Mama Kanumba: Natamani Kwenda Kumuona Lulu Gerezani

Mama mzazi wa aliyekuwa msanii wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba, Mama Kanumba ameibuka na jipya tena huku safari hii anatamani kwenda jela kumuona Lulu.

Mama Kanumba hakuwa na uhusiano mzuri na Lulu kwani mpaka a nafungiwa walikuwa kama wana ugomvi fulani huku Mama Kanumba alidai sababu kubwa ni Lulu kumtupa mama huyo na kutomjali kwa lolote.

Miezi michache iliyopita Muigizaji wa Bongo movie Lulu Michael alifungwa gerezani kwa miaka miwili baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake Steven Kanumba.

Baada ya Lulu kufungwa Mama Kanumba hakusita kuonyesha furaha yake juu ya Lulu kufungwa na baadae alipoulizwa endapo ana mpango wa kwenda kumtembelea Lulu gerezani alisema hajui mpaka afanye mazungumzo na Mungu wake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Mwananchi Communications, Mama Kanumba ameibuka na kusema anatamani kwenda kumuona Lulu jela:

Tangu Lulu kahukumiwa nimekuwa nikipokea lawama na watu kunitusi kuwa mimi ndio sababu, na kusahau ya the kwamba mimi nilishamsamehe kama binadamu na siye niliokuwa mlamlamikaji katika kesi hiyo isipokuwa alishitakiwa na serikali”.

Lakini Mama Kanumba amesisitiza kuwa yote yaliyotokea anamuachia Mwenyezi Mungu kwani yeye kufungwa hakuwezi kumrudishia mtoto wake ambaye amekwisha tangulia mbele ya hali.

Mama Kanumba Afunguka Kulizwa na Wema Sepetu

Mama mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Marehemu Steven Kanumba ‘Florah Mtegoa’, Mama Kanumba amefunguka na kudai kuwa Wema Sepetu amemfanyia kitu mbaya hakutegemea.

Mama Kanumba amedai kuwa hivi karibuni aliwasilisana na Wema Sepetu na kukubaliana wakutane na ndipo Wema alipomuita nyumbani kwake Salasala jijini Dar es salaam lakini amedai alipofika getini hakufunguliwa geti.

Inadaiwa kuwa majirani waliokuwa maeneo hayo walimuona mama huyo akiwa amesimama kwa muda mrefu bila kufunguliwa na wamekiri kuwa ni tabia ya Wema kutofungua geti la nyumbani kwake kama huna appointment yoyote kwake.

Kwenye Interview aliyofanya na gazeti la Ijumaa, Mama Kanumba alifunguka na kukiri kuwa jambo hilo lilitokea ambapo aliongea na Wema hivi karibuni kwa simu ambapo walikubaliana aende nyumbani kwake na ndipo alipokodi bajaji mpaka kwake na alipofika alikuwa akigonga geti walinzi walimwambia hawajapewa maagizo yake na alikuwa akimpigia simu hapokei.

Jamani inauma nyie mtu nimekubaliana naye vizuri unakodi bajaji mpaka kwake kulivyo mbali lakini hajali wala hapokei simu nikaamua kuondoka zangu”.

Mama Kanumba amedai kuwa walikuwa na maongezi ya kawaida tu kwani alikuwa mkwe wake na alikuwa anampenda lakini pia amefunguka na kusema amesikitishwa kwani mpaka hivi sasa hajaombwa radhi na Wema.

Kisa picha ya Mwanae,Mama Kanumba Amwaga Machozi Standi.

Mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba ameshangaza wengi baada ya kuanza kumwaga machozi  katika moja ya stand zinazojaza watu jijini dar anzabaada ya kuona bango lenye picha ya mtoto wake katika maeneo hayo.

Mama huyo ambae alishindwa kuzia hasira zake na kulia alisema kuwa mara nyingi amekuwa akiumia sana na kushindwa kujizuia kutoa machozi kila  anapoona picha au kitu chochote ambacho kinamkumbusha mtoto wake.

kila mara nimekuwa nikiziona picha za kanumba katika mabango , lakini sijui kwanini hii imenifanya nipatwe na uchungu na niishiwe na nguvu kabisa.-Alisema Mama Kanumba ambae anasema kuwa alikuwa akielekea maeneo ya segerea kwa ajili ya kyrekodi movie.

