Lulu Apanga Kuisaidia Jamii Kwa Kupitia Mavazi Yake

Muigizaji wa Bongo movie mrembo Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameibuka na kuweka wazi mipango yake ya kuuza nguo zake na viatu ambapo pesa atakayoipata itakwenda kusaidia wenye uhitaji katika jamii.

Lulu ambaye Mwanzoni alipanga kugawa nguo na viatu kwa mashabiki zake ameamua kubadilisha na badala yake kuuza mavazi hayo kwa watu na kisha pesa atakayoipata itaelekea kusaidia watu wenye shida mbali mbali.

Lulu amethibitisha hayo katika akaunti yake ya Instagram ambapo amekuja na kitu hicho alichokipa jina la “Save My Valentine”.

Wakati Wengine Tumepata Fursa Ya Kuwa Na Furaha Kwa Vile Tulivyonavyo Kuna Baadhi Ya Wenzetu Wamekosa Nafasi Hiyo….. Na HUU NI MPANGO WA MUNGU?, Kuelekea Siku Ya Wapendanao Februari 14,Nimeamua Kuuza Sehemu Ya Nguo Zangu Ambazo Yawezekana Umeshawahi Kuziona au Haujaziona.
Na Pesa Yote Itakayopatikana Kupitia Mauzo Haya Itaenda Kusaidia Vitu/Watu Wenye Uhitaji Katika Jamii.
Please Join me to Save My Valentine.
#Savemyvalentine”.

Lulu Avunja Ukimya Baada Ya Kumaliza Kifungo Chake

Muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu hatimaye amevunja ukimya tangu alipomaliza kifungo chake na kutoa shukrani zake za dhati kwa watu wote.

Mwaka jana Lulu alihukumiwa kifungo cha miaka mieili jela Baada ya kukutwa na hayo a ya kumuua Bila kikusudia aliyekuwa Mpenzi Wake marehemu Steven Kanumba.

Lakini Baada ya kutumikia kifungo chake kwa miezi kadhaa Lulu alipata  msamaha wa kipunguziwa kifungo na kupewa kifungo cha nje ambacho ametumikia na kumaliza Wiki hii.

Baada ya ukimya mrefu kwenye mitandao ya kijamii hatimaye Lulu amefunguka na kuandika haya katika ukurasa wake wa Instagram:

https://www.instagram.com/p/BqO4xVJHf3d/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=fuqi471bjk50

Baba Kanumba Atuma Ujumbe Mzito Kwa Lulu

Baba mzazi wa aliyekuwa staa wa Bongo movie Steven Kanumba, Charles Kanumba ‘Baba Kanumba’ ameibuka na kudai kuwa anamsaka Elizabeth Michael ‘Lulu’ ili ampe ujumbe wake.

Siku chache Baada ya Lulu kumaliza kifungo chake, Baba Kanumba amesema anamsaka Lulu ili aweze kumpa nasaha zake kama baba pamoja na ujumbe aliopewa na babu wa Kanumba.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi, Baba Kanumba alifunguka kuwa siku chache kabla Lulu hajamaliza kifungo, alitokewa na babu wa Kanumba yaani baba yake mzazi ambaye alifariki wakati mwanaye Kanumba anazaliwa na kupewa jina lake.

Babu wa Kanumba alinitokea na kuniambia nimkumbushe Lulu atekeleze mambo ya kimila ambayo nimewahi kumwambia tena ya kwenda kaburini kwa Kanumba na kufanya usafi na kumuombea na hapo atakuwa ameondokana na kile kivuli cha marehemu.

Wakati Lulu anafanya hayo anatakiwa awepo ndugu wa upande wa ukoo wa Kanumba ili kushuhudia na akimaliza hayo atakuwa yupo salama na hatapata mikosi tena kwenye maisha yake na kile kivuli cha Kanumba kitakuwa kimemuondoka lakini vinginevyo atapata taabu”.

