Bekaflavour Agoma Kuwa Chanzo cha Kuvunjika kwa Ya Moto

Msanii Beka flavour amefunguka na kusema kuwa hata siku moja hataki kupokea lawama anazorushiwa kuwa yeye ni moja kati ya sababu ya kundi lao la Ya Moto kuvunjika miaka ya nyuma na kusababisha kila mtu kufuata ustaarabu wake.

Beka anasema kuwa mashabiki inatakiwakufika sehemu na kukubaliana na matokeo na  kuwa kila kitu kina muda wake lakini sio kurusha lawama na kumtafuta mchawi nani katika hilo, Hata hivyo swala la kuvunjika kwa kundilimeweza kusababisha watu kujiongeza na kupambana zaidi.

Beka anasema kuwa kwa kumbukumbu yake anajua kabisa kuwa hakuwahi kugombana na mtu katika lile kundi zaidi ya mmoja tu na haikusababisha kugombana sana kwa sababu walikuja wakakaa sawa.

Utakumbuka kuwa wasanii hawa walikuwa wakifanya kazi pamoja katika kundi moja lakini baadae kila mmoja alikwenda na njia yake baada ya kundi hilokushindwa kuendelea.

Sina Ninachohofia Kuhusu Mapenzi ;-Bek Flavour

Msanii wa muziki Bongo, Beka Flavour amesema kuwa mara kadhaa amekuwa akiweka picha za mpenzi wake kwenye mtandao na haofii chochote kwani wanaaminiana.

Muimbaji huyo amefunguka hayo akipiga stori na Clouds FM ambapo amesema hata hasipo muweka mtandaoni kama si mwaminifu haitosaidia chochote.

“Mwanamke kuchukuliwa na mwanaume mwingine kwa sababu ya kumpost kwenye mitandao ya kijamii basi huyo mwanamke hana mapenzi ya dhati kwa mwenza wake japo kuna baadhi ya watu wanamsumbua kwenye Dm yake ila kwa sababu namuamini (Tunaaminiana) hivyo sina cha kuhofia kwake”  ameeleza Beka

Utakumbuka Beka Flavour aliyekuwa miongoni mwa wasanii wanaounda kundi la Yamoto Band, yeye na mpenzi wake aitwae Happiee Reuter wamejaliwa kupata mtoto mmoja kwenye mahusiano yao.

NImeoa kwa Siri ” Beka Flavour

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Beka Flavour, ameweka wazi kuwa sasa yeye sio msela tena kwani amemuoa rasmi mama mtoto wake, anayejulikana kwa jina la Happy.

Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Beka Flavour amesea kwamba msichana huyo ambaye amezaa naye, ni mke wake rasmi kwani amemuoa kwa imani yake ya dini ya Kiislam, lakini hakutaka kuweka wazi kwa watu.

Mimi nimeoa kabisaa, japokuwa sio kila mtu anajua kuwa nimeoa, unajua ili mtu mwengine ajue kuwa umepitia taratibu zote na kihalali kabisa, lazima uweke wazi kwenye simu, mimi nimeoa kihalalai, si unajua sisi Waislamu mambo yetu chini chini, ila sijataka kuweka wazi”, 

Beka Flavour nameendelea kusema kwamba mke wake alilazimika kubadili dini ili waweze kufunga ndoa ya Kiislam, kwani awali alikuwa na imani ya Kikristu.

Beka Athibitisha , Anakaribia Kuitwa Baba.

Mwanamuziki Beka Flavour amethibitisha kuwa hivi karibuni ataitwa baba kutokana na ukweli kuwa mpenzi wake  wa siku nyingi kwa sasa ni mjamzito.akiongea kwa kujiamini, beka anasema kuwa huyo ndio atakuwa mtoto wake wa kwanza na kwamba katika kundi lao lilivunjika ni yeye pekee ndio alikuwa hana mtoto hata mmoja.

Beka ambae hivi karibuni alitoa wimbo mpya anasema kuwa ametoa wimbo huo ili uwe maalum kwa mwanamke wake huyo ambae alianza nae mapenzi kabla hajaanza muziki na mpaka sasa huku wakipitia mambo mengi hapo katikati ikiwa ni pamoja na ugumu wa maisha lakini hakukata tamaa zaidi ya kuwa anampa moyo na kumfarijikwa kila hali.

