Harmorapa akana kumdiss Majani kwenye wimbo wake mpya

Rappa kutoka bongo, Harmorapa ameachia nyimbo mpya itwaayo Ajitokeze hivi karibuni lakini wimbo huo umezua ngumzo mitandaoni kwani Harmorapa anasemekana kuwa alimdiss aliyekuwa meneja wake wa zamani, P Funk Majani. Kwenye wimbo huo anaskikaa kisema;

“Nishakuwa mfagizi chini ya miti, nazijua kero za majani, maana majani hayafadhiliki, ndiyo maana sipatani na majani”

Hata hivyo Harmorapa amefunguka kuhusu ishu hii na kukana kuwa wimbo huo unamlenga Majani. Harmorapa alikiri kuwa Sasa hivi Majani sio meneja wake lakini hii sio sababu ya kumdiss kwenye wimbo Kama wengi wanavyodai.

“Ni kweli kwa sasa P Funk Majani siyo meneja wangu, ila siyo kweli kwamba nimemdiss kwenye ngoma yangu, kwa sababu hatuko pamoja kikazi ila bado tuna mahusiano mazuri na hatuna ugomvi, wala hajawahi kunitimua hizo ni fununu tu. Ngoma yangu ya Ajitokeze ni ngoma inayonizungumzia mimi, kwamba hakuna anayeweza kutokea akawa kama mimi na kama yupo basi ajitokeze, ila siyo dongo kwa Majani,”

Harmorapa amsifia Alikiba kwa kusema haya

Harmorapa ni msanii ambaye anaitambua kazi ya Alikiba na ingawa wawili hawa hawajapata nafasi ya kukutana…hii haimaniishi kuwa Harmorapa hatamani kufanya kazi na King Kiba.

Katika interview aliyoifanya hivi karibuni, Harmorapa alidai kuwa Alikiba ni msanii mwenye bidii na watanzania wanapaswa kuitilia kazi yake maanani kwa sababu Kiba anabusara kuwashinda wengi Wa kisasa. Harmorapa alisema,

Katika vitu ambavyo tunatakiwa kujivunia ni kuwa na wasanii ambao wanatangaza taifa letu mbele na kujivunia juhudi zao. Naimani heshima, busara na juhudi ndiyo nyenzo pekee wazungu kumwaga wino na kumkaribisha Alikiba meza moja na kumkabidhi kampuni kubwa ya Rockstar4000 kuwa mmiliki mmoja wapo na Director.

Rapa huyu wa Tanzania aliendelea kusisitiza kuwa wasanii wanafaa kujifunza na kujivunia uwepo wa Alikiba kwa kuwa muziki wa bongofleva ulitambulika zaidi baada ya Alikiba kuachia nyimbo zake za kwanza.

Wasanii wa Tanzania inabidi tujifunze na kujisifu kwa kuwa na King Alikiba maana anautendea haki mziki wetu wa bongo fleva, hongera zangu zizidi kutiririka kwa King wewe uliokosa mfano hapa bongo.

Huu ndio ujumbe ambao Harmorapa aliandika baada ya kupanda Ndege kwa mara ya kwanza

Harmorapa ni mmoja wa wasanii ambao hawakuwa na hella wala starehe kabla ya kuanza biashara ya muziki.

Kama msanii ambaye anaelewa shida za kutokuwa na hela, Harmorapa amekuwa mtu ambaye anajipanga ili asiziharibu hella zake na kwa sababu hii imemchukua muda kabla yeye kupanda ndege maishani mwake.

Hata hivyo hivi karibuni aliweka picha huku akiwa kwenye uwanja wa ndege. Kulingana na alichoandika, hii ndio ilikuwa Mara yake ya kwanza kupanda ndege na hangeweza kuificha furaha yake. Aliandika kusema…

“Maisha ni safari ndefu na mpangaji ni mwenyezi Mungu. Ukweli sikuwahi kuwaza katika maisha yangu kama ipo siku nitatimiza moja ya ndoto yangu ya kupanda ndege.
So ndugu zangu nawasihi ni mwiko kukata tamaa, omba Mungu sana atakutimizia ndoto zako. Shukrani #bossladySabuka kwa kunifikisha hapa nilipo, leo pia naomba Mungu ajalie aendelee kua na moyo huo wa kizungu maana kiukweli ni mzungu wa pekee.”

Je Harmorapa nimkali kuvaa kumshinda Dogo Janja?

Inaonekana Harmorapa anafurahia kuandikwa kwenye magazeti kila kichao. Kila wakati msanii huyu kutoka bongo ako kwenye mitandaoni kutafuta kiki lakini kwa sababu inamsaidia kupata pesa, basi Harmorapa hatawacha hadi afike anapotaka.

Wakati huu, Harmorapa ameamua kumuingilia Dogo Janja kwa kusema msanii huyu hawezi kuvaa vizuri kama yeye. Kulingana na Harmorapa kuwa yeye huvaa nguo kali kitu ambacho Dogo hawezi fikia.

Dogo Janja
Dogo Janja

Akizungumza kwenye interview Harmorapa alisema,

“Dogo Janja asijinadi sana kwenye kuvaa, mwambie tupo wanyamwezi kama sisi tunavaa pamba kali. Najua na yeye ni mkali wa kuvaa lakini mimi ni mkali zaidi kwenye hizo, kwanza angalia jinsi nilivyotupia leo, kinyamwezi,”

Harmorapa aliendelea kwa kudai kuwa Dogo Janja bado ni mtoto mkubwa mbaye anajaribu kufanya msmbo ya watu wakubwa.

