Faiza Ally Adai Sugu Bado Ana Mapenzi na Yeye

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali maarufu Faiza Ally amefunguka na kudai mzazi mwenzake Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ bado anampenda.

Faiza amefunguka hayo baada ya sakata lao la juzi ambapo Faiza alimtolea povu Sugu Kwenye mitandao ya kijamii na kumtaka amuheshimu baada ya Sugu kumtuma Mke wake kufanya shopping ya Faiza badala ya kumpa pesa.

Faiza amemwaga povu hilo Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers kwenye ‘sherehe ya 40’ ya Zamaradi Mketema na kufunguka mengi ikiwemo utayari wa kurudiana na Sugu iwapo atarudi walee mtoto wao.

Nadhani Sugu bado ananipenda ndiyo maana hatimizi vizuri wajibu wake wa malezi na matumizi kwa mtoto wake Sasha. Huenda anafurahi mimi ninavyokuwa ninamsema na mimi siwezi kuchoka kumsema mpaka pale atakapoweza kutimiza majukumu yake ipasavyo.

Kama huhitaji kuwa na ishu na mtu basi unaweza kufanya mambo kwenye right way (njia sahihi), lakini ukiona mtu anakutafutia vitu vya kukuumiza ujue bado uko kwenye moyo wake, aweke pesa ya matumizi ya mtoto kwenye akaunti kila mwezi, atimize majukumu yake then ataona kama mimi nitaendelea kumfutalia”.

Faiza na Sugu wamekuwa kwenye mgogoro wa muda mrefu wa kifamilia hasa kuhusu suala la malezi ya mtoto wao Sasha.

 

“Sina Sababu ya Kusema Namuhurumia Kapata Matatizo Shauri Zake”. Amefunguka Faiza Baada ya Sugu Kufungwa

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Faiza Ally ambaye amejipatia umaarufu zaidi kutokana na kuwa mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.

Uhusiano wa Sugu na Faiza sio mzuri siku zote kwani ni mara nyingi wamekuwa watu wa kurushiana maneno Kwenye mitandao ya kijamii huku Faiza akimtuhumu Sugu kwa kukataa kumlea mtoto wao na kupelekea vita kali kati yao.

Siku ya Jumatatu Sugu alihukumiwa kifungo cha miezi mitano Jela baada ya kukutwa na hatia na mahakama ya hakimu mkazi Mbeya ambapo Sugu alihukumiwa kwa kudaiwa kutoa maneno ya uchochezi na lugha ya fedheha dhidi ya raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. J.P Magufuli.

Baada ya hukumu hiyo hatimaye mzazi mwenza wa Sugu, Faiza amefunguka kuhusiana na hukumu hiyo na kusema amechukizwa na kitendo hicho kilichofanyika maana hakikuwa cha haki kabisa.

Faiza amesema hayo kwenye mahojiano aliyofanya na Radio 5 ambapo amedai kitendo hicho kimemuuma kama mzazi mwenzake ingawaje maisha yake yanakuwaga magumu zaidi Sugu akiwa uraiani.

Nikimuangalia kwenye maisha yangu namuona kama adui ambaye hana neno kwangu, kwaiyo mimi sina sababu ya kusema sijui namuhurumia sijui kapata matatizo shauri zake, Hayo matatizo kwa kweli naona akiwa uraiani maisha yangu yanakuwa magumu sana, sijali japo siombi akae jela hivyo lakini saa nyingine naona inabidi aah sijali kwa kweli”.

 

Faiza Ally na Mke wa Mbunge Sugu Kwenye Bifu Kali

Faiza Ally ambaye ni muigizaji wa Bongo movie na mama watoto wa Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amezidi kutibuana na mpenzi wa Sugu anayejulikana kama Happiness Msonga.

Faiza ambaye hajawahi kuficha hisia zake kuwa bado anampenda Sugu licha ya wawili hao kuachana, Sugu ameweka wazi uhusiano wake na mpenzi wake happiness ambaye amekuwa kimya kwa muda mrefu akivumilia maneno yote ya kejeli kutoka kwa Faiza.

Kupitia ukurasa wake wa instagram Faiza alimrushia maneno na kudai kuwa Happiness anamtumia watu wamtukane kwenye mitandao ya kijamii na anafungukua kurasa feki ili kumtukana Faiza na pia amedai kuwa Sugu hawezi kumuoa Happiness kwa sababu ameshaolewa ndoa ya kanisani na mwanaume mwingine anayejulikana kama Minja.

Unafungua account feki unanitukana si unitukane kwenye account yako tupambane sasa kwani uongo? We sio mke wa mtu? Kwa umaarufu gani uwe na fan page zaidi ya sita Na zingine special kwa ajili ya kunitusi? Unajifanya innocent mbele za watu kumbe joka jeusi Mungu anakuona na usaliti kwenye ndoa …pole kaka ninja muwe mnaangaliaga Zaidi mavazi ya kuna vigezo vingi kabla ya kuoa Sio muonekano”.

Pia Faiza hakuishia hapo aliwajia juu mashabiki wote wa Happiness na Sugu waliokuwa wanadai kuwa Happiness ndio wife material yaani ndo mke wa kuoa siyo yeye.

Acha nijibu miye siwezi kunyamaza nisije nikaumwa presha …huyo happy mnaomsifia ni wife material kwa umaterial gani? Au kwasababu Ana ndoa ya kanisani na kamkimbia mumewe kwaajili ya mbunge? au hamjui kwa mini ndoa haifingwi?  na huyo mbunge atafanyeje naye anapenda mteremko wanawake wazuri wanataka matunzo? wamekutana woye mabandidu bora hata baba Sasha ana mvuto kidogo ila huyo mwanamke hamna kitu”.

Pia Faiza alisisitiza kuwa kati yake na Happy yeye ndio mrembo na Happy ni mbaya, sababu ya ugomvi wao Faiza anamzuia mtoto wa Sugu kumuona baba yake.