Akitoa sababu ya kuchelewa kupata mtoto, Beka anasema kuwa kwa jinsi mapenzi aliyokuwa nayo mwanadada huyo aliona kuwa ni bora kwanza akae vizuri kifedha ndipo aone jinsi ya kuongeza mtoto ili asije aka mtesa binti wa watu alikaa nae katika shida na raha zote.

Nimejikuta nimeshindwa kujizuia kupost hii picha na hivi karibuni nitatwa baba,furaha niliyonayo haipimiki kwani huyo atakuwa mtoto wangu wa kwanza.

 

Mimi Ndio Mtu wa Kwanza Kupata Mtu wa Kunisaidia Ilipovunjika Ya Moto:-Beka

Msanii wa muziki anaefanya vizuri kwa sasa na  nyimbo zake mbalimbali Beka Fleva amefunguka na kusema kuwa nashukuru mungu sana kwa sababu  baada ya kuvunjika kwa ya moto yeye ndio alikuwa mtu wa kwanza kupata mtu wa kumsaidia kuendelea na muziki.

Beka anasema kuwa siku meneja wao  wa bendi anatangaza katika media kuwa kuanzia sasa wasanii wa band ya ya  moto watakuwa free kufanya muziki wao wenyewe alikuwa moja  ya watu waliokuwa na stress sana kwa sababu alikuwa keshazoea kuwa anafanyiwa kila kitu wao kazi yao kuimba tu , ukizingatia kuwa walikuwa hawajuani hata na watengenezaji wa muziki kwa sababu hawakulelewa hivyo katika band.

Akiongea katika Clouds 360, beka ansema kuwa baada ya kutoka katika interview siku hiyohiyo mtu mmoja aliyemtaja kwa jina la Silaji alimtafuta kwa simu na kumwambia kuwa anapenda sana muziki wake na anaomba kufanya nae kazi.

Beka anasema kuwa baada ya hapo alipewa ela ya kutoa wimbo wa Libebe na Sikinai na baada ya hapo alianza kupata ela kutoka katika show na kuanza kufanya mwenyewe lakini bado mtu yule aliyemsadia mpaka leo anafanya nae kazi na ndio amekuwa kama mkurugenzi wake.

Beka Atoa Sababu Iliyomfanya Asifike Kwenye Party ya Mboso

Msanii wa kizazi kipya bongo Bakari Abdul maarufu kama Beka Flavour ameongea na kuweka wazi sababu kubwa iliyomfanya asihudhurie katika party ya kutambulishwa kwa aliyekuwa mwanamuziki mwenzie waliokuwa wakifanya kazi pamoja katika kundi la ya moto band kabla kundi hilo halijavunjika Maromboso.

Beka anasema sababu kubwa ni kucheleshwa kwa kadi ya mwaliko wa party hiyo, ambapo  siku analetewa kadi ya mwaliko hakuwepo nyumbani alikuwa anashoot video yake mpya, hivyo amerudi ndipo anakutana na kadi na kushindw kujiandaa kwa muda huo.

taarifa niliipata lakini kadi nilicheleshwa kuipata, na ndio ikawa siku anatambulishwa na mimi niko location ya wimbo wangu mpya.nafika nyumbani usiku  nakutana na kadi  yaani ni usiku kwa usiku.kwaio mimi sikuweza kuwahi na kwenda lakini meneja wangu alituwakilisha.

Hata hivyo Beka anasema kuwa anaamini kabisa kuwa Mboso ni msanii mzuri na ana lengo la kuifisha sanaa ya bongo fleva mbali hivyo nawaomba mashabiki wake wampe sapoti kubwa ili aweze kufanya vizuri.

Mboso na Beka wote walikuwa katika kundi la ya moto kabla halijavunjika , baada ya kuvunjika kila mtu alianza kutafuta ustaarabu wake na kutoka kivyake.hata hivyo wikiendi iliyopita Mboso alikaribishwa rasmi katika lebel kubwa nchini  ya WCB, huku ikitegemewa kuwa wasanii wenzie alikuwa akifanya nao kazi wangeweza kujitokeza kwenye jambo hilo la furaha lakini hali haikuwa kama ilivyo.

wWsanii wengine waliokuwa wakiunda kundi la ya moto kabla ya kuvunjika ni pamoja na aslay na Enock bella ambao nao pia hawakufika .

