Baada ya Seduce me ya Alikiba kufikisha 2M YouTube, Christina Shusho amuandikia King Kiba ujumbe huu

King Kiba anaonekana kuwa yeye ndiye Mfalme Wa Nyimbo za bongo na hii ni baada ya msanii huyo kuachia wimbo wake mpya Seduce me ambao umefikisha milioni 2 siku tatu baada ya kuiwachia.

Mashabiki wake pia wameonekana kupenda wimbo huu ikiwemo Wema Sepetu na wengine Kama muimbaji wa nyimbo za injili, Christina Shusho. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Christina alionyesha mapemzi yake kwa wimbo huu wa King Kiba kwa kuandika;

“Leo unaweza kukuta mtu kaitwa kanisani aongoze wimbo wa sifa halafu akalianzisha Seduce Me, Eeh jamani Kiba we noma, wimbo ni mzuri sana kitaaluma kama anavyopenda kusema bosi Ruge. Hauna picha za aibu , naweza kuuangalia nikiwa na familia, labda sijui maana ya Seduce Me. Timu Kigoma Wamanyema oyeeeee. Cha mwisho Ali Kiba basi siku nyingine tutembelee kanisani ukiwa mfalme huchagui dini wote wako”

Hata hivyo kwa sasa ameweka rekodi mpya ya kuwa msanii wa kwanza Afrika Mashariki kufikisha 2 Million view YouTube na siku tatu.

King Kiba atisha baada ya kuweka rekodi mpya YouTube

Alikiba ama ukipenda King Kiba ameweka rekodi mpya Afrika Mashariki kama msanii ambaye video yake imepata kutazamwa na watu milioni masaa 38 baada ya kuiwachia.

Seduce me imeweka rekodi ya kipekee ambayo hata wakalik ama Diamond Platnumz na Vanessa Mdee bado hawajaweza kufikisha. Kupitia ukurasa wake wa instagram, King Kiba aliweka post akiwashukuru mashabiki wake kwa kufanikisha kuvunja rekodi hiyo. Aliandika;

“Ahsanteni sana kwa upendo, nisingebarikiwa zaidi na kupendelewa bila nyinyi, nyinyi ni wa maana sana kwangu na nafanya haya kwa ajili yenu”,

kampuni ya Rockstar ambayo inamsimamia Kiba pia iliandika ujumbe kusema kuwa wimbo huu umevunja rekodi ya kipekee na ni video zinazotrend Tanzania na Kenya.

“Historia ya kunjwa rekodi imewekwa, Mfalme Kiba na wimbo wake mpya wa ‘Seduce me‘ umekuwa wa kwanza na kipee kwa msanii wa Afrika Mashariki kufikia kutazamwa mara milioni 1 kwenye Vevo/YouTube ndani ya masaa 38 tu, ina ‘trend’namba 1 Tanzania na namba 1 Kenya kwa ‘weekend’ nzima, rekodi imevunjwa.”

“Gombaneni, roganeni mpaka muuane” Huu ndio ujumbe Nay aliowaandikia Ommy Dimpoz, King Kiba na Diamond Platnumz

Rapa wa bongo Nay wa Mitego hatimaye ameingilia vita mpya ya Ommy Dimpoz, Diamond Platnumz na King Kiba kwa kutoa maoni yake.

Kupitia mtandao wa Instagram Nay alifunguka kwa kusema kuwa hakuna anayemuunga mkono lakini jambo linalomkasirisha ni kuwahusisha wazazi kwenye vita hivi vyao vya utoto. Aliandika kusema;

Gombaneni, roganeni mpaka muuane, napenda kusikia changamoto kwenye gemu, ila tusiwaingize wazazi wetu tafadhali, tukananeni matusi yote wenyewe kwa wenyewe ikibidi piganeni kabisa atakaye kufa tutazika na itakuwa historia kama Big na Pac.

