Shilole Amtolea Povu Mange Baada Ya Kumponda Uchebe

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Ashraf ‘Shilole’ amemjia juu mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi baada ya kumponda mume wake Uchebe.

Shilole alifunga ndoa na Uchebe wiki chache zilizopita ambayo ilikuwa ni ndoa ya kimya kimya au ndoa ya siri ilyohudhuriwa na watu wachache lakini iliyozua gumzo kwa sababu ya ugomvi wa familia iliyozua. Lakini tangu ndoa hiyo imefungwa Shilole amekuww na kazi ya kumtetea Uchebe endapo mtu yeyote atamponda.

Siku chache zilizopita Shilole alimtetea tena Uchebe baada ya Mange Kimambi kumponda Uchebe na kudai kuwa ana jina la kienyeji na mbaya. Baada ya kuona hivyo Shilole kupitia ukurasa wake wa Instagram alimwaga povu hili dhidi ya Mange:

Mange my sis nakuheshimu sana pliiiz mume wangu Uchebe mbaya pliiz muache mimi mdogo wako ndio nimeshampenda by the way nina safari ya kuja American soon”.

Lakini baada ya povu hilo Mange alimjibu Shilole kwa kumtaka radhi kumwambia alikuwa anamtania tu aliposema mume wake Uchebe ni mbaya na ana jina la kienyeji ambapo kupitua ukurasa wake wa Instagram aliandika:

I was just joking nakutakia kila la Kheri kwenye ndoa yako ukija kwa Trump basi uje na LA ila use umenisamehe kweli nisije nikaja nikajileta mtegoni alafu nikachezea kipigo cha mwizi maana hiyo sentensi nina safari ya kuja kwa Trump Ina maana nyingi alafu Uchebe shemela nilikuwa nakutania tu mimi mwenyewe jina langu la kienyeji”.

 

 

 

Mange Kimambi Amtolea Povu Zito Wema Baada Ya Kutangaza Kurudi CCM

Mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi amemtolea povu zito muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu baada ya kutangaza kuwa anahama Chadema na kurudi kwenye chama chake cha zamani CCM.

Habari zilianza kusambaa tangu mwanzoni mwa wiki hii kuwa Wema anampango wa kurudi CCM. Leo kupitia ukirasa wake wa Instagram Wema ameujulisha uma wa watanzania kuwa ameamua kuondoka Chadema na kurudi chama chake cha zamani CCM Wema alifunguka kama ifuatavyo:

Siwezi kuendelea kuishi kwenye nyumba inayonikosesha amani, Peace of mind is everything for me natangaza rasmi kuondoka Chadema na kurudi Nyumbani there is no place like home….feels good to be back”.

Baada ya kutoa tangazo hilo la kuamua kurudi CCM Mange hakupoteza muda kutoa maoni yake juu ya kitendo alichofanya Wema, kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange alimwagia Wema povu hili:

Not sure what to say i only blame her for not being strong enough Nyerere alikaa jela for 27 years she could have taken 2 or 3 years ya hiyo kesi yake Kimara nzima imebomolewa nyumba na wanaishi sembuse yeye mwenye kubwa. Na lipshone zako walizozipiga marufuku so what?  Ungekomaa na msimamo wako serikali ingechoka kukuandama Wema your weak very weak! Hujawaangusha Watanzania tu umejiangusha wewe mwenyewe, your fans na Watu wote who cared for you”.

 

Mange: Muda Wowote Wema Sepetu Atatangaza Amerudi CCM

Mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi amefunguka na kudai kuwa muigizaji Wema Sepetu na Mama yake mzazi wamerudi CCM.

Wema alihama chama hicho mapema mwaka huu baada ya kukamatwa kwa kutuhumiwa kuuza na kutumia madawa ya kulevya. Baada ya kuachiwa huru Wema aliita vyombo vya habari na kutangaza nia yake ya dhati kabisa ya kuhamia Chadema.

