Harmonize afafanua script ya video yake mpya kwa mashabiki wasioilewa

Imebidi Harmonize kuwaeleza mashabiki wake uhusiano wa video yake mpya na wimbo wake niambie unaowachanganya wengi. Muimbaji huyu wa Wasafi records amekuwa akiona malalamishi ya mashabiki wake wanoaamini kuwa alikuwa off script kwenye video yake mpya.

Harmonize akiwa na Wolper
Harmonize akiwa na Wolper

Kulingana na lyrics zake za Niambie, Harmonize anaonekana kuwa mtu ambaye hana pesa wala kwake ilhali video ya wimbo huo anaonekana akiishi kwa nyumba ya kifahari na maisha yake kuwa ni ya tajiri kitu ambacho hakiambatani na anachoimba.

Hata hivyo Harmonize alichukua fursa ya kuwafafanulia mashabiki wake alipokuwa kuwa kwenye interview na Prince Ramalove kupitia Kings Fm. Harmonize alielezea maana ya script ya hiyo video kwa kusema…

“Sina mtonyo lakini naishi kwake,sasa nikiishi kwake na yeye ana hela,ntafanyaje?”

Kwa ufupi muuimbaji huyo alikuwa akimanisha kuwa nyumba na magari zinazooonekana kwenye vdeo ni mali za Wolper kwa mujibu wa script.

New Video: Harmonize aachia video yake mpya aliyomshirikisha mpenzi wake kama video vixen

Msanii wa Tanzania Harmonize ameachia mpya video ya wimbo wake mpya Niambie aliofanya miezi 6 baada ya Matatizo.

Harmonize ambaye anafanya kazi chini ya uongozi wa Wasafi records amefurahisha washabiki kwa wimbo huu uonawagusa kidani maana ameimba kuhusus mapenzi, kitu ambacho mashabiki wa bongo hupenda.

Katika video yake, Harmonize alimshirikisha mpenzi wake wa dhati, Jacqueline Wolper. Kwa kufanya hivi, mashabiki wengi wameachwa wakifikiria kuwa mapenzi yake na Wolper ni ya kiki.

Hata hivyo, alifutilia maneno haya mbali alipokiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatano hii, kuwa kuna wakati alipogombana na mpenzi wake lakini sasa wamesuluhisha kila kitu.

“Kuna vitu vilitokea tukajikuta hatuko sawa, lakini Mungu ndio mwenye kheri tukawa tupo pamoja tukajua kabisa kuwa hiki kitu Jack hakipendi au mimi. Sasa hivi kila kitu kinaenda sawa na mapenzi yetu sio ya kiki, nafasi yetu kwenye jamii imefanya ionekane kuwa ni kiki,”

Hata hivyo, tazama video yake mpya hapa.