Young Dee Na Young Killer Uso Kwa Uso

Baaada ya kurushiana maneneo kwa muda mrefu hatimaye wasanii wawili wa ku-rap Young Dee kutoka Dar Es Salaam na Young Killer kutoka Mwanza wamekutana uso kwa uso na kutoleana maneno ya kashfa huku ukishindwa kupatikna muafaka wa mabishano ya kauli zao.Kipindi cha nyuma kidogo wasanii hawa walikuwa katika marumbano ya kurushiana maneno huku kila mmoja akitaka kushinda kwa maneno yake.

Bifu kati ya wasanii hawa lilianza pale ambapo Dogo Janja alianza kwa kusema kuwa yeye ndio msanii bora na mwenye kujua muziki kuliko wasanii wanaojiita ma-young wote, kauli hii ilimfanya Young Dee kuongea pia kuwa hataki kufananishwa na mtu yeyeto kwa sababu yeye ndio aliyewafunguliwa wasanii wadogo njia katika muziki ,hata hivyo marumbano hayo yaliendelea mpaka kufikia hata ya Dogo Janja kumuita Young dee ni ‘muteja’ na hawezi kubishana na mtu kama yeye.

Kwa jitiahada za kipindi cha Friday Nite Live cha EATV, Sam Misago aliwakutanisha wasanii hawa wawili yaani Young Dee na Young killer ili kuongelea kauli aliyosema Dogo Janja ya kutaka kupewa heshima kama wasanii bora kwa vijana wadogo, Young Killer alisiskika akisema”mimi kauli hii siwezi kuichukulia vibaya kwa sababu, mtazamo wa ukali na mtazamo wa kile tunachokifanya ni mashabiki wetu ndio wanaweza kutuweka katika kategori ya nani mkali na nani sio mkali.By the way siwezi kuupinga huu ndo mtazamo wake, kasema na kaona aseme, as long as hatukani mtu” alisema Young Killler

Ilipokuja kwa upande wa Young Dee yeye alisema kuwa msimamamo wake uko palepale kwamba yeyye hataki kufananisha na mtu yeyote kwa kuwa yeye anautofauti na wasanii wengine wowote,’kweli sipendi kufananishwa, na nitasikitika kama utaendelea kunifananisha, na hakuna anaependa kufananishawa, kwaiyo mimi nimezungumzia hisia zangu , na sipendi kwa sababu kuna vitu ninavifanya ,nimeshawahi kurap kwenye beats za mchiriku ,na kama unataka kunifananisha basi lazima utafute lugha nzuri ya kunifananisha”

Kwa upande wa Young Dee, anasea kuwa yeye ni mtu wa kuulizwa kuhusu miziki ya vijana wengi lakini sio kumfananisha na vijana hao,hata hivyo Young Dee alisema kuwa waandishi wanakosea kuuuliza.Hata hivyo kwa mara nyingi Young Dee aliulizwa tena, kwa maoni yake anaonaje muziki wa Dogo Janja na Young Killer anasea”wasanii hao wanajitahidi kwa nasafi zao, kulingana na muziki wanaofanya”

Young Dee alipokutanishwa na Young Killer kujadili kuhusu nani mkali kati yao.

 

Hii ndio sababu mama mzazi wa Young D ajitolea kumlea mjukuu wake

Kuna fununu kuwa aliyekuwa mpenzi na mama ya mtoto wa Young D ameamua kumuacha mtoto wao wa miezi 7 na mama mzazi wa Young D.

Mamisar anasemekana kuwa amemuacha Tamar na mamake Young D baada ya kuondoka ilikujishighulisha na maisha yake. Akizungumza kwenye interview….Mamisar alikiri kuwa maneno haya ni ya Kweli na hata hivyo, mrembo huyu alisema kuwa kwa sasa amerudi kazini na ndio maana aliamua kufanya hivi.

Akizungumza kwenye interview, Mamisar alisema…

Mapenzi hakuna tena kati yangu na Young D, ndiyo maana familia yake iliamua kumchukua Tamar ili kumlea kwani nisingeweza kumlea kwa sababu ninafanya kazi. Nikitaka kwenda kumuona ninakwenda kama kawaida na hata nikitaka kulala huko wiki moja, ninalala.

