Chid Benz Amwaga Povu Baada Ya Kukosekana Kwenye Listi Ya Wasafi Festival

Msanii mkongwe wa muziki wa Hip hop nchini Chid Benz amefunguka na kuwamwagia Povu zito timu nzima ya WCB Baada ya kukosa mwaliko wa kufanya shoo kwenye Wasafi Festival.

Chid Benz amefungukia ishu ya Diamond Platnumz na Timu yake nzima ya WCB kutumia wanamuziki Kama Dudubaya ambaye anaamini amechaguliwa kwa sababu ya umaarufu wa jina lake Konki Konki konki Master.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari, Chid Benz amedai amesikiyishwa kuwa Msanii Kama yeye Anayeimba vitu vya maana hajachaguliwa kwa madai kuwa anatumia madawa ya kulevya ilhali ameshaacha.

Sisi wasanii tunaoimba nyimbo ambazo zinabeba ujumbe na maana hatupati nafasi kabisa utasikia wanasema achana na hao wakina Chidi Benz wanakula unga ila Dudubaya kisa anasema konki konki anajaza watu basi nasibu anampa tour kwenye Wasafi Festival”.

Diamond na timu nzima ya WCB ilimchagua Dudubaya Kama mmoja wa wasanii watakaoshiriki katika tamasha la WCB Baada ya umaarufu alioupata kupitia jina lake la utani la Konki Master.

 

Mose Iyobo Afunguka Baada Ya Kukamatwa na Polisi

Dansa maarufu kutoka kwenye kikundi cha muziki cha WCB ambaye pia ni mzazi mwenzake na staa wa Bongo movie Aunty Ezekiel, Mose Iyobo amefunguka na kueleza masahibu yaliyowapata baada ya kukamatwa na polisi.

Iyobo na timu nzima ya WCB walikamatwa na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani wakati wakielekea mkoani Mtwara kwenye Tamasha la Wasafi Festival 2018 lililofanyika Jumamosi katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani humo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers Iyobo amesema wakiwa kwenye msafara wa zaidi ya magari 8 ya WCB na wasanii wenzao, alijikuta akidakwa na polisi baada ya kuvunja sheria za usalama barabarani kwa kuendesha gari kwa mwendokasi zaidi kuliko uliyoruhusiwa.

Mnenguaji huyo amedai baada ya kukamatwa alikuwa akibishana na askari na kushindwa kuelewana nao, ilisababisha awekwe ndani kwa takribani saa 9 kisha baadaye kuachiwa baada ya kulipa faini.

Ujue tulikuwa tukiwahi kwenye shoo, tukitaka tufike haraka huku mzuka ukiwa mkubwa, kwa hiyo nilikuwa nakanyaga mafuta tu, sikufahamu kama eneo lile sikutakiwa kukimbia kwa spidi kubwa, walinikamata kutokana na kutoelewana nao wakanishikilia. Lakini baadaye waliniachia na shoo tulifanya vizuri“.

 

“Nimechoshwa na Kuhusishwa na Kila Mwanamke”-Diamond Platnumz

Msanii w muziki wa kuzaliwa kimya staa Diamond Platnumz ameibuka na kumwaga Povu zito kwa watu wanamuhusisja kimapenzi na kila mwanamke ambaye anaonekna naye hadharani.

Sakata hilo limekuja siku chache Baada ya Diamond na familia yake kuonekana na mrembo mpya anayejulikana Kama Christina nchini Dubai walipoenda for vacation. We

Kwenye mahojiano na Global Publishers? Diamond alianza kwa kusema kuwa amechoshwa na kuhusishwa na kila mwanamke anayeonekana kuwa na mama yake au kuwa naye karibu tu watu wanasema ni mtu wake.

 

Diamond aliweka wazi msichana huyo wa Kibongo mwenye maskani yake Dubai, alikutana naye kama mwenyeji aliyekuwa akiwatembeza maeneo mbalimbali kama watu wengine ambavyo wanaweza kwenda nje na kupokelewa na marafiki zao.

