Ndoa Ya Abdu Kiba Yadaiwa Kupumulia Mashine

Ndoa ya staa wa Bongo fleva Abdu Kiba ambaye ni Kaka wa Ali Kiba imedaiwa kuwa katika hali mbaya na kuwa mbioni kuvunjika.

Global Publishers wanaripoti kuwa Ndoa hiyo na Abdu Kiba na mkewe Rwahida imeendelea kuwa matatani ambapo imesemwa kuwa Abdul Kiba mara nyingi amekuwa ni mtu wa kurudi nyumbani usiku na mara nyingi anashinda maskani maeneo ya Ilala Mtaa wa Arusha, kitu ambacho mkewe huyo amekiona kama sio sawa na pamoja na hayo bado anaona hakuna upendo ndani.

Baada ya Tetesi hizo gazeti hilo lilimsaka Abdu Kiba ili kupata ukweli wake lakini mara moja aliwataka wazungumze na Meneja wake ambaye mara moja alifunguka:

Hizo habari hata sisi tumezisikia kwamba watu wanasema hivyo lakini naomba kukuhakikishia hakuna ukweli wowote.

Unajua Abdul ni tofauti sana na Ally, yeye mara nyingi anapenda sana kuwa huru sana hivyo watu wakimuona pekee yake wanafikiria hivyo lakini sivyo au wengine wanasema kwa nini hamposti mkewe…”.

Lakini pia na mke wa Abdu Kiba, Rwahida amefunguka na kusema:

Hakuna ukweli wowote mimi na mume wangu tupo vizuri tu kama kawaida hakuna kitu kama hicho“.

 

Ali Kiba Avunja Ukimya Kuhusu Uteuzi wa Jokate

Staa wa muziki wa Bongo fleva Ali Salehe Kiba amevunja ukimya na kufunguka kuhusu uteuzi wa aliyekuwa mpenzi wake Jokate Mwegelo kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe.

Ali Kiba ambaye alikuwa mpenzi wa Jokate amefunguka Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv,  kusema anamtumia salamu za pongezi na kumtakia kila la Kheri;

Siwezi kulizungumzia sana hilo lakini kwa ufupi tu ni kwamba nimefurahi na nampa hongera sana”.

Lakini pia kaka wa Ali Kiba, Abdu Kiba ambaye pia alikuwa na ukaribu na Jokate amefunguka na kumpongeza Jokate:

Namtakia kila la heri na aweze kuongoza vyema Kwenye uongozi wake. Sijapata nafasi ya kuongea naye kwa sababu naamini yuko bize lakini pia sijawahi kuwasiliana naye kwa kipindi kirefu lakini Kupitia hii Interview namtakia kila la kheri Kwenye maisha yake”.

Jokate aliteuliwa siku chache zilizopita na Raisi John Pombe Magufuli kuwa mkuu wa Wilaya ya Kisarawe.

Gigy Money-Nilitembea na Ali Kiba Pamoja na Abdu Kiba

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Gift Stanford maarufu kama Gigy Money ametoa kali baada ya kukiri kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Staa wa Bongo fleva Ali Kiba pamoja na mdogo wake Abdu Kiba.

Gigy Money ameweka wazi kuwa ametembea na ndugu hao wawili lakini sio kwa wakati mmoja bali ilikuwa ni nyakati tofauti maana alikutana nao tofauti tofauti.

Gigy Money alifunguka hayo Kwenye Interview yake na kipindi cha Kikaangoni cha East Africa Tv ambapo alikiri kuwa wakati anaanza Mahusiano nao hakujua kuwa walikuwa ni ndugu:

 Kweli nilitembea nao mbona kawaida kwani nilikutana nao muda mmoja? Kwanza nilivyotembea nao sikuwa najua kama ndugu.

Halafu isitoshe mimi sina makosa mwenye makosa ni Ali Kiba kwani alijua natembea na mdogo bado akanitaka”.

Gigy Money ameanika kuwa Mahusiano Yake na Ali Kiba na Abdu Kiba yalikuwa siku nyingi kabla hajaanza kuwa video vixen ambapo enzi hizo alikuwa anakutana na wasanii club ambapo alikuwa anapenda kutembea na wasanii.

Abdu Kiba- Sitegemei Skendo Kusukuma Muziki Wangu

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Abdu Kiba ambaye ni mdogo wa staa wa Bongo fleva Ali kiba amefunguka na kudai hakuna kitu hapendi kwenye maisha yake ya muziki kama skendo.

Wasanii wengi wa Bongo fleva wanategemea skendo au wenyewe wanaita kiki ili kusukuma Muziki wao kwani wakifanya matukio wakakaa Kwenye midomo ya watu basi itasaidia kuwapa airtime ya bure.

