Paschal Cassian Amshukuru RC Makonda Kufanikisha Safari Yake Ya India

Mshindi wa shindano la Bongo star  search (BSS) mwaka 2009 Paschal Cassian ambaye yupo hoi hospitalini Muhimbili kutokana na ugonjwa wa miguu amepata pesa ya kwenda India Kwa ajili ya matibabu.

Siku ya jana Msanii Mrisho Mpoto ametibitisha kuwa tayari mipango yote ya kwenda kumtibu Pascal Cassian nchini India imekamilika licha ya kwamba Pascal amejikuta akipata changamoto ya Passport ya kusafiria.

Katika mahojiano aliyofanya na Millard Ayo, Paschal Cassian amemshukuru RC Makonda kwa mchango Wake katika kufanikisha safari yake ya kwenda India.

Namshukuru mkuu wa Mkoa Makonda kwa kulibeba hili jambo kama la mtoto wake wa damu lakini changamoto niliyonayo kwa sasa sina Passport mimi na mke wangu, nina omba kwa RC Makonda na Rais Magufuli najua anaona so naomba sana kwa hii serikali pendwa inayosaidia wasiojiweza wanisaidie mimi na mke wangu kusudi niweze kusafirishwa”.

RC Makonda Ampa Milioni 5 Mama Yake na Godzilla

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda amesema atampa pesa kiasi cha Tsh milioni tano, mama mzazi wa aliyekuwa Rapa wa Bongo, marehemu Golden Jacob Mbunda ‘Godzilla’ ili zimsaidie katika kuwatunza watoto wa marehemu.

Godzilla alifariki ghafla Wiki iliyopita Baada ya kuugua ambapo ameacha familia inayomtegemea ikiwemo Mtoto Wake na Mama yake mzazi.

Makonda alisema hayo  Jumamosi, Februari 16, 2019 katika Uwanja wa Salasala wakati akitoa salam za pole kwa familia, ndugu na wasanii kwa kuondokea na msanii huyo aliyeaga dunia usiku wa kuamkia Februari 13, mwaka huu.

Ndugu yetu alikuwa na mipango wa kumsaidia mama yake kiuchumi, akawa amempa milioni nne lakini akawa na malengo ya kumpa milioni tano  ili aweze kuanzisha famasi kama sehemu ya kujitengemea kiuchumi.

Nitampa mama mzazi wa marehemu Godzilla kiasi cha shilingi milioni tano, nitampa Fid Q azilete kwa Mama Jumatano ili zimsaidie kuwatunza wajukuu na kufanya kile alichopanga baada ya kutumia pesa nyingi katika atibabu ya Godzilla”.

Mwili wa Godzila umezikwa jijini Dar Es Salaam katika makaburi ya Kinondoni. Mwenyezi Mungu Ailaze Roho ya Marehemu mahala pema peponi, Amina.

RC Makonda Awachana Wabongo Kisa Ommy Dimpoz

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda ameibuka na kuwajia juu Mashabiki wa muziki wa Bongo fleva ambao wamegoma kuonyesha sapoti kwa muziki wa Ommy Dimpoz Baada ya kuachia wimbo mpya.

RC Makonda akimtolea mfano msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz, amesema kuwa kuna watu kipindi msanii huyo anaugua, walikuwa wanatangaza amefariki dunia, leo amepona na ametoa wimbo wake mpya wa kumshukuru Mungu watu hao wamekaa kimya kama hawajui.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Makonda ameandika ujumbe huu mzito:

Ukitaka kujua watu walivyo wa Ajabu tazama leo, Ommy dimpo alikuwa mgonjwa sana na ikafika hatua ya watu kutangaza Amekufa. Leo amerejea tena akiwa na wimbo wa kumshukuru Mungu wamekaa kimya Kama vile siyo wao waliokuwa wana post kumwombea apone. Angefariki tungeona mitandao yote imechafuka RIP Ommy oooh umeenda bado tunakuhitaji. Unafiki huu sijuwi utaisha lini, tunapenda kutangaza msiba kuliko Uponyaji”.

