Babu Tale Afunguka Baada Ya Tetesi Za Kumtelekeza Hawa India

Meneja wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Babu Tale amefunguka baada ya maneno maneno kusemwa kuwa amemtelekza mrembo Hawa Said nchini India ambako anapata matibabu.

Wiki mbili zilizopita Babu Tale alimpeleka msanii Hawa kwa ajli ya matibabu nchini India baada ya kuifanyiwa vipimo na upasuaji mkubwa Babu Tale amerejea nchini siku chache zilizopita na kumuacha mgonjwa Nchini India.

.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Babu Tale alisema amerejea nchini na kumuacha Hawa India kwa kuwa msanii huyo anaendelea vizuri hivyo baada ya kushauriana na madaktari wake walimwambia asiwe na wasiwasi mgonjwa yupo sehemu salama hakuna ulazima wa yeye kuendelea kumsimamia muda wote.

Madaktari ndiyo walioniruhusu nirudi Bongo na wakanihakikishia hali ya mgonjwa wangu inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo hivyo hakuna ulazima wa mimi kuendelea kuwepo muda wote kama nitahitajika kwa lolote watanijusha.

Baada ya kupata kauli ya wataalamu hao nikaona nirudi nije kuendelea na mambo mengine huku nikiwasiliana nao kiukaribu zaidi”.

Hawa alipelekwa nchini India ambako walienda wakidhani ana ugonjwa wa ini lakini walikuta ana gonjwa wa moyo hii ni baada aliyekuwa mpenzi wake miaka ya nyuma msanii Diamond Platnumz kujitolea msaada huo.

Mama Diamond na Zari Wadaiwa Kuwa Ndani Ya Bifu Zito

Mama mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi. Sandrah au maarufu kama Mama Diamond amedaiwa kuwa kwenye bifu zito na mazi mwenzake na mwanaye mwanamama Zari The Bosslady.

Global Publishers wanaripoti kuwa kuna bifu zito linaendelea kati ya Zari na Mama Diamond huku mtu wa karibu na familia hiyo kuanika kuwa wawili hao waliingia kwenye mgogoro baada ya mama Mondi kubeba ujauzito.

Inaripotiwa kuwa Mama Mondi alipata ujauzito na kumueleza mkwewe huyo kuwa anahitaji daktari mzuri kutoka Afrika Kusini ili ahakikishe kuwa ujauzito huo hautoki kwani anahitaji kupata mtoto na mumewe Maisala Shante ‘Anko’ ili aifurahie ndoa yake.

Unajua kwa nini mama Mondi na Zari waliingia kwenye bifu akamchukia? Ni kwa sababu alimpa siri ambayo alikuwa hajamwambia mtu yeyote ya ujauzito wake yeye akamwambia meneja mmoja wa Diamond ambaye naye alimtania mama bila kujua kuwa ilikuwa ni siri”.

Aidha, mtoa habari huyo alisema kuwa baada ya Zari kumueleza meneja huyo bila kujua kuwa hakutaka mtu ajue na meneja huyo akamtania mama Mondi kuwa ni mama kijacho kitendo ambacho kilimkera ndipo bi’mkubwa huyo alipomchamba Zari.

Unaambiwa mama Mondi alimchamba Zari vibaya na bahati mbaya ujauzito wenyewe ukatoka kwani ulitoka hata kabla hajapata msaada aliokuwa anautaka”.

Baada ya tetesi hioz za bifu na Zari gazeti la Amani lilimsaka Mama Diamond ambaye alikana kabisa bifu hilo na mkwe wake na kufunguka;

Sina bifu na Zari mbona huwa nawasiliana naye kwa njia ya WhatsApp na mara ya mwisho amenitumia picha za watoto na kuhusu kumposti kwenye Instagram mbona tulishaacha kupostiana siku nyingi ndio maana sijamposti lakini hatuna bifu lolote“.

Mama Diamond alipoulizwa kuhusu taarifa za ujauzito alidai kwamba ameshezaa tayari na kwa sasa mtoto wake ameshakuwa mkubwa tuu.

