iliyopita alitengeneza headlines Baada ya kudai    msanii mkongwe wa Bongo fleva T.I.D sio baba wa Mtoto Wake ingawa amekuwa aking’ang’ania hivo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la  Ijumaa Wikienda, kwa njia ya simu akiwa nchini Ujeru­mani, Shekha alisema kuwa anam­shangaa T.I.D anavyokomaa kwamba mtoto ni wa kwake wakati baba halisi ni mwanamuziki wa nchini Kenya, Joseph Makini ‘Prezzo’.

Nimenyamaza kwa muda mrefu lakini sasa nimeshindwa kabisa kuen­delea kuvumilia ndiyo maana naweka wazi na TID ajue kuwa mtoto siyo wake bali ana baba yake.

Uzuri ni kwamba Prezzo ambaye ndiye baba wa mwanangu naye ni mwanamuziki hivyo kama TID anataka amuulize mwenyewe atapata jibu kuhusu nani anastahili kuitwa baba wa mtoto”.

Lakini pia Shekha alimtaka T.I.D kuendelea na maisha yake na yeye aendelee na maisha yake pamoja na mtoto wake kwa sababu hata baba yake ambaye ni Prezzo anamuhitaji pia hivyo waachane kwa usalama hataki malumbano kwani yeye ndiye alisababisha mpaka mambo hayo yakafikia hapo yalipo sasa.

Haya mambo yasingefika huku ila TID ndiye aliyesababisha maana anang’ang’ania vitu ambavyo siyo vyake, naomba aniache jamani na mai­sha yangu huyu mtoto ni wa Prezzo nimemaliza“.

 

Prezzo na Jaguar Wakubali Kulizika Bifu Lao

Mastaa wa Muziki kutoka 254 Kenya, Prezzo na Jaguar wametangaza kulizika bifu lao la muda mrefu.

Kwa kipindi kirefu Prezzo alikuwa akiponda jina la Jaguar kwa kueleza Jaguar anayoifahamu yeye ni aina ya gari, Jaguar naye hakuwa nyuma kujibu hilo, kuna kipindi alimpa Prezzo ofa ya kutibiwa rehab bure.

Wasanii hao wawili walitangaza kumalizika kwa bifu hiko huku kila mmoja akiweka katika ukurasa wake wa Instagram:

Jaguar aliandika maneno haya:

Prezzo naye aliweka picha yao na Jaguar na kusindikiza na ujumbe huu kuonyesha wako safi:

 

 

Prezzo: Bado Nampenda Amber Lulu

Mwanamuziki kutoka 254 Kenya, Prezzo amezidi Kupitia penzi lake kwa aliyekuwa mpenzi wake msanii wa Bongo fleva na video vixen Amber Lulu na kudai kuwa bado anampenda.

Wiki chache zilizopita kwenye birthday party ya Amber Lulu aliweka wazi kuwa ameachana na aliyekuwa mpenzi wake Prezzo na kumtambulisha rasmi mpenzi wake mpya anayeitwa Sam.

Habari za wawili hao kuachana zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii hasa baada ya kuacha kupostiana Kwenye mtandao wa Instagram kama ilivyokuwa kawaida yao.

Prezzo alifanya Interview na FNL ya EATV ambapo yupo nchini Tanzania kwa ajili ya kutangaza rasmi nyimbo yake mpya aliyofanya na Dogo Janja inayoitwa ‘Hamsamia’.

Kwenye mahojiano hayo Prezo alikataa kukubali kama kweli wameachana bali alisisitiza kuwa bado anampenda Amber Lulu na alipoulizwa kwa nini hakumposti Kwenye birthday yake alifunguka:

Kwani unajua birthday ngapi mama yangu hajaniposti Kwenye Instagram na sio kama hanipendi ananipenda ila ndio hivyo sio lazima kumposti ndo watu wajue kama unampenda kwaiyo mimi sikumposti Amber Lulu lakini Bado Nampenda”.

Prezzo alipotakiwa kuongelea kuhusiana na Amber Lulu kumtambulisha mpenzi mpya na kusema ameachana naye alikataa kata kata na kukimbilia kubadilisha mada.

Picha Tata Za Prezzo na Amber Lulu Zaleta Gumzo

Mwanamuziki Prezzo kutoka Kenya na Video vixen maarufu Bongo Amber Lulu wameingia kwenye skendo nzito mara baada ya picha inayowaonyesha wakiwa katika ukaribu kuvuja mtandaoni.

Tukio hilo lilitokea juzi ambapo inasemekana Prezzo alikuja Tanzania kwaajili ya kufanya kazi na msanii Dogo Janja.

Hizi ni baadhi ya picha zinazowaonyesha Prezzo na Amber lulu pamoja;

1
2. Hii ni picha aliyopost Amber lulu akiwa na Prezzo

Katika kipindi cha XXL cha Clouds FM mtangazaji Soudy Brown aliwatafuta Prezzo na Amber lulu walifunguka yafuatayo;

“Nilivyojaribu kumchek kwa simu alipokea na sauti yake ilikuwa inasound kama katoka usingizini nikamuuliza uko wapi? akajibu yupo nyumbani kwa mbaalii nikasikia sauti ya Prezzo nikamuomba Amber lulu ampatie simu Prezzo na yeye alikuwa sound katoka kulala, Nikamuuliza vipi mzee baba umeingia lini Bongo? Akajibu yupo tangu jana, Nikamuuliza uko wapi akajibu yupo boardroom ya Seacliff hotel nikamwambia mbona nasikia mwangwi? Akajibu it’s true wako boardroom na Amber lulu ni rafiki yake na ndugu yake hawezi kumtamani”.

Prezzo alipoulizwa kama yupo tayari kumuita Jaquar Mheshimiwa Mbunge akajibu yeye ni president hawezi kumwita Mheshimiwa mbunge wake.