Juma Nature akana kumlipisha Harmorapa kufanya kolabo naye

Wiki chache zilizopita, rapper mpya kwenye sanaa ya muziki Harmorapa alilalamika kuhusu wasanii wakongwe kuwalipisha wasanii wapya wanapotoa kolabo nao.

“Haipo sawa kwa wasanii wakubwa kutudai sisi ‘underground’ pesa ya kufanyia collabo wakati wanajua bado hata hatuanza kufaidika na muziki wenyewe,” Harmorapa alisema.

Juma Nature, aliyetoa kolabo na Harmorapa, alikana kuwa alimlipisha Harmorapa kufanya kolabo naye. Akiongea na kipindi cha E News cha EATV, Juma Nature alisema Harmorapa hana pesa ya kumlipa.

“Nikisema nimemlipisha Harmorapa pesa kwa ajili ya kolabo nitakuwa nakosea. Mimi ni mtu mzima nilikubali kufanya wimbo na msanii yule kwa sababu ni mkali na anajua muziki pia na imani atafika mbali. Hawezi kunilipa mimi, ana hela gani?,” Juma Nature aliambia EATV.

Harmorapa

 

Juma Nature afunguka baada ya Harmorapa kudai kuwa alikuwa anamdai baada ya collabo yao

Imemchukua Juma Nature wakati kuzungumza kuhusu maneno ambayo Harmorapa aliyosema hivi karibuni akiwa kwenye interview na kipindi cha E News cha EATV. Kulingana na ripoti zinazoenea kwenye mitandao jamii Harmorapa anadai kuwa Juma Nature anamdai pesa ya mavazi aliyovaa kwenye wimbo wake mpya ‘Kiboko Ya Mabishoo’.

Harmorapa
Harmorapa

Harmorapa alisikika akisema,

“Haipo sawa kwa wasanii wakubwa kutudai sisi ‘underground’ pesa ya kufanyia collabo wakati wanajua bado hata hatuanza kufaidika na muziki wenyewe.”

Akizungumza kwenye Kipindi cha E news Juma nature pia alikanusha madai haya akisema kuwa Harmorapa hana pesa za kumlipa ata angekuwa anamdai rapa huyo hawezi kumlipa.

“Nikisema nimemlipisha Harmorapa pesa kwa ajili ya kolabo nitakuwa nakosea. Mimi ni mtu mzima nilikubali kufanya wimbo na msanii yule kwa sababu ni mkali na anajua muziki pia na imani atafika mbali. Hawezi kunilipa mimi, ana hela gani?

Harmorapa awataja mastaa ambao waliompa jina analolitumia sasa

Rapper wa Tanzania, Harmorapa, kwa sasa hivi ni mmoja wa watu maarufu Afrika Mashariki. hii ni kwa sababu ya jina lake na pia nyimbo anazoziachilia.

Kabla ya kuwa staa mkubwa rapper huyo hakuwa anatumia jina hilo lakini baada ya kujitokeza na alikutana na mastaa kadhaa waliomshauri kutumia jina analotumia sasa.

Akizungumza katika show ya Bongo Dot Home cha Times FM, Harmorapper alisema kuwa Roma na Mr T-Touch ni watu ambao walimsihi kutumia jiona la Harmorapa na pia kwa sababu anafanana na mwimbaji wa Wasafi records, Harmonize

“Baadhi ya mastaa wakubwa katika muziki wa hapa Bongo nao walinishauri nijiite hivi, akiwemo brother Roma Mkatoliki na Mt T-Touch,”

Hapo mbeleni rapper huyu wa Tanzania alikuwa akifahamika kama Jembe la Kusini, jina ambalo ata mimi kama shabiki wake naona halingeweza kumake kwa hii industry.