Snura Afungukia Bifu lake na Shilole

Mwanamuziki wa Bongo fleva Snura Mushi Majanga amefunguka kuhusu uwezo wa bifu lake na msanii mwenzake wa Bongo fleva Shilole.

Kwa muda mrefu kumekuwa na habari za kuwepo kwa bifu kati ya Shilole na Snura huku siku za nyuma wasanii hao walionekana wakibishana na hata kurushiana maneno.

Lakini Snura amedai hivi sasa hakuna bifu kati yake na Shilole kwani mambo yaliyotokea siku za nyuma yameachwa huko na hivi sasa wameendeleea mbele

Snura alifunguka hayo Kwenye mahojiano na Bongo 5, ambapo amedai hata tuzo yake aliyopewa na Aunty Ezekiel yeye ndio alimpokelea na akampelekea.

Sina beef hadi juzi kwa Aunt mimi sindonimempokelea zawadi, yeah, hatuna bifu na nimempelekea”.

Snura kwa sasa anatamba na ngoma ‘Vumbi la Mguu’ baada ya kufunika na Zungusha ambayo alimshirikisha Christian Bella.

Nisha- Snura Hawezi Kuninyang’anya Bwana

Muigizaji wa Bongo movie Nisha amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusiana na habari zinazozagaa mtandaoni kuwa msanii wa Bongo fleva na aliyekuwa rafiki yake Snura Mushi amemuibia bwana ake.

Habari za Nisha kunyakuliwa bwana na rafiki yake Snurah zilisambaa wiki iliyopita baada ya Snurah kuweka wazi uhusiano wake na kijana anayeitwa Minu Calypto ambaye mwanzoni alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Nisha lakini baadae alionekana na Snurah.

Baada ya haari hizo kusambaa sana kwa kasi ya 4g Nisha mwenyewe ameamua kufunguka na kusema habari hizo hazina ukweli hata kidogo na kusisitiza kuwa hajachukuliwa bwana na mtu yeyote na hajawahi kugombea bwana na mtu.

Nisha amefunguka na kuiambia Enews ya East Africa TV kuwa habari hizo za yeye kuchukuliwa bwana na Snurah hazina ukweli wowote kwani yeye na mwanaume huyo waliachana miezi sita iliyopita na hata namba ya Simu ya Snurah yeye ndio aliyempatia.

Kwanza mimi sio mtu Wa kusimulia kila kitu ambacho ninacho huyo mkaka nilishaachana miezi sita sahivi Niko kwenye mahusiano mapya na mtu mwingine ambaye anajitambua, Snurah siwezi kumzungumzia sana kwasababu watu wanasema ameninichulia bwana na mimi nasema hajaninyang’anya bwana, kuninyang’anya ingekuwa kama bado Niko kwenye mahusiano na huyo mtu lakini tulishaachana”.

Lakini pia Nisha amesisitiza kuwa yeye na Snurah hawana bifu na pia bado ni marafiki wazuri tu bado wanaongea kwenye Simu kama kawaida na hata alivyomuomba namba ya yule mkaka hakuona soo kumpa kwa sababu walikuwa wameshaachana na yeye ameendelea na maisha mapya kwaiyo hakuna bifu kati yake na Snurah wala na Minu.

Snurah Adaiwa Kunyakua ‘Kiben-10’ Cha Nisha

Muigizaji wa Bongo movie Nisha adaiwa kuwa katika kipindi kigumu kwa sasa baada ya kunyakuliwa mpenzi wake aliyekuwa na umri mdogo kuliko yeye kwa lugha ya mjini ‘kiben-10’ na msanii wa Bongo fleva Snurah Mushi.

Kuanzia wiki iliyopita habari za chino chino zilidai kuwa Snurah kamchukua bwana wa Nisha aliyekuwa naye kwa kipindi kirefu kidogo lakini inadaiwa kijana huyo ni kiben-10 ikimaanisha ana umri mdogo sana kwa wanawake hawa wawili.

Kijana huyo anayeitwa Minu anadaiwa kumwaga Nisha na kuhamisha majeshi yake kwa Snurah jambo ambalo linasemekana kuwa sio mara ya kwanza kutokea kwa Nisha kuibiwa kiben-10 chake kwani mwaka Jana alinyakuliwa tena Barakah the prince aliyekuwa mpenzi wake.

Minu ambaye kwa sasa ana uhusiano wa kimapenzi na Snurah Mushi amekuwa akitawala vichwa vya habari kwa skendo hii hasa kwa sababu hakuweza kujulikana kwa kupitia mziki wake pamoja na kuwa chino ya label ya mwanamuziki Christian Bella.

Pamoja na tuhuma hizo kumuelekea Snurah kama mwizi wa mwanaume wa Nisha, Snurah kupitia ukurasa wa Instagram alifunguka yafuatayo:

Moyo niache nimechoka mbona kuishi mwenyewe inatosha moyo uwapendao sio niache niache hujui kuchagua kule kule nilikoishia kumetosha sitaki Tena”.