Abdu Kiba amesema tofauti na wasanii wengine Muziki wake hautegemei kusukumwa na skendo za mitandao ya kijamii bali ni kazi yake na juhudi zake ndio zinamuweka juu.

Kwenye mahojiano na Gazeti la Mtanzania, Abdu Kiba amesema wasanii wengi wanaopenda skendo hawajiamini na wao ndio chanzo cha kushusha thamani ya muziki nchini.

Muziki ni maisha yangu na kazi inayonipa fedha za kujikimu mimi na familia yangu, napenda kutoa kazi zenye viwango ndio maana mashabiki wananipenda na kuendelea kufuatilia kazi zangu”.

Lakini pia Abdu Kiba ameweka wazi jinsi skendo zinavowabeba wasanii wengi.

Katika vitu nisivyovipenda kwenye maisha ya muziki ni kuishi kwa skendo, mambo kama haya huwa ni sababu ya kushusha thamani ya mtu na kazi yake”.

 

Tazama Picha Za Harusi Ya Alikiba na Abdu Kiba

Siku ya jana tarehe 29/04  Staa wa muziki wa Bongo fleva AliKiba na alitimiza sherehe ya mwisho ya ndoa yake na mrembo kutoka Mombasa Amina Lakini pia harusi hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Serena Hotel.

Lakini pia kilichovutia watu wengi haikuwa tu sherehe kwa ajili ya Ali Kiba na mkewe Lakini pia mdogo wa ALikiba Mwanamuziki Abdul Kiba ambaye na yeye alionekana na mke wake Ruwayda.

Harusi hiyo ilirushwa Love Kwenye chanel ya Azam na pia ilihudhuriwa na mastaa mbali mbali kama vile Mama Salma Kikwete, Ummy Mwalimu, Idris Sultan, Vanessa Mdee na Mimi Mars na wengineo.

Hizi ni baadhi ya picha za harusi hiyo:

 

Abdu Kiba Amefunguka Baada ya Video Yake na Fahyma wa Rayvanny Kusambaa Mtandaoni

Mwanamuziki wa Bongo fleva Abdu Kiba ambaye pia ni maarufu sana kwa sababu ya undugu alionao na staa wa Bongo fleva Ali Kiba, amefunguka na kuongea kwa mara ya kwanza kuhusiana na video iliyomuonyesha yeye na mke wa Rayvanny.

Kipindi cha nyuma kidogo kuna video ambayo ilisambaa mtandaoni ambayo ilimuonyesha Abdu Kiba na baby mama wa Rayvanny anayejulikana kama Fahyma au Fahyvanny wakiwa wamepozi wanapiga stori.

Inajulikana wazi kuwa Rayvanny yupo WCB na Diamond ni bossi wake lakini pia inajulikana kuwa Ali Kiba na Diamond ni paka na panya hivyo hiyo inapelekea makundi haya mawili kuwa na bifu hivyo ilipotokea Rayvanny na Fahyma wameachana kisha video yake na Abdu Kiba ikasambaa mtandaoni maneno mengi yalisemwa kutokana na ushindani wa kimuziki uliopo baina ya Ali Kiba na Abdu Kiba dhidi ya timu nzima ya WCB.

Baada ya sakata hilo Abdu Kiba Amefunguka Kwenye Interview aliyofanya na Millard Ayo Tv ambapo amedai kuwa anamjua fahyma tangu zamani sana na ile video ni ya kitambo kipindi hicho  fahyma alikuwa shabiki wake.

Nilimjulia yule msichana alikokuwa anafanya kazi kule Tv One na tulikuwepo tunafanya Interview ya television na kati kati ya Interview tukarekodi ile video na kipindi kile alikuwa ni shabiki wangu mkubwa lakini hiyo ilikuwa zamani kabla hajawa na Rayvanny nahisi lakini tangu amekuwa kwenye Mahusiano naye sijawasiliana naye”.

 

Abdu Kiba: Tunda Alikuwa Mpenzi Wangu, Nimemiss”.

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na wimbo wake wa ‘Jeraha’ Abdu Kiba ambaye pia ni kaka wa Staa wa Bongo fleva Ali Kiba, amefunguka na kusema aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mrembo Tunda Sebastian.

Tunda ni video queen lakini pia ni maarufu kwenye mitandao ya kijamii kwa sababu ya Msanii Diamond Platnumz. Tunda alijipatia umaarufu wiki chache zilizopita baada ya tetesi kusambaa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na msanii Diamond lakini pia alizidi kupata umaarufu baada ya vieeo zake na Kinje kuvuja mtandaoni.

Ikiwa tunasherekea mwezi wa mapenzi ambapo juzi tu ilikuwa ni siku ya Wapendanao, Abdu Kiba alifunguka kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv ambapo alidai kuwa alishawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Tunda na yalikuwa matamu kiasi ya kwamba alitamani yasivunjike.

