Otile Brown Ajiachia na Mrembo Mpya Baada Ya Kukashifiwa na Vera Sidika

Msanii wa muziki kutoka Kenya Otile Brown ameamua kumuanika mrembo mpya kwenye ukurasa wake wa Instagram siku chache Baada ya sakata lake na Ex Wake Socialite Vera Sidika.

Wiki iliyopita Vera aliweka screenshots za maongezi yake na Otile Brown ambapo ndani yake alimtuhumu kwa kutomrudhisha chumbani kwa madai kuwa alikuwa hamfikishi wanapokuwa sita kwa Sita.

Baada ya tuhuma hizo nzito Otile alijitetea na kusema Vera alikuwa anapenda sana ngono kiasi ya kwamba alikuwa anajichezea mwenyewe hata pale wanapokuwa wamelala wote ambapo Vera alisema anafanya hivyo kwa sababu hakuwa akimridhisha Kama mwanaume.

Lakini siku chache Baada ya sakata hilo na Vera Otile Brown ameonekana kuendelea na maisha yake ambapo ameweka video kwenye ukurasa wake wa Instagram unaomuonyesha akiwa na mrembo mwingine ambapo kwenye video wanaoenekana wakikumbatiana na kucheza kimahaba.

 

 

 

Vera Sidika na Otile Brown Wathibitisha Kurudiana

Socialite maarufu kutoka Kenya Vera Sidika ‘Queen Vee’ na mpenzi wake Msanii wa muziki Otile Brown wamethibitisha kkurudiana baada ya kuachana mapema mwezi jana.

Vera na Otile walikuwa Kwenye Mahusiano kwa Miezi michache lakini walianika Penzi lao Kwenye mitandao ya kijamii kwa sana na hata Vera kuwa video queen Kwenye moja ya video za nyimbo ya Otile.

Wawili hao walitangaza kumwagana mwezi iliopita huku kila mmoja akimnyooshea kidole mwenzake kama kuwa chanzo cha Penzi lao kuvunjika.

Tetesi za wawili hawa kurudiana zilianza kutawala siciao Media wiki hiii baada ya Vera na Otile kukutana Dubai, Lakini sasa kila mmoja amethibitisha Kurudiana baada ya kuposti Kwenye mitandao ya kijamii:

 

Lakini pia wawili hao wameweka video mbali mbali Kwenye mitandao ya kijamii zinazowaonyesha wakiwa wanakula bata Dubai na kuzima taarifa zote za kuachana.

https://www.instagram.com/p/BohEn_BAJAl/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=19ltzdl63wgvk

Otile Brown Akiri Kulikumbuka Penzi La Vera

Msanii wa muziki anayefanya vizuri nchini Kenya Otile Brown amefunguka na kukiri kumiss aliyekuwa mpenzi wake Socialite Maarufu Vera Sidika.

Otile alifunguka hayo Siku chache zilizopita ilipokuwa kumbu kumbu ya kuzaliwa kwa Vera Sidika.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Otile amemposti Vera na kumuandikia maneno mengi matamu huku akikiri kuwa Vera mkarimu na mtu mzuri na kuna wakati anakuwa anamkumbuka sana.

https://www.instagram.com/p/BoWPmfKny-T/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=buv5q7dlscik

 

Vera Sidika yupo Dubai ambako anakula  bata la Birthday yake hivyo hajamjibu Ex wake huyo.

Vera na Otile Brown waliachana mapema mwezi uliopita baada ya kuwa Kwenye Mahusiano kwa Miezi kadhaa huku kila mmoja akimtuhumu mwenzake kama kuwa chanzo cha kuisha kwa Penzi lao.

Vera Aibuka na Jamaa Mpya Siku Chache Baada Ya Kuachana na Brown

Socialite maarufu kutoka Kenya Vera Sidika ‘Queen Vee Bosset’ amedaiwa kuopoa mwanaume mwingine siku chache baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Msanii Otile Brown.

Vera na Otile Brown walimwagana siku chache zilizopita baada ya kila mmoja kumnyooshea kidole mwenziye kwa tuhuma za utapeli wa kimapenzi.

Siku kadhaa kupita baada ya kuachna na Otile Brown Vera ameonekana na jamaa mwingine ambaye hakutambulika kwa jina ambapo wawili hao walionekana wakiwa wanapata msosi katika mgahawa fulani jijini Nairobi.

Vera na Otile walimwagana huku chanzo kikieleza kuwa kila mmoja alikuwa akinufaika kwa upande wake. Inaelezwa kuwa, Vera alikuwa akimtumia Otile kutengeneza jina lake kuendelea kuwa juu wakati Otile alikuwa akimtumia kufanikisha muziki wake akimtumia kama video queen.

