Picha Za Brown Wa Wolper Akiwa Na Mwanamke Mwingine Zavuja

Imekuwa kama mtindo sasa kwa baadhi ya wasanii nchini na watu maarufu kuvujisha picha za utupa au wakiwa faragha na wapenzi wao.Picha zimevuja katika mtandao wa kijamii wa Instagam zikionyesha mwanaume ambae yupo katika mahusiano na msanii wa bongo movies na mjasiriamali maarufu Wolper  Jackline anaejulikana kama Brown zikimuonyesha akiwa na mpenzi mwingine tofauti na Jackline.

Picha hizo zimeleta gumzo kwa sababu wawili hao wanaonekana wapo faragha ilhali mashabki wa Wolper na mwanamitino huyo wanajua kuwa brown ana mahusiano na jackline na sio mtu mwingine yoyote.

Hata hivy wawili hao kuna kipindi cha nyuma ilisemekana kuwa walikuwa wamegombana kutokana na wawili hao kutokupostiana katika mitandao ya kijamii lakini walikuja wakakanusha na kusema kuwa hawajaachana, sasa swali linakuja kuwa je picha hizi zinaweza kuwa ni uthibitisho kuwa sasa hawapo pamoja tena?

Wolper akiwa na mpenzi wake Brown

Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa wasanii wa bongo kuwa wanaachia picha chafu katika mitandao ya kijamii bila kujali ni nani anaangalia picha hizo.Hata hivyo hakuna aliyefunguka  kitu chochote tangu picha hizo kuvuja katika mitandao ingawa mashabiki wao wanaonekana kukerwa na tabia hizo.

 

 

Wolper:Sio Kila Msanii Atapenda Ukifanya Biashara

Wasanii wengi bongo wamekuwa wakijiingiza katika biashara hasa ya mavazi na urembo kwa ujumla, Jackline Wolper nae ni mmoja wapo ambapo amekuwa akiuza nguo na urembo kwa watu mbalimbali lakini kitu anacholalamika Wolper ni kwamba wasanii wamekuwa sio watu wanaokuja sana katika duka lake kwa ajili ya kupata huduma anazotoa wakati alikuwa akitemegea kuwa wasanii ni moja ya watu wake wa karibu ambao walitakiwa kuwa  wateja wake wakubwa katika biashara hiyo.

Jackiline anasema kuwa wasanii ni watu wenye wivu sana ni bora wakanunue kitu kwa gharama kubwa zaidi kuliko kwenda kwa wasanii wenzao wakati wakijua kabisa kuwa wanakuwa wanawafaidisha wasanii hao, na anachokisema Jacky ni kuwa wengi wao wanakuwa wanawakomoa.

Wolper aliendelea kwa kusema kuwa tangu ameanza kuwa na biashara hiyo ni wasanii watatu au wanne tu ndo wamekuwa wakienda kwake kwa ajili ya kuhudmiwa , ilhali biashara kama yake haifanywi na wasanii wengi .

Unapofanya jambo lolote la maendeleo kwa sisi mastaa sio kwamba kila mtu atakuwa anapenda au anafurahi unavyofanikia.Wengi wananuna na kwaio ndio maana hawaji kukusapoti. Alifunguka Jacky

 

Brown Aongelea Mahusiano Yake Na Wolper

Kulitokea tetesi nyingi hivi karibuni kuhusu mahusiano ya msanii wa bongo movies Jackline Wolper na mpenzi wake Brown ambae alifuta picha za Jacky zote baada ya kusemekana kuwa alichukizwa na kitendo cha Jacky kwenda katika birthday party ya Diamond Platinumz na kukutana na mpenz wake wa zamani Harmonize.

Akiongea na Friday Nite Live ya EATV, Brown ambae ni video model  anafunguka na kuongelea mahusiano yake na msanii huyo wa kike wa bongo movies na kusema kuwa Jacky ni mwanamke pekee ambae alishawahi kumpenda na bado ataendelea kumpenda daima na wala hana mpango wa kumuacha.Brown akisema kuwa Jacky ni mwanamke ambae amepitia mambo mengi tangu ameingia katika sanaa na tangu ameanza kuwa maarufu hivyo, maswala madogo madogo ambayo mpaka sasa yanaendelea katika mitandao na maneno anayozushiwa ni ya kawaida kwa sababu alishawahi kukutana na makubwa zaidi ya hayo.