Kanumba alifariki miaka zaidi yamitano iliyopita baada ya kuuawa na mpenzi wake (Lulu Michae) waliokuwa na mtafaruku na kusababisha mauaji yake pindi walipokuwa wakizozana.Hata hivyo Lulu alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani baaada ya kukuta na hatia ya kuua bila kukusudia.

Mama Kanumba Afunguka Kuhusu Picha za Nabii Tito na Mwanae

Mama wa marehemu Steven Kanumba amefunguka baada ya kusambaa kwa picha za Nabii Tito na mwanae maraehemu steven kanumba  miaka ya nyumba kipindi cha uhai wake.Mama huyo amekiri  kuwa mwanae alishawahi kukutana na nanbii huyo lakini nia yake iligonga mwamba.

Mama Kanumba anasema kuwa nabii tito alikutana na Kanumba na kumuomba ajiunge katika kanisa lake alilokuwa amelianzisha kwa niaba ya kuwavutia watu watakaokuwa wanakuja kwa ajili ya kumshangaa Kanumba   lakini kwa upande wake itakuwa faida kwa sababu atakuwa amejaza watu.

Mama Kanumba anasema kuwa marehmu Steven alikataa kata kata kuhusu ombi hilo kutokana na imani yake haukumtaka kufanya hivyo lakini pia Kanumba hakutaka kuhama kanisa analosali hata siku moja.

Kwa upande wa Seth ambae ni mdogo wake na marehemu Kanumba ambae poia kwenye pia hizo amekuwa akionekana amesema kuwa ni kweli Nabii Tito aliwahi kuja ofisini kwa kaka yake zilizopo Sinza-Mori kipindi hicho kaka yake alikuwa hai na kuwashauri wahamie katika kanisa lake lakini walikataa na ndipo alipowaomba wapige nae nae picha.

Tabii tito ni mkazi wa Dodoma alieibuka kama nabii huku akihubiri neno la Mungu kwa kutumia biblia lakini akisapoti unywaji wa pombe kanisani na kuwa kuoa mwanamke zaidi ya mmoja ni swala halali huku alishauri hata kuona wasaidizi wa ndani pia ni sahihi.

Nabii Tito aliendelea kupata umaarufu baada ya kumuomba msanii Wema Sepetu kusali katika kanisa lake na pia aweze kumuoa ilhali yeye mwenyewe akiwa na wake watano na watoto 12, nabii tito alimuona wema aje katika kanisa lake ili aweze kupata idadi kubwa ya wafuasi kwa kuwa watakuwa wanakuja kumshangaa yeye kanisani.

Mpaka sasa Nabii Tito amekamatwa na kufanyiwa vipimo ambapo alikutwa na magonjwa ya akili na kuanza matibabu lakini pia kesi yake ikiendelea mahakamani, kosa kubwa  la Nabii huyo kufanya mahubii ya dini ya kikristo kwa kutumia msalaba na biblia kinyume na taratibu za kanisa.

Mama Kanumba Akanusha Kuwa Na Kinyongo Na Lulu.

Kuna tetesi zimekuwa zikisambaa mtandaoni kuwa kuna chuki kubwa kati ya mma kanumba na msanii Lulu Michael kutokana na matukio ya nyuma yaliyotokea baada ya kifo cha Kanumba ambapo wengi walitegemea kuwa kungekuwa na uhusiano mzuri kati ya mama huyo na msanii Lulu Michael.

Wiki iliyopita mama huyo alifunguka katika vyombo vya habari na kuelezea na kulalamika kuwa Lulu Michael alikuwa akimtukana sana baada ya kutoka jela kwa mara ya kwanza ambapo alikaa kwa takribani mwaka mmoja kipindi upelelezi wa kesi yake ya mauaji ulipokuwa haujakamilika.

mama huyo kwa maelezo yake alionekana  kuwa na chuki na mwanadada huyo na hata kufikia hatua ya kusema kama atataka kwenda jela kumuona Lulu itabidi kwanza aongee na Mungu wake ili aweze kumruhusu kwenda kumuona msanii huyo.

Akiongea katika gazeti la Ijumaa Mama Kanumba anaejulikana kwa jina lake halisi Florah  Mtegoa amesem kuwa tabia ya watu kusambaza maneno na kusema kuwa ana chuki na lulu michael ni uongo kwa sababu yeye hana chuki yoyote na binti huyo na hivi karibuni akipata muda atakwenda kumuona msanii huyo gerezani.

Mama Kanumba anasema kuwa hata kama mahakama isingetaka kumfunga binti huyo bado kwake ingekuwa sawa tu kwa sababu hana lengo lolote la kumuumiza binti huyo na amekuwa akimchukulia kama binti yake.

