Video ya mtoto wa Rayvanny na Fahyma akiwa na Diamond Platnumz

Jaydanvanny ambaye ni mtoto wa kwanza wa mkali wa Wasafi records Rayvanny na mpenzi wake Fahyma ni miongoni mwa watoto maarufu Tanzania.

Ingawa bado yeye ni mchanga, mtoto huyu akona mashabiki wengi mitandaoni na hivi karibuni alipata fursa ya kukutana na mjomba wake, Diamond Platnumz huku wengi wakitamani maisha yake.

Kwenye video hiyo, Jaydan anaonekana kutulia huku Platnumz akicheza na yeye. Tazama video hiyo hapa;

https://instagram.com/p/BYTrlHvAnDB/

“Gombaneni, roganeni mpaka muuane” Huu ndio ujumbe Nay aliowaandikia Ommy Dimpoz, King Kiba na Diamond Platnumz

Rapa wa bongo Nay wa Mitego hatimaye ameingilia vita mpya ya Ommy Dimpoz, Diamond Platnumz na King Kiba kwa kutoa maoni yake.

Kupitia mtandao wa Instagram Nay alifunguka kwa kusema kuwa hakuna anayemuunga mkono lakini jambo linalomkasirisha ni kuwahusisha wazazi kwenye vita hivi vyao vya utoto. Aliandika kusema;

Gombaneni, roganeni mpaka muuane, napenda kusikia changamoto kwenye gemu, ila tusiwaingize wazazi wetu tafadhali, tukananeni matusi yote wenyewe kwa wenyewe ikibidi piganeni kabisa atakaye kufa tutazika na itakuwa historia kama Big na Pac.

Akaendelea kwa kuongeza kuwa;

“Ila kuwaingiza wazazi ni ujinga, sipo upande wowote si kwa Kiba, Dimpoz wala Diamond, endeleeni na vita yenu kama wanawake mmechukuliana mabwana, ila suala la wazazi mnavuka mipaka,”

Ommy Dimpoz amuandikia Barua mamake Diamond Platnumz

Wengi wanapodhania kuwa Ommy Dimpoz ameamua kukaa kimwa – basi msanii huyu wa bongo hivi leo amewaacha wengi wameshtuka baada ya kumuandikia bi Sandra barua kupitia mtandao wa Instagram.

Ommy aliweka picha yake na ya mama Diamond hukua kiandika;

BARUA YA WAZI KWA BINTI YANGU MALKIA WA NGUVU

Salam zako nimezipata mwanagu hivi kweli ww wa kukosa adabu kuamua kunichamba baba yako? Sasa Kosa langu mimi nini????kwani kuna ubaya kumtandikia kitanda Baby wako king?
#unanioneakwakuasijuikurap?
#sijuiNamiminimkatae
#kamayeyealivyokataawaMobeto
#Yaniunamkataamjukuuwangu
#unakubalikuleawatotowa5siowako
#umerogwawwsioburemwanangu
#NilikuwanajuanimezaaSIMBA
#kumbenimezaaKIMBA
#DavidonaeanalalamikuhusuENEKA
#UmeletaJanjaJanjakwenyefallonu
#utakujakuniuakwapreshajomonii
#Nnaedhalilikamimibabayako
#hayanendakatungevesinyingine
#Rahayavitausichanguesilaha
#BABAMALKIA

Tazama post yake hapa;

Fid Q amshirikisha Diamond Platnumz na Rayvanny kwenye mix ya ‘Fresh’ na mashabiki wadai wamemchana Hamisa Mobetto

Fid Q ambaye ni msanii wa muziki wa hip hip Bongo sasa hivi ameachia remix wa wimbo Fresh ambapo ameliwashirikisha Diamond na Rayvanny.

Katika wimbo huu Diamond Platnumz anasikika akirap na kulingana na mashabiki, mwanamuziki huyu anawachambua Kiba na Hamisa Mobetto kwenye maneno aliyotumia.

