Baada ya Wema Kunimwaga Nilichanganyikiwa- Idris

Mshindi wa Big Brother 2014 na mchekeshaji maarufu Idris Sultan amefunguka kwa mara nyingine kuhusiana na mahusiano yake maarufu na Mrembo Wema Sepetu. Idris na Wema walikuwa kwenye uhusiano kwa muda na kuachana mapema mwaka jana wamekuwa kwenye vichwa vya  habari mara kwa mara na hata baada ya wao kukiri kuachana kwao mashabiki wao wamekuwa wakiwaomba warudiane.

Idris na Wema waliachana mara baada ya kutangaza kuharibika kwa ujauzito wa Wema  uliokuwa na miezi michache ambapo baadae walikuja kuweka wazi kuwa ujauzito ule ulikuwa wa mapacha wawili wa kike. Huku wakiwa hawajaweka rasmi sababu ya wao wawili kuachana watu wengi kwenye mitandao ya kijamii walitunga ya kwao.

Katika mahojiano aliyafanya Idris hivi karibuni aliweka wazi kuwa Wema ndio aliyemuacha yeye yaani “alimwaga” na kumuacha ambapo alifunguka kuwa kile kitendo kilimuumiza sana na kumfanya aumie sana na kufikia hatua ya kutembea na wasichana wengi ili mradi ajaribu kumsahau Wema, ambapo alitembea na wanawake zaidi ya thelathini (30) ili ajaribu tu kuziba pengo lililoachwa na madame na aweze kumsahau na kuendelea na maisha yake.

Idris amefunguka na kusema kuwa sasa wamekuwa washkaji tu huku wakisapotiana katika mambo mbalimbali kama yeye alivyoenda kwenye uzinduzi wa filamu yake ni kwasababu ni marafiki wa karibu na sio wapenzi tena.

Ujumbe wa Wema baada ya Manji kuachiwa huru

Jana Septemba 14, kulizagaa stori mitandaoni na vyombo vya habari vingi kuhusu kuachiwa huru kwa mfanyabiashara maarufu nchi bwana Yusuph Manji,kesi hiyo iliyokuwa ikiendeshwa katika mahakama ya Kisutu jijini Dar Es Salaam  jana ilifika ukomo baada ya Manji kuwekwa huru, mrembo wa shindano la Miss Tanzania 2006 na msanii  mkubwa na mkongwe wa Bongo Movies  Madam Wema Sepetu alioneshwa kufarahishwa na tukio ilo la kuachiwa kwa mfanyabiashara huyo na kuamua kuposti picha katika ukurasa wake wa instagram na kuand ika machache yanayoonysha shukrani na furaha “Alhamdullilah” aliandika Wema, Wema ameonekana kufurahishwa na jamba ilo kwa sababu kwa muda sasa mfanyabiashara huyo amekuwa hakiangaika na kesi iyo mhakamani.

Manji na wenzake watatu walikuwa wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wa nchi kwa zaidi ya miezi sita sasa  ambapo walikutwa na mabunda  35 ya vitambaa vya kutengenezea nguo za jeshi  zenye thamani zaidi ya sh. milion 190 , wameachiwa huru jana baada ya mwendesha mashtaka wa mahakama ya Kisutu jijini Dar Es Salaam  kuamua kufuta  kesi iyo.

Katika kuonyesha hisia zake Madam  Wema  Sepetu amekuwa ni mtu anayepost picha za Manji karibia kila mara huku akiandika maneno ya kusikitisha au kumtia moyo mfanyabiashara huyo kuhusu kesi hiyo kwa muda mrefu sana ,kwa mfano mwezi February mwaka huu,  baada ya Manji kupata dhamana ya kesi  na kuachiwa huru Wema alipost katika ukurasa wake wa instagram na kuonyesha kushukuru na kufurahia jambo hilo.

Katika mahakama hiyohiyo pia Wema bado anakabiliwa na kesi yake ya madawa ya kulevya ambayo mara ya mwisho ilisikilizwa wiki hii na bado itaendelea kusikilizwa mahakamani hapo.msanii huyu wa kike amekuwa akifanya vizuri katika tasnia ya filamu kwa sasa na hivi karibuni ametoa filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Heaven Sent’ aliyoshikirikisha wasanii wenzie wengine akiwemo msanii wa kuime anaefanya vizuri kwenye game pia Gabo Zigamba , movie iyo iliyozinduliwa hivi karibuni imepokelewa vizuri na mashabiki.

