Tunda Amesema Haya Kuhusu Uhusiano Wake na Diamond Pamoja na Zari

Video queen maarufu Bongo Tunda amefunguk tena kuhusiana na uhusiano aliokuwa nao na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na mpenzi wake Zari the boss lady.

Wiki chache zilizopita Tunda amekuwa akitawala vichwa vya habari mbali mbali katika mitandao huku mara zote akihisishwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Diamond lakini mara kwa mara amekuwa akikataa na kudai kuwa yeye ni shabiki wake tu na sivinginevyo.

Kwenye interview aliyofanya na Millard Ayo Tv, Tunda amefunguka na kusema yeye yupo karibu na Diamond kama shabiki lakini hana uhusiano naye lakini Zari hajawahi kuwasiliana naye wala kumtafuta kwa sababu hana cha kimwambia.

Narudia tena Mimi nahisi nasemwa sana kuwa na mahusiano na Diamond kwa sababu niko free kuweka wazi kwamba Diamond ndiye msanii ninaye mkubali sana kwa hapa Bongo tofauti na msanii mwingine sijawahi kuweka wazi nahisi ndio inapelekea watu kufikiria hayo lakini yule sio mpenzi wangu ni mtu tu ambaye namuheshimu   na yeye mwenyewe anaelewa support yangu kwake lakini sio mapenzi”.

Kwenye mahojiano hayo Tunda aliulizwa endapo ameshawahi kukutana na Zari au kumtafuta ili azungumze naye na jibu alilotoa kwa kung’aka ni amtafute Zari ili amwambie nini maana yeye anamkubali Diamond na wala sio Zari.

Tunda pia amefunguka na kudai kuwa hivi sasa yuko busy na kazi zake za kisanaa ambapo ameshirikishwa kwenye video mpya ya Barnaba.

Tunda Afungukia Tetesi za ‘Kuliwa’ na Diamond

Socialite maarufu Bongo, Tunda amekana tetesi zilizoenea mjini kuwa anatembea na msanii maarufu wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Habari ya Tunda kutembea na Diamond na kuwa mchepuko wake ndio imekuwa habari ya mjini kwa kipindi cha wiki nzima sasa huku tetesi zikienea kwa kasi ya ajabu kuwa hivi sasa Tunda tayari ana ujauzito wa Diamond

Skendo hii imeendelea kuingilia kati uhusiano wa Diamond na mama watoto wake Zari kwani kupitia page yake ya Instagram amekuwa akimrushia madongo machache baba watoto wake hadi kufikia hatua ya kumu-unfollow kwenye Instagram.

Huku hayo yote yakiwa yanaendelea Tunda amezidi kushikilia msimamo wake na kusisitiza kuwa hana uhusiano wowote na Diamond na anashangazwa na habari hizo kwani anamheshimu sana Diamond.

Tunda alifunguka maneno haya machache alipoulizwa na paparazi kuhusiana na ishu hiyo:

Nimechoka mimi kuongelea hili suala, Mimi na Chibu hatuna uhusiano wowote wa kimapenzi nilishasema yaani hii ni mara ya nne nasema yule ni mtu ambaye namheshimu halafu unajua mimi ni timu WCB, nawapenda WCB wote ndio maana unaona nimekaa upande wa WCB kwaiyo haya mambo ya mimi kutoka na Naseeb siyo kweli, Naseeb ni mtu tu ambaye namheshimu na nampenda, halafu sina mimba kila siku mimba tu aaha nimechoka sina mimba mimi mbona jamani”.

 

Penzi la Tunda na Diamond Lazidi Kufichuka, Tunda Kuonekana Madale.

Hakuna  penzi la siri hata  siku moja na hata kama mtajitahiid kulificha vipi ipo siku itajulikana hasakama mtaamua kuendlea na penzi hilo.Inawezekana Diamond anashindwa kujifunza kutokana na mambo kadhaa yanayomtokea kwa wanawake anaotembea nao lakini pia wapo mashabiki ambao kutwa kucha wanakuwa macho kwa ajili ya kuangalia nani kafanya nini na kuwa na muda wa ku-prove kama kitu fulani kinatokea au la.

Imepita muda kidogo tangu kuwepo na skendo za hapa na pale kuhusu penzi kati ya Tunda na msanii mkubwa Diamond Platinumz, ambapo inavyosemekana ni kuwa wili hao kwa sasa wana mahusiano ya kimapenzi tena hasa baada ya kuwa wanonekana baadhi ya sehemu pamoja ingawa wanafanya kwa siri.