Rayvanny naye alipewa nafasi ya kuimba chorus na kama kawaida, msanii huyu aliweza kuipa nyimbo hii fleva.

Isikize nyimbo hii hapa;

 

 

 

Zari Hassan na Diamond Platnumz washerehekea siku ya kuzaliwa ya mtoto wao, Princess Tiffah

Diamond na mpenzi wake Zari The Bosslady walisherehekea siku ya kuzaliwa ya Princess Lattifah Jumapili hii iliyopita kwa kumuandikia ujumbe ambao umewaacha wengi wakifurahia kupitia mitandaoni yao ya Instagram.

Hii ni baaad ya Zari alipojifungua mtoto wa kwanza wa miaka miwili iliyopita. Kupitia mtandao wa instagram, wazazi hao walionyesha furaha zao kupitia ujumbe wao.

Zari aliandika,

“It’s princess world…happy birthday my one and only princess_tiffah.”

Na akaongeza kusema;

“My Princess….. May God see you through with nothing but the best. May you be blessed from this day forward. Most of all, May you be a Godly child. Without God we are nothing. Happy birthday @princess_tiffah,”

Diamond Platnumz naye akaandika;

“Happy 2 years mama, Words Can’t express how much i love you my Tee….

Tiffah ni miongoni mwa watoto maarufu Africa yote.

 

Faiza Ally amchana Hamisa Mobetto

Faisal Ally ambaye anajulikana sana kwa sababu ya movie zake za Bongo na pia mitindo yake ya kimavazi hivi karibuni alifunguka kuongelelea ujauzito wa Hamisa Mobetto ambaye ni video vixen na model kutoka bongo.

Hata hivyo hii ndio mara ya kwanza Faiza Ally kutoa maoni kuhusu mrembo huyu tangu isemekane kuwa anamtarajia mtoto wa Diamond Platnumz ambaye ni mume wa Zari Hassan.

Akizungumza na 3 Tamu, Faiza alisema kuwa, yeye Kama mwanamke hajafurahishwa na maneno yale ikiwa ni kweli kuwa Hamisa Mobetto ana ujauzito unaodaiwa ni wa msanii wa CEO wa Wasafi Records. Ally alisema,

Unajua wasichana wengi hawajithamini wanafanya vitu bila kufikiria, kama huyo Hamisa nasikia ana ujauzito wa huyo msanii (jina kapuni) na kama ni kweli mimba ni ya huyo mtu, kakosea sana, napenda kuongea kitu kinachonigusa kwenye nafsi yangu akichukia atajijua.

Hata hivyo Diamond aliweka wazi hivi karibuni kuwa yeye na Hamisa Mobetto hawamtarajii mtoto pamoja na kuwa uhusiano was ni wa kibiashara tu.

Amber Lulu ataja sababu amazomtamani Diamond Platnumz

Amber Lulu ambaye anatamba sasa kwa kutokea kwenye video za mziki za Bongo ni mrembo ambaye anatisha.

Kwa hivi sasa anafanya vyema kwenye career yake na ingawa bado yeye ni mdogo. Hata hivyo, hivi karibuni alifunguka kumuongelea Diamond Platnumz huku akisema kuwa ni mmoja wa wasanii ambao anatamaniwa na warembo wengi.

Lulu alisema kuwa Diamond Platnumz anaonekana Kama mwanaume kwenye bidii na ikiwa hangekuwa na familia pia yeye angejaribu bahati yake, akiongea na Times FM, Lulu alisema…

 

“Kibongo Bongo sijaona mwanaume zaidi ya Diamond kwanza ana ni inspire na maisha yake yaani anajiweka kazi na kila kitu na sio kwamba na wish ku’date nae tuu bali kufanya nae kazi pia,”

Aliendelea kwa kusema,

“Kama ikitokea kutembea nae is ok….sio mimi peke yangu kila mwanamke anawish kuwa nae…kila mtu mimi naamini wachache sana ambao hawamuhitaji.”