Mimi na msichana huyo tunafahamiana ameonekana kweli na mama yangu na wamejiachia kwenye picha tofautitofauti lakini ifahamike kuwa alikuwa akitupa kampani tu kama mwenyeji na si mapenzi,”

Mimi na msichana huyo tunafahamiana ameonekana kweli na mama yangu na wamejiachia kwenye picha tofautitofauti lakini ifahamike kuwa alikuwa akitupa kampani tu kama mwenyeji na si mapenzi,”

Huko niliteketeza fedha nyingi ambazo nisingependa kuzitaja lakini nilifanya kwa ajili ya familia yangu kwani mafanikio niliyonayo ni kwa dua wanazoniombea mama yangu na ndugu zangu pia sikufanya kwa ajili ya mwanamke na nisingekataa kuongozana na mrembo huyo kwani alikuwa kama mwenyeji”.

Mrembo huyo alizua gumzo mtandaoni mara Baada ya kuonekana katika picha kadhaa za mjini Dubai akiwa na Mama Diamond na hata Diamond na familia yake.

Siri ya Mmiliki wa WCB Yafichuka

Baada ya kuwa na figisu nyingi sana hasa kuhusu matamasha yanayoendelea  nchini  yaani fiesta inayoendeshwa na Clouds media na lile la Wasafi Festival ambayo imeacha tension kubwa sana katika pande hizo mbili , watu wamekuwa wakichokonoa mambo mbalimbali na kufikia hatua ya kusema kuwa inawezekana hata  wasafi tv ni ya Clouds Media pia.

kwa evidence zilizotolewa zinasema kuwa jina la roots ya wasafi tv ni kutoka Clouds Media hivyo inawezekana kuwa bosi wa Clouds ndio bosi wa wasafi hiyo wawili hao  hawakupaswa kuwa na ushindani na kurushiana madongo kwa kiais hiki.

katika moja ya page ya udaku ya shilawadu ambacho ni moja ya kpindi kinachorushwa na clouds mdia waliandika “inasemekana kuwa picha hii ilipigwa siku moja ndugu zetu walipokuwa studio wakifunga mitambo na mafundi wetu, satelite ilisajiliwa na kwa jina la clouds na tv yenyewe ni hii…..jifanye unajikuna…tusitoane damu bure wakati sisi wote ni vidampa tu …Bosi wetu ni mmoja …TABUIKOPALEPALE.”

“Natamani BASATA Waniruhusu Kuperfom Mwanza”- Rayvanny

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Rayvanny ameibuka na kuwaomba tena BASATA wampe ruhusa ya kuperfom wimbo wa Mwanza stejini.

Wiki chache ziliopita Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) liliufungia rasmi wimbo wa ‘Mwanza’ wa Rayvanny aliomshirikisha Diamond Platnumz kwa madai ya kukiuka maadili ya Kitanzania kwa kuimba matusi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Rayvanny alisema angetamani sana kwa mara ya kwanza apafomu Wimbo wa Mwanza katika jukwaa la Wasafi Festival lakini anashindwa kutokana na adhabu ya Basata ya kuufungia wimbo huo ambao yeye anakiri kuwa hakuutunga kwa nia ya kupotosha watu bali kuburudisha.

Kiukweli natamani sana wangeniruhusu tu japo nipafomu katika shoo zangu maana mapokezi ya huu wimbo ni makubwa mno mpaka yananifanya nitamani kuupafomu katika jukwaa la Wasafi Festival Jumamosi hii”.

WCB wanategemea kupigwa bonge la shoo kwenye tamasha Lao la Wasafi Festival linalotarajiwa kufunguliwa rasmi Jumamosi hii tarehe 24 mkoani Mtwara.

“Wasafi Festival ni Tamasha Kubwa Halijawahi Tokea Tanzania”-Afande Sele

Msanii mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva nchini Afanse Sele ameibuka na kuweka wazi kuwa hivi sasa hakuna msanii mkubwa Kama alivyokuwa Diamond na hivyo tamasha lake la Wasafi Festival ndio litafunika.

Suala hili limekuja kutokana na sakata linaloendelea kupamba moto hivi sasa la mabishano ya Nani zaidi kati ya Wasafi Festival na Tamasha la Clouds la Fiesta.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari, Afande Sele ameibuka na kusema hivi sasa Tamasha kubwa sana Tanzania ni Wasafi Festival na halina mpinzani kumaanisha Fiesta linakalishwa na Wasafi.