Shaidi kesi ya Wema Sepetu aongea

Ikiwa ni muendelezo wa kesi inayomkabili tanzanian sweetheart wema sepetu iliyokuwa inasikilizwa leo tarehe 12 septemba,msanii huyo amefika mahakamani na kusikiliza kesi yake.kesi iyo ambayo bado imekuwa ikionekana kuwa na utata katika kupokea ushahidi leo tena shaidi amefunguka kuhusu kile walichokikuta walipoenda kupekuwa nyumbani kwa msanii huyo.

Shaidi huyo aliyejulikana kwa jina la Inspekta wille ameiambia mahakama ya hakimu mkazi kisutu kuwa walikuta msokoto wa bangi katika kabati la vyombo  nyumbani kwa wema sepetu , shaidi huyo anasema kuwa walipofika nyumbani kwa wema walimkuta mdada wa kazi wa nyumba hiyo, ivyo wakaomba kuonana na mjumbe wa nyumba kumi.’Mjumbe alifika na tukamwambia tunataka kukagua nyumba  iyo ili kutafuta dawa za kulevya’

Shaidi huyo aliendelea kwa kusema kuwa walianza kukagua na kwenda jikoni ambapo  walikuta msokoto mmoja  wa bangi juu ya kabati pamoja na  lizra, shaidi huyo anasema kuwa baada ya kumaliza kukagua jikoni walienda chumba cha nguo cjha wema ambapo pia walikuta msokoto mwingine unaozaniwa  pia kuwa ni  msokoto wa bangi.

Shahidi huyo anaongezea pia kuwa hata baada ya kukagua chumba icho waliingia chumba cha wadada wa kazi ambapo huko pia walikuta msokoto mwingine wa bangi amabao unaonekana kuwa ulishatumika ukiwa ndani ya kiberiti, na baada ya hapo walisaini hati ya ukamataji na kumkatama wema kumpeleka kituo cha polisi  lakini muda wote huo wa ukaguzi shahidi anasisitiza kuwa walikuwa sambamba na mdada wa kazi kama ambavyo wema mwenyewe alivyoomba.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo vielelezo husika vilitakiwa kukabidhiwa kwa mahakama na shahidi lakini wakili mtetezi wa upande wa pili alikata   na kudai vielelezo vina mapungufu baadhi, hata ivyo kesi iyo bado inaendelea.

Ikumbukwe kuwa wema ni mmoja wa wasanii ambao walikumbwa na sakata la kukutwa na madawa vya kulevya aina ya bangi nyumbani kwake kipindi vita vya madawa ya kulevya ilipoibuka tanzania, kesi ambayo iliwakumba wasanii wengi ,lakini wengine walishamaliza kesi zao .

Wema Sepetu akesha akimlilia Tundu Lissu

Tukio la kushambuliwa na kupigwa risasi kwa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambaye ni wakili na Mwanasheria mkuu wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  Limewaliza wengi ikiwemo staa wa Bongo movies, Wema Isaack Sepetu ambaye anadaiwa kukesha akilia hivyo kuibua sintofahamu kwa watu waliomzunguka kwa mujibu wa marafiki  wa karibu wa Wema wamesema kuwa taarifa hizo zilimchanganya hasa ukizingatia kuwa Lissu ni ndugu yake na pia ni waili wake katika kesi inayomkabili ya matumizi ya madawa ya kulevya. Baada ya Wema kupata taarifa hizo aliangua kilio usiku na mchana kutwa, mwishoni mwa wiki iliyopita alibadilisha staili ambapo alikuwa halii badala yake aliamua kujifungia ndania akimuombea kiongozi huyo . Wema alipoulizwa kama madai hayo yana ukweli wowowte alijibu:

“Hakuna kitu kilichoniumiza kama  hicho na bado kitaendelea kuniumiza hadi nione anko Lissu anaendelea vizuri kama mwanzoni”.