Hata hivyo Brown alisema kuwa meseji zilizovuja hivi karibuni zikimuonyesha Jacky anachat na mpenzi mpya wa Harmonize sio za ukweli hata kidogo kwasababu hata yeye alipoangalia meseji zile alijua kuwa ile haikuwa charting ya mpenzi wake. ‘Zile meseji si zake, sio Jacky kabisa mimi najua mwandiko wa mwanamke wangu,yaani hata kama mtu akichukua simu ya Jacky akachart na mimi ninakuwa najua kabisa huyu sio Jacky’

Brown alifunguka na kusema kuwa kati ya wanawake kumi alikuwa nao tangu aanze mahusiano ,Jacky bado anampa namba moja na kutaja baadhi ya mambo ambayo yanamfanya amuweke Jacky katika nafasi iyo aliyataja pia kuwa ni “Nampenda sana Jacky nae ananipenda sana, kwanza ana heshima ni tofauti  na wanawake wengine ukimwambia kitu atakujibu weweeeee..,pili Jacky ni mcha mungu sana , familia yake ni ya dini na familia yangu ni ya dini pia.

Akiendelea kuongea, Brown alikana tetesi za watu kusema kuwa pamoja na kuwa Jacky yupo na yeye lakini yupo mwanaume mwingine mwenye fedha anaemuhudumia Jacky kifedha na kusema kuwa wao wamependana hivyo wanachojari ni mapenzi na wala sio kingine”kama alikuwa anafanya hivyo ni  kwa wanaume waliopita lakini sio kwangu maana ye mwenyewe anajua nini ninampa

Jackline Wolper Ampa Shavu Harmonize

Kwa jinsi ambavyo Wolper na Harmonize walivyokuwa wakitupiaa maneno katika mitandao ya kijamii inakuwa ni vigumu kuamini kuwa leo hii Wolper anaweza kumsapoti Harmonize kwa kitu chochote, lakini hali imekuwa tofauti kwa mwanadada huo ambae ni msanii mkubwa wa tasnia ya filamu nchini lakini pia kwa sasa amekuwa akijihusisha na ujasiriamali wa nguo  jijini bongo.

Katika ukurasa wake wa instagram jana oktoba 17, Wolper ameshangaza mashabaiki wake wengi na kuwaacha na butwaa  baada ya kuposti video zaidi ya tatu ambazo zinamuonyesha akiimba na kucheza wimbo mpya wa mpenzi wake huyo wa zamani Harmonize wimbo ambao unaitwa Shulala, aliomshirikisha Koredo Bello msanii kutoka Nigeria huku chini akiandika caption ya kumsifia msanii huyo kuwa kibao icho ni kizuri,

haka kanyimbo kazuri sana  na video ndo usiseme!!Raaaj bhana umejua kunyoosha, kama bado ujaangalia video ya haka kawimbo pita  kwenye bio ya @harmonize _tz. #uliyemchokozakaja #shulala #naukinibipuTuNakupigia.” aliandika Jackline Wolper

Kitu cha kuhoji na kinachowashangaza wengi ni kwamba juzi tu zilivuja meseji zikionyesha Wolper akimwambia Sarah ambae ndie mpenzi mpya wa msanii huyo kuwa kama amemshindwa Harmonize  basi amuache yeye amrudie kwaio mashabiki wengi wameanza kutoa majawabu kuwa inawezekana Wolper kaamua kufanya kweli na kumrudia Harmonize.