“Akumbuke alianzia chini mpaka kufika alipo sasa” Harmorapa amjibu Afande Sele

Kwa sasa hakuna mtu ambaye hamjui Harmorapa kutoka Tanzania. Rapa huyu amekuwa kwenye mitandao kadhaa na wengi hupenda kuongelea nyimbo zake lakini Afande Sele hivi karibuni alidai kuwa hakuwa anamjua Harmorapa hadi liletokeo la Nape kushikiwa Bastola.

Afande Sele
Afande Sele

Maneno haya yanaonekana kuwa yalimuudhi muimbaji huyu ambaye amefunguka kupitia mahojiano yake na EATV. Harmorapa alisema kuwa yeye hana maneno mengi ya kusema lakini kwa sasa Afande Sele anapaswa kujua kuwa hakuna mtu anayeanzia juu kwani pia yeye alianzia chini ndipo afike alipo sasa.

“Niseme tuu yeye kwanza mwenyewe akae chini na kujua na kukumbuka kuwa alianzia chini mpaka kufika level fulani watu wakamkubali.”

Aliendelea kusema,

“Ajue mimi kama Harmorapa sina maneno mengi ila kazi zangu ndiyo zitakuja kumuelekeza kuwa Harmorapa uliyekuwa unamuongelea ndiyo huyu kupitia kazi yangu ndiyo itakuwa imemnyoosha au vipi? na ku’prove ukali wa Harmorapa.”

Huyu ndiye mrembo mpya wa Harmorapa? (Picha)

Kuna uvumi kuwa Harmorapa amepata mrembo mpya ambaye amewaacha wengi wameduwaa kwa muonekano wake.

Harmorapa
Harmorapa

Harmorapa ambaye anajulikana kupenda kiki hata hivyo hajazungumzia jambo hili kwani kwa sasa anajitahidi kusambaza wimbo wake mpya, Nundu aliyoiwachia jana.

Kulingana na picha ambazo zinasambaa mitandaoni rappa huyu wa Bongo amekuwa akionekana na mrembo huyu kitu ambacho kimewafanya wengi kumfikiria kuwa wanatoka pamoja.

Hata hivyo sio siri kuwa rapa huyu anakimbizwa na wanawake ambao wanatamani maisha yake ya sasa. Angalia picha ya mrembo huyo akiwa na Harmorapa hapa:

Harmorapa
Harmorapa

Harmorapa aeleza sababu za kutomiliki bastola kama wasanii wenzake

Ni kweli kuwa Harmorapa anatisha wasanii wenzake ambao amewaonyesha kivumbi muda mfupi baada ya kuwa staa maarufu Tanzania.

Sasa hivi anapesa zake na anamiliki gari kubwa lakini bado hajafikiria kumiliki bastola yake kwa kuwa ana ulinzi wa kutosha. Alizungimza katika kipindi cha Dj Show cha Radio One, Harmorapa alieleza kuwa bado hajafikiria kuwa na bastola kwakuwa ana personal bodyguard ambaya hutembea na yeye kila mahali aendapo.

“Sasa hivi nina pesa nyingi, nina gari nini. Lakini sijawaza au kufikiri siku nije kumiliki bastola kwa sababu eti nina pesa sijawaza kwa muda huu ila sijajua huko mbeleni iatkuwaje,”

Aliendelea kwa kusema kuwa ulinzi alionao hauwezi kubali mtu amkaribie. Kulingana na yeye bodyguard wake ameshiba tosha na ndio maana haoni haja ya bastola.

“Nikisema kwaajili ya kujilinda unajua sasa hivi mimi nina bodyguard wangu ameshiba na ameenda hewani. Hata ninapokaa kwenyewe nina ulinzi mpaka umfikie Harmorapa kuna kazi kubwa sana na unaweza usionane naye,” ameongeza.

Huyu ndiye msanii wa Kenya ambaye Harmorapa anataka collabo naye

Harmorapa anamipango ya kutamba nchini Kenya na kwa sababu hii amemtaja msanii ambaye amekuwa akitaka kufanya kazi naye kwa muda sasa.

Akizungumza na Bongo 5 msanii huyu ambaye anafanya vyema nchini Tanzania alisema kuwa anamkubali Prezzo na anaipenda kazi yake. Aliweza kueleza kwa sasa msanii ambaye angependa kufanya at least project moja na yeye nchi za Afrika Mashariki ni Prezzo peke yake.

Prezzo
Prezzo

“Prezzo namkubali sana toka kitambo, tokea niko chini shule ya msingi. Nilikuwa namkubali sana swagga zake na rap zake zilikuwa zinanifurahisha sana na zinanifurahisha mpaka kesho kiukweli.”

Aliendelea kusema iwapo atapata nafasi, Afrika mashariki itaweza kuona collabo yake na Prezzo. Lakini kwa sasa anangoja nafasi hii ikitokeze na kwa kiukweli ataweza kuifanya Tanzania proud.

“So kwahiyo natamani sana one day nifanye naye collabo kwahiyo kama nikipata nafasi kufanya naye itakuwa very good nitashukuru Mungu,”