Aunty Ezekiel ataja njia aliyotumia kupunguza unene wa mwili wake!

Mrembo wa filamu Bongo za bongo Aunty Ezekiel amefunguka kueleza namna alivyoweza kupunguza mwili wake ulionenepa baada ya kuzaa cookie miaka 3 iliyopita.

Aunty Ezekiel

Muigizaji huyu alisema kuwa alishindwa kupunguza mwili wake hata baada ya kujaribu njia kadhaa. Akizungumza na motomoto news mrembo huyu alisema kuwa ilimbidi kusafiri hadi nchini Thailand kufuata dawa ya kupunguza unene.

Hii ni baada ya kuona kuwa mwili wake ulikuwa unanenepa na kwa sababu ulimnyima raha na kumfanya aonekane mzee basi akaenda Thailand ambapo alipata dawa inayomsaidia sana. Ezekiel alisema;

“Dah, yaani hata nikivaa nguo najiona wazi sipendezi hivyo katika pitapita yangu nikaambiwa kuna dawa nzuri Thailand, nikaenda na baada ya kuanza kutumia, naona ina manufaa makubwa na nadhani inaweza kuwasaidia watu wengine wasiopenda unene,”

“You are a super powerful mom” Idris Sultan amwandikia Zari ujumbe wa kumtia nguvu baada ya mama yake kufariki

Sio katika wote utampata Idris Sultan akiwa serious. Wakati wote mchekeshaji huyu huwa na utani mwingi hasa kupitia mtandao wake wa Instagram.

Hata hivi leo ameonekana kuonesha kuwa pia yeye anaweza kuwa mtu wa kumtia nguvu kupitia maneno yake. Leo amemwandikia Zari ujumbe ambao umewaacha wengi kama wameduwaa baada.

Idris alifanya hivi baada ya Zari kuwajulisha mashabiki wake kuwa mama alifariki leo asubui. Mchekeshaji huyo aliandika kusema;

Amber Lulu awajibu wanaomsingizia kuwa anatumia ‘unga

Hakuna kitu ambacho kinachomkera Lulu Amber kama watu wanaodai kuwa anatumia madawa ya kulevya! Amber Lulu ambaye ni msanii na mrembo wa video za bongo amewakanya watu hawa akiwaambia waje basi wampeleke ‘sober house’ (rehab).

 

Msanii huyu alifunguka kuhusu maneno haya akizungumza na 3-Tamu ya Tanzania. Amber Lulu aliendelea kuwa wanaomsema wanapaswa kumpeleka apate tiba badala ya kumsema.

“Nimekuwa nikisemwa kila siku kuwa ninatumia unga, sasa nasema kama kuna mtu ana uhakika na hilo, basi anipeleke sober house nikatibiwe. Ni vyema watu wakajua kuwa hata mimi ni binadamu, ninaumizwa na kuse­mwasemwa,”

Hata hivyo alisema kuwa mtumiaji wa Unga hujulikana, kwa hivyo wampe muda waone ikiwa yeye anatumia madawa haya ya kulevya.

Ni kweli kuwa Vanessa Mdee na Juma Jux sababu ya Jacqueline Patrick?

Kuna fununu kuwa Vanessa Mdee na Juma Jux waliachana kutokana na sababu zisijojulikana! Hata hivyo kulingana na Ubuyu wa global publishers, kunauwezekano kuwa wawili hawa waliachana kwa sababu ya aliyekuwa mpenzi wa Juma Jux wa zamani, Jacqueline Patrick ‘Jack’.

Juma Jux na aliyekuwa mpenzi wake, Jacqueline Patrick ‘Jack’.

Jacqueline Patrick ambaye anatarajiwa kuachiliwa kutoka sasa za gereza nchini China, amesemekana kuwa yeye ndiye chanzo cha wawili hawa kuachana. Kulingana na habari mitandaoni, jack anatarajiwa kuachiliwa mwezi huu na ndio maana Jux yuko China akimgonja mrembo aliyetiwa ndani baada ya kupatwa akisafirisha madawa ya kulevya China.

Chanzo cha maneno haya kiliwambia Global publishers Kuwa;

“Unajua Jack anatarajiwa kutoka gerezani ndani ya mwezi huu na ikumbukwe wakati anafungwa alikuwa bado kwenye uhusiano wa kimapenzi na Jux hivyo ndiyo maana mapenzi ya Jux na Vanessa yamekwisha. Kwa sasa Jux yupo nchini China na inasemekana atarudi na Jack kwani inadaiwa ameenda huko kwa ajili ya shughuli zake binafsi lakini pia anamsubiria Jack atoke lupango na wataendelea na mapenzi yao kama zamani,”

Hata hivyo Juma Jux alikataa kudhibitisha ikiwa habari hizi ni za kweli.