Msanii wa Bongo AT asimulia ugomvi wa Diamond Platnumz na Alikiba ulipoanzia

Ni wengi bado wanajiuliza ni nini kilichotokea Kati ya Diamond Platnumz na Alikiba kuwafanya wawili hao kukosana.

AT ambaye ni maarufu Bongo alisimulia tukio la Kiba na Naseebu akizungumza kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, muimbaji huyo maarufu wa muziki wa mduara alisema;

“Tulikuwepo tupo Oman kwenye hotel moja inaitwa Dream tulikuwa tuna show, kwa hiyo walikuwa wanacheza game, Alikiba amechagua Real Madrid na Diamond Barcelona, mimi nimekaa pembeni naangali watu wanacheza game yao. Ali akawa amefungwa mbili, akawa anataka kupiga free kiki kwenye game Diamond akamsukuma akamwambia halafu mwanangu nakutafuta siku nyingi. Alikiba akanyanyuka ikabidi na mimi ninyanyuke sasa, nikamuuliza Ali tatizo nini mbona kama mnataka kupigana halafu tupo ugenini wazee vipi?  Akaniambia huyo dogo kuna vitu anavifanya mimi sijavipenda.”

Aliendelea kwa kusema,

“Mwisho wa siku naona kama vile vitu vinaendelea halafu watu wanakurupuka wala tatizo wao hawalijui. Ebu watafute ukweli ulipo, sijui huyo kamtoa kwenye wimbo huyo, kuna jambo lingine ambalo lipo. Kiukweli kuna vitu ambavyo pengine wao wenyewe wanavijua ni vikubwa zaidi,”

Diamond Platnumz aeleza sababu hataki Tiffah awemsanii kama yeye

Wasanii wengi duniani hawapendi kuwaonyesha Watoto wao mitandaoni na ukiwaukiza, hii ni kwa sababu wanahofia watoto wao kuishi maisha kama wanayoishi.

Mmoja wao ni Diamond Platnumz ambaye anahofia mwanawe, Tiffah Dangote kuwa msanii. Akizungumza kwenye mahojiano na Larry Madowo wa NTV Kenya Diamond alisema kuwa Tiffah akiwa msanii atatembea na wanaume wengi kitu ambacho yeye mwenyewe hataki kukiona ama kusikia. Alisema,

“Mtoto wangu wa kiume ningependa awe msanii lakini mtoto wangu wa kike sitaki awe msanii, watamla sana. Mtoto akiwa msanii watu wanaomjua wanakuwa wengi, watu wanaokujua wakiwa wengi na kutongozwa kunakuwa kwingi, sasa watanipa presha. Ukiwa mwanaume lijali na ukiwa kwenye nafasi kama yangu lazima wataliwa. Nilikuwa kwenye kutafuta tafuta, mpaka nilivyompata Zari na kweli nimetulia,”

Tazama interview hiyo hapa:

Diamond Platnumz aeleza kwanini vijana wanashindwa kuingia Wasafi Records

Ni wengi ambao wanatamani kujiunga na label ya Wasafi Records. Hata hivyo kulingana na sheria ambazo Diamond Platnumz ameziweka wasanii wachache ndio tu wamehitimu

Akizungumza kwenye kipindi cha XXL cha Clouds Fm Diamond Platnumz alisema kuwa yeye hutaka wasanii ambao wanaubunifu wa kujiandikia nyimbo kwa sababu hii inasaidia kuangalia maudhui na uzuri wa wimbo.

“Kwanza Rich Mavoko ndiye mgumu kwenye kupitisha nyimbo, ikitoka hapo Ravvanny aipitishe, Queen Darleen aipitishe, ikitoka hapo niipitishe mimi, iende kwa Mkubwa Fella na Babu Tale waipitishe na Sallam aipitishe, ukitoka hapo wewe ni mwanaume haswa.”

Diamond aliendelea kwa kusema,

“Kwa hiyo wengi wanakuwa na uwezo mkubwa. Labda unaweza ukaja ukasikia kitu kidogo, ukasema ukiweka hapa kitu flani itakuwa poa zaidi, yaani ukiandika unaandika haswa.”