 

Mwarabu Fighter Afunguka na Kueleza Alivyoteseka Kufanya Kazi Kwa Diamond

Bodyguard aliyejizolea umaarufu Bongo baada ya kufanya kazi kwa staa wa Bongo fleva nchini Diamond Platnumz, Mwarabu Fighter amefunguka na kuanika magumu aliyopitia kufanya kazi kwa Diamond.

Katika mahojiano aliyofanya na mtandao wa Bongo 5, Mwarabu Fighter amefunguka na kuanika mazingira magumu aliyopitia wakati anafanya kazi kwa staa huyo:

Nilikuwa nakatwa mshahara nikichelewa kwenye tukio siku unaenda kupokea mshahara unakuta hata laki na nusu hakuna halafu unakutana na kijikaratasi kikieleza na kukupa ufafanuzi kuwa siku fulani ulichelewa pia unakumbuka siku fulani?”.

Lakini pia Mwarabu Fighter ameweka wazi kuwa kuna baadhi ya siku za mapumziko alizokuwa anatakiwa apumzike nyumbani alikuwa anapigiwa simu aende kazini na kupewa dakika  kumi au kumi na tano.

Mwarabu Fighter ameweka wazi kuwa wakati anafanya kazi kwa Diamond aliishia kupata ajali ya pikipiki mara nne katika harakati za kuwahi kazini.

Babu Tale Aweka Wazi Hali Ya Hawa Baada Ya Upasuaji Wa Moyo

Meneja wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Babu Tale ambaye yupo nchini India kwa ajili ya kusimamia matibabu ya Msanii wa Hawa Said ameweka wazi kua anaendelea vyema baada ya upasuaji.

Hawa amefanyiwa upasuaji wa moyo chini ya madaktaru bingwa watano na sasa Babu Tale anasema Mrembo huyo amepata fahamu baada ya kufanyiwa upasuaji huo mkubwa.

Baada ya opersheni hiyo kufanyika Babu Tale ameandika:

 

Kassim Mganga-Tusionee Wivu Mafanikio Ya Diamond

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Kassim Mganga ameibuka na kumkingia kifua staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz na kuwataka watu wasimuonee wivu.

Diamond Platnumz anatajwa kuwa moja kati ya wasanii walioiweka Bongo fleva katika ramani ya kimataifa baada ya kufanya kolabo na Staa kutoka Naigeria Davido miaka Michache iliyopita.’

Mmoja kati ya wasanii ambaye amejitokeza na kumkingia kifua Diamond ni Kassim Mganga ambaye ameibuka na kuwataka Wasanii Wenzake na mashabiki kutomuonea wivu Diamond.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Kassim Mganga amefunguka haya kuhusu kipaji cha Diamond:

Tusimuonee wivu kwa sababu amefanikiwa sana, ila Diamond amebadilisha sana muziki wetu”.

Pamoja na kwamba Diamond sio mmoja ya wasanii ambao waanzilishi wa muziki wa Bongo fleva lakini anatajwa kuwa msanii ambaye amekuza na anaendelea kuikuza Bongo fleva.

Ndoa Ya Dogo Janja na Irene Uwoya Haijavunjika- Kassim Mganga

Msanii wa muzik wa Bongo fleva kutokea Tip Top Connection Kassim Mganga ameibuka na kudai ndoa ya staa wa Bongo fleva Dogo Janja na Mkewe Uwoya haijavunjika.

Kassim Mganga ambaye alikuwa mmoja kati ya watu wachache waliohudhuria ndoa ya Dogo Janja na Uwoya Mwaka jana mwishoni amesema hana taarifa ya ndoa hiyo kuvunjika.

 

Kwenye moja ya Interview alizofanya hivi Karibuni katika kituo kimoja cha habari Kassim amefunguka na kudai kuwa hajui kama Ndoa hiyo imevunjika kwa kuwa hajapata taarifa Rasmi.

Sina taarifa ya kuvunjika kwa ndoa kati ya Dogo Janja na Irene Uwoya ninachojua bado wako pamoja mpaka hivi sasa”.

Lakini pia Kwenye Mahojiano hayo Kassim amewataka watu wasimuonee wivu Diamond kwa ajili ya mafanikio anayoyapata kwani kiukweli amebadilisha sana muziki wa Bongo fleva.