Siku za hivi karibuni kumekuwa na tetesi kuwa Wema anampango wa kurudi CCM ingawa alikataa lakini leo asubuhi Mange kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram alitangaza kuwa Wema amerudi CCM:

Breaking News Wema Sepetu na mama yake wanarudi CCM very soon…Mimi nilijua tu nilipomuona Wema kaenda Rwanda kakacha tarehe ya mahakamani bilauoga nilijua tu kuna mkono wa CCM, kuna mtu Mkubwa CCM aliniletea taarifa kuwa nyumba ya mama Wema inabomolewa wasiporudi CCM wamepewa muda wa kufikiria, na notice ya kubomolewa nyumba wameshapewa. That’s their family house, ila kaniambia mama Wema kashakubali kurudi sahivi anam-convince Wema, kaniambia Wema keshakubali kurudi lakini anaona aibu ni jinsi gani atai-face jamii…yaani unaambiwa mama Wema alivyoambiwa nyumba yake inabomolewa fasta akakubali kurudi CCM. Na kesi kaambiwa akirudi CCM itakwisha vizuri ila akikataa kurudi kila siku atapelekwa mahakamani mpaka arudi na asiporudi anaweza kufungwa”.

Pia Mange aliendelea  kufunguka na kudai kuwa Ana uhakika asilimia 100 kuwa Wema atarudi CCM:

Kilichobaki ni Wema kutangaza tu kwaiyo Watanzanua kaeni sawa muda wowote Wema na Mama yake wanatangaza kurudi CCM na wakisharudi CCM Magufuli habomoi nyumba zao na wakirudi wameambiwa lazima wamsifie na waseme wameona Chadema haifai na yeye ndio anafaa”.

 

 

Mange: Diamond Amezoea Kuchukua Kazi za Wasanii Wengine Bila Kuwalipa, Lazima Awalipe Msondo Ngoma

Mwanasiasa na mwanaharakati maarufu mtandaoni Mange Kimambi ameibuka na kudai kuwa msanii Diamond Platnumz amezoea kuiba nyimbo za wasanii mbali mbali hivyo ni lazima awalipe Msondo ngoma fidia ya shilingi milioni 300.

Mange amedai kuwa Diamond amekuwa na kawaida ya kuchukua na kutumia nyimbo za wasanii wengine bila kuwalipa fidia na msanii pekee aliyemlipa kwa kutumia nyimbo yake ni Saida Karoli.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange amefunguka yafuatayo;

Wanamuziki wengi hata Chris Brown wanachukuaga hata vipisi vidogo vya nyimbo za watu au hata kurudia nyimbo nzima lakini huwa wanawalipa wenye nyimbo tatizo la Diataka kuchukua kazi za watu bila bila kuwalipa chochote, Kwanza nashangaa ile nyimbo ya Hallelujah mpaka leo hajashtakiwa tu ile ndio nimbi ambayo amechukua kazi za watu kupita kiasi kutoka kwa wanamuziki wa Tanzania na Marekani. Kwa level aliyofikia Diamond anatakiwa awe anawalipa watu anapotumia kazi zao au kama hataki kulipa awe anapiga akili anatoa vitu original bila kuunganisha na kazi za watu wengine. Ila hii ya kuchukua kazi za watu alafu anajikausha as if katoa kichwani kwake sio haki especially sababu anaowachukulia kazi zao wanahitaji pesa kushinda yeye, awalipe bwana”.

Pia Mange aliendelea kuongelea msanii aliyewahi kulipwa na Diamond baada ya kutumia kazi yake ;

I hope atajifunzia hapa na kuanza kuwalipa watu kama alivyomlipa Saida karoli na wimbo wake wa Salome. Hao Msondo Ngoma hata angewalipa milioni 5 nina uhakika wangekubali ila alitakiwa kuingia nao mkataba kabla ya nyimbo yao ya ‘Zilipendwa’ haijatoka #TukutaneMahakamani”.