Mheshimiwa Lissu anasemekana kuendelea vizuri tangu asafirishwe kupelekwa Nairobi, Kenya kwaajili ya matibabu zaidi. Wema alijenga ukaribu na Lissu baada ya kuhamia Chadema mapema mwaka huu baada ya kukabiliwa na kesi ya kuuza na kutumia madawa ya kulevya ambapo pia Lissu alikuwa mmoja kati ya mawakili wake pia katika ukurasa wake wa instagram Wema aliandika:

“…Nini hiki jamani…??? Oh lord help my Uncle… If anything happens to him then nadhani wengi wetu vitatutokea maana hatutokaa KIMYA..!! Ni kutokaa kimya ndo kumempelekea haya yote kutokea.. Nimeikumbuka Tanzania tetu ya miaka miwili iliyopita…sio Tanzania hii isiyo na amani ..Am praying for my Uncle Lissu”.

Idris aeleza kwanini Wema Sepetu hakuenda kwenye uzinduzi wa viata vyake ‘SultanXforemen’

Idris alihudhuria uzinduzi wa filamu ya Wema Sepetu ‘ Heaven Sent’ ambayo ilifanyika Mlimani City takriban wiki moja hivi.

La kushangaza ni kuwa Wema Sepetu hakuhudhuria uzinduzi wa viatu vya Idria zinazoitwa ‘SultanXforemen’. Uzinduzi wa viatu hivyo uliudhuliwa na mastaa kadhaa akiwemo Iren Uwoya, Gabo,Selin, Mc Piilipili, Ally Rehmtullah,Quick Raka lakini Wema Sepetu hakuonekana.

Idris alidhibitisha kuwa alimualika Wema Sepetu kwa uzinduzi huo. Mchekeshaji huyo alifunguka na kusema kuwa alimpigia simu Wema ambaye alimpa sababu ya yeye kushindwa kuja kwa uzinduzi huo.

“Nilimualika Wema sema unajua nyie wanawake mambo yenu hivyo ameshindwa kuja ikabidi ni mpe ridhaa, wakati naongea naye kwenye simu alivyosema sitaweza kufika basi nikamjibu uliza kiatu,” amesema Idris.

 

Idris ajibu madai kuwa amerudiana na Wema Sepetu baada ya kuonekana pamoja Milimani city

Wema Sepetu na Idris Sultan waliachana mapema mwaka jana miezi michache tu baada ya mrembo huyo kupoteza ujauzito wake. Wema alikua amepachikwa mimba na Idris.

Jumamosi hii Agosti 26 Wema na Idris walionekana wakiingia Milimani city wakiwa pamoja. Staa hao wawili walihuduria uzinduzi wa filamu ya ‘Heaven Sent’ iliyofanyika Milimani city mall.

Wema Sepetu na Idris walivyo wasili Milimani City

Tokeo ya Wema na Idris kuingia ukumbini wakiwa pamoja ulizua madai kuwa wapenzi hao wa zamani wameamua kurudiana ndo sababu ya ‘kutangaza’ mapenzi yao hadharani.

Ata hivyo Idris alikana madai hayo alipohojiwa. Mchekeshaji huyo aliweka bayana kuwa kwa sasa hayupo katika mahusiano na mtu yeyote.

“Mimi siko na mtu yeyote kimahusiano, am single. Niliona amepost kuwa anataka date mie nikasema nampitia kwa hiyo sikuwa na haja ya kuomba date wala nini nikasema maana mzuri nampitia, kwa bahati nzuri nikakuta hamna mtu aliyempitaia huwenda waliokuwa anatolewa baru,” Idris alikiri.

 

Mahakama yatoa muelekeo kuhusu kesi ya Wema Sepetu kukutwa na bangi

Muigizaji wa filamu ya Bongo Wema Sepetu amerejea mahakamani leo Agosti 18 kwa kuskizwa kwa kesi ya yeye kukutwa na bangi inayomkabili.

Siku chache zilizopita wakili wa upande wa washtakiwa (Wema Sepetu na wenzake wawili walioshtakiwa kwa kupatikana na bangi) na wakili wa serikali walikua na mvutano kwasababu ya ushahidi mpya.

Soma pia: Kesi ya Wema Sepetu yazua mvutano mzito

Leo hakukua na mvutano wowote katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba alitoa muelekeo kuhusu kesi hio ya Wema Sepetu.