Lakini Mzee Kanumba alisema hamlazimishi Lulu kufanya hayo mambo na pia amekiri kuwa hana kinyongo na Lulu hata kidogo na kumtakia kila la kheri maishani.

Sina kinyongo na Lulu, nimefurahi sana yeye kumaliza kifungo na ninamuombea mafanikio makubwa sana kwenye maisha yake, ninahitaji na ninamsaka sana kwa udi na uvumba maana nina mengi ya kumwambia kama mwanangu”.

 

Majizzo: Lulu Wewe ni Mtu Wa Muhimu Kwangu

Mfanyabiashara maarufu na mmiliki wa Kituo cha televisheni cha TV E na kituo ch redio cha EFM Francis Siza maarufu kama Majizzo amezidi kumkumbuka mpenzi wake Elizabeth Michael ‘Lulu’.

Ikiwa leo ni siku ya kusheherekea kumbu kumbu ya kuzaliwa kwa Lulu ambaye yupo gerezani Majizzo amemkumbuka Lulu kwa kumuandikia ujumbe mzito wa kumkumbuka.

Lulu alifungwa miezi kadhaa iliyopita baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake na nguli wa filamu za kibongo Steven Kanumba.

Majizzo amemuandikia ujumbe huo mpenzi wake Lulu Kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amemtaka awe jasiri Lakini pia amemuhaidi kuwa yeye ni mtu muhimu sana maishani mwake:

Nisha Aongea Na Wanaomkashifu Lulu Michael

Msanii wa bongo movies Salma Jabu maarufu kama Nisha  bebe, amefunguka na kuwaonya baadhi ya watu ambao tangu kesi ya msanii lulu michael ianze kusomwa katika mahakama jijini Dar Es Sallam wamekuwa mstari wa mbele kumuongelea mwanadada huyo.Msanii huyo amesema kuwa kwa kipindi kama hichi ambacho Lulu anapitia wakati mgumu sio muda wa kumnanga bali ni muda wa kumpa faraja na kumuombea apite katika kipindi ichi kigumu.

“tangu kesi ya Lulu ianze kusikilizwa upya, kuna watu wamekuwa wakimkashifu kila kukicha, kwa maneno ya ajabu bila kujua kuwa  hakuna ajuaye kesho yake, ni vyema tukampa faraja rafiki yetu, katika kipindi ichi kigumu anachokipitia” alifunguka Nisha

kwa kipindi cha muda mfupi ambacho Lulu amekipitia , akiwa anakabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia kumekuwa na maneno mengi katika mitandao yanayomsema vibaya mwanadada huyo,inawezekana kwa kukusudia au bila kukusudia lakini iki ni kipindi ambacho  mashabiki na watu wa karibu na Lulu wanapaswa kuwa na maneno ya kumpa  faraja ili aweze kushinda kesi hiyo, maamuzi mengine  na hukumu hutolewa na mahakama hivo watu wa mitandaoni hawapaswi kumuhuku msanii huyo.

Hata hivyo,imekuwa ni kama desturi kwa baadhi ya watu ambao wanakuwa haweleweki wamelalia upande gani, wanapoona mtu amefanya vizuri hujitokeza kumpongeza na anapopata matatizo wanaanza kumsema vibaya, huu ndio wakati ambao Lulu anapaswa kuiona nguvu kubwa ya mashabiki wake.

Kesi ya Lulu ambayo ilianza kusikilizwa Oktoba 19 , imeendelea jana ambapo Lulu alipata nafasi ya kuongea na kujitetea kwa nafasi yake,huku mashahidi wengine wakiwa tayari wameshatoa ushahidi wao kuhusu kifo cha marehemu kanumaba ambae alikuwa mpenzi wake na Lulu.Kifo icho kilitokea baada ya msanii huyo wa kike na mpenzi wake kuwa katika ugomvi uliosababisha purukushani za Kanumba kudondoka na kufa papo hapo.

