Young Dee Na Young Killer Uso Kwa Uso

Baaada ya kurushiana maneneo kwa muda mrefu hatimaye wasanii wawili wa ku-rap Young Dee kutoka Dar Es Salaam na Young Killer kutoka Mwanza wamekutana uso kwa uso na kutoleana maneno ya kashfa huku ukishindwa kupatikna muafaka wa mabishano ya kauli zao.Kipindi cha nyuma kidogo wasanii hawa walikuwa katika marumbano ya kurushiana maneno huku kila mmoja akitaka kushinda kwa maneno yake.

Bifu kati ya wasanii hawa lilianza pale ambapo Dogo Janja alianza kwa kusema kuwa yeye ndio msanii bora na mwenye kujua muziki kuliko wasanii wanaojiita ma-young wote, kauli hii ilimfanya Young Dee kuongea pia kuwa hataki kufananishwa na mtu yeyeto kwa sababu yeye ndio aliyewafunguliwa wasanii wadogo njia katika muziki ,hata hivyo marumbano hayo yaliendelea mpaka kufikia hata ya Dogo Janja kumuita Young dee ni ‘muteja’ na hawezi kubishana na mtu kama yeye.

Kwa jitiahada za kipindi cha Friday Nite Live cha EATV, Sam Misago aliwakutanisha wasanii hawa wawili yaani Young Dee na Young killer ili kuongelea kauli aliyosema Dogo Janja ya kutaka kupewa heshima kama wasanii bora kwa vijana wadogo, Young Killer alisiskika akisema”mimi kauli hii siwezi kuichukulia vibaya kwa sababu, mtazamo wa ukali na mtazamo wa kile tunachokifanya ni mashabiki wetu ndio wanaweza kutuweka katika kategori ya nani mkali na nani sio mkali.By the way siwezi kuupinga huu ndo mtazamo wake, kasema na kaona aseme, as long as hatukani mtu” alisema Young Killler

Ilipokuja kwa upande wa Young Dee yeye alisema kuwa msimamamo wake uko palepale kwamba yeyye hataki kufananisha na mtu yeyote kwa kuwa yeye anautofauti na wasanii wengine wowote,’kweli sipendi kufananishwa, na nitasikitika kama utaendelea kunifananisha, na hakuna anaependa kufananishawa, kwaiyo mimi nimezungumzia hisia zangu , na sipendi kwa sababu kuna vitu ninavifanya ,nimeshawahi kurap kwenye beats za mchiriku ,na kama unataka kunifananisha basi lazima utafute lugha nzuri ya kunifananisha”

Kwa upande wa Young Dee, anasea kuwa yeye ni mtu wa kuulizwa kuhusu miziki ya vijana wengi lakini sio kumfananisha na vijana hao,hata hivyo Young Dee alisema kuwa waandishi wanakosea kuuuliza.Hata hivyo kwa mara nyingi Young Dee aliulizwa tena, kwa maoni yake anaonaje muziki wa Dogo Janja na Young Killer anasea”wasanii hao wanajitahidi kwa nasafi zao, kulingana na muziki wanaofanya”

Young Dee alipokutanishwa na Young Killer kujadili kuhusu nani mkali kati yao.

 

Young Killer amjibu Nay Wa Mtego baada ya kumdiss

Nay Wa Mtego ni msanii ambaye anajulikana kuwachana wasanii wenzake kupitia mziki wake. Hapo mbeleni ameskika akiwachana akina Wema Sepetu, Ommy Dimpoz na wengi kupitia nyimbo zake.

Nay wa Mitego

Hivi karibuni aliachia wimbo mpya ‘moto’ ambapo aliskika akimwambia Young Killer “Young Killer chali, safari ya Mwanza inanukia, usiwadharau waliokufanya ukatoba” kitu ambacho kimemfanya Killer kumjibu Nay.

Kupitia mtandao wa Instagram Young Killer aliandika, “Nasikia kuna mtu kanidiss” kuonyesha kuwa alikuwa ameupokea ujumbe wa Nay. Hata hivyo jambo hili halikumshtua rapper huyu kwani alimjibu Young Killer kwa kuandika ” #Ney True Boya,” kupitia mtandao wake wa Instagram.

Hata hivyo, hakuna anayejua kinachoendelea kati ya wawili hawa.

 

“Namtambua Young killer toka zamani” Lava Lava

Mkali mpya wa Wasafi Records Lava Lava amedai kuwa anamtambua Young Killer toka zamani wakati alikuwa aki hustle na THT.

Lava Lava ambaye kwa sasa amepata maarufu tangu kuachia wimbo wake mpya ‘bora Tuachane’ alifunguka kwa kusema kuwa wakati bado alikuwa anatafuta njia ya kuingia kwenye Bongo Industry aliweza kukatana na young killer ambaye kwa hivi sasa hamkumbuki kwa kuwa wakati huo hakuwa maarufu.

Akizungumza na Bongo 5, Lava Lava alisema,

“Msodoki mimi namkubali sana lakini pia ni mtu ambaye nilikuwa nakutana naye. Young Killer hanijui mimi lakini leo namwambia, kipindi nahustle THT alikuwa kwenye Super Nyota walikuwa wanakuja sana THT kuweka kambi hadi tukafanya tangazo fulani wote, lakini hakumbuki, yeye akaweka sauti yake mimi nikaweka yangu. Kwa hiyo mimi namjua kwanzia kule chini kabisa lakini yeye katika kutokumbuka kwake tukikutana tunaheshimiana.”