Hakimu huyo alisema kesi hiyo imehairishwa hadi Agosti 31, mwaka huu ili kutolewa maamuzi, na tarehe 12 na 13 Septemba kesi hiyo kusikilizwa mfululizo.

 

 

Kesi ya Wema Sepetu yazua mvutano mzito

Wakili wa Upande wa washtakiwa (Wema Sepetu na wenzake wawili walioshtakiwa kwa kupatikana na bangi) wamepinga ushahidi kutoka kwa Ofisi ya Mkemia Mkuu.

Kulikua na mvutano mzito katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salam Jumanne Agosti 15 baada ya wakili wa Wema Sepetu na wenzake walili kudai kuwa kuna baadhi ya vitu vimeonekana katika ushahidi kutoka kwa Ofisi ya Mkemia Mkuu ambavyo havikuwepo awali.

Upande wa washtakiwa ambao unaongozwa na wakili Peter Kibatala na Tundu Lisu ulipinga kauli ya wakili wa serikali Constantine Kakula kudai kuwa ushahidi huo upo lakini hakutamka kuwa ushahidi huo ulifungwa ndani ya bahasha

Wema Sepetu awatemea mate waliokuwa mashoga zake wa damu

Muna Alphonse ‘Muna’, Kajala Masanja na Wema Sepetu walikua marafiki wa dhati lakini warembo hawa walikosana na kila mmoja kuenda zake.

Wema amesisitiza kuwa hajawahi kuwakumbuka waliokuwa mashoga wake wa damu, hii ni baada ya madai kuwa staa huyo wa filamu za Bongo anawamiss rafiki wake.

Muna Alphonse

Akiongea na Star Mix, Wema alieleza kuwa hajawahi kuwakumbuka rafiki zake hao ambao huko nyuma walikuwa kama kumbikumbi.

“Sitaki kusema dhambi jamani sijawahi kuwamisi hawa watu (Muna na Kajala) kabisa naona kama niliwafuta kwenye kichwa changu maana najikuta kuna watu nawakumbuka lakini hao hapana,” alisema Wema.

Kajala Masanja

Wema Sepetu aeleza kwanini anapenda kuishi na wanaume mashoga nyumbani kwake

Wema Sepetu amefunguka kuhusu tabia yake ya kufanya urafiki na wanaume tata (mashoga) na ata kuishi nao nyumbani kwake.

Akiongea na Global Publishers, Wema alieleza kuwa anawapenda na anafurahi sana kutangamana na mashoga kwani yeye hana chuki nao kama watu wengine.

“Mimi sijui ni kitu gani lakini ninawapenda sana hao watu na ninafurahi sana kuwa nao maana hata mama alikuwa hapendi kabisa kuona wapo kwangu lakini sasa amewazoea na ninaona nao ni binadamu kama mimi,” Wema Sepetu alisema.

Mrembo huyo pia alifunguka kuhusu nia yake ya kutaka kufunga uzazi atimiapo umri wa 32 (kwa sasa ana 29) iwapo hatakuwa amefanikiwa kupata mtoto.

Wema Sepetu akiwa na ujauzito

“Ndiyo na tena safari hii nisipobahatika kupata mtoto hadi ninafikisha umri wa miaka 32 nitafunga kizazi,” Wema Sepetu alieleza.

 

 

Uchunguzi uliofanywa kwa mkojo wa Wema Sepetu unashangaza mahakama

Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilitoa majibu kuhusu uchunguzi uliofanywa kwa mkojo wa Wema Sepetu. Mrembo huyo na wenzake Angelina Msigwa (21) na Matrida Abbas (16) walishtakiwa kwa utumzi wa bangi, walishikwa na msokoto mmoja wa bangi mapema Februari mwaka huu.

Jana kesi ya Wema Sepetu inayoendelea katika Mahakama ya Kisutu ilichukua mkondo mpya hapo jana baada ya ripoti kutoka kwa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

Wema Sepetu akitoka Mahakamani

Elias Mulima kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali akisoma ripoti ya uchunguzi uliofanywa kwa mkojo wa Wema Sepetu. Mulima aliambia Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba, kuwa ripoti hio ilidhibitisha kuwa chembechembe za bangi zilipatikana katika mkojo wa Wema Sepetu.