Wapo baadhi ya watu maarufu na wasanii walionyesha kuwa karibu na Lulu Michael katika kipindi hiki kigumu kwa kutokea mahakamani na kumpa maneno yenye faraja mwanadada huyo akiwepo Dr.Cheni, na Muna love ambao muda wote wamekuwa nae mahakamani.

Mashabiki Wapata Wasiwasi Utetezi Wa Lulu Mahakamani

Ikiwa bado kesi inaendelea na utetezi ukizidi kufunguka mahakamani,  jana msanii Elizabeth Lulu Michael alipata nafasi ya kutoa ushahidi na kujitetea kabla ya kupewa hukumu ya kesi ya kuua bila kukusudia inayomkabili.Hata hivyo baadhi ya mashabiki wake katika mtandao wa instagram wamekuwa wakitoa comment zenye kuonyesha  mashaka yao juu ya utetezi wake na kwamba inawezekana wakampoteza msanii wao.Katika baadhi ya utetezi wake ambapo baadhi ya mashabiki wake wanasema kuwa lulu ameanza kutia mashaka katika kutoa ushahidi huo kwa sababu baadhi ya maneno aliyoyatoa yanakuwa yakitia wasiwasi ingawa maamuzi na hukumu ya kesi iyo iko mikononi mwa mamlaka ya mahakama.

mashabiki wamekuwa wakioji, kama kweli lulu alikuwa akipigwa na marehemu mbona hakuwahi kutoa ushahidi wa kipigo chochote alichowahi kupigwa, na je kama siku ya tukio alipigwa na panga kama alivyosema mbona hakuna uthibisho wa alama za kipigo hicho, je kwanini baada ya mpenzi wake kudondoka  Lulu aliondoka na kuelekea coco beach ambapo baadae ndipo alipokamatwa na polisi.Hayo ni baadhi ya maswali na mashaka ambayo mashabiki wake wamekuwa wakijiuliza na kufikia hatu aya kuacha majaji kuamua kesi iyo.

Akiwa kama kijana na msanii ambae ndio anaelekea kufanikiwa zaidi katika kazi zake , Lulu anakabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia ,tukio lililotokea miaka minne iliyopita baada ya kutokea kifo cha mpenzi wake Steven Kanumba.Steven Kanumba alikuwa moja ya wasanii wakongwe waliojitolea kufanya tasnia ya bongo movies kukua.

Hata hivyo, kama mashabiki na familia na watu wa karibu wa msanii huyo, bado hawapaswi kuonyesha wasiwasi ,zaidi ya kumtia moyo na kumuombea kesi ipite, kwa sababu mwisho wa siku  waliokuwepo katika tukio ndio wanaoweza kusema kilichotokea na Lulu ni mmoja wa watu hao na uamuzi wa mwisho siku zote utolewa na mahakama.

kwa muda huu Lulu hapaswi sana kujikita ktika mitandao ya kijamii kwa sababu kuna mngi yanayozunguka ambayo yanaweza kumuongezea matatizo zaidi. TUNAMTAKIA KILA LNEYE KHERI KATIKA HILI!!!

Mdogo wa Kanumba Atoa Ushahidi Kesi Ya Lulu

Ikiwa ni kama muendelezo wa kesi ya mauaji ya bila kukusudia ya mfalme wa bongo moves Steven Kanumba, kesi inayomkabili aliyekuwa mpenzi wake ambae pia kwa sasa ni malkia wa bongo movies na amekuwa akifanya vizuri sana katika kazi yake Elizabeth Lulu Michael, shaidi wa kwanza ametoa ushahidi wake oktoba 19 kuhusu alichokuwa anakijua kuhusu mauaji hayo.

Seth Bosco ambae ni ndugu wa marehemu kanumba alitoa ushahidi wa kile kilichotokea katika kifo hicho miaka mitando iliyopita, akitoa ushahidi huo mbele ya mahakama, Seth Bosco alisema kuwa siku ya tukio la kifo cha Kanumba wawili hao walikuwa na mgogoro ambao ulisababishwa na msanii Lulu Michael kuongea na simu na na simu hiyo ilisadikika kuwa ni ya mwanaume mwingine.