 

Mange Afunguka Kuhusiana na Ugonjwa Uliompata Hamisa na Kumpa Shavu Baada Ya Kushinda Tuzo

Mshawishi wa mambo ya siasa mtandaoni, Mange Kimambi ameibuka na kumtetea mrembo Hamisa Mobetto baada ya kugubikwa na skendo baada ya kusemekana amechanganyikiwa.

Tangu wiki iliyopita habari zilienea mtandaoni kuwa mzazi mwenxie na Diamond, Hamisa Mobetto amechanganyikiwa na kile kilichohusishwa na Imani za kishirikina huku watu wengi wakidai kuwa Hamisa ametupiwa uchawi na hivyo kusababisha yeye kuwa kama chizi.

Jana kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mange alifunguka kuwa habari za Hamisa kuchanganyikiwa kwa kulogwa zinasambazwa na maadui tu bali ukweli ni kuwa Hamisa alikuwa anaumwa malaria:

Hamisa alipatwa na malaria kaliii ikapanda hadi kichwani, ila hadi hivi sasa anaendelea vizuri. Hizi stori za kuwa amegeuka chizi and so forth ni chumvi tupu zimeongezwa…..But its true alikuwa anaumwa na ishu ni malaria kali ambayo ilipanda kichwani, ila sasa hivi anaendelea vizuri tuendelee kumuombea”.

Pia Mange alimpongeza Hamisa kwa kushinda tuzo aliyokuwa anagombania na washiriki wengine. Ambapi Mange aliandika

“Hongera kwa kushinda tuzo Toto”

Jana kupitia ukurasa wake wa Instagram Hamisa alitangaza kuwa ameshinda tuzo aliyokuwa anawania;

 

Well…. what can I say? team Hamisa Mobetto we won babies Thank you a guys soo sooo much for your votes Ahsaaanteni saana stardqt awards thank you babies, Ila nini tuzo yetu kuifuata iko pale pale”.

 

 

Mange Ampa Mbinu Hizi Hamisa Ili Azikombe Pesa za Diamond

Mwanasiasa maarufu mtandaoni Mange Kimambi, ameibuka tena na jipya huku safari hii amempa mbinu mpya Hamisa atakazotumia ili aweze kupata pesa ya kulea mtoto wake kutoka kwa Diamond.

Tangu Diamond na Hamisa waweke wazi kuwa wamezaa mtoto kumekuwa na visa baada ya visa hasa baada ya Hamisa kudai kuwa Diamond amegoma kutoa pesa ya matumizi kwaajili ya malezi ya mtoto, kitu kilichopelekea Hamisa kumpeleka Diamond mbele ya sheria.

Baada ya habari kutapakaa kuwa familia ya Diamond inamkataa mtoto wa Hamisa na Diamond hataki kutoa pesa ya malezi, Mange ameibuka tena na safari hii kadai kuwa zari, Diamond na familia yao wanataka kumchosha Hamisa ili akate tamaa na kuifuta kesi yake mahakamani dhidi ya Diamond.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange alimpa mbinu hizi Hamisa ili aweze kupata pesa kwaajili ya malezi ya mwanawe.

Nimepitia kidogo sheria ya matunzo ya mtoto wa Tanzania inafanana na ya marekani, wanaangalia kipato cha wazazi na matunzo yanatolewa kutokana na kipato cha mzazi, ila tatizo wanawake Tanzania wanashindwa kuthibitisha kipato cha mwanaume mahakamani, Hamisa kama uyashindwa kupeleka ushahidi wa kipato cha Diamond utaishia kupewa laki mbili kwa mwezi. Kwanza ujue Diamond hawezi kutaja kipato chake cha kweli mahakamani inabidi umlazimishe”.

