Tuzo Haziendi kwa Jina Wala Historia Yako :-Nikki wa Pili

Msanii wa bongo fleva nchini Nikki wa Pili nae ameamua kufunguka na kuzngumzia swala la tuzo linalozungumziwa na kila mtu katika mitandao ya kijamii.

Tuzo za sinema zetu ambazo zilitolewa wikied iliyopita na kuwaa cha watu midomo wazi hasa baaada ya kupatiwa tuzo hizo watoto wadogo ambao ndio wameingia  katika tasnia muda sio mrefu.

Watoto hao ambao walishindwanishwa na wasaniii wengine wakubwa na wenye vipaji vya muda mrefu , walichukua tuzo hizo na kuwaacha wasanii wakubwa wakitokwa na mapovu ya kukataa kulinganishwa na watoto wadogo.

Hata hivyo baada ya tuzo hizo, wasanii waliongea kila mtu la kwake na kusema kuwa watoto hao walitakiwa kuwekwa katika kategoria ya kwao na sio kama za wasanii wakongwe,

Akiongelea kwa mtazamo wake, mwanamuziki huyo alisema kuwa hakuna tuzo zinazotolewa kwa sababu ya jina au ukubwa wa umri wa mtu bali ni tathmini ya kazi uliyoifanya kwa muda fulani.

Anasema “tuzo haziedi kwa jina wala historia yako, ukubwa au kwa yale uliokwisha fanya….tuzo hupima kile umefanya kwa mwaka husika.”

Nikki wa pili Awaingiza Wasanii Wenzake Darasani

Msanii Nikki wa pili amefunguka na kuongelea swala la wasanii wengi kuongezeka nchini huku wakiwa na majina makubwa na umaarufu kuliko hata kipato wanachoingiza kutokana na majina yao na uatajiri wao haulingani na  vile wanavyoongelewa.

Nikki  anasema kuwa wasanii wengi wanahitaji elimu ya masoko ili kuongeza wasanii wenye majina na vipato pia kwa sababu wasanii wengi wamekuwa wakifurahia kupata majina na kusahau kuwa majina hayo yanahitaji nkuendana na  utajiri wao.

Nikki wa pli anasema “Kuibali sanaa kuwa kipato ni hata ngumu sana, iwe uchoraji au uchongaji au kitu chochote, wasanii wengi wanabaki na snaa zao kama hobi tu  na sio kitu cha kupatia kipato.somo la marketing pia linahitajika sana kwa wasanii  branding na huduma kwa wateja pia kwa wasanii ni muhimu pia.

Maneno ya Nikki yanakuja kutokana na ukweli kuwa wasanii wamekuwa wengi na wnegi wamekuwa na majina lakini pesa wanayipata kutokana na sanaa hiyo haiendani na majina yao na hii uthihirika zaidi pale ambapo wasanii wanapopata matatizo kama magonjwa na kujikuta wakiomba misaada sana.

Nikkki Atoa Ushauri kwa Linex

Msanii wa hip-hop nchini  Nikki  wa Pili amefunguka na kutoa usahuri kwa wasanii wote ambao wanatamani kufaya kazi kubwa na makampuni makubwa nchini kuwa hata kama wanakuwa wanachaguliwa na makampuni kufanya kazi hizo haimaanishi kuwa wao ni bora zaidi kuliko wengi swala la muhimu ni kuboresha kazi zao hili waweze kufanya izuri.

Huku akimtaja msanii Linex sunday mjeda,, nikki wa pili anasema kuwa kwa sasa watu wengi wa makampuni hawapendi sana kupata hasara kwa kufanya kazi na msanii ambae hajitumi , hivyo wanatakiwa kufanya kazizenye ubora na kupambana kazi kuwa bora kwa sababu hata makampuni pia hayataki hasara.

Nikki amekuwa moja ya wasanii walio wazi sana inapokuja maswala ya kazi, pesa na ushauri kwa wasanii na vijana pia hivyo  muda wote amekuwa akisema na makundi hayo ili kuwasaidia katika mafanikio.

Nikki Atoa Sababu ya Kumchagua na Kumvisha Pete Mpenzi Wake

Mwanamuziki Nikki wa pili ambae wikiendi iliyopita aliamua kuvunja ukimya na  kumvisha pete mwanamke aliyekuwa nae katika mahusiano kwa muda mrefu  na hata kuanza harakati za kufunga ndoa.