 

Harmonize Ajibu Tuhuma Za Makonda Za Kuvuta Bangi

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutokea katika Label ya WCB, Harmonize amefunguka na kukiri tuhuma zlizotupiwa na mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda kuhusu kuvuta Bangi.

Wiki iliyopita RC Makonda alimtuhumu Harmonize  kwamba huwenda akawa anatumia bangi baada ya kuonekana akivuta sigara yenye moshi mzito katika moja ya video ambayo aliiweka mitandaoni.

Katika hali ya kujitea Harmonize ameibuka na kukataa kabisa tetesi hizo na kusema wazi kuwa moshi ambao umeonekana kwenye video za Instagram ulikuwa moshi wa sigara na sio wa Bangi.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize alijibu tuhuma hizo kwa njia za utani akilihusisha na suala la Simba kufungwa goli 5 na Al Alhy ya Misri.

WAKATI MWINGINE TUACHENI UTANI TUWENI SERIOUS …!!! HIVI MIE NILIEJIPOST NA MIMOSHI YA SIGARA TENA SIGARA EMBASY HIYO BANGE YENYEWE NAISIKIA KWENYE BOMBA…!!! NA HAWA WACHEZAJI WA @SIMBASCTANZANIA
NANI WAKUSOKOMEZWA NDANI TUKITUA BONGO…???? ??? HEBU ANGALIENI WANAVOTESA WATU WASIOKUWA NA HATIA ?
MINAZANI TUNGEANZA NA @HAJISMANARAKWANZA AKAMATWE ACHUNGUZWE….!!! ??”.

 

“Harmonize Akitua Tu Tanzania Akamatwe Apelekwe Jela”-Makonda

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda amefunguka na kutaka msanii wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize achunguzwe na kama anatumia bangi basi Akamatwe na aswekwe rumande.

Mheshimiwa Paul Makonda ameagiza vyombo vya usalama kumchunguza msanii Harmonize kama anatumia bangi au lah! ili achukuliwe hate za za kisheria.

Makonda amezungumza hayo siku ya jana  Alhamisi Januari 31, 2019 wakati akizungumza na wasanii katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam. Amesema katika mtandao wa Instagram ameona picha ikimuonyesha Harmonize anayetamba na wimbo Paranawe akivuta kitu hicho hivyo ameomba ichunguzwe kama ni bangi au lah

Nimemuagiza Gavana wa huko achunguze ile ni bangi au nini na ikigundulika ni bangi atakapotua tu hapa ni pingu na kupelekwa lock up, Vizuri namlea mwenyewe na mtoto anapokosea lazima umshikishe adabu bila kujali unampendaje”.

 

RC Makonda Aagiza Harmonize Akamatwe Kama Anavuta Bangi

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda ameagiza Msanii wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Harmonize Akamatwe kama atakutwa na hatia ya kuvuta bangi.

Makonda ameyasema hayo siku ya jana katika mkutano Wake aliyofanya na wasanii mbali mbali wa Bongo fleva na Bongo Movie ambapo amekemea matumizi ya madawa ya kulevya.

Makonda ameweka wazi kuwa serikali inafanya kazi kubwa ya kupambana na matumizi ya madawa ya kulevya na hivyo haitawavumilia watu ambao watasika kujiingiza huko.

Makonda ameweka wazi anataka Harmonize achunguzwe kama anatumia bhangi kama anavyoonekana kwenye pich zake kwenye Mitandao ya kijamii na kama kweli basi Akamatwe awekwe Ndani.