Unajua hivi sasa Wasafi ndio Real Madrid ya Tanzania ndio tamasha bora  na linaonekana kuja kuwa kubwa kuliko yote kwaiyo kushiriki katika tamasha la Wasafi ni fahari na pia naunga mkono juhudi za wadogo zetu ambao wameamua kukata minyororo ya watu waliokuwa wanatufanya watumwa na kutunyanyasa kwaiyo Wasafi ndio mapinduzi ya burudani kwanza inaongozwa na wasanii wenyewe”.

Lakini pia Afande Sele amewatolea Povu zito Clouds Fm na kuwatolea tuhuma za kutumia nguvu zao na cheo chao kuwanyanyasa wasanii na kuwataka wafanye vile wanavyotaka wao.

“Wasanii Kuweni na Misimamo na Hata Mnapotakiwa Tajeni Dau Manalolitaka”-Diamond Platnumz

Msanii wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ameibuka na kuwataka wasanii kuwa na msimamo na kuchagua malipo yanayoweza kuwafaidisha wao na familia zao.

Maneno hayo yamekuja ikiwa ni muendelezo wa mivutano kati ya Wasafi na Clouds Fm ambapo Diamond na timu yake nzima wamekuwa wakimtuhumu Ruge ambaye ni Mkurugenzi wa Clouds kwa kuwanyonya na kuwaonea wasanii.

Baada ya mvutano wa muda mrefu na majibizano yao ya siku mbili hizi kuchochewa na shoo zao zitakazofanyika jumamosi ambapo Fiesta mwaka huu imeweka wasanii wengi ambao ni wakongwe na Wasafi wanaamini wamefanya hivyo Baada ya kuwapa changamoto.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Diamond amewndelea kuwatupia vijembe Clouds na kuandika haya:

Usipomshirikisha Diamond Utamshirikisha Nani :-Lavalava

Msanii wa muziki kutoka kundi la WCB lavalva amefunguka na kusema kuwa hivi karibuni anategemea kufanya nyimbo nyingine ukiaachana na ile aliyotoa hivi karibuni na wimbo huo anategemea kumshirkisha bosi wake Diamond platnumz.

Lavalva anaonekana kumsifia sana bosi wake kwa kusema kuwa katka muziki wa bongo ukifanya nyimbo usipomshirikisha Diamond utamshirikisha nani mwingine.

Akiongea na na waandishi anasema ” wimbo na Simba nitatoa hivi karibuni shida ya simba bwana wala hazoeleki kabisa na usipomshirikisha simba utamshirikisha nani mwingine kwenye muziki huu wa bongo.

Katika kundi la WCB ni lavalva pekee ndie ambae bado hajafanya wimbo na Diamond zaidi ya ule wa jibebe walioimba wakiwa wasanii wa kundi lote.

Diamond Awatupia Kijembe Clouds Fm Baada Ya Kumgeukia RC Makonda

Msanii wa muziki wa Bongo fleva na Mkurugenzi wa  WCB Diamond Platnumz ameibuka na kuwatupia kijembe Clouds Fm Mara Baada ya kumgeukia RC Makonda.

Sakata la Wasafi Festival na Fiesta limeendelea kupamba moto ambapo inaonekana live kwamba kila mmoja anataka apige tamasha kubwa kuliko mwenzake.

Kwa muda mrefu kumekuwa hakuna maelewano kati ya pande hizo mbili kwaiyo ilivyotokea uwezekano wa kuwepo tamasha kwa siku moja lakini katika Mikoa tofauti.

Diamond Platnumz amewarushia kijembe Clouds Fm kwa kusema wameomba poo kwa mlezi wao akimaanisha Paul Makonda Baada ya kuonekana akilitangaza tamasha hilo na kuwataka watu wajae siku ya tukio.

Inafahamika kwamba mlezi wa Wasafi ni mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Mkonda hivyo baada ya jana Clouds kumtumia Makonda katika moja ya video akiongelea inshu ya Ruge na kwamba yeye mwenye atakuwepo Fiesta imekuwa habari nyingine tena.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond ameandika:

Diamond Aiangukia BASATA Aomba Japo Kuperfom ‘Mwanza’ Stejini

Msanii wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ameibuka na kuiomba ruhusa Baraza la Sanaa kutumia wimbo wake walioufungia wa Mwanza kuperfom stejini.