Akaendelea kwa kuongeza kuwa;

“Ila kuwaingiza wazazi ni ujinga, sipo upande wowote si kwa Kiba, Dimpoz wala Diamond, endeleeni na vita yenu kama wanawake mmechukuliana mabwana, ila suala la wazazi mnavuka mipaka,”

Baada ya Diamond Platnumz kuzindua perfume yake, King Kiba kuingiza bidhaa moto moto sokoni

Japo King Kiba amekuwa kimya kwa muda sasa msanii huyo amefunguka na kusema kuwa sasa hivi anajiandaa kuachia bidhaa kadhaa kutoka kwa AK na sasa King Kiba.

Ali Kiba

Kwa sasa muimbaji huyo wa Aje ameachia shati na kofia ambazo zimekuwa zikiuzwa Afrika Mashariki. Lakini kwa sasa anatarajia kuachia viatu, glasses na energy drink. Alisema haya kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

“AK ni brand ya Alikiba nashukuru imekuwa kubwa watu wanavaa lakini pia ipo na ya King Kiba nayo ni brand yangu na zipo official kabisa na kazi zitakapoanza watapata product zote.”

Aliongeza kwa kusema kuwa anamalengo makubwa na ndio maana bidhaa zake zinachukua muda kuachiliwa sokoni.

“Kuna malengo makubwa sana tumeyaweka lakini siwezi kusema sasa hivi ila kuna jeans, viatu na glasses tayari zishatoka soon wataziona maana hizi zitakuwa za kwanza sababu tayari zishatoka na kuna energy drink”

Mashabiki wa King Kiba wamtolea Barakah the Prince hasira baada ya kumpost Chibu

Ingawa Baraka the Prince alifanya wimbo na King Kiba Nisamehe haamanishi kuwa hawezi msupport Diamond Platnumz. Hata hivyo hivi sivyo mashabiki wa Kiba wanavyofikiria. Hivi Karibuni muimbaji huyu wa Bongo, Baraka the Prince aliupost wimbo mpya wa Diamond Platnumz na kilichofuatia ni matusi kutoka team Kiba.

Soma: Baada ya kufanya collabo na King Kiba, Barakah The Prince aeleza changamoto alizopitia

Barakah The Prince
Barakah The Prince

Mashabiki wengi ambao wamekuwa wakicomment kwa picha hii wanashangazwa na Baraka kupost wimbo huu kwa sababu wengi wanajua Baraka yuko kwenye lebel moja na Alikiba.

Kama mnavyoelewa Kiba na Diamond wamekuwa na beef kwa muda sasa kwa hivyo Baraka asingeweza kupost chochote kuhusu Diamond Platnumz, wengine wamecomment kwa kutopendezwa na post hiyo wengine wamepost kumpongeza.

Kupitia Instagram Barakah the prince aliandika kusema…

Chanzo cha kutengenezewa maden na makaka poa..ila mama alinifunza kukaa kimya..eeehh mungu niokoe vita

Baada ya kufanya collabo na King Kiba, Barakah The Prince aeleza changamoto alizopitia

Mwimbaji wa Tanzania Barakah the Prince ameeleza baadhi ya changamoto alizopitia baada ya kutoa colabo ya wimbo wake Nisamehe aliyomshirikisha King kiba. Hii ni kufuatia tofauti zilizopo kati ya team Kiba na team Diamond Platnumz.

Akizungumza katika interview na kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha Salama Jabir, Barakah alisema kuwa ilikuwa vigumu kupata support kutoka team Diamond ambao hawampi support Kiba.

Ujue Alikiba ni brand kubwa na ni brand ambayo ina mvutano na vitu vingi, kwahiyo unavyofavya collabo na Alikiba kuna mawili hapo, kuna nyimbo kufanya vizuri na kuna nyimbo kufanya vizuri wastani, wa kawaida kwasababu ya ule mvutano wa kibiashara ambao upo kati yake na timu nyingine

Ingawa halalamika kuwa jambo hili liliadhiri wimbo wake, muimbaji huyu amekiri kuwa timu hizi mbili zinangumvu ya kuaffect career ya muimbaji bongo. Kwa hivi sasa anaendelea kuzipush nyimbu zake kabla atoe project nyingine mwaka huu.