“Nawasihi wakongwe ambao hawajaoa nao waoe kwani” Profesa Jay asema!

Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule anayefahamika sana kama Profesa Jay amefunguka kuwasihi wakongwe wa muziki kutia bidii ili pia wao waweze kuoa kama alivyofanya hivi karibuni na mpenzi wake, Grace.

Profesa Jay

Profesa Jay ambaye alianza muziki akiwa na umri mdogo ameonelea kuwa wasanii ambao wamekuwa naye kwenye muziki kwa miaka mingi pia waoe kwani Mungu atawapa baraka zaidi, baada ya kutulia na mwanamke mmoja badala ya kuwabadilisha kila wakati,

Rapa huyu wa bongo alisema haya akizungumza na Wikienda huku akisema,

 Nawasihi wakongwe ambao hawajaoa nao waoe kwani pale wanapokabidhi mapenzi yao mbele za Mungu ndipo baraka zaidi na neema za Mungu zinaambatana nao katika maisha yao yote kwa sababu ndoa ni furaha na amani pia.

Hata hivyo AY ameonekana kuzifuata nyayo zake baada ya kumvisha (engage) Pete mrembo wake siku kadhaa zilizopita.

“Vanessa Mdee ananipa stress” Lulu Diva afunguka

Mwanamziki Lulu Diva ambaye anaonekana kutamba Afrika Mashariki kupitia wimbo wake Wa utamu amedai kuwa Vanessa Mdee ni mwanamke anayempa stress kila kukicha.

Vanessa Mdee

Mrembo huyu alisema haya katika mahojiano yake na Uwazi Showbiz. Kulingana na Lulu Diva, Vanessa Mdee ndiye ni mwanamziki ambaye ameweza kupenya kwenye muziki haraka huku akipata kollabo na wasanii wa kutoka inje – kitu ambacho wasanii wa kike bado hawajaweza kufanya. Lulu alisema:

“Bongo kwa wanamuziki wa kike kiukweli anayenipa stress ni Vee, kila mtu anafahamu kuwa ni mkali na anajituma kwenye muziki wake, sasa mimi malengo yangu ni kufanya kazi kwa juhudi ili kufika mbali, kwanza kuwa hapo alipo yeye na baadaye kupita zaidi,“

Hata hivyo Lulu Diva alisema kuwa anandoto za
kufanya muziki wa kimataifa siku moja.

Vanessa Mdee awajibu mashabiki wanaodai kuwa Video yake mpya inafanana na Energy ya Keri Hilson

Mrembo Vanessa Mdee ameiwachia kazi yake mpya ‘Kisela’ ambayo imeonesha uwezo wa kufanya vyema ingawa wengi wanadai kuwa inafanana sana na ile ya Keri Hilson ‘Energy.’

Akiongea na kipindi cha The Playlist cha Times FM, Vanessa kwa mara ya kwanza alisema kuwa hakutarajia kuwa mashabiki wangefikiria kuwa aliiga wimbo huo wa Keri Hilson huku akiongeza kuwa uandishi wa script ya video ya wimbo wake ulifanywa na director wa video hiyo, Clarence Peter. Vmoney alisema,

“To be honest mimi napenda sana huo wimbo, I love the video, I love Keri Hilson but I did,’t think about that video at all. In fact hii script mimi sikuandika kabisa, usually na play part kwenye script write lakini sikuandika kabisa, aliandika Clarence, alinitumia the hall script. When I was doing I said okay great but now when people started to refer nikasema duuh! Maybe but there’s no original concept,”

 

Hata hivyo kunauwezekano kuwa inspiration ilitoka kwenye wimbo huo wa Energy kwani pia maudhui yake yanaambatana.

“Fahyma anichungi” Rayvanny asema haya baada ya video yake akiwa na Gigy Money kusambaa mitandaoni

Huenda Rayvanny anafuata nyayo za Diamond Platnumz – hii ni baada ya video yake na Gigy Money iliposambaa mitandaoni huku wakionekana kuwa na ukaribu usio wa kiurafiki tu.

Hata hivyo magnificent huyo wa tuzo ya BET 2017 ameiambia Times Fm kuwa yeye na Gigy Money ni marafiki tu na pia mpenzi wake Fahyma anafahamu haya. Aliendelea kuongeza kuwa yeye na Fahyma hawachungani kwa hivyo hili si jambo linaloweza kumletea shida na mama wa mtoto wake. Msanii huyo alisema,

“Hawezi kuchukia, halafu pia mimi sichungwi am live my life, president of own life, so nobody anaweza akaingilia akasema usifanye hiki, so Fahyma hana noma sometimes anaweza akafanya vitu vyake mimi simuingilii.”

Hata hivyo alidai kuwa video yake na Gigy Money ilikuwa ya utani lakini wambea waliona kuineza ilikumletea utata.