Lakini pia kumekuwa na vita kali kati ya Tunda na Hamisa, mwanamke ambae amezaa na Diamond mtoto mmoja wa kike, Tunda amekuwa akirusha madongo gizani huku yakilenga kumpata Hamisa ambe pia alishapitia majanga mengi ya kugombana na mzazi mwenzie na Diamond (Zari) kwa sababu hiyo hiyo.

huko mitandaoni mashabiki wameanza kumpa taarifa zari juu ya uwepo wa tunda kila siku madale ambako diamond anaishi na kuna baadhi ya picha zikimuonyesha hata mdogo wake wa kike na mwandada tunda akiwa hukohuko madale ambapo famili hiyo kwa sasa wameweka kambi.

moja ya mashabiki alimwambia zari kuwa kwa sasa tunda anapika na kupakua  madale na zari alimjibu vibaya lakini swala ni kuwa taarifa hizi wanazokuwa wanampa Zari zinakuwa na ukweli ndani yake ingawa mwanamama huyo anaonekana kutojali na baadae yanakuja kutokea kama yaliyokuwa yanatokea kwa Hamisa.

                                                  

Alichojibu zari baada ya kuambiwa habari za Tunda.

 

Diamond na Tunda Wabambwa ‘Live’ (picha)

Mwanamuziki mkali wa Bongo fleva Diamond Platnumz amejikuta tena kwenye skendo ya kuhusishwa kimapenzi mrembo mwingine baada ya Irene ambaye ni Tunda.

Kumekuwa na maneno maneno kwenye mitandao ya kijamii kwa muda mrefu juu ya uhusiano uliopo kati ya Diamond na mrembo Tunda lakini mara kwa mara Tunda amekuwa akikana tuhuma hizo kwa kusisitiza kuwa Diamond ni rafiki tu lakini skendo hizo zimechukua sura mpya hivi karibuni.

Ni miezi michache tu habari zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Tunda alikuwa ana ujauzito wa Diamond ingawa ilionekana dhahiri ni mjazito alikataa na baadae mimba hiyo ilipotea na Tunda kwa mara nyingine tena akakataa tuhuma hizo.

Lakini wikiend hii sakata hili limechukua sura mpya baada ya tuhuma hizi kusindikizwa na picha zilizowaweka pamoja wakati mmoja na sehemu moja. Picha hizo zilimuonesha Tunda ambapo kwenye mtandao wake wa Snapchat aliandika ” Kwaheri mpenzi nitakuona baada ya muda mfupi” na baada ya muda mfupi alipigwa picha akiwa na Diamond.

 

Diamond na Tunda wakiwa sehemu moja baada ya kupigwa picha kwa bahati mbaya na Babu Tale

Baada ya picha hizo kusambaa Mange Kimambi aliibuka na kuandika haya kupitia ukurasa wake wa Instagram kuhusiana na uhusiano wa Diamond na Tunda:

Huyu Tunda na Diamond ni Couple ya siku nyingi, Diamond ana obsession ya huyu mtoto, mwaka Jana alikuwa ana mimba ya Dai baadae akaamua kuitoa lakini safari kamesema kakishika mimba ya Dai nyingine kanazaa”.

Lakini pia kuna picha iliyosambaa mitandaoni iliyomuonyesha Diamond na Tunda wakifanya video call huku wakiwa na tabasamu zimetawala nyusi zao.

 

Diamond Platnumz Amepata Skendo Nyingine Safari Hii na Mrembo Tunda

Model na muuza nyago kwenye video maarufu Kama Tunda the bossbabe amejikuta katika skendo na Msanii maarufu wa kizazi kipya Diamond Platnumz baada ya habari kuenea kuwa amebeba ujauzito wa Diamond.

Waswahili wanasema lisemwalo lipo na kama halipo basi laja. Msemo huu umedhihirika tena kwa msanii pendwa na supastaa anayependwa kuongelewa sana bongo na si mara zote anaongelewa kwaajili ya mziki wake bali mara nyingi ana-make headline kwa maisha yake binafsi ya kimahusiano.

Diamond amerudi tena kwenye skendo na mrembo mwingine anayejulikana kama Tunda anayedaiwa kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi na kinachowavutia wengi ni kuwa inasemekana kuwa Tunda ana ujauzito wa Diamond.

Habari hizi zimeenea kwa kasi ya ajabu kwani Tunda amekuwa akiweka picha za Diamond kwenye ukurasa wake wa Instagram kila kukicha kitendo kinachowafanya watu waamini kuwa Tunda ana uhusiano wa kimapenzi na Diamond.

Baadhi ya picha za Diamond alizoweka Tunda kwenye ukurasa wake wa Instagram ni hizi:

Siku za nyuma tetesi ziliwahi kuenea kuwa Diamond ana uhusiano na Tunda kitendo ambacho kilikanwa mara moja na mti wa karibu Wa Diamond na kudai kuwa ni jitihada za wait kusambaza maneno ya uongo ili waweze kumgombanisha Diamond na mama watoto wake na kipenzi chake Zari, lakini hivi sasa inasemekana kuwa sio tu tetesi kwani baada ya miezi tisa mnaweza mkamuona Diamond akielekea tena kwenye vyombo vya habari kumkubali mtoto.