Ni kweli Video vixen Tunda anamtarajia mtoto wake wa kwanza?

Ingawa tetesi zinazosambaa mitandaoni Ni kweli, basi Tunda anamtarajia mtoto na alikuwa mpenzi wake wa zamani, Young Dee.

Hapo awali mrembo huyu alikuwa amekanusha taarifa kuwa alikuwa mjamzito. Hata hivyo hivi karibuni aliweka picha ya Utrasound akionyesha mtoto mdogo anayeendelea kuwa kumaanisha kuwa anatarajia kupata mtoto.

Hata hivyo, hakuandika ujumbe unaodhibitosha kuwa anamtarajia mtoto lakini mashabiki wake waliacha ujumbe wa kumpa pombe mrembo huyu pamoja na Younge Dee.

Tazama picha hiyo hapa;

Young Dee afunguka kuhusu uhusiano wake na mama ya mtoto wao

Young Dee ambaye anatambulika na warembo wengi amefunguka kwa mara ya kwanza kuzungumzia uhusiano wake na mamisa ambaye ni mama wa mtoto wao.

Kama inavyojulikana…Young Dee alikana kutoka kimapenzi na mrembo huyu huku akisisitiza kuwa hawakuwa wamepanga kupata mtoto Paloma. Aliendelea kwa kudai kuwa kwa sasa yuko single na uhusiano wake na mamisa umebaki kama ilivyokuwa hapo mbeleni:

 

“Am single and am buys, sina mahusiano, ni kitu ambacho naweza kusema kibinadamu kinatokea kama baraka tu kwa sababu hakuwahi kuwa mpenzi wangu, imebaki kama ilivyokuwa mwanzoni.”

Hata hivyo pia alizungumzia mziki wake mpya kwa kusema,

“Kikubwa imedhihirisha kuwa watu bado wanapenda muziki mzuri, watu bado wanapenda muziki wa hip hop. Kwangu mimi ni kitu ambacho kimenipa faraja na nguvu ya kuendelea kufanya kazi nzuri.”

Young Dee akana kutumia madawa ya kulevya

Msanii wa Bongo Young Dee anasemekana kuwa ameyarudia matumizi ya madawa ya kulevya baada ya MDB Kudai kuwa hii ndio sababu waliacha kufanya kazi naye.

Hata hivyo Young Dee amedai kuwa yeye hajarudia kutumia dawa za kulevya. Aliendelea kwa kusema kuwa yeye hajawai kuwa muathiriwa wa dawa za kelevya na kwa sasa anajijenga mwenyewe ilikuisaidia family yake.

Akizungumza kwenye interview na Bongo 5 young Dee alisema…

Aliyekuwa meneja wa Young Dee adai kuwa msanii huyu amerudia kutumia madawa ya kulevya

Young Dee amejipata matatani baada ya Max Rioba aliyekuwa meneja wake kupitia label ya MDB kusema kuwa msanii huyu amerudia madawa ya kulevya na kuwa hana bidii kwenye kazi yake tena.

Max alifunguka kusema haya baada ya Young Dee kudai kuwa alimtoroka meneja huyu baada ya kujua kuwa alitoka na mrembo wake, Tunda. Hata hivyo Max amedai kuwa msanii huyu wa bongo amepoteza muelekeo wake kama anaweza kusingizia kuwa alitoka na Tunda ilhali anajua kilichofanya wawili hawa kuacha kufanya kazi pamoja.

Young Dee na aliyekuwa meneja wake, Max

Akizungumza kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Maz alisema,

“Mimi sikuwahi kumfukuza huyo mtoto kwaajili ya Tunda. “Nimemfukuza sababu ya matumizi yake ya dawa za kulevya na utovu ya nidhamu na ujinga ujinga wake. Kwani mara ngapi Tunda amekuwa na Dee tukiwa naye hapa, yeye Dee kasema ni moja kati ya sababu za kuondoka hapa, sio kweli sina chochote na huyo mtoto,”

Max aliendelea kwa kusema,

“Nachojua ni kwamba ana wakati mgumu sana kwenye game, industry imebadilika, kuna watoto wamekuja wanafanya vizuri, ndio maana anaendelea kusema Dimaond hawezi kushuka kwa sababu anajijua anachofanya, Dee hana heshima na nidhamu kwenye kazi hana.”