Picha za Amber Ruty Zinaleta Joto”-Rc Makonda

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam , Paul Makonda amefunguka na kuwataka wasanii wote kutumia mitandao ya kijamii vizuri na kuitumia kwa ajili ya manufaaa ya tanzania na sio vinginevyo,

Rc Makonda amefunguka na kusema kuwa kwa wasanii wana nafasi kubwa sana ya kutangaza  utalii wa tanzania na kila kitu kinachoptakina ahuko na sio kuweka picha za ajabu ambazo pia zinavunja maadili ya watanzania.

Akiongea mbele ya waziri mkuu Khassim Majaliwa pamoja na waziri wa maliasili na utalii Khamis Kigwangala , Rc Makonda amefwaomba viongozi kuwatumia wasanii katika kutangaza utalii lakini pia wasanii pia wazitumie nafasi hizo ipasvyo.

niwaombe wananchi wa dar watumie nafasi walizonazo kutangaza utalii wetu wa Tanzania, wasanii wenye wafuasi wegi watumie kutangaza utalii wa watanzania pia ili Dunia ijue kile kilichopo tanzania kuliko kusambaza picha chafu mtandaoni kama za Ambr Rutty zinazoleta laana na joto.

 

 

RC Makonda Atangaza Kumaliza Bifu na Ruge na Uwepo Wake Fiesta

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda ametangaza rasmi kumaliza Bifu lake na Mkurugenzi wa Clouds Fm Ruge Mutahaba na kutangaza kushiriki katika tamasha la Fiesta.

Siku ya jana kuna taarifa zilitoka kwamba Ruge Mutahaba anaumwa hoi na hivi sasa yupo nchini South Africa  kwa ajili ya matibabu.

Baada ya kuwepo Bifu la siku nyingi kati ya Makonda na Ruge hatimaye RC Makonda ameonekana kuweka tofauti zao pembeni na kuungana na Clouds Fm ili kukamilisha Fiesta.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Clouds Tv, RC Makonda ameelezea mahusiano yake kwa sasa na Boss wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba ambapo amesema wamekuwa karibu kama mtu na kaka yake.

Ruge ni kaka yangu, na nikwambie hivyo nilivyompata Keagan (mtoto wa RC makonda) ametunga wimbo maalumu kwa ajili ya Keagan. Unafahamu kama alivyokuwa India (Kwenye matibabu)  Mimi nilikuwa na wasiliana nae?. Unafahamu kuwa alishawahi kuja nyumbani kumuona mtoto?. Unafahamu kuwa alishawahi kuja nyumbani kwa ajili ya maombi? Ruge ana watoto… Fiesta nitakuwepo na itakuwa kubwa kuliko”.

Lakini pia Mhe. Paul Makonda amethibitisha kuwa hata yeye atahudhuria kwenye fainali ya Tamasha la Tigo Fiesta, itakayofanyika katika viwanja vya Leaders Jumamosi hii.

Diamond Awatupia Kijembe Clouds Fm Baada Ya Kumgeukia RC Makonda

Msanii wa muziki wa Bongo fleva na Mkurugenzi wa  WCB Diamond Platnumz ameibuka na kuwatupia kijembe Clouds Fm Mara Baada ya kumgeukia RC Makonda.

Sakata la Wasafi Festival na Fiesta limeendelea kupamba moto ambapo inaonekana live kwamba kila mmoja anataka apige tamasha kubwa kuliko mwenzake.

Kwa muda mrefu kumekuwa hakuna maelewano kati ya pande hizo mbili kwaiyo ilivyotokea uwezekano wa kuwepo tamasha kwa siku moja lakini katika Mikoa tofauti.

Diamond Platnumz amewarushia kijembe Clouds Fm kwa kusema wameomba poo kwa mlezi wao akimaanisha Paul Makonda Baada ya kuonekana akilitangaza tamasha hilo na kuwataka watu wajae siku ya tukio.