Wakili wa Wema – Peter Kibatala hata hivyo alisema ripoti hiyo kutoka kwa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ulikua na upungufu mwingi wa kisheria.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu Thomas Simba alihairisha kesi hio ya Wema Sepetu hadi Agosti 4, mwaka huu.

 

“Wema Sepetu alitoweka” Haitham aeleza kwanini Wema Sepetu hakuonekana kwa wimbo wake ‘Playboy’

Haitham aligonga vichwa vya habari baada ya kutangazwa kuwa alimshirikisha Wema Sepetu kwenye wimbo wake mpya ‘Playboy’.

Lakini video ilipotolewa watu walipigwa na butwa kwani Wema Sepetu hakua kwenye video hio wala ata sauti yake haikusikika kokote.

https://www.youtube.com/watch?v=solY_OOnas0

Haitham sasa amefunguka kuhusu Wema Sepetu kutoonekana katika video yake. Akiongea na E-News ya EATV, mrembo huyo alisema Wema hakupatikana siku ambayo walikua wanashoot video yake.

Haitham hata hivyo hakueleza sababu zilizomfanya Wema Sepetu kushindwa kufika wakati walikua wanashoot video. Alisema kutoonekana kwa Wema katika video yake kulisababisha madhara kiasi.

“Na script ambayo tumefanya sasa inayoonekana kwenye video wasichana watatu ilibadilishwa fasta baada ya Wema kutokutokea kwenye video, so script ya mwanzo ambayo Wema alipaswa kuwepo aliandika yeye director na baada ya mabadiliko kutokea akabadilisha scrip. Kwa upande wingine yameathiri kidogo sio sana kwa sababu kuna baadhi ya mashabiki wa Wema walitamani kumuona kwenye video, kwa hiyo ameathiri kidogo kwa wale mashabiki walikuwa wanatamani kumuona,” amesisitiza, Haitham alisema.

 

“Nishajikubali hali yangu” Wema Sepetu aongelea hali yake ya kushindwa kupata mtoto

Wema Sepetu amepoteza ujauzito zaidi ya mara mbili; mara ya mwisho mrembo huyo kuwa na mimba alikuwa anatajaria kupata watoto mapacha.

Ujauzito wa Wema Sepetu hata hivyo ulipotea ghafla Februari 2016, alikuwa na mahusiano na mchekeshaji Idris Sultan wakati huo.

Soma pia: Idris aongelea uchungu wa mama kupoteza ujauzito mwaka moja baada ya Wema Sepetu kupoteza mapacha wao

Wema Sepetu alilazimishwa kuongelea hali yake ya kushindwa kupata mtoto baada ya kupigwa vita kwenye mtandao wa Istagram.

Muigizaji huyo wa Bongo Movies aliwakashifu kina dada wajawazito kwa kuonyesha picha za nusu utupu. Wema alimsifu muigizaji mwenzake Esha Buheti kwa kusitiri ujauzito wake.

“Mashallah Esha wangu… Staha hadi Raha…. Sijawahi Elewa Wanawake wakishaenda kwenye Maternity shoots kwanini wanataka sana wakae uchi…. This Is Very Beautiful my Darling…. Allah Bariq Tumbo lako ujifungue salama my love… Unajua navyokupenda…. Hii iende kwa wanaokaaga Uchi wakiwa wanapiga picha za Mimba Jamani… ??? @esha.s.buheti,” aliandika Wema.

Esha Buheti

Watu wengine walimshambulia Wema kwa kudai kuwa mrembo huyo alikua anawaonea wivu kina dada wajawazito kwasababu yeye alishindwa kupata mtoto.

“Yaani ni Hivi, Hakunaga Jipya Now Mwaweza nitukana nikashtuka… Maana mi mwenyewe nishajikubali hali yangu… Labda niulize tu, Niko peke yangu nilokosa mtoto au ambaye sijazaa…??? HAPANA…!! Soooooooo Back to The Main Point, Nilichosema na nitakachoendelea Kusema, MUACHE KUTUWEKEA MIPICHA YA MITUMBO YENU YENYE MSTARI WA UJAUZITO… Yaani inshort, Muache kupiga picha za UTUPU kwenye Maternity Shoot zenu…. @esha.s.buheti Nakupenda mama…. You are the Definition of Womanhood & Motherhood… Na unajua Utamaduni wetu nini unataka…. Haya Wazungu endeleeni na Uzungu wenu…. Tukaneni na hapa pia…. Eti u thought I would keep quite jus cause mmeniita Jina nilolizoea… So nisi speak my Heart… Y’all are Very Funny….!!!! ??? Allah akutangulie kipenzi changu…. Baby,” Wema aliwajibu walompiga vita.