Jackline Wolper na Harmonize ni moja ya couple iliyo-trend sana mjini kipindi cha nyuma na kuwaaacha watu wengi midomo wazi wa sababu Harmonize alikuwa na umri mdogo kuliko Jacky, lakini kutokana na mapezi waliosema kuwa nayo hawakuona tofauti yeyote,baadae Jackline na  Harmonize walikuja kutengana na kusababisha wawili hao kutupiana maneno ya matusi mitandaoni.,huku sababu ya kuachana kwa wawili hao ikitajwa kuwa ni baada ya Harmonize kupata mwanamke mwingine wa kizungu ambae alikuwa akimpa ela nyingi Harmonize.

Ugomvi wa Harmonize na Wolper ulisababisha mpaka Harmonize kuingia studio na kumtungi Jacky wimbo ambao uliongea mambo mengi yaliyohusu mahusiano yao yaliyopita, ukiachia hapo Sarah ambae ni mwanamke wa Harmonize pia alikuwa akigombana sana na Jacky kwa sababu ya Harmonize.Hata hivyo Jacky ndo kashaamua kumpa shavu Harmonize , hatujui kama ni kiki au anataka tu kumuumiza roho mwanamke mwenzie.

 

Penzi La Jacky Na Brown Matatani Tena

Msanii wa Bongo Movie Jackline Wolper na mpenzi wake Brown wamejikuta wakiaanza kuongelewa tena katika mitandao kuhusu mahusiano yao ambayo yana dalili za kuonekana kuvunjika, wawili hao ambao walikuwa wakiandamwa kwa muda mrefu katika mitandao huku baadhi ya mashabiki wakimtukana Jacky kuhusu umri mdogo wa mwanaume aliyenae.Hata hivyo kwa muda sasa Jacky amekuwa akimkingia kifua mpenzi wake huyo na kujibu tuhuma zote zinazomuhusu ikiwa hata kutukana mashabiki zake ilimradi tu kumuweka mpenzi wake huyo katika hali ya usalama.

Wikiendi iliyopita kulikuwa na shamrashamra nyingi kutokana na mfululizo wa sherehe za msanii mkubwa Diamond Platinumz kutimiza kadhaa, sherehe ambazo zilihudhuliwa na baadhi ya watu maarufu nchini.Hata hivyo katika kilele cha sherehe hizo zilizzofanyika katika ukumbi wa Hyatt Regency Jackline Wolper alikuwa ni mmoja wa wasanii walioalikwa katika party hiyo ,lakini swali  ni kwanini Jacky hakutokea katika shughuli iyo na mpenzi wake huyo mpya.

Hata hivyo kuna picha zilizosambaaa mitandaoni , zinazomuonyesha msanii huyo wa kike wakisalimiana kwa kupeana mikono na mpenzi wake  wa zamani Harmonizee, inasemekana kuwa baada ya picha hizo kusambaa mpenzi mpya wa Jacky(Brown) alifuta picha zote za Jacky katika kurasa zake  za instagram.Swali linakuja je, kuna nini kinaendelea kati ya wawili hao, je ni kweli wameachana kutokana na wivu wa picha ya Jacky na Harmonize?Au ugomvi wao ulikuwa kabla ya hapo?

Akijibu tuhuma hizo, kupitia U Head ya XXL  ya Clouds Tv, Jackiline Wolper alipoulizwa kuhusu kufutwa kwa picha zake katika instagram ya mpenzi wake alijibu kuwa yeye hajui chochote taarifa hizo ndo anazipata muda huo,'”Kumbe kafuta, mimi sijaingia instagram,mi sijaona soudy huwezi ukaamini, izo taarifa ndio unanipa wewe” aliongea Jacky katika simu

Hata hivyo Jacky alipoulizwa sababu za mpenzi wake huyo kutokuudhulia katika party hiyo alisema kuwa , mpenzi wake huyo sio mtu wa kuudhuria katika party , huwa hapendi sana na mpenzi wake huyo ni siku ya tano sasa anaumwa kichwa pamoja na malaria , na hata hivyo yeye kutokea katika ile party ni kwa sababu ya heshima ya Diamond na sio vinginevyo.

kuhusu kufuta picha Jacky alisema kama amefuta ni kwa sababu maneno ya watu wamemfanya mpenzi wake huyo kupanick tu, lakini hawana ugomvi wowote.Lakini hata hivyo mpaka sasa Jackline Wolper amefuta picha zote za bff wake huyo na bff nae amemuacha kumfuata Jacky katika ukurasa wa instagram (unfollow)