Wiki chache zilizopita wimbo wa ‘Mwanza’ ulitoka lakini mara moja BASATA waliufungia wimbo huo kwa madai ya kukiuka maadili ya Kitanzania kwa kubeba ujumbe wenye lugha ya matusi.

Lakini Diamond Platnumz amefunguka na kuwaomba Basata kuutumia wimbo wao ba Rayvanny wa Mwanza kwenye tamasha lao la Wasafi Festival 2018.

Kupitia ukurusa wake wa Instagram Diamond ameandika hayo.

Wasafi Festival Kuwashusha Wizkid na Mr. Eazi

Mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz amethibitisha ujio wa staa wa muziki kutoka Nigeria  Wizkid kwa ajili ya kuperfom katika tamasha la Wasafi Festival.

Diamond Platnumz  amethibitisha hilo kupitia ukurasa wa Instagram baada ya ku-comment kwenye post ya Rayvanny ambayo alipost video fupi ikiwaoyesha Diamond na Wizkid muda mfupi baada ya kumalizika kwa tamasha kubwa la muziki la One African Music Festival lililofanyika Dubai wikiendi iliyopita.

Kwenye video hiyo Diamond alithibitisha kuwa atamshusha msanii huyo mkubwa Afrika kwenye tamasha hilo litakalofanyika Dar Es Salaam baada ya kuzunguka mikoa mingine.

Lakini pia na msanii Harmonize ameamua kuweka wazi meseji zake alizokuwa anawasiliana na msanii kutoka Nigeria akiomba kuja kushiriki angalau katika moja ya tamasha la Wasafi Festival Tanzania.

Diamond Ana Mapungufu Lakini Tunayavumilia :-Lavalava

Msanii kutoka katika kundi la WCB lavalva amefunguka na kusema kuwa Diamond ni bosi wao na amaekuwa akifanya nae kazi lakini diamond ni moja ya  mabosi ambao wana changamoto kubwa kwa sababu mpaka akubali kupokea nyimbo yako na kukubali kuitoa inachukua muda mrefu sana kuikagua kwa sababu anataka wasanii wake waweze kushindana vizuri katika soko la muziki.

Lavalava ambae ametoa wimbo mpya unaitwa nitake nini anajinadaa vyema kabisa kwa ajli ya wasafi Festival wiki hii huku wakiamini kuwa wazo hilo la bosi wao ni zuri kwa sababu linawasaidia kupanua wigo wao wa muziki.

Lavalva anaendelea kusema kuwa kuna ugumu sana kuishi ndani ya WCB kama mwanamuziki kwa sababu kuna ushindani mkubwa sana wa ndani kwa ndani baina ya wasanii wenyewe ili kupata wasanii wazuri na kutoharibu jina la kundi.

kwaio Diamond ana mapungufu yake pia lakini ana kazi kubwa sana ya kutuelimisha na kutufundisha  kwamba tusiyachukulie poa hayo mambo kwa sababu yanamadhara yake pia, 

Akiongea kuhusu Alikiba kutaka kudhamini  tamas ha lao kupitia kinywaji anasema kuwa hajui kuhusu swala hilo kwa kuwa na yeye amekuwa akilisikia tu lakini kama kweli hilo ni jambo zuri kibiashara.

Fid Q Awaomba Radhi WCB Baada Ya Mgogoro Wa Wasafi Festival na Fiesta

Mwanamuziki wa hop hop nchini Fid Q ameibuka na kumuandikia ujumbe wa kumuomba radhi meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale mara Baada ya mgogoro wao.

Sakata hilo kati ya Fid Q na Wasafi lilianza maraa Baada ya Fid Q kuamua kufanya shoo kwenye Fiesta ya Clouds na kukataa kufanya shoo Wasafi Festival siku ya jumamosi tarehe 24.

Baada ya kufikia uamuzi wa kufanya show Fiesta alifanya tangazo la Tigo Fiesta ambalo linasambaa mtandaoni akitafsirikiwa kwamba alitupa dongo kwa Wasafi Festival.