Rommy Jones Adai Mwanamke Pekee Anayemfaa Diamond ni Zari

Kaka wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Rommy Jones ameibuka na kudai mwanamke pekee  anayemfaa mdogo wake ni Mpenzi wake wa zamani na mzazi mwenzake Zarinah Hassan ‘Zari’.

Mahusiano ya Diamond yameendelea kutengeneza headlines Kwenye mitandao ya kijamii hasa sasa kutokana na warembo wawili ambao ni Kim Nana na Lynn kuonekana kugombani Penzi la staa huyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Rommy Jones, amefunguka kuwa mke pekee ambaye anamfaa mdogo wake huyo ni mzazi mwenziye Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’.

Nasema ukweli ndani ya moyo wangu, Zari ni mwanamke ambaye anafaa kuwa mke na kuwekwa ndani kwa sababu anajielewa na anasimama kama mama kuanzia kwenye ulezi wa watoto wake na kila kitu ndani ya nyumba”.

Rommy amesema anatamani Zari awe shemeji yake wa maisha na ikiwezekana wafunge ndoa kwani ana kila sifa ya kuwa mke na ndiye mwanamke pekee anayeweza kumuweka sawa mdogo wake na akaenda kwenye njia sahihi.

Unajua kila familia ingependa sana kuona mtoto wao anapata kitu kilicho bora, yaani mke ambaye anaweza kusimama vyema kama mama hivyo mimi leo nikiamka Diamond aniambie anamuoa Zari, nitafurahi sana kwa sababu najua atakuwa amepata kilicho bora kabisa”.

Lakini pia Rommy hakusita kuwaongelea Lynn na Kimnana ambapo amesema;

Unajua Diamond kwa hao (Lynn na Kim Nana) ni kama tu zile za mwanaume kutenda kosa na kuchepuka nje, lakini akawa na msimamo na mwanamke wake, kwa hiyo kwa hao siwezi kumuongelea sana kwa sababu pia sisi hata siku moja hatukai na kujadiliana naye mambo yake ya kimapenzi, ila ukizungumzia mke, basi nitakuambia ni Zari tu”.

Babu Tale Afungukia Matibabu Ya Hawa Nchini India na Ugonjwa Unaomsumbua

Meneja wa Msanii mkubwa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Babu Tale amefunguka na kutaja ugonjwa unaomsumbua Msama Hawa na kudai sio ini kama ilivyoaminika hapo Mwanzoni.

Wiki iliyopita Babu Tale aliondoka na Hawa kwa ajili ya kwenda kufanyiwa matibabu nchini India baada ya Diamond kujitolea msaada wa zaidi ya Milioni 450 kwa ajili ya matibabu yake.

Babu Tale ametoa taarifa kuwa  Hawa atafanyiwa upasuaji wa moyo jioni ya leo Lakini pia Wataalamu wameangalia kila kitu na hawajaona tatizo kwenye Ini kama iliyokuwa inaripotiwa awali.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Babu Tale ameandika:

Asante Mungu tumefika salama India na tumefanya vipimo vyote upya salama na jibu lililotoka kwa wataalamu kwa asilimia 95% awajaona tatizo linalohusiana na ini kwa mgonjwa ila ni moyo ndio uliokua unapelekea mgonjwa kujaa maji mwilini ivyo basi kutaitajika kufanyika upasuaji mkubwa ambao utakua na uangalizi mkubwa wa wataamu then wametuakikishia baada ya hapo mgonjwa atapata nafuu na inawezekana izo 5% zilizobaki itakua poa na tatizo la ini alitokuwepo kikubwa tunaomba mtuombee dua na msiache kumuombea pia @diamondplatnumz apatenguvu ya kuendela kumsaidia kwa maana kutoa ni moyo. Kikubwa sana naomba tumuombee Hawa coz anaingia kwenye upasuaji mkubwa na hii ni atua ya yeye kua salama. Mungu tusimamie”.

 

Mume wa Mama Diamond Kwenye Skendo Nzito na Mke Wa Mtu

Maisala Shante ambaye ni Mume halali wa Mama mzazi wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Bi Sandrah amejikuta katika skendo nzito na Mke wa mtu.