Wolper na Harmonize ndani ya Bifu Zito

Mwigizaji wa Bongo movies Jackline Wolper na mpenzi wake wa zamani mwanamuziki kutoka WCB, Harmonize wamejikuta katika bifu zito baada ya kuingia katika vita ya kurushiana maneno mtandaoni.  Wolper na Harmonize waliachana miezi michache iliyopta kwa kile alichokidai Wolper kuwa Harmonize alimsaliti na kutembea na msichana mwingine anayejulikana kwa jina la Sarah, katika mahojiano aliyoyafanya Wolper hivi karibuni alielezea machungu aliyoyapata baada ya kugundua kuwa Harmonize anatembea na msichana huyo mwingine kwa ajili ya tamaa ya pesa.

Baada ya kukaa kimya bila kutoa maelezo yoyote siku ya leo Harmonize ameachia wimbo wake mpya unaojulikana kama “Nimechoka” wimbo aliomuimbia mpenzi wake wa zamani Wolper wimbo ambao alituma kwenye ukurasa wake wa instagram na ujumbe usomao:

“Naomba nikupe jukumu la kumtumia #EX wako ambae kila kukicha anakuzumgumzia tena kwa ubaya na kutengenezea mazingira ya chuki katika jamii na umwambie nimechoka”, “Tena mwambie asijekuwa anajidanganya eti unamuwaza…!!! Ni kwasababu umeumbwa na stara hunaga uropo ropo wa kuongea vya ndani pia unaweza kung’oa mkali zaidi yake”.

Wolper naye kwa kupitia ukurasa wake pia alimjia juu Harmonize na kumrushia maneno:

“…Tusilazimishane kuongea nimeshaachana na wewe kiusalama ongelea vilivyopo kwako saivi sio mimi, Nilishatokaga huko kirahisi unaweza ukadeal na style yako ya mziki bila kunihusisha maana unampa hofu pia BFF anahisi labda kuna kitu kumbe hakuna, usiniharibie mahusiano yangu mapya , BFF wangu ni bora kuliko wewe ni adimu na sitaki kumpoteza kwa ajili ya watu kama wewe…Mimi ni Jackie Wolper ambae siwezi kuacha kuongea ukinianza namaliza kwa wale wanaosema bora kunyamaza subirini yawakute alafu mjipe huo ushauri”.

Harmonize na Wolper tangu wameachana kila mtu ameendeelea na maisha yake kwani Wolper ana mpenzi mpya anayejulikana kama Brown na Harmonize yupo na mpenzi wake mpya Sarah lakini tangu wameachana wawili  hao wamekuwa wakirushiana vijembe vya hapa na pale huku kila mtu akimtuhumu mwezie kwa kutokuwa mwaminifu kwenye mapenzi yao.

Baada Ya Kimya Kirefu, Wolper Afunguka Chanzo Cha Kuachana Na Harmonize

Ikiwa ni zaidi ya miezi mitatu kupita tangu penzi la msanii wa bongo movie na mjasiriamli jackline wolper na msanii wa bongo fleva harmonize kuvunjika, wolper aamua kufunguka kuhusu chanzo cha wao kuachana,wolper anasema kwa muda mrefu alikuwa kimya huku watu mitandaoni kila mmoja akisema lake kuhusu wawili hao.Ikumbukwe kuwa ni muda mfupi tu tangu kuachana kwao ,wawili hao kila mmoja alianza kujirusha na mpenzi mpya bila kujali mahusiano yao yaliyopita huku wolper akikiri kabisa kuwa mahusiano yake na harmonize ndio mahusiano yaliyovunjika na kumuuma sana kuliko yote, ikiwa ni mahusiano yake ya nne.