Beka Flavour Awachana Wanaotafuta Kiki Kwa Ku-fake Maisha

Beka flavour ni moja ya wasanii wanaofanya vizuri sana kimuziki kwa sasa kutokana na ngoma yake kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya habari, akiwa  ana-hit na ngoma yake ya Libebe Beka anapata shavu kubwa sana kutokana na hit song hiyo.

Hivi karibuni msanii huyo ameibuka na kuongelea wasanii wanaojifanya kutafuta kiki ya muziki kupitia ku-fake maisha yao  na kujiona wao ni wa gharama sana kuliko watu wengine.Akitolea mfano wa wasanii wawili wa kike Shiloleh  ambae wiki ilyopita alisema kuwa anavaa nguo za bei ghali sana na Gigy Money ambae amekuwa akijitapa kuwa anatumia ela nyingi sana kuvaa na kutengenza nywele ambapo alisema amevaa wigi la milioni.

Beka amesema kuwa wasanii hao wamekuwa wakitafuta kiki tu lakini hakuna cha milioni wala nini,hata hivyo anasema kwa upande wake hawezi kufanya ujinga wa kujidanganya kiasi hicho.

Hakuna cha milioni wala nini zaidi ya kutengeneza kiki tu mjini,wasanii wana mbembwe sana.Wengine wanadanganya wana mali nyingi sana lakini hakuna kitu chochote kile.Kwa upande wangu mimi siwezi kufeki uhalisia wa maisha yangu  hata siku moja  na siwezi kuendesha maisha yangu ya muziki kwa kutegemea kiki hata mara moja  maana najiamini sana na kazi zangu

Imekuwa ni kawaida kwa wasanii wa bongo kuendekeza kiki na kujifanya wanafanya shopping na kununua vitu vya gharama wakati katika uhalisia hakuna kitu chochote kile, wengine wamekuwa wakiishi maisha tofauti ya kipato wanachoingiza hiyo yote waonekana kuwa wanaela nyingi wakati wanaishi maisha magumu.

Gigy Money ni mmoja ya wasanii ambao hivi juzi juzi alisema katika media kuwa amevaa wigi la zaidi ya milioni  moja na kuwa anaishi nyumba zaidi ya milioni nane ya kodi.

Wasanii wanapaswa kuishi maisha yao kulingana na uhakisia wao kwa sababu mashbiki wao wanavyowapenda na kuwasapoti hawaangalii vipato vyao zaidi ya kazi nzuri wanazofanya.Na vilevile wanapodanganya aafu ikagundulika ni uongo inakuwa inapunguza imani ya mashabiki kwao.

Beka Flavour Asema Hayuko Tayari Kurudi Ya Moto Band

Moja wa wasanii walikuwa wakiunda kundi la Ya Moto Band amefunguka na kusema kuwa kwa sasa yeye hayuko tayari kabisa kurudi Ya Moto Band hata kama kundi hilo litarudi kwa sababu kila mtu kwa sasa anasimama mwenyewe na anajua kuwa kundi ilo lilishakuffa.

Beka alisema kuwa wakati wanaondoka katika kundi ilo kipindi linavunjika waliondoka bila kuwa na ela yoyote , ilhali kipindi wanafanya kazi walikuwa wakipewa ela kidogo sana kwa ajili ya matumizi binafsi huku wakiwa wamependekeza kuwa ela zinazopatikana kutokana na kazi yao zifanyiwe matumizi kama vile kujenga nyumba lakini waliondoka bila ela yoyote,

“Mimi saivi uniambie nitoke kwenye uongozi wangu mpya afu nirudi Ya Moto sidhani kama itawezekana kabisa,unajua kuwa watu hawajui tu kuwa lile kundi lilishakufaga siku nyingi tu, kwa sababu saivi kila msanii yupo katika uongozi wake,sidhani kama kuna mtu atakubali atoke huko alipo kwenye uongozi wake aje tena kurudi katika kundi la Ya Moto Band” Alifunguka

Msanii huyo ambae saivi anafanya vizuri na kibao chake cha sikinai, anasema kuwa kwake yeye ni furaha anapoona wasanii aliotoka nao kundi moja wanapofanya vizuri, akiongelea upande wa Aslay anasema kuwa anafurha kuona aslay sasaa hivi amekuwa msanii anaeongelewa kila sehemu kutokana na kazi zake nzuri.