Akiongea na EATV, Nikki anatoa sababu kubwa za kumfanya kuamua kumuamini mpenzi wake huyo na kuamua kumvisha pete huku sababu kubwa akisema kuwa ni mwanamke mwenye mapenzi ya kweli na anaamini kuwa anampenda.

kwanza ananipenda, icho cha kwanzalakini cha pili tunaweza kuelewana tukiwa katika huzuni, furaha na hata maumivu pia.yeye anaweza kuelewa kuwa hapa nikki yuko hivi kwa sababu ya hivi lakini pia anauwezo wa kuelewa kuwa Nikki  ana mabaya yake mengi na mazuri pia, kitu ninachiweza kupungukiwa anaweza kujaza.

Nikki Wa Pili Amvisha Pete Ya Uchumba Mpenzi Wake

Msanii wa muziki wa hip hop nchini kutoka katika kundi la Weusi Nikki wa pili amemvalisha pete ya uchumba Mpenzi Wake wa siku nyingi anayejulikana kwa jina la Joan.

Bongo 5 wanaripoti kuwa Tukio  hilo lilitokea siku ya Jumamosi mkoani Arusha nyumbani kwa msanii huyo ambapo rasmi aliaga ukapera.

Shughuli hiyo ilihudhuriwa na wasanii wenzake Kama vile Kama yake Joh Makini, Dogo Janja, Lord Eyes na Juma Jux.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nikki wa pili alimuweka Mpenzi Wake huyo na kumsindikiza kwa maneno matamu na kuandika:

Queen, malkia, mwenye moyo wangu…….nuru ya uzuri wako imulike njia ya maisha yetu…..Nakupendaaaa sanaaaaaaaaa #sikuyetu ahadi ya kwanza nimetimiza”.

Nikki wa Pili Awazindua Watanzania kuhusu maktaba mpya ya UDSM

Msanii kutoka katika kundi la Weusi Nikki wa Pili alipata nafasi ya kuzungumzia uzinduzi mpya wa maktaba mpya ya kitaifa iliyojengwa chuo kikuu cha udsm ambapo ilifungukiwa November 27 na Mh rais.

akiandika  kama moja ya watu wanatajwa kuaminika asana kwa mawazo yao kwa vijana , Nikki ukiachana na kuwa msanii lakini pia amekuwa moja ya watu wanaohamasisha sana juu ya maisha na kutia bidii katika kile wanachokifanya na kukiamini.

katika ukurasa wake wa Twitter Nikki wa Pili aliandika “maktaba ya kuchukua wasomaji 2100 ina maana ni fursa kila siku kwa vijana 2100 kujivunia maarifa, itumieni sana itumieni vizuri ili kujenga maarifa vizuri kupanga mawazo na pia kutafuta ukweli wa kile unachoweza kujielezea , hili ni pori adhimu katika maisha, maktaba ni  uhai wa jamii.”

Nikki wa pili anasema kuwa vijana wanatakiwa kujifunza kuitumia maktaba hiyo kwa kujijengea kutafuta habari na maarifa mbalimbali  ili kuwa na wigo mpana wa mawazo.

Nikki Wa Pili Aandika Barua Ya Kumlilia Ruge

Msanii wa muziki wa Hip hop nchini Nickson Simon maarufu kama ‘Nikki wa pili’ amefunguka na kuweka wazi barua aliyomuandikia Mkurugenzi wa Clouds Media Ruge Mutahaba.

Siku chache zilizopita familia ya Clouds Media iliweka wazi kuwa Ruge yupo hoi hospitalini kutokana na maradhi ambayo yamekuwa yakimuandama kwa kipindi kirefu sasa.

Msanii Nikki wa Pili amefunguka mengi kuhusu Ruge na hata kutaja mambo mengine mengi ambayo amemfanyia ambayo mpaka leo yameweza kumpa mafanikio makubwa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nikki wa Pili aliandika maneno haya:

Muda wa kipindi kirefu sana katika maisha yangu ya shule nilikuwa naamini mim ni mtu wa kukaa nyuma, nisiye na uwezo wa kuzungumza mbele za watu, sikuwa nanyoosha mkono darasani hata kama najua jibu, nilio soma nao chuo wanajua nilivyo kuwa natoroka presentations.

