Enock Bella :Upendo wa Ya Moto Bado Uko Pale Pale

Moja ya wasanii ambao waliokuwa wanaunda kundi la Ya moto Band Enock Bella amefunguka na kusema kuwa watu wengiwameku wakisema kuwa kundi la ya moto band limekuwa halina mawasiliano na wamekuwa katika mgogoro tangu wametengana na kwamba hawataweza kufanya chochote pamoja lakini maneno hayo si ya kweli hata kidogo.

Enock Bella amesema  hayo alipouwa akiongea na Times Fm katika kipindi cha The Playlist  na kuongezea kuwa watu watakuja kushangaa sana pale ambapo wasanii hao watakuja kufanya   kazi tena pamoja hata kama kila mtu yuko chini ya uongozi wake.

Itafika sehemu tutachukua nyimbo za ya moto band na kuzipeleka tena kwa mashabiki wetu,usishangae kusikia kuna ngoma yangu na Aslay, au ukasikia ngoma yangu na beka au  moja  kati ya hao na Maromboso.bado upendo wetu uko palepale.

Baada ya Ya Moto Band kusambaratika katika umoja wa band yao wasanii hao walianza kufanya kazi kila mmoja chini ya uongozi wao huku Aslaya akiwa wa kwanza kutoa nyimbo zake na zimekuwa nyingi kuwazidi wote , huku Maromboso nae akiwa amechukuliwa na uongozi mpya wa wasafi  na kwa sasa ameanza kuachia ngoma zake.

 

Beka Flavour Asema Hayuko Tayari Kurudi Ya Moto Band

Moja wa wasanii walikuwa wakiunda kundi la Ya Moto Band amefunguka na kusema kuwa kwa sasa yeye hayuko tayari kabisa kurudi Ya Moto Band hata kama kundi hilo litarudi kwa sababu kila mtu kwa sasa anasimama mwenyewe na anajua kuwa kundi ilo lilishakuffa.

Beka alisema kuwa wakati wanaondoka katika kundi ilo kipindi linavunjika waliondoka bila kuwa na ela yoyote , ilhali kipindi wanafanya kazi walikuwa wakipewa ela kidogo sana kwa ajili ya matumizi binafsi huku wakiwa wamependekeza kuwa ela zinazopatikana kutokana na kazi yao zifanyiwe matumizi kama vile kujenga nyumba lakini waliondoka bila ela yoyote,

“Mimi saivi uniambie nitoke kwenye uongozi wangu mpya afu nirudi Ya Moto sidhani kama itawezekana kabisa,unajua kuwa watu hawajui tu kuwa lile kundi lilishakufaga siku nyingi tu, kwa sababu saivi kila msanii yupo katika uongozi wake,sidhani kama kuna mtu atakubali atoke huko alipo kwenye uongozi wake aje tena kurudi katika kundi la Ya Moto Band” Alifunguka

Msanii huyo ambae saivi anafanya vizuri na kibao chake cha sikinai, anasema kuwa kwake yeye ni furaha anapoona wasanii aliotoka nao kundi moja wanapofanya vizuri, akiongelea upande wa Aslay anasema kuwa anafurha kuona aslay sasaa hivi amekuwa msanii anaeongelewa kila sehemu kutokana na kazi zake nzuri.

“Mimi nazidi kumuombea mwenzangu, maana amekuwa ni mmoja wa wasanii ambao wanazungumziwa sana  kutokana na kazi zake nzuri anazofanya,lakini napenda pia kuwaambia watanzania kuwa wasanii  ambao tulikuwa tukiunda kundi hili la Ya Moto Band Mungu alitupa vipaji vyetu maarum, kuna kitu aliweka ndani yetu , kwaio sio muda mrefu  mtakuja kuona haya ninayoyasema kwani kila mmoja wetu  ana upekee wake kwenye kazi. alisema Beka Flavour.

Kundi la Ya Moto Band lilikuwa ni moja ya makundi yalikuwa yakifanya vizuri nchini Tanzania , lakini baadae lilikuja kuvunjika huku hakuna uongozi uliotaka kuweka wazi sababu za kuvunjika kwa kundi ilo.Hata hivyo baadhi ya wasanii wa kundi ilo wameanza kuonyesha juhudi zao nje ya kundi akiwemo Aslay.

Wasanii waliokuwa wakiunda kundi la Ya Moto Band

Mh.Temba Asema Sababu Za Kuvunjika Kwa Ya Moto Band

Imekuwa ni kama desturi kwa baadhi ya makundi mengi ya muziki kuvunjika na kushindwa kuendelea kufanya kazi pamoja, ilhali wanakuwa tayari walishateka soko la muziki na mioyo ya mashabiki wa muziki, ndicho kilichotokea kwa kundi la muziki wa Ya Moto Band , kundi lililokuwa likifanya vizuri na kupendwa na watu wengi katika muziki wao waliokuwa wanaufanya,lakini pia umaarufu wao haukuwa tu nchini Tanzania bali hata nje ya nchi, .Kwa sasa kundi ilo la muziki limevunjika huku kila msanii akitafuta ustaarabu wake wa kufanya kazi zake za kimuziki, inaweza kuwa bahati nzuri au kipaji cha msanii ndicho kinaweza kumpelekea kuendelea kufanya vizuri katika muziki kwa upande wao.

Sababu za kuvunjika zimekuwa nyingi lakini hakuna anaekuja na jibu kamili kuhusu kuvunjika kwa kundi ilo , Mh. Temba ameibuka na kuongelea sababu za kuvunjika kwa kundi ilo, akiwa kama mmoja wa waanzilishi na mlezi wa kundi ilo la muziki tangu wakiwa chini mpaka wameanza kujulikana Mh. Temba anaasema kuwa shida kubwa ya kuvunjika kwa kundi ilo ni kuvamiwa na watu wenye ela.

Akiongea na East Africa  katika kipindi cha Planet Bongo, Mh.Temba anakiri kuwa kundi ilo lilianza kuingiliwa kati na watu wenye fedha na kutaka kuwamiliki wasanii bila kuangalia wasanii hao wametoka wapi huko nyuma.”mimi nakupa mfano wa hawa Ya moto band,utaona labda mtu anasimamia msanii fulani,,mbona hakumchukua mwanzoni wakati  hajulikani, kabla hatujamkuza na kuwa superstar” alifunguka Mh.Temba

kwa maoni yake anasema kuwa kama hao wenye pesa walitaka kusaidia wasanii basi wanapaswa kutafuta vipaji vipya mitaani viko vingi na wanaitaji kuinuliwa lakini sio kuja kuingilia kwa wasanii ambao tayari walishakuzwa na wana majina tayari’huyo mtu kama anauwezo  kwanini asingekuwa na vipaji vyake,wewe unaona nuru tayari inangaa ndo  unaenda kuchomoa pale” aliongezea Mh. Temba

undi la Ya Moto Band lilikuwa likiundwa na Aslay, Enock Bella, Maromboso na  Beka Flavour, lakini kwa sasa kundi ilo kila mmoja anafanya kazi kwa kujitengemea huku Aslay akiwa  chini ya menejimenti ya Chambuso . Hata hivyo baaada ya kundi ilo kuvunjika msanii anaeonekana kufanya vizuri kuliko wote  ni Aslay huku wengine wakioneka kushindwa kabisa kutokana na ukimya wao.kundi ili kuvunjika na dalili mbaya ya kupotea kwa vipaji vya muziki.