Kupitia video hiyo, Fid alisikika akisema “Yani nyinyi mnataka kusubiri watu wafanye halafu na nyie mfanye, kawambie acheni upumbavu ni moja kubwa” kauli ambayo ilitafsiriwa ni dongo kwa kwambi hiyo.

Baada ya sintofahamu hiyo Fid q aliamua kutoa kauli yake huku akiomba radhi wa WCB kama walimtafsiri vibaya kwani hakuwa na nia ya kuwarushia vidongo.

PART 1: Nimeonelea si vibaya nikifungua hiki kigazeti changu na sentensi hii—-.> “ Keki ya taifa ni kubwa sana na ina vipande vingi vya kuwatosha wachakarikaji wote wenye kuistahiki “

Na kwakua Allah ndio mtoaji riziki, mimi kama mimi sina hayo mamlaka au hata hiyo roho mbaya ya kutamani wachakarikaji wenzangu mkwame ktk harakati zenu, ninasema hivi ni kwasababu siku zote huwa siamini kama nitapungukiwa kitu nyinyi mkifanikiwa, na siamini hivyo kwasababu ninajiamini mimi ni mchakarikaji na kipande changu cha KEKI bado kipo mezani kinaningojea ( cha muhimu ni PUMZI na DUA tu ).. ni ukweli tupo kwenye tasnia moja na kila mmoja wetu anajaribu kufanya lile alionalo sahihi ili kusogea mbele, na iko wazi mmeshafanya na mnaendelea kufanya mengi makubwa, nami bila kusita siku zote nimekua ni mtu wa kuwapongeza iwe kwa njia ya mitandao au tukutanapo ana kwa ana.. mie hufanya vile kiroho safi pasina chembe yoyote ya unafiki. ••••••••••••
Nimeyasema hayo hapo juu ili tu uweze au muweze kupata picha halisi ya kilichomo moyoni mwangu na pia kuwakumbusha ya kwamba mimi pia ninao uhuru wa kufanya shughuli zangu za sanaa na yeyote ambaye nimeridhia nae kimaslahi pasina kujali kama jicho la pembeni yangu linaiona faida iliyopo au laah.. sioni ni busara kwa nyie kuja na kujaribu kunipangia yupi nifanye nae au yupi nisifanye nae ili kuwaridhisha machoni/ mioyoni mwenu.. na kama mnaamini ni haki yenu ya msingi mimi kuyafuata hayo matakwa yenu basi naomba nikujuzeni ndugu zangu mtakua mmeonyesha UBINAFSI wa hali ya juu kwenye hili.. pia kumbukeni mimi pia nishawahi kuwa na matatizo na MJENGO.. lakini nilijikuta ninapambana peke yangu hadi UTULIVU uliporejea pasina msaada wa mtu yeyote.. na sikupambana peke yangu kwasababu hamkua na taarifa, taarifa mlikua nazo lakini ninafikiri mlikua mmetingwa na shughuli zenu za ujenzi wa taifa kiasi kwamba hamkuona kama kuniongezea nguvu ingesaidia lile zoezi kuisha haraka.. amini msiamini sijawahi kumuwekea mtu yeyote kinyongo kwenye hilo, na hiyo kitu ilinifunza sana juu ya suala zima la KUJIPAMBANIA MIE MWENYEWE kwenye situation yoyote ile na KUTOKUPIGANA VITA NISIYOIJUA au ISIYONIHUSU.

PART 2: Yote na yote.. Kiukweli yale maneno ya kwenye promo ya “MOJA KUBWA” sikutegemea kama yangekua na uzito huu uliopelekea ndugu yangu uchafukwe kiasi cha kunifungulia bomba la matusi humu insta.. kwanza sikumbuki hata kama niliyatamka kwa nia ya kuleta msigishano huu.. Lakini kama kweli nimewakwaza… Naomba mnisamehe kibinadamu kwa hilo ,naomba tumuache SHETANI apite na mwisho naomba nimalize kwa kusema.. BURUDANI sio VITA <hivyo ninawatakia kila la heri/ MAFANIKIO ya hali ya juu ktk MAPINDUZI YA BURUDANI huko MTWARA.. KEKI YA TAIFA NI KUBWA SANA NA INA VIPANDE VINGI VINAVYOTOSHA KUMFIKIA KILA ANAYESTAHIKI KWA KUDRA ZAKE MUWEZA WA VYOTE…. MAULID NJEMA ??”.

