Mange Amkingia Kifua Mobetto Dhidi Ya Familia Ya Diamond Kufuatia Tuhuma Za Uchawi

Mwanaharakati wa mambo ya siasa na mdau wa mitandao ya kijamii Mange Kimambi amemkingia kifua Hamisa Mobetto baada ya familia ya Diamond kumuandama na skendo za ushirikina.

Mama Diamond na Esma Platnumz wamemtuhumu Hamisa kwa uchawi ambapo wamedai kuwa alienda kwa mganga kwa nia ya kumloga Mama Diamond na Esma ili wampende na aolewe na Diamond.

Mange ameibuka na kumtetea Hamisa dhidi ya tuhuma hizo na hata kuwatupia maneno ya shombo familia ya Diamond na Wema Sepetu ambaye pia ameonekana kumsema na kumtupia vijembe Hamisa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mange Kimambi ameandika maneno haya:

https://www.instagram.com/p/BnMqWQFFRTt/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1d4duzu19snyf

Familia Ya Diamond Yamtuhumu Mobetto Kwa Uchawi

Familia ya staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz imerudi kwenye headlines kwa bifu lao na mzazi mwenza wa Diamond, Hamisa Mobetto.

Bifu la Hamisa na Familia ya Diamond lilianza baada ya Hamisa kuzaa na Diamond ambapo Hamisa alisambaza picha zake na Diamond na hata kuwaitia Shilawadu Mama Diamond na Esma.

Mama Diamond na dada wa Diamond, Esma wamekuwa wawazi juu ya chuki yao kwa Hamisa lakini siku mbili hizi pande Hizi mbili ziliingia kwenye mzozano mkali kwenye mtandao wa kijamii.

Mama Diamond na Esma wamemtuhumu Hamisa kwa uchawi ambapo wamedai kuwa Hamisa alienda kwa mganga kwa nia ya kumloga Mama Diamond na Esma ili wampende na aolewe na Diamond.

Inasemekana kuwa kuna voice note ambayo Hamisa alirekodiwa na mganga akiwa anaongea na kwa kuwa mganga huyo anafahamiana na Mama Diamond basi akamtumia.

Esma, Mama Diamond na Wema wameonekana kumtupia vijembe Hamisa kwa tuhuma za uchawi:

Hamisa hajakana wala kukubali tuhuma hizo za uchawi lakini kuna baadhi ya mashabiki zake wamekuwa wakidai kuwa skendo hiyo imetengenezwa na Mama Diamond na Esma ambao wamefoji Voice note.

Esma- Sina Ubaya na Hamisa Akitaka Tuongee Tutaongea

Dada wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz amefunguka na kuweka wazi uhusiano wake na mzazi mwenzake na kaka yake Hamisa Mobetto.

Siku za nyuma Hamisa na Esma walikuwa mashoga wakubwa sana lakini urafiki huo uliingia doa mwaka jana baada ya Hamisa kumtangaza Diamonf kama Baba wa mtoto wake ndipo matatizo na Familia ya Diamond yalipoanzia hapo.

Mpaka leo hii kuna sintofahamu bado kati ya Hamisa na Familia ya Diamond lakini Esma anafunguka na kuweka wazi kuwa hana bifu na Hamisa na kama akitokea kutaka kuongea naye basi yeye kwake ruksaa moyo mweupe.

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Esma ameweka wazi kuhusu hali yake ya Mahusiano na Mobetto:

Hamisa alikuwa akikosea mimi nilikuwa namsema kwa sababu mimi sina ubaya na mtu na ninaongea na mtu yoyote na Hamisa akitaka tuongee tutaongea yaani mimi naongea na watu wote”.

Esma pia alifunguka kuhusu mtoto wa Hamisa Dylan ambaye amekuwa akionekana naye sana siku za hivi karibuni:

Sisi hatuna tatizo lolote na mtoto halafu yule ni mtoto halafu pia ni damu yetu kwaiyo tu nampenda”.