Inafahamika kwamba mlezi wa Wasafi ni mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Mkonda hivyo baada ya jana Clouds kumtumia Makonda katika moja ya video akiongelea inshu ya Ruge na kwamba yeye mwenye atakuwepo Fiesta imekuwa habari nyingine tena.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond ameandika:

Aunty Lulu Aunga Mkono Operesheni Ya Makonda

Msanii wa filamu za Bongo movie Lulu Semagongo maarufu Kama Aunty Lulu ameibuka na kudai anaunga mkono jitihada za mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda za kupambana na Mashoga.

Wiki mbili zilizopita Mheshimiwa Paul Makonda alitangaza rasmi vita na Vijana wanaofanya Mapenzi ya jinsia moja maarufu Kama Mashoga katika mkoa wa Dar Es Salaam.

Katika mahojiano yake na Global Publishers, Aunty Lulu amedai amefurahishwa mno na hatua aliyoichukua Makonda kwani naye ni mmoja wa mastaa waliokuwa wakiishi na mashoga, lakini Mungu akamuokoa na kuachana nao hivyo zoezi hilo litasaidia kwani mashoga hao wamesababisha hata wanawake wasiolewe.

Ninampongeza sana Makonda maana hawa mashoga ni janga la kitaifa, naomba akishawakamata wakipimwa na kugundulika wanafanya ufuska huo, wakusanywe kwenye uwanja mkubwa wachapwe viboko baada ya hapo ndiyo wapelekwe gerezani kwa sababu wanawake tunakosa kuingia kwenye ndoa kwa sababu yao”.

Lakini pia Aunty Lulu alimuomba Makonda azungumze na Rais John Pombe Magufuli ili msako ufanyike kwa nchi nzima kwani mashoga wengi wamekimbia jijini Dar na kwenda mikoani.

RC Makonda Atoa Tamko la Jela Kwa Amber Rutty na Atangaza Vita na Mashoga Wote

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda ametoa tamko rasmi kuhusiana na video cahfu za mrembo Amber Rutty na mpenzi wake lakini pia kuhusiana na ongezeko la mashoga katika jiji la Dar es Salaam.

Kwenye mahojiano na waandishi wa habari, RC Makonda ameweka wazi kuwa Amber Rutty na mpeniz wake wapo lupango muda huu wakati wanasubiriwa kupandishwa kizimbani na kuweka wazi kuwa adhabu yao ni kifungo cha jela;

Tayari yule binti anaitwa Amber Rutty pamoja na bwana yake wapo chini ya polisi tangu kipindi kile nilivyotoa maelekezo na niseme kuwa kosa lile liko wazi na sheria inasema ni aidha kifungo cha maisha au miaka 30 hiyo yote ni kuonyesha ni jinsi gani serikali isivyopendezwa na mienendo inayomomonyoa maadili ya taifa letu”.

Lakini pia Rc Makonda alitangaza vita na mashoga wote ambao wanajihusisha na shughuli za kufanya mapenzi kinyume na maumbile;

Naomba nitoe fursa hii kwa wakazi wa Dar es Salaam namba yangu ya simu inafahamika nimepata taarifa kwamba kuna mashoga wengi sana kwenye mkoa wetu na mashoga hawa ndio kazi yao wanajinadi kwenye mitandao ya kijamii kwaiyo nawaambia wananchi kama kuna shoga yoyote unamfahamu leo mpaka jumapili napokea taarifa za kupatikana kwao”.

 

Rc Makonda Amtetea Wema Kuwa Tanzania Sweetheart Amtaka Mobetto Awe Buguruni Sweetheart

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Mh. Paul Makonda ameibuka na kumkingia kifua Muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu na kusema analistahili Jina la Tanzania Sweetheart na sio Hamisa Mobetto.

Kwa wiki chache zilizopita Wema Sepetu amekuwa akifanya interviews mbali mbali na amekuwa akibainisha kuwa yeye ndiye Tanzania Sweetheart na sio Mobetto kama mashabiki zake ambavyo wamekuwa wakilazimisha.