Muda wa kipindi kirefu sana katika maisha yangu ya shule nilikuwa naamini mim ni mtu wa kukaa nyuma, nisiye na uwezo wa kuzungumza mbele za watu, sikuwa nanyoosha mkono darasani hata kama najua jibu, nilio soma nao chuo wanajua nilivyo kuwa natoroka presentations.

Akaniambia wewe ni public speaker mzuri, akaanza kunipa nafasi ya kuzungumza mbele za watu nilikuwa naona na kosea lakini kila niliposhuka alikuwa anaiambia umefanya vizuri sana ongeza hichi na hichi.

Leo nimekuwa naalikwa vyuoni, kwenye makongamano, semina,taasisi, kampeni mpaka makanisani, kama mzungumzaji au mtoa mada, na hata mitandaoni huwa naandika mawazo yangu bila woga, ingekuwaje nisingekutana na Ruge Mutahaba.

Mungu akupe wepesi urudi katika uzima wako, RG (genius)”.

Inaripotiwa Ruge yupo nchini Afrika Kusini akipatiwa matibabu kutokana na matatizo ya figo ambayo yanamsumbua kwa miezi kadhaa sasa.

 

Mawazo ya Afande Sele Yalipangwa Katika Ufahamu Mdogo :-Nikki wa pili

Msanii kutoka katika kundi la Weusi amefunguka na kusema kuwa mawazo ya msanii Afande Sele ambae aliwahi kusema kuwa wasanii wa kundil la weuzi wamekuwa wakipata tuzo za muziki wa KILI kila mara kuwa walikuwa wakipewa tuzo hizo kwa kuangaliwa kabila lao na wala sio kitu kingine.

Nikki wa pili anasema kuwa swala hilo yeye hakubaliani nalo hata kidogo lakini pia anaamini kuwa afande sele alikuwa akisema hivyo huku akiwa na ufahamu mdogo wa kile anachokiongea.

Ingawa Nikki hataki kuonekana kama anajibizana na Afande Sele kwa kile alichokisema lakini bado anasisitiza kuwa kama ni kweli watuaji wa tuzo hizo wangekuwa kweli wanaangalia makabila  kama alivyosema Afande kuhusu kabila la wachaga basi alimia 90% ya tuzo zingekuwa zinaenda uko lakini haikuwa hivyo.

Nikki anasema kuwa afande sele arudi akajipange kusema upya kuhusu hilo kwa sababu anaamini kuwa hata kama alikaa muda mrefu kuchunguza na kuchambua swala hilo alilifanyia utafiti kwa uelewa mdogo.

 

Nikki Wa Pili Amwaga Povu Zito Kwa Wasanii Wakaa Uchi

Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Nikki Wa Pili amewaji juu na kuwatolea povu zito mastaa ambao wameandamwa na skendo ya kuweka picha na video chafu zenye maudhui yasiyo ya kimaadili  kwenye mitandao ya kijamii.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Nikki wa Pili amewachana watu hasa wasanii wanaotafuta kiki kupitia vitu visivyo na maana.

https://www.instagram.com/p/BpYt1DMjQna/?utm_source=ig_web_copy_link

Amber Rutty, Wema Sepetu na Gigy Money ni baadhi tu ya mastaa ambao hivi sasa wanatengeneza headlines kwa vitendo vyao vya kuachia picha chafu kwenye mitandao ya kijamii huku baadhi yao wameshachukuliwa hatua za kisheria.

Nikki wa Pili Amkosoa Mwl Nyerere

Kila mwaka inapofika October 14 ,tanzania inakuwa inaadhimisha kifo cha baba wa taifa mwl julius kambarage Nyerere, kiongozi aliekuwa muhasiis wa Taifa letu na aliyetukomboa kutoka katika mikono ya wakoloni.Mwl alifanya mengi mazuri na makubwa yakutufanya tumkumbuke kila siku lakini imekuwa vizuri zaidi kutenga siku yake maarumu ili kumuenzi .

moja ya wasaii na wanafalsa nchini, nikki wa pili ambae amekuwa moja ya chachu kubwa kwa vijana kutokana na kuongea bayana bila kuogopa kitu pale anapoona jamii inakosea bila kuwa na mfungamanowa upande wowote ameibuka na kunagalia baadhi ya mambo ambayo yeye anaona kuwa yalikuwa ni makosa kwa uongozi wa mwalimu.

