TID: Wasanii wananyanyaswa na wadau wa muziki

TID amelalamika kuhusu rushwa ambayo wasanii wanalazimishwa kutua na wadau wa muziki. Staa huyo anadai wasanii wananyonywa na wadau ambao wameweka pesa mbele.

TID anasema kuwa kuna baadhi ya wadau ambao wanaomba rushwa kutoka kwa wamamuziki ile ngoma zao ziweze kupenya kwenye masikio ya mashabiki.

Hit maker huyo wa kitambo anasema kitendo hicho kimewalazimisha wasanii wengi kutenga bajeti ya kufanya matangazo ya kutosha ili kazi ziweze kusikika mitaani na sehemu mbalimbali.

“Nakerwa sana na watu ambao hawajui jinsi gani sisi tunasumbuka. Unalipa studio, video na mambo kibao kwa ajili ya kufanikisha kazi, cha ajabu DJ anaweza akataka kupiga lakini mtangazaji anakwambia acha mpaka atoe kitu huu ni uuaji wa vipaji na ninapigana nao sana. Sasa wameshatujengea kwenye mindset kuwa ukiandaa ngoma andaa na pesa ya kutulipa ili kazi itembee” TID alisema akiwa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio.

 

Paul Makonda asema vijana wengi wameacha madawa ya kulevya tangu awachukulie watu maharufu hatua

Paul Makonda anaonekana kuwa mtu anayefuraha nyingi baada ya kufanya vijana waache kutumia madawa ya kulevya. Katika sherehe zilizofanyika hivi majuzi, Paul Makonda alisikika akisema kuwa vijana wengi wameacha madawa kupitia jitihada alizofanya kwa kushirikiana na Watendaji wengine wa Serikali.

Soma:“Mkome kunihusisha na watu wasio jua kitu chochote kuhusu maisha yangu” Wema Sepetu awaonya mashabiki
Mh Makonda huyu amesema kuwa jambo hilo linawafurahisha wazazi wengi walikuwa wanahofia watoto wao kupotea kwa kutumia madawa haya. Ingawa si wote wamebadilika, Makonda anaendelea kujitia moyo kuwa siku itafika na pia wao watanaswa na mkono wa serikali kuwanyosha.

Mwezi uliopita Paul Makonda aliwapeana amri kuwa Wema Sepetu, Romy Jones, TID na wengine wakamatwe kwa kushukiwa kuwa walikuwa wanahuika na mauzaji na matumiaji ya dawa za kulevya.

Lakini kwa sasa Paul Makonda amemsifu TID kwa kusema kuwa anaendelea vizuri na pia afya yake inaendelea kuwa nzuri. Hivi sasa anvutia kisura na ikiwa amejitolea kuachan madawa kabisa, basi mwezi ijayo atakuwa mtu wa maana tena