Mbali na Seth Bosco, kulikuwa na shahidi mwingine ambae ni daktari aliepokea mwili wa marehemu ambae siku ya jana hakuweza kufika kutokana na hudhuru ya kuumwa, hata hivyo shahidi huyo anatarajiwa kufika mahakamani kwa ajili ya ushahidi siku inayofuta ya tarehe 20.

Baadhi ya watu walihudhuria mahakamani hapo ni pamoja na Muna akiwa kama rafiki wa karibu wa familia ya Lulu Michael,Dk.Cheni, mama mzazi wa Elizabeth Lulu Michael ,a mama mzazzi wa Kanumba ambae muda wote alionekana kuwa ni mtu  hasiye na furaha.

Steven Kanumba na Elizabeth Michael walikuwa na mahusiano ya kimapenzi ,Kanumba alifariki April 2012 baada ya kuanguka kulikosadikika kulisababishwa na ugomvi  aliokuwa nao na mpenzi wake huyo.Hata hivyo ksi hiyo inayomkabili Lulu Michael ni kesi ya kuua bila kukusudia.Kesi ya Lulu itaendelea leo tarehe 20 Oktoba 2017.

Mungu awatie moyo familia zote zinazohusika katika kesi hii.

Elizabeth Michael  akiwa mahakamani

 

Hii ndo sababu Elizabeth Michael ‘Lulu’ lazima ang’are kushika kila mtu kwenye sherehe yoyote

Muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameweka wazi kuwa yeye lazima apendeze zaidi kuliko mtu yoyote anapoenda kwenye sherehe yoyote ama ata akiwa katika kazi zake za filamu.

Sababu ya Lulu kupenda kupiga pamba ni kuwa anapenda kuvaa na kuonekana tofauti kila mara kwani kung’ara ndo jambo ambalo linampa furaha yeye.

“Mi napenda kupendeza kila wiki, kama nitatoka na kuwa sehemu iliyopendeza na nguo za kipekee kuna wakati nawatania rafiki zangu nikiwaambia waandae tu shughuli nije niwafunike kwa pamba kali,” alisema Lulu.

Elizabeth Lulu aeleza kilichomvutia kwa Ally Remtullah

Mbunifu wa mavazi nchini Ally Remtullah aliandaa sherehe katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam kusherekea kutimiza miaka kumi katika kazi yake ya ubunifu wa mavazi.

Ally Remtullah anatajika sana kwa kazi yake, wasanii wengi na watu mashuhuri wamefanyiwa ubunifu na kushonewa nguo maalum na Ally Remtullah.

Ally Remtullah

Muigizaji wa filamu za Bongo – Elizabeth ‘Lulu’ Michael ni miongoni mwa wasanii ambao walihudhuria sherehe iliyoandaliwa na Ally Remtullah kusherekea kutimiza miaka kumi katika kazi yake ya ubunifu wa mavazi.

Akifanya mahojiano na Bongo 5 kwenye karamu hio, Lulu alisema mtaji wa shilingi elfu arobaini tu alioanza nao Ally ndo kitu kilichomvutia kwake.

“Remtullah ni mtu mwema na anayependa kazi yake, akijaribu mambo mapya huku akiyaimarisha aliyoyapata.  Kilichonivutia kwake ni kwamba mtaji alioanza nao ni mdogo sana wa shilingi elfu arobaini tu.  Hivyo nawaasa Watanzania wasikate tamaa, watumie kiasi chochote cha pesa walicho nacho ili kujilete maendeleo,” alisema Lulu.