Lakini pia Esma amemtupia Dongo Hamisa kuhusiana na wimbo wake alioachia hivi karibuni wa Madam hero kudai ni wimbo wa kusikitisha sana na akiongia yeye studio atamtupa mbali.

 

Petit Man Ayatetea Mapishi Ya Mke Wake Esma

Hamad Manungwa maarufu kama Petit Man ameibuka na kumkingia kifua mke wake Asmah Khan ‘Esma Platnumz’ baada ya kutuhumiwa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa hajui kupika.

Siku chache zilizopita Esma aliposti picha ya chakula alichomuandalia mume wake kama futari lakini mambo yaligeuka kwani mashabiki walimjia juu na kumsema hajui kupika.

Lakini Petit ameibuka na kusema wote wanaotokwa na maneno kuwa mke wake hajui kupika hawajui wanachokiongea kwani yeye ndio anajua anapikiwa nini kila siku.

Petit alifunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers ambapo alizidi kufunguka:

Unajua mimi sibishani hata siku moja na watu wa mitandaoni kwa sababu najua wazi sio mke wangu aliyepika ile futari. Akipika yeye chakula kinakuwa cha uhakika, nikila nasikia raha hadi najivunia kumuoa, hao wanaosema Esma hajui kupika, wana lao jambo”.

Baada ya Tuhuma hizo kuzidi Esma aliposti chakula kingine huku akisisitiza kuwa chakula watu walichokiona hakupika yeye.

 

Esma- Wema Ndio Ana Mapenzi Ya Kweli Alimpenda Naseeb Sio Diamond

Dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Platnumz amemwagia sifa kibao aliyekuwa wifi yake Wema Sepetu kwa kudai ndio mwanamke aliyempenda kweli Diamond.

Kama utakumbuka Wema na Diamond walikuwa wapenzi kwa muda mrefu tangu Wema alipokuwa Miss Tanzania kwa kipindi hiko Diamond alikuwa ndio anaanza muziki.

 

Esma alianza kwa kumposti  Wema na  kuanza kumsifia kuwa amependeza na mavazi yake ya kinigeria ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram aliweka posti:

Baada ya posti hiyo kuzua gumzo baada ya Esma kuendelea kuitana wifi na Wema hata baada ya Wema kuachana na kaka yake Diamond, na Esma alifunga kazi kwa kumwagia sifa Wema huku akikiri yeye ndio wifi aliyempenda kweli Diamond kwani alianza naye mapenzi wakati hana kitu mpaka leo staa.

Wema uwifi hauishi leo wee ndio forever wiii wa kihistoria mtoto wa watu unajua kuishi ulimpenda Naseeb na sio Diamond”.

 

Pamoja na kwamba Wema aliachana na Diamond muda mrefu uliopita lakini amekuwa bado karibu sana na familia yao.

Nitafurahi Kama Diamond Atamuoa Wema: Esma Platnumz

Dada wa supastaa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Esma Khan amefunguka na kudai kuwa atafurahi endapo kaka yake atamuoa Wema Sepetu.

Tangu Diamond atangaze kufunga ndia mwaka huu baada ya kuachana na mama watoto wake na mpenzi wake wa miaka mingi Zarinah Hassan ‘Zari’ swali pekee lililopo midomoni ni mwanamke gani ambaye Diamond anaweza kumuoa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na ‘Over the weekend’ alifunguka kuwa kwa upande wake hawezi kumchagulia mke kaka yake lakini Kama moyon wake ukiamua kurudi kwa Wema basi yeye moyoni mwake furaha zaidi.

Unajua Naseeb ndio anajua zaidi mke anayemfaa, lakini kama pia ataamua kurudi kwa Wema, mimi nitafurahi zaidi kwa sababu ni mtu ambaye tunapatana sana na ninampenda pia”.

Tangu Diamond atangaze ndoa kabla mwaka huu haujaisha kuna wanaodai atakayeolewa ni Wema wengine wanasema ni Zari na pia kuna wanaodai ni Hamisa.