Pia Mange aliendelea kufunguka mbinu ambazo Hamisa atatumia kupata kipato halisi cha Diamond:

Ushahidi wa Kwanza ni uombe mahakama ikupe order ya bank account zote anazoweka pesa Diamond kuanzia mwezi wa 1 mwaka 2015, kampuni zote zilizoratibu show zake zote wapeleke order ya mahakamani wapeleke contract, kampuni zote zilizompa matangazo kama Danube na Vodacom na Diamond Karanga wote wachape barua za mahakama wapeleke mikataba.

Then peleka order ya mahakama kwa kampuni ya WCB na ile website yao wanayotunia kuuza nyimbo za wanamuziki na pia ichape barua ile Chibu perfume anayo share na Kusaga wote wachape barua waonyeshe mikataba yao na Diamond anaingiza shilingi ngapi. Ukitoka hapo wachape barua TRA kutoa rekodi ya malipo yake ya TRA”.

Mange alimalizia kwa kumshauri Hamisa asikate tamaa kumlea mtoto wake kwani kama alimpigania mpaka Diamond akamkubali mtoto wake hadharani basi aendelee kumpigania mpaka pale atakapokubali kumlea mtoto wake.

Lulu Hana Utu Wala Ubinadamu Kwa Familia Ya Kanumba, Mange Amtolea Uvivu Lulu

Mchambuzi wa mambo ya siasa Mange Kimambi ameongelea tena kesi ya Lulu safari hii akiweka hisia zake wazi na kusema Lulu ameonyesha jeuri kwa familia ya Kanumba hasa mama yake mzazi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mange amefunguka yafuatayo:

Ngoja niwe mkweli kwanini nimeshindwa kuwa na huruma kwa Lulu, ni sababu alivyoishi maisha yake kwa miaka mitano iliyopita, Hakuonyesha hata chembe ya kujutia kwa kilichotoke hasa kwa familia ya marehemu. Lulu alitakiwa atambue kuwa yeye ndio sababu marehemu hayupo duniani, angeonyesha ubinadamu utu hata kwa Mama Kanumba ambaye alikuwa anamtegemea kwa kila kitu, angalau angemjali yule mama, yote Tisa kumi Lulu kushindwa kwenda makaburini kwaajili ya Kanumba day? hapa ndo nilipomuona huyu msichana hana utu, hivi mtu unaanzaje kuwa na huruma kwa Lulu wakati yeye hana huruma kwa wale aliowasababishia majonzi? Hivi mmewahi kumsikia Lulu anafanya kumbukumbu ya Kanumba?

Mange pia hakuishia hapo aligusia suala la mauaji ya mpenzi wake mwingine aliyefariki baada ya Kanumba, Seki.

Kama Lulu angeonyesha ubinadamu kwa tukio hilo sidhani kama nisingekuwa upande wake ningesema amejifunza kitu, Ila mimi hakina kitu kinaniuma kama Lulu kuishi kama vile hana Deni kwa familia ya Kanumba yaani kama vile wasimghasi, Kanumba angekuwepo leo Mama yake asingekuwa anahangaika na daladala na Bajaji sahivi. Lulu anaenda mahakamani anachekacheka, anapiga picha na watu anachezea Simu kwa furaha yote wakati mama wa marehemu yupo mule ndani? Anapishana na mama Kanumba mahakani bila hats salami hiyo nifair kweli? Mama Wa marehemu yupo pale na majonzi yeye ndio kwanza anaenda pale na staili mpya ya rasta kichwani , kavaa high heels na kupanda migari mikubwa anaenda kumuonyesha mama aliyepauka kwa kupanda daladala tu ambaye mkikaa mnamuombea kwa Mungu? Akitoka mahakamani anaenda kupiga picha anabembea huku anakenua!  Hana utu wala ubinadamu huyo msichana period”.