Vera Sidika Avunja Penzi Lake na Otile Brown

Socialite maarufu kutoka Kenya mwanadada Vera Sidika amefunguka na kuweka wazi kuwa ameamua Kuvunja Mahusiano Yake na aliyekuwa mpenzi wake Msanii wa muziki Otile Brown.

Vera ambaye amekuwa Kwenye Mahusiano na Otile kwa Miezi kadhaa ameweka wazi kuwa ameamua kuachana na mpenzi wake huyo kwa sababu aligundua alikuwa hampendi.

Vera ameandika kuwa Otile alimpenda kwa ajili ya umaarufu na hakuwa na mapenzi ya kweli kwake bali alimtumia kwa ajili ya kukuza idadi ya mashabiki zake.

Vera amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram:

https://www.instagram.com/p/Bmk3NAqgb1G/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=myiyclwvhz5h

 

https://www.instagram.com/p/Bmk3S6IAniJ/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=kikmqughw3ww

Vera Sidika na Otile Brown Wathibitisha Kuwa Wapo Pamoja

Socialite maarufu kutoka Kenya, Mrembo Vera Sidika na mpenzi wake ambaye ni msanii wa muziki Otile Brown wamezima tetesi zote za kuachana na kuthibitisha kuwa bado wapo pamoja.

Tetesi za wapenzi hao kuachana zilianza Mwanzoni mwa wiki hii baada ya wapendanao hao kufuta picha zao pamoja Kwenye mitandao ya kijamii na hata kuacha kufuatana Kwenye Instagram.

Lakini sasa wawili hao wanazima tetesi hizo na kuweka wazi kuwa hawako hata Kwenye mipango ya kuachana kwani siku ya jana Otile Brown ameachia wimbo mpya ambao kamuimbia mpenzi wake huyo.

Wimbo huo ambao unaitwa ‘Baby Love’ na ameimbiwa Vera ambaye pia ni video Queen Kwenye video hiyo ambayo mpaka sasa inafanya vyema kwenye mtandao wa Youtube.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera pia ameandika:

When bae sings for you and it melts your heart (literally) I love you baby @otilebrown you’re the best and OMG your voice! I know I say this all the time but damn papi!!!!Just can’t get enough ???? …you’re one special, talented human ?“.

 

Vera Sidika Kumpeleka Mpenzi Wake Brown Kwa Wazazi

Socialite maarufu kutoka pande za +254, Kenya Vera Sidika amedaiwa kuwa tayari kumpeleka nyumbani kwao kwa wazazi wake mpenzi wake Otile Brown.

Vera na mpenzi wake Otile Brown ambaye ni staa wa muziki kutoka pande hizo wamesemekana kuwa Kwenye Mahusiano kwa miezi kadhaa sasa na Vera yupo tayari wazazi wake wamuone mpenzi wake.

.

Kwa mujibu wa Mtandao wa SDE, Vera ambaye yupo katika uhusiano wa kimapenzi na Otile kwa zaidi ya miezi sita, anafanya hivyo ili mpenzi wake huyo aweze kuwatambua ndugu pamoja na familia zake alikokulia huko Jimbo la Magharibi ya Kenya. Katika safari hiyo, wawili hao wataongozana na mtangazaji wa redio maarufu, Jalang’o.

Lakini pia wawili hao wamezidi kuonyesha mapenzi yao ni mazito baada ya kuonekana wakienda hospitalini kwa daktari kupima virusi vya Ukimwi mara kwa mara.

Vera Sidika na Otile Brown Mapenzi Hadharani

Socialite maarufu kutoka nchini Kenya Vera Sidika amejikuta akimwagiwa mahaba na mpenzi wake ambaye ni mwanamuziki pia kutoka nchini humo anayeitwa Otike Brown.

Vera Sidika alijizolea umaarufu Afrika Mashariki kutokana na umbo  lake matata amejikuta akidondoka Kwenye penzi la kijana huyo.

Wawili hao wamekuwa Kwenye Mahusiano ya kimapenzi kwa muda sasa na wameonyeshana mapenzi katika sehemu mbali mbali za hadhara Ikiwa ni pamoja na kuweka picha zao za kimahaba Kwenye mitandao ya kijamii.

Lakini hivi karibuni Otile alianika kuuwambia ulimwengu mzima kuwa anampenda Vera kwani alimuoa Kwenye moja ya shoo zake na kumpa maneno matamu mrembo:

Nakupenda sana wewe mwanamke (Vera)… wewe ni kila kitu kwangu… na kinachonivutia zaidi kwako ni jinsi ulivyoumbika… niamini, nimewaona wanawake wengi lakini upo tofauti nao sana, wewe mvumilivu, una busara na mtu spesho”.