Pretty Kind- Nimeokoka, Sasa Naimba Nyimbo Za Dini

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind ametangaza rasmi kuachana na Bongo fleva na kugeukia Muziki wa Gospel/ nyimbo za dini.

Pretty Kind amefunguka na kuweka wazi kuwa amefikia uamuzi huo Baada ya kuamua kuachana na mambo ya kidunia na kumrudia Mungu Wake kumaanisha kwamba ameokoka.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Pretty Kind alisema baada ya kumrudia Mungu, ameamua kuachana na muziki wa kidunia na sasa anaandaa nyimbo za Injili ambazo ataziachia hivi karibuni.

Tangu nimeokoka maisha yangu yamekuwa ya furaha mno na nina amani moyoni tofauti na nilivyokuwa naendekeza maisha ya kidunia hivyo ili kudhihirisha furaha aliyonipa Mungu, sasa ninaanza kuimba nyimbo za Injili ili ziwe ushuhuda wa kuwabadili na wengine“.

 

 

Nimekoma Kwenda Kujiuza India-Pretty Kind

Video vixen na msanii wa muziki wa Bongo movie Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind amefunguka na kudai ya kwamba hivi sasa hawezi kurudi tena nchini India kujiuza kama ilivyokuwa siku za nyuma bali anatulia kwa matumaini ya kuolewa.

Siku za nyuma Pretty Kind aliwahi kuweka wazi kuwa aliwahi kuishi nchini India ambapo kutokana na ugumu wa maisha alijikuta anafanya biashara za kujiuza mwili wake  ili kujiingizia kipato.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Pretty Kind alifunguka baada ya kuulizwa sababu ya utulivu wake wa hivi karibuni, huku wengi wakidhani amerejea kwenye biashara ya ukahaba nchini India ndipo aliposema kuwa kamwe hawezi kurudi nchini humo na maisha hayo ameshayasahau.

Unajua watu wakiona umetulia watakusaka kwa lolote, mimi ninakua sasa mambo yote nimeacha ninachotaka sasa ni mchumba wa kunioa hivyo nimejituliza ili nione kama nitafanikiwa kwa hili kwani maisha ya sasa huwezi kupata mume bila kutulia”.

 

 

Pretty Kind Afurahia Kuvunjika Kwa Penzi La Mobetto na Diamond

Video vixen na Msanii wa Bongo fleva Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind ameibuka na kuchekelea kuvunjika kwa mahusiano kati ya staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Hamisa Mobetto.

Wiki chache zilizopita Mobetto aliweka wazi kuwa baada ya miaka kumi ya kuwa pamoja na Diamond na kuzaa mtoto mmoja wameachana rasmi na kila mmoja kuendelea na maisha yake.

Baada ya taarifa hizo za kuachana kwa Mobetto na Diamond Pretty Kind ameibuka na kudai amefurahishwa na Taarifa hizo kwa sababu yaliyotokea ni Mungu kaamua kumuumbua Mobeto kutokana na uchawi aliokuwa anamfanyia Diamond na hilo ni fundisho kwa wasichana wengi wanaoamini uchawi katika mapenzi.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Pretty Kind ametiririkia haya:

Kilichomtokea Mobeto ni fundisho kwa wasichana wengi na wanatakiwa kujua kwamba mapenzi hayalazimishwi na kamwe uchawi hauna nguvu katika mapenzi”.

Lakini pia Pretty Kind asihangaike sana kutangaza kuwa ameachana na Diamond huku akiwa bado anamuhitaji pia ajue kwamba hawezi kuolewa na msanii huyo bali yupo mke wa Diamond atakayeolewa hivi karibuni kwake yeye haiwezi kutokea.

Pretty Kind Adai Ali Kiba Sio Staa

Video vixen na Msanii wa Bongo fleva Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind ameibuka na kudai Msanii maarufu wa Bongo fleva Ali Kiba sio supa staa kama watu wengi wanavyodhani.

Ali Kiba ni moja kati ya wasanii wa Bongo fleva ambaye amekuwa kwenye chati na amekuwa akiwekwa Kwenye listi ya wasanii wanaofanya vizuri kwa sasa.

Lakini Pretty Kind ameibuka na kudai kuwa Ali Kiba hana hadhi au status ya kuwa supa staa kwa kuwa hajafabya baadhi ya mambo ambayo yanaweza kumuweka kuwa Staa.

Pretty Kind amefunguka na kusema hawezi kumuweka Ali Kiba Kwenye kundi la mastaa kwa sababu muziki wake haujulikani nchi za nje zaidi ya hapa nyumbani Tanzania:

Mimi ninachoongea ni ukweli na wala sina timu ya aina yoyote ila  Ali Kiba Isupa staa kwa sababu bado hajaitangaza vizuri nchi yetu muziki wake unaojulikana hapa kwetu tu simchukii ila nasema ukweli”.

 

Pretty Kind na Calisah Wadaiwa Kuwa Kwenye Penzi Zito

Muigizaji wa Bongo movie na msanii wa Bongo fleva Suzan Michael amedaiwa kuwa Kwenye Mahusiano ya kimapenzi na Model maarufu Calisah Abdulhameed.

Calisah ambaye ameshakuwa Kwenye Mahusiano na mastaa kadhaa kama vile Jacqueline Wolper na Wema Sepetu amesemekana kuweka kambi kwa Pretty Kind.

Global Publishers wanaripoti kuwa chanzo ma­kini kilieleza kuwa Pretty Kind amekuwa akioneka­na mara kwa mara maeneo ya Sinza, Dar akiwa na Calisah wakionyeshana mahaba niue hivyo ndiye mtu wake kwa sasa.

Baada ya Tetesi hizo kusambaa hivi karibuni gazeti hilo lilimsaka Pretty Kind ili kujua ukweli wa mambo Lakini mara moja alikataa taarifa hizo na kudai Hazina ukweli wowote.

Siyo kweli tupo karibu na Calisah kwa sababu ya kazi na siku ikimalizika mashabiki wataiona”.

 

Pretty Kind Ahaidi Kumpindua Mobetto Kwa Diamond

Msanii wa Bongo fleva Suzan Michael maarufu kama Pretty Kind amefungukia azma yake ya kumpindua Hamisa Mobetto na kumchukua Diamond.

Pretty Kind amefunguka na kudai ameamua kusema hayo hadharani kwani Diamond amekuwa akimnyima usingizi siku nyingi kwa mapenzi aliyonayo kwake.

Kwenye Interview aliyofanya hivi karibuni na Global Publishers Pretty Kind alifunguka na kusema:

Nitamn’goa tu Diamond kwa Mobetto kwa sababu nampenda sana, ananikosesha usingizi huyu Mobetto asidhani amefika. Kuna wakati niliona ilikuwa ni ngumu kumpata Diamond kwa kuwa Mama yake alikuwa akimpenda sana Mobetto lakini sasa naona njia nyeupe baada ya Mobetto kuchezea kichapo”.

Hivi karibuni imesekana kuwa hali si shwari kati ya Hamisa Mobetto na Mama mzazi wa Diamond Bi. Sandra baada ya kudaiwa alimpa kipigo cha mbwa mwizi baada ya kumkuta nyumbani kwake Madale.

Diamond alirudisha majeshi yake kwa Hamisa mapema mwaka huu baada ya kumwagwa na kama watoto wake Zari.