“Mimi nazidi kumuombea mwenzangu, maana amekuwa ni mmoja wa wasanii ambao wanazungumziwa sana  kutokana na kazi zake nzuri anazofanya,lakini napenda pia kuwaambia watanzania kuwa wasanii  ambao tulikuwa tukiunda kundi hili la Ya Moto Band Mungu alitupa vipaji vyetu maarum, kuna kitu aliweka ndani yetu , kwaio sio muda mrefu  mtakuja kuona haya ninayoyasema kwani kila mmoja wetu  ana upekee wake kwenye kazi. alisema Beka Flavour.

Kundi la Ya Moto Band lilikuwa ni moja ya makundi yalikuwa yakifanya vizuri nchini Tanzania , lakini baadae lilikuja kuvunjika huku hakuna uongozi uliotaka kuweka wazi sababu za kuvunjika kwa kundi ilo.Hata hivyo baadhi ya wasanii wa kundi ilo wameanza kuonyesha juhudi zao nje ya kundi akiwemo Aslay.

Wasanii waliokuwa wakiunda kundi la Ya Moto Band

Beka Flavour: Mimi ndiyo Justine Beiber wa Bongo

Msanii aliyekuwa katika kundi ya Yamoto Band – Beka Flavour amefunguka na kusema kuwa yeye ndo Justine Beiber wa Bongo.

Akiongea na E-Newz ya EATV, Beka alisema kuwa yeye sasa ameachana na mambo ya kiki kwasababu anataka kuboresha muziki wake.

“Siku hizi hamna muziki wa maneno mengi na kiki sema mimi nilikuwa naona vile vitu vilikuwa vinaendelea mtandaoni. Ukweli hamna kitu kama hicho mimi nafanya muziki wangu binafsi halafu ninaamini ni wakwangu, mimi ndiyo Justine Beiber wa Bongo,” amesema Beka Flavour.

Beka Flavour

Staa huyo pia aliwakashifu wanahabari kwa kumliganisha na Aslay ambaye alikuwa naye Yamoto Band. Beka alisema kuwa yeye hafanyi muziki ya ushindani na kuongeza kuwa hana tatizo na msanii wowote wa Bongo.

“Wanatakiwa watusapoti, siyo poa wanavyoandika wanatushindanisha halafu mimi sifanyi muziki wa ushindani na miaka 100 siwezi nikafanya muziki wa ushindani sina tatizo na msanii yeyote kutoka Tanzania.”

 

Beka Flavour: Aslay si msanii mkubwa kwamba mimi nimuogope. Ali Kiba ndo anaweza

Msanii Beka Flavour sasa anavurugana na Aslay kuonyesha ubabe katika muziki. Bifu yao ni kama ile ya Ali Kiba na Diamond igawa bado haiwezi.

Ubishi kati ya Beka Flavour na Aslay unadhihirika jinsi wanavyoachia nyimbo zao zikifwatana. Akiongea na eNewz, Beka Flavour alisema hawezi kumruhusu Aslay kutoa ngoma bila yeye kuachiza nyimbo zake zishindane na za hasimu wake.

“Nimepanga kuachia wimbo mpya wiki mbili zijazo lakini kama Aslay akiachia tena kazi mpya sitaweza kumvumilia na mimi nitaachia mashine ili zipambane mbele kwa mbele maana mimi nimeshapanga ratiba zangu na siwezi kuzivunja,” Beka Flavour alisema.

Beka Flavour

Staa huyo hata hivyo alisema Aslay sio msanii mkubwa wa kumuangalia wakati anafanya kazi zake, alidai kuwa Ali Kiba ndiye kioo chake Tanzania.

“Mimi natoa nyimbo zangu kulingana na jinsi ambavyo nimepanga ratiba yangu na uongozi wangu. Sijashindwa kuachia wimbo eti kwa sababu Aslay katoa ngoma mpya ila matatizo niliyopata ya kupelekwa polisi ndiyo yaliyonifanya nisogeze vitu mbele. Aslay siyo msanii mkubwa kusema kwamba mimi nimuogope au nimfikirie. Hapa nchini msanii mkubwa ni Alikiba na ndo kama kioo najitazama lakini siyo Aslay. Mimi natazama wasanii wakubwa nje ya nchi lakini siyo ndugu yangu,” Beka Flavour alifunguka.