Nikki  ameandika yafuatayo kama makosa ya baba wa taifa

  • mwalimu alirithi serikali ya ukoloni  na  hakuibadili sana..sifa ya seriali ya kikoloni ni  ya serilai ya ukoloni ni ukandamizaji wa wananchi na wananchi hawana sauti…hata sera ya vijiji na ujamaa ilitekelezwa kwa mabavu.
  • chama kilichoshika hatamu hakikutenganisha chama na serikali…chama kikawa na nguvu mbele ya serikali
  • katiba ya rais ya kifalme na wala isyoshirkisha wananchi wakati wa kuiandika.
  • kufungiwa kwa jarida la wanafunzi la cheche..lililokuwa likihoji juu ya utekelezaji wa sera ya ujamaa ilikuwa ni uminyaji wa demekrasia na sauti za wananchi kuhusu maendelea ya jamii zao.
  • kudhoofisha ushurika na kuingiza siasa ndani yake.HAPPY  NYERERE DAY…NYERERE MY NUMBER ONE.

Nikki Wa Pili- Sitafuti Kiki Ni Ndoto Yangu Kugombea Uraisi

Msanii wa muziki wa hip hop nchini kutokea katika kundi la Weusi, Nickson Samson maarufu kama Nikki wa Pili amefungukia mipango yake ya Kugombea uraisi mwaka 2025.

Wiki iliyopita Nikki wa Pili alitrend Kwenye mitandao ya kijamii kwa taarifa ya kwamba ana mipango ya kugombea uraisi na hata kuna mashabiki walimtuhumu kwa kutafuta kiki Kupitia ishu hiyo.

Kwenye mahojiano na gazeti la Risasi Vibes, Nikki wa Pili alianika kwamba siyo kiki bali ni kweli ana mpango wa kuwania Urais wa Tanzania.

Watu wanaweza kufikiri kwamba ninatafuta kiki, lakini ukweli ni kwamba ni ndoto yangu siku moja kuwa Rais wa Tanzania. Kwa sasa ninasogeza umri, baada ya mwaka 2025, nitafahamu ni chama gani kitanipa tiketi.

Kuhusu nafasi hii ‘CV’ yangu inajieleza na namna ambavyo watu wananiamini, nitaendelea kufanya mambo ya kujenga uaminifu zaidi ili baadaye niwatumikie Watanzania”.

Siku za nyuma mbunge wa Kigoma Mh. Zitto Kabwe alishawahi kumtaka Nikki Wa Pili ajiunge na ACT Wazalendo Kupitia ukurasa wa Twitter jambo ambalo Nikki alikataa na kusema yeye sio mwanasiasa.

Nikki Wa Pili Atangaza Ndoto Yake ya kuwa Raisi, Wasanii Wamsapoti.

Akiwa kama moja ya wasanii wanaojitahidi sana kutoa maneno yenye kuhamasisha katika jamii,nikki wa pili kwa mara ya kwanza ameweka wazi kuwa ndoto yake kubwa  ni kuwa rais, ingawa msanii huyo kwa sasa hajaweka wazi kuwa yeye ni mfuasi wa chama gani lakini amekuwa akihamasiha sana vijana kupitia mitandao ya kijamii.

katika ukurasa wake wa  twitter, Niki wa Pili aliandika”Ndoto yangu ni kuja kuwa Rais

Hata baada ya kuweka tweet hiyo , baadhi ya wasanii walionekana kumsapoti msanii huyo kwa kumpongeza kwa kuwa na ndoto hiyo huku wakimtaka asikate tamaa,mmoja kati ya wasanii hao ni Dogo Janja ambae aliandika

ndoto yako ipalilie tu ndugu yangu, anayeona haliwezekani hilo ni tatizo lake sio kwako, husda ni tunu ya Taifa, isikusumbue fanya mambo yako #Nikiwapiliforthepresidency

 

 

Kiki Sio Mafanikio kwa Msanii:- Nikki wa Pili

Msanii wa bongo fleva Nikki wa Pili amefunguka na kusema kuwa katika maisha ya msanii kiki sio kitu cha lazima sana mpaka kufanikisha maswala ya muziki wake kwa sababu kuna vitu vingi ambavyo anatakiwa kuvifanya katika kazi hiyo.