“It’s just a joke, Gigy ni mshikaji wangu na ni wa Mbeya pia, namjua before hajanza mbwembwe zake na ni mtu ambaye yupo happy muda wote mimi naona anaenjoy maisha yake”.

Peter Msechu asema haya kuhusu mwili wake

Muimbaji wa nyimbo za bongo Peter Msechu ni mwanaume ambaye anajitambua na kujiamini. Msechu alionesha haya hivi karibuni katika mahojiano yake katika kipindi cha 5 selekt.

Akizungumza Msechu alidai kuwa hana tatizo lolote na ukubwa wa mwili wake. Aliendelea kusema haimzuii wakati wa mahusiano ya mapenzi huku akiongeza kuwa yeye hufumiwa kila siku anafumaniwa wanaodai kuwa wana watoto wao. Alisema,

“Wakati Timbulo anasema mshumaa mambo ya kuachwa mimi na Yakawa yaani na wanawake wengi, mimi nafumaniwa kila siku kwa hiyo mimi na nguvu ya kujitahidi kwenda na mwili wangu huu,”

Msechu aliendelea kwa kusema,

“Mimi nafanya sana mazoezi watu wengine ooh Msechu sijui mnene, mimi wanawake mtaani wanaongozana nasingiziwa kila kukicha watoto eti watoto wangu, kwa hiyo msinichukulie poa niko vizuri kila idara.”

Z-Anto amtaja mnigeria atakaye shirikiana na yeye hivi karibuni

Z-Anto ambaye ni mmoja wa wasanii ambao walianza muziki zamani ameonyesha uwezo wa kurudisha nyimbo kama za hapo mbeleni baada ya kuachilia nyimbo kadhaa.

Hata hivyo bado hajapata nafasi ya kushirikiana na wasanii wengi lakini kuna uvumi kuwa staa huyu wa Bongo Fleva, huenda akafanya kolabo na pacha wa Kundi la P-Square, Peter Okoye.

Akizungumza na Over Ze Weekend, Z-Anto alianza kuupongeza uongozi wake wa South For Life (SFL) kwa kumsaidia kuachia nyimbo mzuri zinazovuma kwa sasa. Aliendelea kuwashukuru kwa kkumuunganisha na wasanii wakubwa akiwemo Peter Okoye. Z-Anto alisema,

“Ni furaha ya juu niliyonayo. Yote kwa sasa nawaachia South For Life kwani nipo chini yao, endapo mipango itakaa poa basi mtanisikia nikipaa kimataifa,”

Mashabiki wake Wa Afrika mashariki kwa hivi sasa wanaingojea kuiona project yake.

Hawa kutoka ‘Nitarejea’ alioshirikishwa na Diamond adaiwa kupotelea kwenye vileo!

Nitarejea ni wimbo ambao bado unafanya vizuri Hata baada ya kuachiwa mwaka Wa 2013. Diamond Platnumz alimshirikisha muimbaji anayejulikana kama Hawa na kutokana na sauti yake nzuri, mrembo huyu alitarajiwa kwenda mbali lakini hivyo sivyo mambo yalienda.

Hawa anasemekana kuwa alipata mtoto wake Wa kwanza anayedaiwa kuwa mtoto wa Diamond Platnumz na baadaye akafunga ndoa na mwanaume mwingine ambaye amemsababisha kuingilia vileo kutokana na ‘stress.’

Sasa hivi mrembo huyo amekiri kuwa maisha yake ilipotelea kwenye unywaji wa pombe kali aina ya gongo, kiasi cha kumfanya apoteze mwelekeo maishani mwake.

Akizungumza na Global TV Hawa alisema kuwa alijipata kwenye maisha haya baada ya mumewe kuondoka na kumuacha bila mawasiliano yoyote kwa muda wa miaka miwili baada ya kukaa kwenye ndoa yao kwa muda mfupi.

Kutoka na kufikiria sana, Hawa alitafuta namna ya kutoa ‘stress’ na akaingia kwenye vileo ambavyo vimemdhoofisha kimwili. Amedai kuwa amekonda huku akiomba msaada kutoka kwa mashabiki na wadau kumsaidia kuepuka maisha haya ambayo yanampeleka vibaya.

 

Profesa Jay atajavitu ambavyo vilimpendeza katika harusi yake

Msanii na mbunge kutoka bongo Profesa Jay alifunga pingu za maisha na mpenzi wake Grace – huku akiwavutia wengi kutoka Tanzania.

Sherehe ya harusi yake ilihudhuriwa na wasanii kama Diamond Platnumz, AY na wengi waliotumbuiza wageni na wazazi wa Profesa Jay na Grace.