 

WCB Watangaza Mdhamini Wa Wasafi Festival, Ali Kiba Atupwa Kule

Msanii wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ametangaza kinywaji rasmi kitakacho dhamini Tamasha la Wasafi Festival linalotegemewa kuanza tarehe 24 November.

Mpaka siku ya jana ilikuwa inaaminika kwamba Ali Kiba kupitia kinywaji chake cha Mo Faya ndio watakuwa wadhamini rasmi wa Wasafi Festival hii ni Baada ya Diamond kukubali mwaliko wa Ali Kiba kudhamini tamasha hilo.

Siku mbili zilizopita Diamond alitangaza kuwa kinywaji Fulani ndio kitadhimini kinywaji hiko ambapo kupitia ukurasa wake wa Twitter aliandika:

Management imenambia kuna Kinywaji kesho kinaingia Rasmi onboard kama Mdhamini Mkuu wa #WasafiFestival2018 …Labda nikitaarifu tu kuwa kijiandae kutengeneza Storck za kutosha maana sio tu kunywewa, bali hata wengine watataka kukiogea kwa promo ntayokipa…. “.

Lakini jambo hilo limekuwa tofauti kwani usiku wa jana Diamond ametangaza kuwa kinywaji rasmi kutakacho dhamini Tamasha la Wasafi Festival ni Pepsi ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika:

https://www.instagram.com/p/BqNo1pehxso/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=irbye9kwk5xm

Mpaka sasa bado haijajulikana Kama Ali Kiba Kupitia Mo Faya bado atadhamini tamasha hilo au ndio basi katupwa kule lakini hawajatoa mrejesho wowote.

“Kukua Kwa Sanaa Haimaanishi Lazima Wasanii Waimbe Matusi, Tubadilike”-Mwana FA

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva anayetamba kwa miondoko yake ya kuchana Mwana FA amesema kuwa kukua kwa sanaa nchini sio lazima wasanii watunge nyimbo zenye maudhui machafu au video zenye muonekano mbaya kwenye jamii, bali ni kufanya kazi kwa bidii na kwa kufuata kanuni na sheria.

Mwana FA amefunguka hayo alipokuwa anaongelea sakata linalokamata headlines hivi sasa la Wimbo wa Rayvanny na Diamond kufungiwa kutokana na kudaiwa kukiuka maadili ya Kitanzania.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Mwana FA alifunguka haya zaidi:

Mimi napenda kuwashauri wasanii kuwa wanapotoa kazi zao wahakikishe wanatoa nyimbo ambazo zitaburudisha Lakini pia zisivuke mipaka ya kuharibu jamii kwasababu ukuaji wa Sanaa sio lazima wasanii watukane kwenye nyimbo au wawe uchi kwenye video zao hapana tubadilike kuna njia nyingi sana zilizo kwenye maadili”.

Mwana FA amesema hayo jana Novemba 14, 2018 muda mfupi baada ya kutoka BASATA ambako alienda kuwaombea msamaha wasanii wa WCB, Diamond na Rayvanny kuhusu kufungiwa wimbo wao wa Mwanza

Hawa Atoa Shukrani Zake Kwa Diamond na WCB Baada Ya Kumaliza Matibabu

Msanii wa Bongo fleva Hawa Said maarufu kama Hawa ntarejea wa Diamond amevunja ukimya Mara Baada ya kumaliza matibabu nchini India na kumshukuru Diamond na WCB.

Msanii Diamond Platnumz na timu nzima ya WCB ndio ilisimamia matibabu yote ya Hawa mpaka anapiga kabisa Baada ya kuugua mpaka kutaka kufa miezi michache iliyopita.

Mrembo huyo amemshukuru Mungu pamoja na Watanzania kwa dua zao kwani mpaka sasa anaendelea vizuri na uvimbe wa tumbo umeondoka kwa asilimia kubwa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Babu Tale ameweka wazi salamu kutoka kwa Hawa:

https://www.instagram.com/p/BqM4FSDlEiw/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1ex61xjcr1qbp

Awali msanii huyo wa kike aliripotiwa kuumwa ugonjwa wa ini lakini alipofanyiwa vipimo nchini India walimkuta na ugonjwa wa moyo.