Global Publishers wanaripoti kuwa Wamenasa SMS za Shamte ambazo alikuwa anachati na mwanamke ambaye anaaminika kuwa mke wa mtu na kuibua maswali juu ya ukaribu wao ilhali wote wapo kwenye ndoa.

Mwanamke ambaye anadaiwa kuwa mke wa mtu alikuwa anachat kimahaba Lakini pia inadaiwa Kwenye meseji hizo walikuwa wanatumiana picha kudhihirisha mambo yamekolea.

Gazeti la Risasi lilimsaka Mwanamke huyo ambaye alikataa kabisa tetesi za Mahusiano na Shamte na kufunguka haya:

Nimekuambia simu yangu ilipotea, unachoniambia mimi sikikumbuki kabisa kama niliwahi kuchati na huyo mwanaume chochote, lakini pia kama nitakuwa nimechati naye kuna ubaya gani, si mwanaume kama wanaume wengine“.

Baada ya mwanamke huyo kubanwa na kufunguka hayo, Risasi Jumamosi lilimtafuta Shamte ambaye alidai kuwa hana tabia za kuchati na wanawake.

Nakuheshimu kama mwandishi kukujibu swali hili, mimi sijawahi kuchati na wanawake ovyo, kama una namba ya huyo mwanamke nitumie ndio nitakujibu“.

Shamte ni mume halali wa Mama Diamond, walifunga ndoa mwaka jana na baada ya ndoa hiyo kukazuka ‘vijineno’ ikiwemo madai kuwa mwanaume huyo ni marioo na ndoa yao haitadumu. Hata hivyo, wawili hao wameendelea kuwa pamoja na kuwafanya watu waamini kwamba, kweli mapenzi hayachagui umri, kikubwa ni kuwepo kwa mapenzi ya kweli.

Mama Wema Afungukia Mahusiano Ya Wema na Diamond

Mama Mzazi wa staa wa Bongo Movie Wema Sepetu, Mariam Sepetu amefunguka na kuongelea uhusiano wa binti yake Wema na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Wema na Diamond waliwahi kuwa Kwenye Mahusiano ya kimapenzi kwa muda mrefu kwa miaka ya nyuma lakini tetesi za wao Kurudiana hazijawahi kuisha.

Katika interview aliyofanya na Gazeti la Amani, Mama Wema alifunguka mara baada ya mwanahabari wetu kumuuliza kama atakuwa tayari kupokea posa ya Diamond kama atajirudi na kuomba nafasi nyingine kwa bintiye, alisema wawili hao imebaki stori.

Wewee, sikiliza nikwambie bwana, Wema na Diamond kwa sasa wamebaki kuwa marafiki tu. Haiwezi kutokea tena wakarudiana. Mimi ndiyo namjua Wema vizuri, ana moyo wa aina yake ndiyo maana unaona pamoja na kuwa wameshaachana lakini bado wanakuwa karibu, wanashirikishana mambo yao kiroho safi.

Wema ana maisha yake sasa hivi, Diamond ana yake, kamwe hawawezi tena kurudiana“.

Hivi sasa itakuwa ngumu kwa Wema kurudi kwa Diamond kwani tayari Wema ana mpenzi wake ambaye amekwisha tangaza naye ndoa Lakini pia Diamond na yeye ana wanawake wake wengine.

Aikah Afunguka Kuhamia WCB

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Kutoka katika kundi la Navy Kenzo Aikah Marealle amefunguka na kuongolea taarifa za kuhamia WCB.

Baada ya kutoa hit single ambayo inaendelea kufanya vyema mpaka sasa ‘Katika’ waliomshirikisha Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz kuliibuka tetesi kuwa Nahreel na Aika wamehamia chini ya WCB.

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers , Aika  amesema kuwa, amekuwa akisikia kwa watu wengi juu ya kuhamia WCB mara baada ya kuachia wimbo wao  na Diamond jambo ambalo halina ukweli.

Yaani watu wengi wanasema nimehamia WCB lakini ukweli ni kwamba tuna meneja anayetokea huko anaitwa Sallam na amekuwa akitusimamia sasa sijui hayo mengine yanatokea wapi.

Nilikaa na mwenzangu tukatunga Wimbo wa Katika tukaona ni vizuri tukamshirikisha Diamond ndiyo ikawa hivyo sasa nashangaa hao wanaoungaunga maneno”.