Hata hivyo hivi karibuni msanii huyu alifunguka kutaja mambo matatu yaliyomvutia Profesa Jay katika harusi yake. Akizungumza na FNL ya EATV Profesa alisema,

“Chakwanza ni support kubwa ya watu wangu wa mtaa, nikaona watu wote wapo pale especially wasanii wenzangu walikuwepo sana sana, wengine walishindwa kuja kwa sababu mbali mbali,”

Aliongeza kusema;

“Pili media ime-play part yake vizuri sana, lakini kikubwa mbacho namshukuru Mwenyenzi Mungu mbele za haki nimejitahidi hata kuungainsha siasa zetu za Tanzania. Viongozi wote waliopata kuongea  walisema huyu jamaa ametuunganisha, watu wa vyama vyote walikuwa pale, watu wa dini zote walikuwepo pale, ni kitu kikubwa namshukuru Mungu,”

Huyu ndiye mrembo anayetoka na Gnex_thebaddest Wa Clouds FM?

Kuna fununu kuwa mtangazaji wa CloudsFM Gnex_thebaddest anatoka kimapenzi na mrembo mmoja ambaye ni mwanahabari kutoka Kenya, Kamene Goro.

Hii ni baada ya Gnex_thebaddest kuachia picha kadhaa kupitia mtandao wake Wa Instagram huku akimsifia mchumba wake kwa maneno matatu.

Kamene Goro pia amekuwa akiweka picha za Gnex_thebaddest akiziambatanisha na ujumbe unaodhibitisha kuwa wawili hawa wanauwezekano wa kuwa wapenzi.

Mrembo huyu wa Kenya anafanya kazi na kituo kinachoitwa Ebru Tv na ni mtangazaji wa habari za adhuhuri na anatambulika sana kutokana na umbo lake linalowatia wengi wasiwasi. Tazama picha zake hapa:

 

Sababu ya kesi ya Masogange kutosikilizwa mwezi huu

Agnes Gerald anayetambulika kama Masogange bado anangoja kusikilizwa kwa kesi yake baada ya kutofika mahakamani Jana, Julai 13, 2017 kama ilivyohutajika.

Kulingana na wakili wa mrembo huyu, inasemekana kuwa hangeweza kufika kutoka na kuumwa kwa mwili. Wakili wake, Reuben Simwanza akizungumza na hakimu aliomba radhi kwa mteja wake.

Agnes Masogange
Agnes Masogange

Hata hivyo wakili wa Serikali, Constantine Kakula, hakufurahishwa na maneno haya huku akikumbusha mahakamani kuwa hapo mbeleni Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, alikuwa amepeana amri ya kuwa kesi hiyo ianze kusikilizwa Jana.

Agnes Masogange

Wakili wa Masogange aliweza kuisihi mahakama kuihairisha kesi kesi hiyo hadi July 25, 2017. Masogange hata hivyo ameshtakiwa kwa makosa ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroine na Oxazepam na Heroine.

County Boy aeleza mipango yake ya kuwa kutanisha Alikiba na Diamond Platnumz

Mwananziki Country Boy kutoka Tanzania amefunguka kudai kuwa ana mipango ya kuwakutanisha Diamond Platnumz na Alikiba – kitu ambacho tunajua ni ngumu kufanyika.

Msanii huyu akizungumza na Daladala Beat ya Magic Fm alidai kuwa kwa hivi sasa anataka kuwashirikisha wasanii hawa kwa wimbo wake mpya, huku akitarajia kuwa watasikizana. Country Boy alisema;

“Round hii nataka nilete different sound kwa sababu tayari am rapper nataka nitengeneze sound mpya. Nawataka hawa malegendary wawili, hapa Alikiba, hapa Diamond ila siwashirikishi katika track moja, kila mtu na ngoma yake,”

Aliendelea kwa kusema…

“Kila mtu na upande wake natengeneza sound mpya, nahisi nitaleta kitu kikubwa. Ninachoshukuru kwa Mungu mimi nipo flexible naweza kurap katika beat yoyote,”

Hata hivyo wacha tuone Kama Country Boy ataweza kufanya hivi.

Aunty Ezekiel aachia picha mpya kuonesha Princess Cookie alivyokuwa mkubwa!

Muigizaji wa filamu Aunty Ezekiel anafurahia kumuona Cookie akiendelea kuwa mkubwa kila kuchao.

Cookie

Mrembo huyu hivi karibuni aliachia picha mpya za mtoto wake kupitia mtandao wa Instagram huku mashabiki wakiduwaa kumuona alivyokuwa.

Sasa hivi cookie ako karibu kufikisha miaka minne na tunavyojua ni kuwa mtoto huyu amejiunga na shule ili kujifahamisha na wenzake.

Hata hivyo, Ezekiel anaonekana ameipa kazi yake ya uigizaji ili kumpa mtoto wake attention. Tazama picha zao mpya hapa chini;