Msanii wa muziki wa bongo fleva nchini Profesa Jay amefunguka na kutoa dukuduku lake la moyoni baada ya kuona kuwa kuna wimb kubwa la wasanii wamekuwa wakimsumbua katika simu yake wakitaka kupata sapoti kutoka kwake lakini wao wamekuwa hawasapoti muziki wake kabisa.
Profesa Jay anasema kuwa watu hao wamekuwa katika kumsumbua kila inayoitwa leo ili aweze kuwatangazia kazi zao lakini wao wanapoona nyimbo yao wanashidwa kutoa sapoti kama ile anayoitoa yeye katika nyimbo zake, hivyo Profesa Jay anasema kuwa hataki kusumbuliwa tena.
Alindika :ATTENTION PLEASE..hii ni kwawasanii wenzangu ambao kila nikitoa nyimbo wamekuwa wakika kimya wanauchuna, ..hawaoni na wala hawataki kunisapoti lakini wao kila kukicha wapo katika INBOX yangu wakiomba niwapost na kuwafanyia hivyo mara kwa mara, kuanzia sasa hivi msije inbox kwangu maana mnakoelekea mtapata na hilii….