Sina chuki na Lulu kabisa na tulikuwa karibu nae sana tu,lakini nafikia watu  watu wake wa karibu wanaomzunguka ndio wanaosababisha ukaribu wetu kuparanganyika sana.Lakini moyoni mimi nina mpenda sana Lulu , mimi nina imani ya kikristo kabisa, kwaiyo siwezi kufurahia kuona mwenzangu anapata matatizo , na ipo siku nitamtembelea gerezani.- Aliongea mama huyo.

Lulu alipata hukumu yake ya kuua bila kukusudia mwanzoni mwa mwezi Novemba , ambapo kifungo chake anatakiwa kukitumikia kwa miaka miwili baada kukutwa na hatia ya kumuua Kanumba.

 

Mama Kanumba: Wema Sepetu Ni Mwanamke Wa Kuoa

Mama mzazi wa marehemu Kanumba ambae alikuwa ni msanii mkubwa wa bongo movies  ambae safari yake ilikatika baaada ya kupata umauti baada ya kuuwawa na aliyekuwa mpenzi wake kipindi hicho Elizabeth Lulu Michael mwaka 2012, april 12.

Akizungumza katika Exclusive interview na waandishi wa habari wa kipindi cha Chilawadu kinachorushwa clouds Tv siku ya Ijumaa mama huyo alipata bahati ya kuzungumzia maisha aliyokuwa akiishi mtoto wake huyo kipindi cha uhai wake.

Akijibu swali aliloulizwa kuhusu ni wanawake wangapi Kanumba alishawahi kuwaleta nyumbani na kuwatambulisha mama kanumba alisema kuwa Kanumba alikuwa msiri sana na katika wanawake wote ni Wema Sepetu tu ndie aliewahi kutambulishwa na kuletwa nyumbani kama rafiki ingawa hakusema moja kwa moja kuwa ni mpenzi wake , lakini Wema alikuwa  msichana wa kuoa.

Katika wanawake wote  Kanumba alinitambulisha wema sepetu, na katika wanawake wote  wema alikuwa ni mwanamke anaepaswa kuolewa.Wema ni mwanamke alikuwa akija nyumbani akikuta unapika utaacha atapika yeye kama unaosha vyombo basi ataosha na alikuwa akija kwangu anakuja na madela.

Wema septu akiwa na marehemu Kanumba enzi za uhai wake.

Akiendelea kuongezea Mama Kanumba anasema kuwa hata katika baadhi ya interviews alizowahi kufanya kipindi cha uhai wa marehemu alikuwa akimwambia kila siku ukitaka kuzaa basi unapaswa kuzaa na Wema.Hata hivyo Mama Kanumba anaendelea kusema kuwa katika vitu anavyompendea wema ni kwamba yeye ni msanii wa kwanza siku zote kuongea kila siku  kuwa Kanumba ndio aliyemtoa.

Wema ni mwanamke ambae nilitaka kila siku aweze kuzaa na kanumba, yaani angezaa  na Kanumba ningefurahi sana.Yeye ni binti ambae siwezi kumlinganisha na binti yeyote yule kwa sababu alifundwa na akafundika kabisa achana na haya mambo ya sasa hivi ya kwenye mitandao.

Lakini kitu kingine ninachompendea Wema ni kwamba yuko straight forward sana,ni msanii pekee aliyewahi kukubali kuwa Kanumba ndie aliemuingiza katika sanaa.,

Mama Manumba alisema kuwa pamoja na kuwa wawili hao waligombana lakini hakuwahi kujua kuwa waligombana ingawa alikuwa akiona tu kwenye medias. lakini alitamani sana wema siku zote awe mkwe wake hao wenine yeye alikuwa hawajui kwakuwa kanumba alikuwa msiri sana.

 

Mama Kanumba: Nilikuwa Naumia Nikimuona Lulu Anakula Raha, Nimefurahi Alivyofungwa Sahivi Zamu Ya Familia Yake Kulia

Mzazi wa marehemu Kanumba, Mama Kanumba amefunguka kuhusu furaha aliyokuwa nayo baada ya muuaji wa mtoto wake muigizaji Lulu Michael kuwekwa ndani kwa miaka miwili.

Tangu hukumu ya Lulu mengi yamesemwa huku watu wakigawanyika na misimamo kutofautiana kwani kuna watu wanasema kuwa afadhali Lulu amefungwa na kuna wanaosikitika Lulu kufungwa kwa sababu ni binti mdogo.