Tetesi hizo za Kuhamia WCB zilipamba moto mara baada ya Msanii kutoka WCB Harmonize kusema wazi kuwa wasanii hao wanahamia Kwenye Label yao taarifa ambazo Navykenzo walidai ulikuwa ni utani.

Husna Ajaribu Bahati Yake Kwa Diamond

Mrembo ambaye aliwahi kufanya vyema Kwenye Mashindano ya Miss Tanzania 2011/2012 Husna Maulid ameibuka na kudai kuwa na yeye ni mmoja kati ya warembo wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Sakata hilo la Husna lilitokea siku chache zilizopita baada ya kuweka picha yake Instagram na kusindikiza na maneno ‘Roho Ya Simba’ na kuonyesha yupo Madale nyumbani kwa Diamond jambo lililosababisha mashabiki kumjia juu.

Mashabiki walimshambulia kwa kitendo cha kumuweka na yeye kwa Diamond ilhali anajua kwamba tayari ana wanawake kadhaa tayari Kwenye Mahusiano naye.

Baada ya povu hilo la mashabiki, Husna alifanya mahojiano na Global Publishers ambapo alimwaga povu kwa watu wanaosema anamtaka Diamond ambaye ni bwana wa Lynn.

Unajua kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, huyo Lynn ni nani, siwezi kumuhofia yeye wala mwanamke mwingine yeyote maana kila mtu na bahati yake, wanaotukana watukane watachoka”.

Hivi Diamond tayari amekwisha mmwaga Lyyn na Yupo Kwenye Mahusiano na Mrembo mwingine anayeitwa KimNana.

Lynn Amkana Diamond Baada Ya Kumwagwa

Socialite na Video vixen maarufu Kwenye mitandao ya kijamii Irene Godfrey maarufu kama Lynn au Officiallyn ameibuka na kudai hajawahi kuwa kwenye  uhusiano wa Kimapenzi na Diamond.

Lynn alijipatia umaarufu baada ya kutokea kwenye video ya wimbo wa Rayvanny ‘Kwetu’ lakini baada ya hapo amekuwa maarufu kwa kusemekana kuwa Kwenye Mahusiano na Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Wiki chache zilizopita Lynn alitrend Kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonekana mikononi mwa Diamond kama mpenzi wake kwa siku kadhaa na hata kudaiwa kumfanyia bonge la Birthday party na hata kumnunulia gari.

Lakini Penzi hilo halikuwa la muda mrefu kwani siku mbili baadae Diamond alionekana na warembo wengine wawili tofauti ikiwemo Tunda na Kimnana ambaye yupo naye mpaka leo.

Sasa Lynn anaibuka na kusema hajawahi kuwa Kwenye Mahusiano na Diamond na kudai ana mpenzi wake ambaye jana tu ametoka kumzawadia gari aina ya BMW.

Kwenye Interview yake na kituo kimoja cha habari Lynn amemwaga povu hili kuhusu Diamond:

Hakuna kitu sipendi kama watu wanao judge watu Kwenye social media na kuongea vitu ambavyo hawavijui kama wewe apo unaponiambia natoka na Diamond! Jamani mimi sipo na huyo mtu nina boyfriend wangu ambaye Nipo naye Kwenye relationship strong kabisa na muda wowote watu wanaweza kumjua”.

Siju za hivi karibuni Lynn alionekana katika vita ya maneno na wanawake kadhaa wa Diamond kama vile Hamisa, Kimnana na Tunda lakini bado anadai hamjui Diamond na hajawahi kuwa naye.

Zari Adaiwa Kutafuta Mwanasheria Wa Kumshughulikia Diamond

Mfanyabiashara maarufu Afrika Mashariki na mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari The Bosslady amedaiwa kutafuta mwanasheria kwa ajili ya kumsimamia mzazi mwenzake.

Tangu Diamond na Zari walipoachana mapema mwaka huu wamekuwa wakijaribu kutafuta njia bora ya kulea watoto wao wawili wadogo na mara kwa mara Zari amemtuhumu kwa kushindwa kutimiza majukumu yake kama Baba.

Global Publishers wanaripoti kuwa Zari mwanasheria kwa ajili ya kumsimamia Diamond ili awalee watoto wake katika misingi bora licha ya kuwa wameshatengana.