Lakini kwa sasa Diamond Platnumz amemsign Lava Lava ambaye amenonekana kuwa mkali baada ya kuachia wimbo wake mpya.

“Zari anaumia kumuona Ivan akiwa kwa hali maututi” Diamond Platnumz asema

Diamond Platnumz hivi karibuni alifunga kusema sababu ambazo hajaweza kumpost aliyekuwa mpenzi wa Zari wa zamani, Ivan Don kumtakia kupona haraka.

Akizungumza na kipindi cha Clouds FM Diamond Platnumz alisema Kuwa anaona watu watasema kuwa anatafuta kiki kwa kumuweka Ivan Don kwenye Instagram yake kwa sababu wengi hudhania kuwa wawili hao hawapatani baada ya Diamond kumchukua Zari Hassan ambaye alikuwa mke wa Ivan kabla ya wao kuachana.

Hata hivyo Diamond Platnumz amesema kuwa amekuwa akiwasiliana na Zari kila wakati anapoenda kumuona Ivan Don hospitalini. Aliendelea kwa kusema kuwa Zari anaumia kumuona baba ya Vijana wake akiwa kwenye hali hiyo. Lakini kwa sasa wote wanamubea ili apate nafuu nataka.

“Ni kweli mzazi wake Zari anaumwa, na yuko serious. Na kila siku huwa namuhimiza Zari akamuone mzazi mwenzie kwasababu najiuliza asingekuwa anaenda familia yangu ingemuonaje, kwa hiyo maskini dada wa watu kila siku huwa anaenda,” Diamonda alikiambia kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM. Sijawahi mpigia simu kwasababu yuko serious sana na pia sikuweza kumpost kwasababu watu waneanza kusema labda natafuta kiki maskini ya Mungu kumbe wala,

Diamond Platnumz aendelea kuwakanganya wengi kwa kingereza chake

Sio kila mtu ambaye alibarikiwa kujua kingereza akiwa mdogo na ndio maana kuna watu ambao bado hata sasa hivi bado wanapata shida kuwasilia na wenzao kwa kutumia lugha hii.

Mmoja wa hawa ni Diamond Platnumz ambaye amekuwa mitandaoni kwa kuwachanganya mashabiki wake anapoandika ujumbe wa kingereza kupitia mtandao wake wa Instagram.

Msanii huyu amerudia kosa hili baada ya kuweka picha ya manukato yake na kuandika ujumbe ambao haueleweki kwa kutumia lugha ya kingereza. Aliandika kusema,

i wish you know, how in Love i am with this fragrance …. CHIBU PERFUME!!!! by @diamondplatnumz #TheScentYouDeserve Artwork and ? by @kifesi @chibuperfume

Hata hivyo mashabiki wake hawakumpa nafasi ya kupumua walipoanza kumponda na kumcheka mkali huyu wa wasafi. Mmoja aliandika Broo wengine hatuja soma hatuelewi kizungu jaribu kutuwekea na lugha yetu ya kiswahili tunafuatilia Sana habari zako tunahitaji kujua.

“Sio mbaya mkiniita Gigy Dangote” Gigy aeleza anavyompenda Diamond Platnumz

Gigy Money ambaye ni video vixen mkubwa kutoka Tanzania amewaacha wengi wakijiuliza uhusiano wake na Diamond Platnumz ni upi baada ya yeye kuweka picha yake akiwa na CEO huyo wa Wasafi records huku akiandika kusema anavyompenda.

Mwana dada huyu ambaye amefanya kazi na wasanii kama Harmonize hata hivyo hakuwa na nafasi ya kuwajibu mashabiki wake ambai walitaka kujua kama alikuwa anammezea msanii huyu.