Siku chache zilizopita akiwa katika Birthday Bash ya Wema iliyofanyika katika viwanja vya Mlimani City, Makonda aliweka wazi kuwa Wema ndiye Tanzania Sweetheart pekee ila kama wengine wanalitaka hilo Jina wanaweza kuwa Buguruni Sweetheart.

Wema ni Tanzania Sweetheart kwa sababu kuna vigezo, na kwanza hujiiti Jina mwenyewe, watu wanakupa Jina kama alivyopewa na Baba yake na mama yake Jina Tanzania Sweetheart wengine wanaweza kuwa Buguruni Sweetheart sio dhambi au Manzese Sweetheart”.

Vita kali ya Jina la Tanzania Sweetheart ilianza baada ya mashabiki Mtandaoni kusema wanamvua Jina hilo Wema na kumpa Mobetto kwa sababu Wena amepoteza umaarufu wake na kuwachukiza mashabiki zake kwa matendo yake ya mitandaoni.

RC Makonda Amtaka Majizzo Afunge Ndoa na Lulu Haraka

Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda amefunguka na kumtaka mkurugenzi wa EFM, Majizzo afunge ndoa na msanii Elizabeth Michael haraka iwezekanavyo la sivyo atamfunga.

RC Makonda amefunguka hayo Kwenye mazungumzo na waandishi wa habari kwenye tamasha la Komaa Concert jana jijini Dar es salaam, ambapo amesema kuwa kutokana na imani yake hataki kuwaona marafiki zake wanakuwa mabachela na kuahidi kuwafunga jela endapo watakiuka ahadi zao za kuoa.

Marafiki zake aliwataja na kuwataka waoe mara moja ni pamoja na Majizzo, Leo Mutuz, Meya wa Kinondoni na kuhaidi kuwafunga endapo hawatafanya hivyo.

Nina ndoa kubwa tatu lazima nizisimamie na wasipooana nawafunga, moja ni Majizzo unajua mimi ni mkristo kwenye Biblia inasema wengine wataokolewa kwa moto. Sasa Majizzo tayari yupo kwenye mipango na binti yangu Lulu wameshakuja nyumbani tumeshafanya vikao vingi vya kupanga harusi.

Lakini kuna harusi nyingine ya Meya wa Kinondoni nimemwambia na yeye asipooa namfunga. Lakini kuna Lemutuz naye asipooa namfunga. Kwa hiyo kuna watu watatu hawa lazima mipango yao ya harusi ikamilike mwaka huu na waoe”.

Tangu Lulu atoke jela Kumekuwa na tetesi kuwa yeye na mpenzi wake Majizzo wapo katika mipango ya kufunga ndoa na hata Makonda alikuwa wa kwanza kutangaza Ndoa hiyo.

 

Hili ndilo jambo RC Makonda alipiga marufuku kutokea jana, 6th April 2017 pale Dar es Salaam

Wasanii na wasambazaji wa filamu Tanzania walitua kwenye ofisi ya RC Makonda wakiwa na malalamiko mengi. Walidai ya kwamba hawanufaiki na kazi zao za filamu kutokana na kuwepo kwa maharamia wanaoziiba kazi hizo kwa kuzi-download kisha kuzisambaza kimagendo kwa bei ya kutupa bila ridha yao na zikiwa hazina stempu ya mamlaka ya mapato.

Kwa hilo RC Makonda alichukua hatua hapo hapo kupiga marufuku kuanzia Alhamisi hii tarehe 06 Aprili, 2017 uuzwaji, uingizwaji wa filamu za nje ambazo hazina stika za TRA ndani ya mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha alisema baada ya siku kumi ofisi yake kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kanda Maalum wataendesha msako wa kuwakamata wote watakaokuwa wamekiuka agizo hilo.

Akiongea na waandishi pamoja na wasanii hao, Mh Makonda aliwaagiza watu wa bodi ya filamu kufanya tadhmini ya haraka kubaini ni maduka mangapi yanayouza mikanda ya filamu jiji Dar es Salaam ndiposa aweze kuchukua hatua inayotakikana.