Chanzo cha karibu cha Familia hiyo kimeiambia gazeti la Ijumaa Wikienda kuwa Zari ni mwanamke ambaye yuko ‘siriaz’ na malezi ya watoto hivyo ameamua kumwekea mzazi mwenzake huyo mwanasheria ili aweze kuwajibika kwa asilimia mia moja bila kukosa hata jambo moja la msingi.

Unaambia siri ya Diamond kwenda Sauz (Afrika Kusini) kila mwezi ni baada ya kuwekewa mwanasheria huyo ambaye anamfuatilia kwa karibu ili kuhakikisha haendi kinyume na matakwa ya sheria.

Unajua hata akiwa na shoo vipi ameambiwa ajipange ili kutofautiana na ratiba za watoto na akifika nyumbani pale kwa Zari wanalala chumba tofauti ingawa siku nyingine anakwenda kulala hotelini”.

Baada ya taarifa hizo GPL lilimsaka Diamond ambaye alifungukia tuhuma hizo na kusema:

Waswahili nimewazoea sana tu, wasiponiongelea na Zari hawaoni sawa, mimi huwa nakuja huku kwa ajili ya kuwaona watoto wangu, natimiza majukumu kama baba, hayo mengine nawaachia wao”.

 

Irene Uwoya Amkwapua Bodyguard Wa Diamond

Muigizaji wa filamu za Kibongo Irene Uwoya ameonekana akiwa na Bodyguard maarufu Kwenye mitandao ya kijamii Mwarabu Fighter.

Mwarabu Fighter alijizolea umaarufu alipokuwa mlinzi binafsi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz lakini aliacha kazi kwake mapema mwaka huu baada ya kutibuana.

Uwoya ambaye amekuwa akitengeneza sana headlines Kwenye mitandao ya kijamii siku mbili hizi amerusha video iliyomuonyesha akiwa na Mwarabu fighter kazini.

Uwoya kuonekana na Bodyguard kama Mwarabu Fighter kumezidi kuzusha tetesi za kuwepo Mkono wa Kigogo ambaye anasimamia maisha ya gharama anayoishi Uwoya kwa hivi sasa.

Baadhi ya wasanii ambao wameonekana na walinzi wao binafsi katika siku Hizi za karibuni ni pamoja na Jacqueline Wolper na msanii wa Bongo fleva Barnaba Boy.

Baba Diamond- Natamani Diamond Angenialika Tandale

Baba mzazi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma maarufu kama Baba Diamond ameibuka na kudai mwanaye hakumualika kujumuika naye Tandale wiki iliyopita.

Wiki iliyopita Diamond aliongozana na Familia yake yote akiwemo mama Yake na dada zake pamoja na Familia nzima ya WCB katika charity event aliyofanya maeneo ya Tandale Maguniani.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Baba Diamond amefunguka na kusema anatamani angekuwepo kama sehemu ya kukumbuka maisha yao waliyoyapitia miaka ya nyuma akiwa na mwanaye huyo kwani historia aliyoitoa Diamond ilimgusa.

I wish na mimi ningekuwepo pale. Nilitamani kushuhudia pia mambo mazuri aliyoyafanya mwanangu maana awali nilidhani ni jambo dogo, lakini baadaye nikaona ni jambo kubwa sana.

Nilipofuatilia kwenye TV nikaona mwanangu anatoa Bajaj, anatoa bima, anatoa mikopo kwa akina mama, pamoja na bodaboda kwa kweli moyo wangu ulifurahi sana.

Ile ishu ya kuuza mitumba aliyoizungumza, hata mimi niliuza. Pengine pia ningeweza na mimi kuwatia moyo mamia ya watu waliofurika pale.

Nilisikia alisema amepanga kufanya kila mwaka hivyo bado naamini Mungu akitujalia uzima, ishallah mwakani anaweza kunialika kwani hakuna tatizo kati yetu”.

Diamond amekuwa hana Mahusiano mazuri na Baba yake kwa miaka mingi hii ilitokana na Baba Diamond kumtelekeza Diamond wakati mdogo na hivyo kulelewa na mama yake ambaye yupo naye karibu zaidi.