Kupitia mtandao wake wa Instagram, Gigy aliandika kusema…

Nampenda sana Chibu sio kwamba ajui ?ila sio mbaya mkiniita gigy dangote❤ amen? #ilatunapendezana @diamondplatnumz

Mashabiki wengine waliacha majibu ya kumponda mrembo huyu wakimfananisha na Zari Hassan huku wengine wakimwabia mtu anayemfaa sana ni Harmorapa. Tazama picha hiyo hapa chini.

“Mimi simtaki Naseeb tena!” Wema Sepetu amwambia shabiki wake Instagram

Japo ni wengi bado hutarajia Wema Sepetu na Diamond Platnumz kurudiana, mrembo huyu ameweka wazi kuwa hamtamani Diamond tena na mapenzi yao yalikwisha kitambo sana.

Wema Sepetu alisema haya baada ya mmoja wa mashabiki wake aliandika kumuuliza iwapo ameshindwa kumpata Diamond Platnumz kupitia Instagram. Shabiki huyo aliandika kusema,

Wema Kwa uzuri huo umeshindwa kumkamata Diamond mpaka anakupa mawazo wanaume hawana lolote jitahidi

 

Kupitia tu Instagram Wema pia yeye alimpa shahidi huyo jibu ambalo lilidhibitisha kuwa mrembo huyu ameyaacha maisha yake ya kitambo na hivi sasa anatarajia mwanaume ambaye atamchukua alivyo. Wema aliandika kusema,

@Veronikakihonga Sasa baby alokwambia mi namtaka Diamond ni nani…?Life has to go on… Yule ni baba wa watoto wawili Jamani… Its about time u guys accept that me and Naseeb are no more. Mnachotakiwa ni kuniombua ni nipate mwanaume Bora na sio Bora mwanaume…Mwenye heshima zake tena ambaye hata haijulikani…Kajisemea dada angu @mangekimambi…mwenye hela miiingi

Wema Sepetu na Diamond Platnumz washerekea pamoja katika party ya Sallam

Waliokuwa wapenzi Diamond Platnumz na Wema Sepetu jana uikutana katika sherehe ya kuzaliwa ya Meneja wa Diamond Sallam Sharaff.

Sherehe hii ambayo ilifanyika Castle Lite iliwavutia wasanii kadhaa ambao walijitokeza kama wamevaa mavazi ya kizamani huku ikiwakutanisha Wema na Diamond Platnumz.

Ingawa wawili hawa hawajaonekana wakiwa pamoja katika picha ambazo zinasambaa mitandaoni, wengi wameachwa wakijiuliza ikiwa walipata nafasi ya kuongea kwani hii ndio mara ya kwanza kwa wiwili hawa kuwa katika sherehe moja tangu kuachana mwaka wa 2015.

Hata hivyo Wema Sepetu alionekana kurembeka kwa mavazi yake na mapambo yake ya kawaida.Tazama picha yake hapa.

Wema Sepetu katika party ya Mendez

Huu ndio ujumbe Diamond Platnumz amemwandikia professor Jay kupitia Instagram

Diamond Platnumz amewaacha wengi wakishangaa baada ya ujumbe aliomwandikia mbunge wa Mikumi Joseph Haule a.k.a Prof Jay. Msanii huyo wa Wasafi records aliandika kumwambia Prof Jay sababu ambazo yeye hakujitolea kutumbuiza kwenye kampeni zake mwaka uliopita.

Hit maker wa Marry me aliandika kusema,

“Ndio Maana kwenye Jimbo lako sikuja kupiga kampeni bro…kwakuwa niliijua mapema thamani na umuhimu wa Uwepo wako kwenye hilo jengo….. @professorjaytz

Hata hivyo wengi wasichokielewa ni kwa nini msanii huyo alimchana mwenzake ata baada ya yeye kumshughulikia bungeni baada ya kudaiwa kuwa anadeni la TRA la milioni 400.

Wasanii wengine hata hivyo wamekuwa wakimuunga mkono Prof Jay ambaye anawashungulikia wasanii kwani pia yeye anaelewa shida ambazo wao hupitia.