Akiongea katika mahojiano na mwanahabari millard ayo ,wolper anasema sakata lilianza siku ya kumbukumbu yake ya kuzaliwa ambapo yeye alikuwa  Burundi kikazi  na mpenzi wake huyo wa zamani alipost picha yake katika ukurasa wake wa instagram na kumsifia sana lakini cha kushangaza baada ya siku mbili picha ile ilifutwa na alipouliza aliambiwa wanatafuta kiki ya wimbo mpya, wimbo ambao unakwenda kwa jina la  “happybirthday” ulioimbwa na harmonize kwa ajili yake”nimefuta baby nataka tutengeneze kiki ,unajua kuna wimbo mpya nimekuimbia” wolper asimulia.

Hata hivyo wolper anasema kuwa kipindi icho chote harmonize alikuwa tayari ameshaanza mahusiano na mwanamke mwingine anaejulikana kwa jina la sarah, mwanamke ambae alikuwa anamkataza harmonize kupost kabisa picha za jacky mitandaoni, mwanamke yule alpoona wolper anazidi kumpost harmonize mtandaoni alijua kuwa bado hawajaachana ivyo sarah aliamua kumtafuta wolper”mwanamke alikuwa hataki kudanganywa ,alichofanya akanitafuta,alichukua namba yangu ya ofisi instagram”  asimulia wolper. Kipindi icho mwanamke yule alikuwa ameshawatafuta na kuwatumia picha baadhi ya watu wangu wa karibu ikiwepo mdogo wangu, na hata alipomfikia wolpre mwenyewe alimwambia aachane na harmonize maana tayari yuko na mwanamke mwingine”unajua wewe ni kama unajichoresha,endelea na maisha yako,harmonize ana mwanamke na wanategemea kuzaa”  jacky aendelea kusimulia

Hata hivyo Jacky anasema kuwa pamoja na kwamba yeye kingereza  kinampiga chenga lakini cha Sarah kilikuwa kina kona sana,akimaanisha mwanamke mpya wa harmonize hakuwa na kingereza kilichoonyooka.

Wolper aeleza kinachomfanya kunona sana

Watu wengi wanadai kuwa kula kwingi ndiyo kinacho sababisha Jackline Wolper kuongeza uzito. Kuna ata wale ambao wanasema mwigizaji huyo wa filamu za Bongo havutii tena.

Nini haswa kinasababisha mwili wake Wolper kuwa mnene? Wolper mwenyewe amekiri kuwa pombe ndiyo inayomsababishia unene.

“Unajua sikuwa mnywaji na nilikuwa nikiichukia pombe sababu nikinywa ndio napata hamu zaidi ya kula chakula kingi, hivyo kwa sasa nimeanza harakati za kurudisha mwili wangu wa mwanzo uliokuwa ukinionyesha vizuri kwa mashabiki wangu na pia nipo kwenye harakati za kuachana na unywaji wa pombe,” Wolper alieleza.

 

 

 

Msanii kutoka Wasafi Harmonize azungumza mara ya kwanza kuhusu uhusiano wake na Wolper

Msanii Harmonize juzi alikuwa kwenye Clouds fM na alizungumzia mambo mengi kuhusu wimbo wake na sana sana kuhusu uhusiano wake na Wolper.

Harmonize aliulizwa na Mami baby kama ilikuwa kiki au nini baada ya kudaiwa kuachana na Wolper na ukaribu wao kurejea leo wakati anaachia wimbo wake mpya.

Harmonize

“kuna vitu vilitokea tukajikuta hatuko sawa lakini Mungu ndio mwenye kheri tukawa tupo pamoja tukajua kabisa kuwa hiki kitu Jack hakipendi au mimi ila sasa hivi kila kitu kinaenda sawa na Mapenzi yetu sio ya kiki, nafasi yetu kwenye jamii imefanya ionekane kuwa ni kiki nilianza naye nikiwa sina hata gari”  Harmonize alieleza.

Alihakikisha lakini hawakuwa pamoja;

“Ukiona mtu anatumia nafasi yako kuvuma ni jambo la kumshukuru Mungu, sikatai yupo kwenye miahangaiko atatoka, Mungu amjalie najua wote tunatoka kwenye familia za kimaskini ni wakati wake sasa kuonyesha alichojaliwa” Alimtakia Wolper kila la heri.