Elizabeth ‘Lulu’ Michael

 

 

Mama yake Lulu Elizabeth Micheal adai kuwa hataki kutajiwa mambo na harusi ya mwanae tena

Mama Lulu, Lucresia Karugila amedai kuwa hataki waandishi wa habari kushinda wakimsumbua na suala la ndoa ya mwanae. Mama huyu ambaye hakuoneka kuwa na furaha alisema haya baada ya mwandishi mmoja wa Global publishers kujaribu kujua kikao cha harusi hiyo kimefika wapi.

Mama Lulu

Lucresia Karugila anasemekana kuwa alidai kuwa hana kitu cha kusema kuhusiana na ndoa ya lulu kwani hakuna anayetaarifa za kudhibitisha kuwa mwanae anaoleka na alikyekuwa mpenzi wa Hamisa Mobeto, Majay.

Mama huyo aliendelea kudai kuwa amechoswa na suala hili na kwa sasa hataki kuhusishwa na mambo ya kijinga. Mazungumzo yake na mwandishi huyo yalienda hivi.

Amani: Mama nataka kujua nini kinaendelea kwenye vikao vya mwisho vya harusi ya Lulu na ….(akitajiwa jina
la mchumba wa Lulu), wewe kama mama unasemaje?

Mama Lulu: Sitaki kabisa, kwanza una mama wewe? Sitaki kusikia ukinifuatilia na nilishakuambia tangu zamani, sitaki uniulize mambo ya kijinga kama hayo, hayanihusu kwa vyovyote, tena nisikusikie
kabisa, niache nifanye mambo yangu ya msingi, unasikia? Achana na mimi, tiiiii….titiiiiii (akakata simu).
Jitihada za kumpata Lulu kwa lengo la ufafanuzi juu ya jambo hilo la heri ziligonga mwamba kufuatia simu yake kutokuwa hewani hivyo jitihada bado zinaendelea.

Elizabeth Lulu awajibu wanaomsema kuwa ni mfupi

Muigizaji wa filamu za Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ amewajibu wanaomnanga kwenye mitandaoni ya kijamii kwasababu ya ufupi wake.

Staa huyo amewataka wakosoaji wake waache kujadili ufupi wake ambao sasa umekuwa mada mara kwa mara mitandaoni.

Lulu alijitetea kwa kusema wakosoaji wake wanafaa wampime kwa akili zake maana yeye harefuki mwili ila anarefuka kiakili.

“Niwaulize tu wanamuoanaje Lulu wa miaka ile na Lulu wa sasa? Mimi sina haja ya kukua umbo halafu akili ikawa ndogo, nakua kiakili hivyo hata nikiwa na umbo hilihili miaka yote sioni tatizo,” alisema Lulu.

 

“Natarajiwa kuwa mke halali hivi karibuni” Elizabeth Michael ‘Lulu’ afunguka kuhusu harusi atakayofanya

Ole wao wanaume waliotaka uhusiano wa kimapenzi na Elizabeth Michael ‘Lulu’. Staa huyo wa Bongo movies atakua bibi wa mtu hivi karibuni.

Bahati, msanii wa nyimbo za injili kutoka Kenya, ni miongoni mwa wanaume wengi waliotaka kumchumbia Lulu.

Lulu sasa yupo tayari kufanya harusi na mpenzi wake wa muda mrefu Francis Shiza ‘Dj Majizo’- mmiliki wa Redio EFM.

Elizabeth Lulu na Francis Shiza ‘Dj Majizo’

Habari hii imetokea baadaya ya kuzuka uvumi kuwa Lulu aliachana na mpenzi wake.  Akizungumza na Mtanzania, Lulu alisema kuwa wanaotamani aachane na DJ Majizo watapigwa na duwaa atakapofanya harusi na mpenzi wake.

“Siku zinakaribia na karibu tarehe ya ndoa yangu itatangazwa kwa uwezo wa Mungu, hapo ndipo waliotamani tuachane wataziba midomo, maana natarajiwa kuwa mke halali hivi karibuni,’’ Lulu alinukuliwa na Mtanzania.