 

Wema Sepetu na Mange Kimambi Wamesaidia Kukusanya Zaidi Ya Milioni 60 Kwaajili Ya Matibabu Ya Lissu

Mwanaharakati wa siasa mtandaoni Mange Kimambi na Muigizaji wa bongo movie Wema Sepetu wametajwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kama watu wanaozidi kuchangia kwenye matibabu ya mbunge wa Singida mjini Tundu Lissu.

Tundu Lissu alipigwa risasi mwezi uliopita na watu wasiojulikana akiwa mkoani Dodoma kwaajili ya kuhudhuria vikao vya bunge vilivyokuwa vinaendelea. Tangu hapo amelazwa mjini Nairobi Kenya.

Kwenye kikao alichofanya Jana na waandishi wa habari Mh. Mbowe aliwataja Mange na Wema kwa mchango wao mkubwa:

Naomba niwashukuru Watanzania wanaoishi nje ya nchi kwa michango yao ya dhati naomba nimshukuru Dada yetu Mange Kimambi anayeishi nchini Marekani kwa kuanzisha account ya ‘go fund me’ iliyowezesha kukusanya dola za kimarekani elfu ishirini na tisa na mia saba sawa na shilingi za Kitanzania milioni sitini , tunatambua mchango wa Mange na Wema Sepetu katika kuhamasisha Watanzania kuchangisha pesa hizo  kupitia mitandao ya kijamii, hivyo tunapenda kuendelea kuheshimu wajibu waliochukua”.

Pia Mh. Mbowe aliwahakikishia kuwa Tundu Lissu anaendelea vizuri kwani ameshatoka ICU na sasa anakula mwenyewe bila mirija na kupumua bila oksijeni.

Mange na Wema walitumia ushawishi wao kuwaomba watu waendelee kumchangia Mh. Tundu Lissu na kwa kiasi kikubwa watu waliitikia wito na kuzidi kutoa walicho nacho.

 

 

Mange Kimambi: Diamond Kaweka Rekodi Feki

Mange Kimambi ameibuka upya na kudai kuwa rekodi ambayo Diamond Platnumz ameweka ni feki Hili limekuja baada ya Diamond kuachia wimbo wake mpya siku mbili zilizopita uitwao Hallelujah aliomshirikisha  mwanamuziki Morgan Heritage, wimbo huo ulifanikiwa kufikisha jumla ya views million mbili kwenye mtandao wa Youtube ndani ya siku moja.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mange alifunguka yafuatayo juu ya suala hilo;

“#IssaFakeRecord Amenunua viewers huo ndo ukweli!!! Samahani kwa ntakaowakwaza…. Baba Dully ajifunze kukubali na kushindwa sometimes, hakuwa na haja ya kununua viewers ili tu avunje rekodi ya Ali Kiba”.

Mange aliendelea kusimamia msimamo wake juu ya suala hilo japokuwa alipokea ushindani mkubwa shidi ya mashabiki wa Diamond ambao walimlaani vikali;

“Mtanitukana sana Team Diamond ila wote mnajua kuwa sisemagi uwongo na maneno yangu kwa njia moja au nyingine huwa lazima mwisho wa siku yawe ya kweli! Naamini soon mtakuja kujua kuwa Mange aliwaambia ukweli kuwa Diamond alinunua viewers! Leo mtanichamba ila siku moja ukweli utajulikana. Haiwezekani nyimbo imetrend namba moja Tanzania peke yake ikapata waangaliaji milioni moja ndani ya masaa kum na tano wakati Seduce me iliyotrens Afrika Mashariki nzima ilipata waangaliaji milioni moj ndani ya masaa thelathini na nane, it doesnt make sense ata all #fact”.

Diamond alivunja rekodi hiyo iliyowekwa na hasimu wake Ali Kiba ambaye kwa kupitia wimbo wake wa seduce me alifikisha waangaliaji milioni 1 ndani ya masaa 38 na Diamond juzi alifikisha waangaliaji wa Video yake hiyo milioni 2 ndani ya siku moja.