Mabishoo wamtupia chupa Harmorapa akitumbuiza Maisha Basement

Harmo rappa alinusurika kifo usiku wa Jumapili 02 April 2017, baada ya kupigwa chupa na shabiki mmoja akiwa stejini. Msanii huyo alikuwa na show ya ‘USIKU WA KOMELA’ na kama kawaida mashabiki walijitokoza kwa wingi kumuona star huyu akiwatumbuiza.

 

Harmo rappa atupiwa chupa stejini
Harmo rappa atupiwa chupa stejini (photo credits)

Hata hivyo, Harmo rapper alipopanda jukuani kuperform wimbo wake mpya ‘Kiboko ya mabisho’ alishtukia akirushiwa chupa iliyokuwa na bia na mmoja ya mashabiki aliyekuwa ukumbuni mwa mashabiki wenzake.

Kulingana na ripoti shabiki huyo alitupa chupa hiyo baada ya Harmo rappa kuimba mstari mfupi wa wimbo wake, tulikuwa WASAFI kabla ya WCB, maneno yao machafu hayaniharibii CV…. ulio mkasirisha shabiki huyu mkubwa wa wasafi.

Shabiki aliyemtupia Harmo rappa chupa stejini
Shabiki aliyemtupia Harmo rappa chupa stejini

Hata hivyo chupa hiyo ya bia haikumfikia Harmo rappa kwani alikwepa na kuitoraka. Baada ya tukio hilo, klabu ya Maisha Basement wasiwasi lakini bouncers waliweza kumtoa rappa huyu stejini kabla ya kumtafuta kijana aliyesababisha fujo hizo.

Baada ya muda jamaa huyo alipatikana na bouncers waliomhoji kujua kilichomsababisha kufanya kitu kama hicho. kuwa ameshachakazwa na wananchi wenye hasira kali. Kulingana na alichosema, inaonekana huyo hakuwa shabiki wa Harmo rapper. Hata hivyo alikamtwa na kupelekwa polisi na sasa hivi anangoja kupelekwa kotini.

 

“Wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,” Harmorapa ambia watu wanaomuongela vibaya

Staa na rapa wa Tanzania, Harmorapa hivi majuzi aliweza kufunguka kuhusu watu ambao wanamtusi na kumuongelea vibaya tangu awe maarufu.

Rapper huyo ambaye amekuwa akifanya vizuri Tanzania na Afrika Mashariki kupitia nyimbo zake hivi sasa ndiye anayepata kiki kubwa Bongo na anavyoonekana, Harmorapa atakuwa na umaarufu kama wa Diamond Platnumz iwapo ataendelea kurelease projects ambazo watu watapenda.

Hata hivyo, akizungumza na Bongo 5 rapa huyu alisema kuwa habebwi na kiki na kuwa kazi yake ndiyo inafanya awemaarufu kwa hivyo wanomchukia wanafanya kazi bure na kuwa ataendelea kuachilia nyimbo zake kama kawaida.

“Watu ambao wanahisi Harmorapa hatodumu kwenye game kwanza wanakosea halafu pia naweza nikasema kwamba wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,”

Aliendelea kwa kusema kuwa…

“Kama mimi binafsi nimejipanga sana vya kutosha. Unajua kwamba maneno yao mimi hayanivinjii chochote ni ile sawa na kumpiga chura teke na kumwongezea mwendo. Wanavyoniongea mimi ndo wananipa power na wananipa maujuzi na wananipa kuweza. Ni wao wananiweza mimi kuweza na kukaza ilmradi niweze kufanya kazi nzuri.”

Harmorapa  pia amehaidi mashabiki wake projects kubwa ambazo ataachilia mwaka huu.