Niki amemjibu Master J amabe ni msanii wa muziki wa siku nyingi  aliyesema kuwa muziki  na soko la sanaa la sasa hivi ni lazima kufanya kiki ndio uweze kuuza muziki wako na sio kama zamani enzi zao.

Niki anasema kuwa vitu vngi vinafanya msanii kufanikisha muziki wake ikiwa pamoja na kufanya video nzuri, uhusiano mzuri na wasanii wenzake na pia kuwa karibu na mdia zitakazosaidia kusambaza muziki wake.

sio kweli kwamba muziki ndi unafanikisha maisha ya msanii mbona kuna wasanii wengi tu wanafanikiwa kwa bila kuwa na kiki wala picha za utupu, kwa mfano sisi weuzi tumefanikiwa sana bila kuwa na kiki.

Nikki wa Pili Atupa Dongo kwa Babu Tale, ni Baada ya Kwenda South kwa Zari

Msanii wa Hip-Hop nchini, Nikki wa Pili amemtupia dongo Babu Tale baada ya babu tale kwenda afrika ya kusini na kurudi huku akitangaza kuwa lengo lake ku ilikuwa ni kwenda kumbebeleza zari ambae ni zazi mwenzie na diamond ili kurudiana na diamond.

Akiandika katika ukurasa wake wa instagram, Nikki wa Pili alisema kuwa kazi ya babu tale kutumwa haijaanza leo ameanza kutumwa tangu akiwa kijana enzi hizo anatumwa na kaka yake ku-burn CD  na sasa hivi anatumwa na Diamond kubembeleza ndoa.

babu tale alikuwa akitumwa empty CDs na majani  pale bongo records ili ku-burn CD s za wasanii wa kaka yake,siku hizi natumwa akabembeleze ndoa SAUZI…. kweli swala la uadilifu katika utumishi  linaendelea.

Napenda Wanawake Natural, Hamtomuona Mke Wangu na Make-up

Rapa wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika kundi la Weusi, Nikki wa pili amefunguka na kuweka wazi kuwa anapendelea kuwa na mwanamke ambaye hajirembi ‘natural’ hivyo msitegemee kumuona mke wake na make-up.

Niki wa pili amekuwa akimposti sana mpenzi wake Kwenye ukuras wake wa Instagram ambapo msichana huyo huoneka akiwa natural sana habari mawigi, anabana tu nywele zake lakini pia hapaki make up sana.

Wiki iliyopita Dogo Janja alimchana Niki na kumwambia mwanamke make up natural aiachie misitu comment ambayo ili trend sana lakini sasa Niki wa pili an Afunguka kuhusu kauli yake ya kupenda mwanamke ambaye hapaki make up.

Kwenye Interview aliyofanya na Enews ya East Africa Tv Nikki wa pili alifunguka na kuweka wazi mke wake hatokaa apake make up:

Hakuna kitu kizuri kama mwanamke ambaye yupo asilia natural kwani sisi binadamu ni wazuri kwa sababu ni asili  na mara nyingi ukibadilisha asili unakuwa unaiharibu na mimi naamini uzuri wa msichana upo kwenye asili yake hivyo msitegeemee kumuona amepaka make up labda lipstick kidogo”.

Niki wa pili amekuwa Kwenye Mahusiano na mrembo huyo ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa kipindi kirefu kidogo.

 

Ukiwa na Mchepuko Hakikisha Mchepuko Wako Mzuri Kuliko Demu Wako- Nikki wa Pili

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kurap kutoka katika kundi la Weusi, Nikki wa pili ameibuka na kutoa ushauri kwa wanaume wenzake wanaopendelea michepuko.

Nikki wa pili alizua sintofahamu baada ya ujumbe wake alioutupia kwenye ukurasa wake wa Instagram kutafsiriwa vibaya ambapo aliandika:

chiti na demu mkali mpaka demu Wako akikufumania naye badala ya kumpiga mangumi anamuomba kupiga naye picha, na kumuuliza anatumia mafuta gani, amewezaje kuwa na ngozi nzuri hivyoo na namna alivyotunza shepu na kutokuwa na tumbo kabisa, so akiondoka haondoki na machozi anaondoka na notes alafu akukubali kuwa wewe mbaya yaani yeye mwenyewe kabahatisha kuwa na wewe”.