 

Haitham aeleza faida ya kumshirikisha Wema Sepetu kwa wimbo wake – ‘Playboy’

Muimbaji Haitham alimshirikisha Wema Sepetu kwa wimbo wake mpya ‘Playboy’ ambayo alitoa siku mbili zilizopita.

Haitham amekiri kuwa amenufaika pakubwa na umaarufu wa Wema Sepetu. Akiongea na XXL ya Clouds FM, muimbaju huyo alisema kumshirikisha Wema kwa wimbo wake kumeongeza uzito wa jina lake.

“Toka nimetoa ngoma na Wema nimeona watu wamenipokea vizuri tena zaidi na zaidi lakini sio kwa sababu nimefanya na Wema pekee yake tu, kwa sababu ya muziki mzuri, watu pia wanasema muziki ni mzuri,” amesema Haitham.

Tazama wimbo wake hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=OCHVKnItJE0

Wema Sepetu ashirikishwa kwa wimbo mpya – ‘Playboy’ (Video)

Wema Sepetu ameshirikishwa kwa wimbo nyingine, Muigizaji huyo wa filamu za Bongo aliwai kushirikishwa na msanii Snura Majanga kwa wimbo unaoitwa ‘Shoga Yake Mama’.

Msanii Haitham kutoka Mj Records ametoa ngoma mpya inayoitwa ‘Playboy’ ambayo alimshirikisha Wema Sepetu. Mtayarishaji wa muziki kutoka Mj Records Daxo Chali aliambia Planet Bongo ya East Africa Radio kuwa alimtafuta Wema ili afanye kolabo na Haitham.

“Niliona wimbo wa Haitham unahitaji mtu nikafikiria nifanyaje, lakini wakati huo huo nilikuwa na mpango wa kuja kufanya wimbo ambao ningependa kuona Wema Sepetu anakuwepo, basi kwenye huu wimbo mpya wa ‘Play boy’ nikaona huyu humu atakaa. Nikaanza kumtafuta Wema Sepetu, kuna siku kweli akafika na kufanya. Wema Sepetu anajua sana kuimba watu wengi hawajui hilo, sema tu hizo ‘melody’ ndiyo zilimsumbua maana ni za kiswahili lakini zinaimbwa kama kifaransa lakini kwingine amenyoosha,” alisema Daxo.

Tazama wimbo huo – ‘Playboy’ hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=OCHVKnItJE0

“Shepu nilijaliwa nayo” Wema Sepetu aisifu umbo lake (Picha)

Mtoto kajaliwa umbo kusema! Wema Sepetu ‘alichokoza’ wanaume baada ya kuweka picha zake kadhaa kwenye mtandao wa Instagram.

Mrembo huyo alichangamua watu kwa Instagram kwa kuonyesha umbo lake kwa maringo kwenye photo shoot mpya.

Wema aliongelea kila sehemu ya mwili wake huku akisema kuwa ameridhika na vitu zote ambazo alipewa na Maulana.

“Shepu ya mwendokasi… Ndo niliojaliwa nayo… Kama imeanzia kiunoni kwenda magotini ndo niliojaliwa nayo… Kama wewe hauna basi mshukuru Allah… Ndo nilivyoumbwa jamani… Sio mimi bali ni Maulana ndo alionibariki nayo… Hata ingekuwa kwanzia kichwa hadi Vidole vya miguuni ni sawa pia… Ndo niliojaliwa nayo…. Sometimes najiangalia kwenye kioo sijimalizi… Ndo majaliwa yangu… Ndo yangu basi… Imenizidia… Allah Subhanah wataallah ndo amenipa… Aaaah….!? Sio shepu ya kawaida… Niacheni na Shepu yangu jamani… Ndo nishaimiliki mie… Siwezi kuitoa…. ????” Aliandika Wema Sepetu.