Hii ndiyo sababu ya Chid Benz kumchana Chin Bees

Chid Benz ambaye ni mmoja wa wasanii wa hip hop walioanza kuachia nyimbo zao kitambo ameonelea kumkanya Chin Bees ambaye anatumia jina linalokaribiana na staa huyu.

Sababu za Chidi Benz kumwambia Chin Bees atafute jina lingine ni kwa sababu majina hayo yanafanana na kunauwezekano wa kuwakanganya mashabiki wake.

Ingawa wawili hawa wanafanya nyimbo tofauti Chid Benz anamtaka Chin kuwa mbunifu na kutafuta jina ambalo halifanani na lake. Msanii huyo alisema,

“Siku moja nimeona Shetta anamuangalia Instagram nikamuuliza huyo ni nini?, akaniambia ni Chin Bees, nikamuuliza anafanya muziki gani, akaniambia Bongo Fleva!. Sisemi kwa ubaya ila sikuelewa ile style anayofanya yeye ni tofauti sana na mimi mtu mzima mwenye hit kama 32 najua nikiingia kwenye stage nachapa tu,”

Akipiga stori na Planet Bongo ya EA Radio aliendelea kusema;

“Huyo Chin Bees ana single hata saba kweli?, atafute jina lingine,”

“Ni gonjwa ambalo mimi bado napambana nalo” Chid Benzi afunguka kuhusu vita yake dhidi ya utumiaji wa dawa za kulevya

Utumiaji wa dawa za kulevya ulifanya afya ya Chid Benzi kuzorata kwa kiasi kwamba alikonda sana, picha zake akiwa ameathirika na dawa hizo ziliwashtua watu wengi zilipotea katika mitendao ya kijamii.

Chid Benzi akiwa ameathirika na utumiaji wa dawa za kulevya

Chid Benzi bado anapambana na madhara ya utumiaji wa dawa za kulevya. Rapa huyo amefunguka kuhusu vita yake dhidi ya utumiaji wa dawa hizi.

“Unajua kwanza hili janga ambalo mimi niko nalo ni ugonjwa na ni ugonjwa ambao ni mgumu sana, halafu vilevile unaendana na kichwa cha mtu na maisha halisi ya mtu jinsi anavyoishi, kwa hiyo ugonjwa wenyewe unaendana na vitu ambavyo unafanya kila siku mpaka unajikuta unaingia tena kwenye mambo hayo. Kwangu mimi kuna vitu vingi ambavyo vilichanganyikana hapo katikati vilivyopelekea mimi kuchanganyikiwa na kurudi kule, lakini bado ni gonjwa ambalo mimi napambana nalo kuliondoa napigana nalo kwa hiyo watu wajue Chid anapigana nalo hili jambo” alisema Chid Benzi.

Chid Benzi akiwa sawa

 

 

Ujumbe aliyotoa Ray C kwa Chid Benzi kuhusu utumiaji wa dawa za kulevya

Rapa Chid Benzi ni miongoni mwa wasanii ambao walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya. Afya yake Benzi ilikua ya kuogofya kabla ya menaja wake Diamond- Babu Tale kumpeleka Sober House kule Bagamoyo.

Chid Benzi akiwa amekonda alipoathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya

Ray C, ambaye pia aliathirika na dawa za kulevya, amemuombea Chid Benzi kwa Mungu ili aweze kutoka rasmi kwenye mtihani wa dawa za kulevya.

Mrembo huyo alimpa moyo Chid Benzi kwa ujumbe aliyotoa, alisema kuwa anaamini rapa huyo ataweza kushinda vita dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya.

Ray C alisema anataka Benzi atoka rasmi kwenye mtihani wa dawa za kulevya kwasababu anataka kutoa wimba nyingine na yeye.  Ray C and Chid benzi walishawahi kutoa wimbo pamoja – ‘Nihurumie’.

Ray C Alimsifu Benzi na kusema rapa huyo yupo miongoni mwa marapa wakali zaidi Tanzania. Alisema pengo aliyowacha Benzi linaonekana.

“Chid benzi ni bonge la msanii na kwa upande wa Hip hop nadhani ni ‘one of the best artist’ na kwa sasa hayupo pengo lake linaonekana. Nampenda sana Chid Benzi  na ninamuombea sana kwa Mungu aweze kutoka katika janga hilo la madawa na akirudi natamani kufanya nae kazi nyingine. Aweke nia naamini atatoka.

“Binadamu wote lazima wapitie mitihani lakini tatizo mitihani hiyo lazima itakuwa inatofautiana. Haifurahishi kabisa kumuona mtu anateseka na matumizi ya dawa .Kama binadamu lazima uwe na nafasi ya kujifikiria kwa sababu hakuna mtu anayeweza kubebea ugonjwa au matatizo. Naamini Mungu aliyenisaidia mimi nikatoka kule atawasaidia wote siyo Chidi tuu bali wote wenye nia ya kuachana na yale mateso,” alisema Ray C.

Chid Benzi