Kwenye interview hiyo aliyofanya siku ya Valentine’s Day Abdu Kiba alizidi kufunguka:

Mahusiano ambayo yaliwahi kunifurahisha ambayo sikutamani hata yavunjike long time ago lakini kipindi hiko nipo na Tunda ambapo tulikutana kupitia social media nilimwelewa na vile vile alinielewa kwaiyo tukaweza kukutana na mwishowe wote tukaelewana ila muda kidogo kama miaka mitatu iliyopita na tulikaa kwenye mahusiano kwa miaka miwili lakini kwa sasa hatupo wote”.

Abdu Kiba amekiri kuwa penzi lao lilikuwa la siri kutokana na mazingira waliokuwa nayo ambapo amesema sehemu yao kuu ya kukutana ilikuwa kwenye gari hivyo watu wao wa karibu sana ndio walioshtukia mchongo.

Abdu Kiba na Timbulo Ndani ya Bifu Nzito Baada ya Kuibiana Nyimbo

Msanii wa Bongo fleva Abdu Kiba ambaye ni mdogo wa staa wa Bongo fleva Ali Kiba amejikuta kwenye mvurugano na msanii mwenzake Timbulo baada ya kituhumiana kuibina mashairi ya nyimbo.

Wasanii hawa wawili waliingia katika mgogoro mkubwa sana Timbulo na Abdu Kiba baada ya wote wawili kujikuta wanaimba mashairi yanayo fanana huku Timbulo akimtupia lawama na kumuuliza kwa nini atumie mashairi yake.

Kizaazaa hiki kilianza baada ya habari kusambaa kuwa kuna rekodi ambayo imefanywa na Timbulo na kumshirikisha msanii mwingine anayeitwa Promise ambayo inafanana kabisa mashairi na nyimbo mpya ya Abdu Kiba inayoitwa jeraha.

Baada ya hapo kilichotokea ni kila mtu anamrushia mwenzake maneno na kumlaumu kwa kumuibia mashairi. Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Timbulo amefunguka na kusema anamlaumu Abdu Kiba kwa kumuibia mashairi yake:

Mengi yatasemwa lakini ukweli utabaki pale pale mimi ninavyozungumza najua ukweli na Abdu na yule mtu anayehusika kwenye huu wimbo anaujua ukweli anajua stori yake ilivyo alafu kitu ambacho kimenikera tangia mwanzoni ni pale nilipoona wimbo umetolewa halafu wamekosea wamesema wimbo unaitwa promise wakati mwenye wimbo anaitwa promise na jina la wimbo hata silikumbuki lakini mimi namlaumu Abdu maana like alichokiimba Abdu mimi ndio nimetunga mashairi yote aliyoimba”.

Baada ya kutupiwa lawama hizo AbduKiba alifunguka na kusema nyimbo ile kapewa na Promise ambaye ni mmiliki wa nyimbo hiyo na yale mashairi yote yaliandikwa na yeye mwenyewe lakini baadae Timbulo ndio aliomba kuimba mashairi hayo. Abdu Kiba alitoa povu zito huku akidai kuwa Timbulo amemdhalilisha kwa kumnyooshea kidole na kumtuhumu kwa wizi.

Abdu Kiba afunguka kwanini hamfollow mtu yeyote ata kaka yake Ali Kiba kwenye Instagram

Kakake Ali Kiba amechukua mkondo kama wa rapa wa kimataifa – Eminem ambaya hamfollow mtu yoyote kwenye mtandao wa instagram.

Eminem ambaye ni mfalme wa rap ako na wafwasi milioni 12.7 kwenye Instagram lakini hamfwati (follow) mtu yeyote kwa Instagram.

Abdu Kiba amechukua mkondo huo pia, msanii huyo wa Bongo Fleva ako na wafwasi laki 384 kwa Instagram lakini hamfwati mtu yoyote hata kaka Ali Kiba.

Abdu alifunguka na kusema kuwa yeye hamfollow yeyote kwasababu hackers waliiba account yake na na alipoirejesha ilimbidi kuwaondoa watu wote waliokuwepo.

“Nikizungumzia akauti nakumbuka mwezi mmoja nyuma nikiwa Marekani akaunti yangu walihack kwa hiyo nilikaa karibia wiki tatu siko kwenye mtandao wa instagram, nilipoweza kuirudisha akauti yangu ndipo nilipoamua nisimfollow mtu yeyote kwa sababu watu niliowakuta mule sio watu wangu. Kwa hiyo niliwa-unfollow nikabakia siwezi kumfollow mtu tena. Sijafuta utaratibu wake bali ni maamuzi yangu, wategemee any day naweza nikamfollow mtu yeyote,” Abdu Kiba alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.