Mmiliki wa kampuni ya Global Publishers amlenga Ali Kiba baada ya kumkosoa Babu Tale

Eric Shigongo, mmiliki wa kampuni ya Global Publishers, alianza mgogoro na Wafasi alipodai kuwa Diamond anaingizwa shimoni na Naseeb Abdul, Babu Tale na Salaam.

Madai yake Shigongo yalimkera sana Babu Tale na kumlazimu kumwonya kutoingilia biashara yake na kuwachafulia jina wasanii wake.

Soma pia: Meneja wa Diamond Babu Tale amrarua mmiliki wa kampuni ya Global Publishers Eric Shigongo

Mfanyabiashara huyo sasa amefunguka na kuamua kumshauri Alikiba kuhusiana na muziki wake na namna ambavyo anatakiwa kuishi kwa mipango ili hata siku asipokuwepo kwenye ramani ya muziki awe na maisha yenye tija kulingana na kazi alizofanya nyuma.

“Kwanza kabisa nianze kwa kukiri kuwa sikuwahi kukutana na Alikiba ana kwa ana mpaka miezi miwili iliyopita nikiwa katika Hotel ya Double Tree, iliyopo Masaki, Jijini Dar es salaam. Nilikwenda pale kwa ajili ya chakula cha mchana na mke wangu. Muda mfupi tu baada ya sisi kuingia walifika Alikiba na meneja wake Christine Mosha (Seven) wakaja moja kwa moja kwenye kona tuliyokaa na kutusalimia. Kitu cha kwanza nilichojifunza na kukipenda kwa Alikiba ni unyenyekevu, kijana huyu ni mnyenyekevu mnoooo! Kitu hiki peke yake ukiachana na muziki wake kilinifanya nimpende Kiba. Walipoondoka mimi na mke wangu wote tulikiri KIBA NI MNYEYEKEVU NA NDIYO SABABU AMEFANIKIWA SANA KATIKA MUZIKI.

Shigongo

“Alikiba, meneja wake na Watanzania wenzangu lazima mnisikilize hapa; MAFANIKIO MAISHANI HUJA NA KITU NYUMA YAKE, mara nyingi kitu hicho huwa kuwapuuza na kuwadharau waliokufikisha ulipo. Kuwatenga bila kufahamu hao ndiyo wanunuzi wa kazi zako ama wasikilizaji wa muziki wako na wakikuachia tu utatumbukia shimoni na huo ndiyo utakuwa mwisho wako. Ali kiba anapaswa kufahamu kwamba hawezi kuwa Champion for life, hata akiwa bora kiasi gani lazima siku moja atakuja mtu bora zaidi yake. Kabla ya Chris Brown alikuwepo Usher Raymond, kabla ya Rihanna alikuwepo Beyoncé, kabla ya Floyd Maywether alikuwepo Mike Tyson, kila zama na bingwa wake. Leo ni Kiba kesho atakuwa mwingine” alisema Shigongo.

Shigongo aelekeza mawaidha yake kutoka Diamond na kuipelekea Ali Kiba..hivi ndivo alivyo mshauri kuhusu wazazi wake

Mmamiliki wa Global publishers bado anaendelea kutoa mawaidha yake kwa wasanii wa Tanzania.

Alianza na Diamond ambapo alitukatanwa na mashabiki na sasa ako kwenye Ali Kiba ambapo alizungumzia mambo mengi mpaka ile ya kifamilia.

Hivi ndivyo alivyomweleza Ali Kiba:

1. ‘Detachment from fans’, hii ina maana ya kujitenga kutoka kwa mashabiki zake. Linaweza kuonekana kuwa jambo dogo lakini limekuwa likiwaangusha wanamuziki wengi duniani. Hili ni la kwanza ambalo anatakiwa kujiepusha nalo kama atataka kuwa juu kwa kipindi kirefu.
2. Ali ni mnyenyekevu, hataki makuu lakini kwa kazi yake ilivyo inambidi kidogo aongeze thamani, hapa nina maana kwamba Ali ajiepushe na suala la kusafiri bila meneja anapokuwa ndani au nje ya nchi kwenye shoo. Simaanishi kwamba hasafiri naye, hapana, namaanisha kwamba asifikirie kutokusafiri naye kwani hii huongeza thamani ya msanii anapoongozana na timu yake, hasa meneja au mameneja.

3. Asiyumbishwe na ushindani. Huu upo kote duniani na ndiyo maana ni rahisi kusikia Nicki Minaj anashindana na Iggy Azalea. Anachotakiwa ni kuweka chapa zake katika aina fulani ya muziki ili vizazi vijavyo viweze kumkumbuka kwa muziki wake fulani kama anavyojulikana Michael Jackson kwa muziki wa Pop.

4. Afanye sana kazi za kijamii. Hili linaonekana kuwa jambo dogo sana lakini unapoamua kufanya kazi za kijamii inakuweka karibu na mashabiki zako na pia unabarikiwa kulingana na kile unachokifanya.
5. Asiweke nguvu zake nyingi katika mambo yasiyokuwa na tija. Hili huwa linamfanya mwanamuziki kupotea haraka. Skendo hazikufanyi kusikika bali zinakufanya kupotea kwani mashabiki zako watakuwa wanahitaji muziki, hawahusikii inavyotakiwa, skendo zinakuwa nyingi kuliko kazi. Kiba amejulikana kwa sababu ya muziki, hajajulikana kwa sababu ya skendo, waliosikika kwa skendo acha wafanye skendo ila kama umejulikana kupitia muziki, fanya muziki.

6. Awasaidie wazazi wake kwa kila kitu. Wazazi ndiyo nguzo muhimu sana hapa duniani. Unaweza kuona unafanikiwa lakini unapomwacha mzazi ni lazima kutakuwa na vitu vibaya vitatokea, huwezi kuviona sasa hivi, kuna siku ukishaanza kushuka, kuna sauti moja ya upole itasikika moyoni mwako, itakwambia kwamba tatizo halikuwa kukosa thamani, halikuwa kukosa mapromota, tatizo kubwa lilikuwa ni mama au baba kwani Mungu aliwachagua hao wawe wazazi wako kwa makusudi yake.

7. Nilipokutana na Seven na kuzungumza naye, nilibahatika kumwambia kuhusu gharama kubwa, kwa unyenyekevu mwingi, alikiri kuwepo kitu hicho na ndiyo maana shoo zake si nyingi sana nyumbani. Namnukuu Seven: “Ni kweli Eric, gharama zipo juu lakini ndivyo tunavyotoza hata huko nje. Ili kidogo tufanye shoo za kutosha hapa nyumbani, basi wadhamini wajitokeze wengi japo na sisi gharama zishuke kwa kuwa wakijitokeza wengi, na sisi tutaingiza kingi hivyo hata malipo yatakuwa madogo. Kama akija mdhamini mmoja, inajulikana kwamba lazima shoo iwe ya gharama sana. Lakini mbali na hilo Eric, naandaa kufanya shoo za hisani mara kwa mara ili kuisaidia jamii kwani naamini itamfanya Ali kuwa karibu na mashabiki zake.”

Aliendelea kuongea kwamba malipo ya nyumbani yana kila sababu ya kushushwa kwa kuwa Tanzania ipo chini kiuchumi, si kama Afrika Kusini au nchi za Ulaya. Mashabiki watuelewe tu kwamba tunajua kwamba wanatofautiana kifedha, hatuwezi kuwatenga kwa kuwa wote ni mashabiki zetu, tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha shoo zinamfikia kila mtu,” alimalizia Seven.