Bahati Kutoka Kenya Bado Yupo Na Lulu Kichwani Kwake

Mwanamuziki wa nyimbo za injili kutoka Kenya Bahati amekiri Elizabeth Michael maarufu kama Lulu bado anamchanganya kichwani baada ya kuharibu makubaliano yao siku za nyuma.

Bahati alishawahi kufunguka na kusema mwaka 2016 alitoka nchini Kenya mpaka Tanzania kwa ajili ya kumtaka Lulu awe Video vixen Kwenye wimbo wake unaoitwa Maria lakini alipofika hotelini ambapo walipanga kukutana kwa ajili ya kikao Lulu hakufika

Bahati alidai baada ya Lulu kumgeuka na kukataa kutokea mwishoni kabisa hivyo ikabidi amuweke Jokate kwenye video ya wimbo huo ingawa chaguo lake lilikuwa Lulu.

Safari hii  Bahati amerudi tena Tanzania kwa ajili ya kufanya kazi na msanii wa WCB, Mbosso, hata hivyo bado anakumbuka alichofanyiwa na Lulu.

Ilikuwa meeting ya video vixen, kama alinifanyia hivyo je anayempenda inakuwaje?, na mimi nilikuwa nimeweka shilingi kidogo, naongea kwa uchungu”.

Siku za nyuma msanii huyo alishawahi kukiri kuwa anampenda Lulu na kama angepata bahati ya kuwa naye basi bila Shaka angejiona mwenye bahati.

Bahati Ampongeza Diamond kuwa Msanii wa Kwanza Kuanzisha Lebo

Msanii wa muziki wa injili kutoka nchini kenya,Bahati amemsifia na kumpongeza msanii mkubwa bongo na afrika kwa ujumla Diamond Platinumz kuwa msanii wa kwanza Afrika kuanzisha lebo na kuwainua wasanii wengi we waliokuwa na vipaji na wakakosa watu wa kuwapa sapoti.

Bahati ambae nae pia amekuwa na lebo yake ya kutengeneza wasanii wanaochipukia inayojulikana kama EMB, amesema kuwa Diamond ni mfano wa kuigwa kwa sababu ameweza kuanzisha na kuisimamaia lebo hiyo na kuweza kufanikiwa kujulikana kila sehemu na watu wengi sasa wamekuwa wakifata mfano kutoka kwake.

Akijitahidi kumfananisha Diamond na wasanii wengine wa nje , Bahati anasema kuwa wasani wakubwa kama kina Chris Brown hawajaaanzisha lebo kwa miaka yote waliokuwepo katika muziki kwa sababu kuanzisha lebo na kuipa muda wa kukua na kuimarika ni kazi sana sio kama watu wanavyodhani .

Nataka kutoa shukrani nyingi sana na kumpongeza sana founder wa wasafi,Diamond Platinumz.unajua watu wanatoka lebo nyingi lakini wansahau kum-thank huyu mtu  na kum-acknowledge the visionary wa Afrika  Diamond kwa kuwa msanii wa kwanza kuonyesha na kuanzisha lebo na kusema zinaweza work .so big up kwanza kwa Diamond na vision yako ya Wasafi 

Bahati pia anawaomba wasanii wengine wanaotaka kuanzisha lebo wafanye kwa kuwa na vision ya kuanzisha lebo na sio kufanya tu kwa kuwa diamond au nani amefanya basi na mimi nifanye.

Napenda kuwapa neno pia wasanii wengine wanaotaka kuanzisha lebo kuwa wanapotaka kuanzisha lebo waw na vision na sio kwa sababu diamond amefanya au bahati kafanya,utajikuta unapoteza ela nyingi sana lakini hautaweza kupata vingine , lakini kikubwa utapata ambacho ssio cha muhimu sana ni likes za instagram tu.lakipi unapoanzisha lebo ni lazima uwe na roho ya kusaidia na kushikana mkono ili kuinua wengine.-Aliongea Bahati

Bahati alishawahi kufanya nyimbo  na moja ya wasanii wanaotoka katika lebo hiyo ambae ni Rayvanny na wimbo wao uliweza kufanya vizuri.

Mwanamuziki wa Kenya Bahati aelezea masaibu aliyopitia chini Lulu Michael

Mwanamuziki wa Kenya Bahati wakati huu ako Tanzania kwenye tour yake ya wimbo wake na Ray Vanny ambao uliachiliwa juzi na ambao unapatikana wasafi.com.

Katika pilka pilka hizo alijipata kwenye Magic FM ambapo alizungumzia mambo mbali mbali ikiwemo Lulu Michael na vile alipomhangaisha.

Kwa wote wanaojua msanii huyo, amekuwa akizunguliwa na Lulu Michael kwa muda mrefu na kwa hio alitaka akue kwenye video yake ya Maria.

Alikuja hadi Dar kumfata Lulu lakini hakufanikiwa.

Hii ni siri ambayo nadhani hata Wakenya hawakujua, AY peke yake ndiye alijua. Nilitoka Nairobi kuja hapa [Dar es Salaam] natafuta connection na Lulu kwasababu nataka awe kwenye ile video [Maria] ambayo nimemweka Jokate. Nimekaa kwa hotel Lulu amekataa kushika simu mpaka ikafika mahali nikamwambia ukija kuniona Mungu atakubariki, siku ya pili akakataa kabisa nikamwambia mshikaji AY acha tu nirudi nyumbani. Nikarudi hivyo,” Alieleza.

Bahati ameongeza kuwa sababu ya kufanya kazi na Ray Vanny katika wimbo wao mpya ‘Nikumbushe’ ilikuwa ni mipango yake ya muda mrefu ili muziki wake uweze kupata tobo hapa nchini.

Rayvanny afunguka kuhusu namna alivyoweza kushirikiana kimuziki na Bahati – muimbaji wa Gospel kutoka nchini Kenya

Watu wengi walishangaa baada ya Rayvanny and Bahati kutangaza kuwa wameshirikiana kimuziki, wawili hao walitoa wimbo unaoitwa ‘Nikumbushe’.

Rayvanny sasa ameeliza namna alivyoweza kushirikiana kimuziki na muimbaji huyo wa nyimbo za injili kutoka Kenya.

“Kwanza mimi nimekuwa nikimfuatilia Bahati kwa muda mrefu na nilikuwa nikifikiria nikikutana naye nitaimba wimbo wa aina gani na mimi niliwa narap huko nyuma lakini nimejua kuimba kwa kupitia kanisani. Kwa hiyo haikuwa ngumu kwangu kufanya kwa sababu ni wimbo wakijamii zaidi ndio maana wimbo hauonyeshi kama ni wa Injili au wakidunia,” Rayvanny alisema akiongea katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM.

Tazama ‘Nikumbushe’ kwenye video hapo chini: