Ruby afunguka sababu za kutemana na Soudy Brown wa Clouds FM

Mrembo na msanii wa bongo Ruby amefunguka kwa mara ya kwanza kudai kuwa hapo awali alitoka kimapenzi na mtangazaji wa Clouds FM, Soudy Brown kwa miaka miwili lakini wakaachana.

Kulingana na Ruby aliwachana na Soudy Brown kwa kuwa mtangazaji huyo hakuwa na msimamo. Akiongea kwenye mahojiano Ruby alisema;

“Nikisema nitoke na mastaa wenzangu sio kwamba hawanisumbui wananisumbua sana lakini nawajua tayari the way walivyo. Lakini vitu vingi ambavyo naona wanafanyiwa wasanii wenzangu na mimi kweli nikawe na msanii?

Aliongeza kusema;

”Hapana siwasemi kwa sifa mbaya wasanii lakini mimi siwezi kuisha nao kutokana na tabia zao kwa sababu mimi ni mwepesi sana kuumia. Mimi mwanaume ambaye nimetoka naye kwenye mapenzi na yupo kwenye industry yetu only ni Soudy Brown, na nimeishi naye kwa mwaka mmoja na miezi sita,”

Kuhusu mimba aliyokuwa anasemekana amebeba – Ruby alikana kwa kusema kuwa hajawai kutoa mimba.

 

Ni nini kinachoendelea kati ya Alikiba na Ruby?

Ubuyu mtaani ni kuwa Alikiba na Ruby kuwa wamekuwa watu wa karibu sana na kuzua maswali mitandaoni ya kijamii.

Habari hii imevuma mda mchache baada ya Alikiba alisemekana kuwa alimvisha pete ya uchumba mwandani wake aitwaye Amina kutoka nchini Kenya.

Ruby
Ruby

Hata hivyo baada ya kuonekana na Ruby sana wengi wanaamini kuwa wawili hao wanauwezekano wa kuwa wapenzi ikiwa hawafanyi wimbo mpya pamoja.

Ruby ambaye aliweza kuzungumzia jambo hili aliwasihi watu hataki kuulizwa kuhusu mahusiano yake…. Ruby alisema,

“Sorry, sitaki kuulizwa kuhusiana na hayo mambo, naomba niulizwe kuhusu kazi zangu tu!”

Alikiba naye hajazungumzia jambo hili kwa sasa hata hivyo kuna uwezakano kuwa yeye na Ruby wanapanga kuachia wimbo mpya hivi karibuni.