Baada ya kifo cha Kanumba, Lulu alikuwa karibu sana na Mama Kanumba lakini baadae ghafla ule ukaribu ukaisha na kusababisha tetesi kuenea kuwa wawili hao wamegombana huku sababu ikiwa haijulikani.

Kwenye mahojiano ambayo Mama Kanumba alifanya na Global TV alifunguka yafuatayo:

Kwa kweli tunashukuru haki imetendeka kwaiyo kama familia ya Lulu wamelia mimi ninalia kila siku wao miaka miwili tu atatoka mimi mtoto wangu sitamuona tena yaani harudi tena, Baada ya hukumu kutolewa tulienda makaburini kufanya misa lakini mimi sherehe yangu nitaenda kuifanya kanisani kwa kutoa shukrani ya pekee. Kwa muda mrefu familia yetu imekuwa ikiumia tukimuona Lulu nakula raha anaenjoy anafurahia iiltuumiza sana kwa muda mrefu ni bora mtu usimuone lakini anaposti anavyokula raha kweli tulikuwa tunahuzunika sana, lakini kesi ilivyoanza tulitegemea kesi haki itatendeka na tunashukuru Mungu ametutendea kwa kweli”.

Mara ya kwanza hukumu ilivyotolewa hakimu wa Lulu, Peter Kibatala aliweka wazi nia yao ya kukata rufaa lakini habari zimeenea kuwa kutokea jela Lulu amekataa kukata rufaa badala yake ameamua kutumikia kifungo chake chote cha miaka miwili.

Baada Ya Hukumu ya Lulu Kutolewa , Mama Kanumba Amwaga Chozi

Ikiwa ni dakika chache tu baada ya hukumu kutolewa leo Novemba 13 juu ya kesi iliyokuwa ikimkabili mwanadada Lulu Michael kuhusu kuua bila kukusudia ambapo msanii huyo amehukumiwa miaka miwili jela kwa kukutwa na hatia hiyo.

Mama wa marehemu Steven Kanumba ambae ndie alikuwa mpenzi wa eElizabeth Lulu Michael ameonekana nje ya mahakanma akilia kwa sauti hukua akisema kuwa anaishujkuru sana mahakama na serikali yake wa ujumla juu ya maamuzi waliotoa kuhusu kesi hiyo,mama huyo huku akilia amesema kuwa akitoka mahakamani hapo ataelekea makaburini alipolazwa Kanumba ili kwenda kumpumzisha kwa amani sasa tangu alipokuwa amezikwa .

mimi sina la kusem kwa sasa hivi ila la kwanza namshukuru mwenyezi mungu sana,pili ninaishukuru mahakama kwa kutenda haki na pia naishukuru sana seriakli yangu na hata nikitoka hapa nitaenda makaburini naamini  sasa naenda kumzika  na akapumzike kwa amani.-aliongea Mama Kanumba huku akilia kwa sauti

Kesi ya Lulu ambayo ilisikilizwa ushahidi wote mwezi uliopita ilikuwa imebaki kusikilizwa hukumu tu ambapo leo ndio ilikuwa mwisho wa kesi hiyo , hata hivyo leo tangu kumekucha kume kuwa na tension kubwa ya watu mbalimbali katika mitandao ya kijamii wakimuombea mwandada huyo kheri katika hukumu yake huku wengne wakiomba hasihukumuiwe kwa chochote,

Hata baada ya kutolewa wa hukumu hiyo watu wengi wameonyeshwa kuumizwa na hukumu iyo akiwepo Wema Sepetu ambao kwake ilikuwa ni habari mbaya tena ya kushtukiza sana.lulu atatumikia kifungio hicho cha kuua bila kukusudua kwa muda wa miaka miwili gerezani.

Lulu alikutwa na kesi hiyo mwaka 2012, ambapo alimuua Kanumba aliyekuwa mpenzi wake bila kukusudia kutokana na ugomvi wa mapenzi waliokuwa nao wawili hao ambapo katika purukushani hizo Kanumba alidondoakana kuanguka chini na ndipo mauti yalipomkuta.Hata hivyo baada ya kusikilizwa kwa ushaihidi kutoka kwa watu wa pande zote mbili  mahakama imeamuru lulu kutumikia kifungo hicho baada ya kuona kuwa katika ushahidi wake mwandada huyo alishindwa kuongea vitu vyote vilivyokuwa vimetokea siku ya tukio.