Fahamu Mzee wa Likwidi Alivyorejesha Furaha ya Ommy Dimpoz

Mwanamuziki Ommy Dimpoz amefunguka na kusema kuwa kipindi chote ambacho alikuwa akumwa na yuko hospitali alikuwa akifarijika sana kila alipokuwa akimwangalia msanii mzee wa likwidi kwa vituko vyake.

Ommy anasema kuwa mara nyingi alikuwa akicheka sana mpaka baadhi ya watu walikuwa wakismhangaa hasa madaktari wake kutokana na furaha aliyokuwa akiipata akimuona msanii huyo jinsa anavyofanya vituko.

Anasema “Yuko jamaa anaitwa piere likwidi, yaani kila nilipokuwa namtazama nilikuwa nacheka sana, hasa ile style yake ya kuongea…haiiiiii…mamaaa…. nakufaaa…mpaka madaktari kule ujerumainwalikuwa wakiniuliza nawajibu tu nkuwa haya ni mambo ya tanzania hamuwezi kuyajua.

“Gombaneni, roganeni mpaka muuane” Huu ndio ujumbe Nay aliowaandikia Ommy Dimpoz, King Kiba na Diamond Platnumz

Rapa wa bongo Nay wa Mitego hatimaye ameingilia vita mpya ya Ommy Dimpoz, Diamond Platnumz na King Kiba kwa kutoa maoni yake.

Kupitia mtandao wa Instagram Nay alifunguka kwa kusema kuwa hakuna anayemuunga mkono lakini jambo linalomkasirisha ni kuwahusisha wazazi kwenye vita hivi vyao vya utoto. Aliandika kusema;

Gombaneni, roganeni mpaka muuane, napenda kusikia changamoto kwenye gemu, ila tusiwaingize wazazi wetu tafadhali, tukananeni matusi yote wenyewe kwa wenyewe ikibidi piganeni kabisa atakaye kufa tutazika na itakuwa historia kama Big na Pac.

Akaendelea kwa kuongeza kuwa;

“Ila kuwaingiza wazazi ni ujinga, sipo upande wowote si kwa Kiba, Dimpoz wala Diamond, endeleeni na vita yenu kama wanawake mmechukuliana mabwana, ila suala la wazazi mnavuka mipaka,”

Ommy Dimpoz amuandikia Barua mamake Diamond Platnumz

Wengi wanapodhania kuwa Ommy Dimpoz ameamua kukaa kimwa – basi msanii huyu wa bongo hivi leo amewaacha wengi wameshtuka baada ya kumuandikia bi Sandra barua kupitia mtandao wa Instagram.

Ommy aliweka picha yake na ya mama Diamond hukua kiandika;

BARUA YA WAZI KWA BINTI YANGU MALKIA WA NGUVU

Salam zako nimezipata mwanagu hivi kweli ww wa kukosa adabu kuamua kunichamba baba yako? Sasa Kosa langu mimi nini????kwani kuna ubaya kumtandikia kitanda Baby wako king?
#unanioneakwakuasijuikurap?
#sijuiNamiminimkatae
#kamayeyealivyokataawaMobeto
#Yaniunamkataamjukuuwangu
#unakubalikuleawatotowa5siowako
#umerogwawwsioburemwanangu
#NilikuwanajuanimezaaSIMBA
#kumbenimezaaKIMBA
#DavidonaeanalalamikuhusuENEKA
#UmeletaJanjaJanjakwenyefallonu
#utakujakuniuakwapreshajomonii
#Nnaedhalilikamimibabayako
#hayanendakatungevesinyingine
#Rahayavitausichanguesilaha
#BABAMALKIA

Tazama post yake hapa;

Ommy Dimpoz aeleza sababu zake za kukaa kimya kwa muda mrefu

Mkali wa nyimbo za bongo Ommy Dimpoz amekaa miezi kadhaa bila kuachilia project mpya. Japo anasemekana kuwa amepotezwa na vijana wadogo ambao wamekuwa wakionekana wamevalia sare zake na viatu muimbaji huyu ametoa stori nyingine.

Akizungumza katika interview Ommy Dimpoz alifunguka kwa kusema kuwa anauchukua muda wake kutengeneza kitu ambacho akiachilia mashabiki wake watafurahia.

Ommy Dimpoz

Aliendelea kwa kuongeza kuwa hajapotezwa na mtu yeyote kama watu wanavyosema. Alihaidi kuwa hivi karibuni ataachilia nyimbo mpya miezi kadhaa baada ya kufanya kazi na Alikiba.

“Siyo kweli kuwa nimepotea, kwanza najiandaa kuachia kazi mpya ambayo ina ubora wa hali ya juu, wanaosema nimepotea wasubiri waone maajabu yangu,”

Hata hivyo, Ommy Dimpoz ameonekana kunyamaza wakati ambao wasanii wa bongo wanapepea na nyimbo mpya.