Wolper akumbwa na haya baada kuonyesha uso wa mpenzi wake

Wolper ambaye anatoka na kijana amayeaminika kuwa Mudigi wake ameanza kuchambuliwa na mashabiki ambao wanamtambua.

Ingawa wameamua kutoficha mapenzi yao, kuna tatizo kwani picha moja ya Brown imeachiwa kwenye mitandaoni akionekana na mwanaume mwenzake na hivi sasa watu wanadai kuwa Brown amewai kuwa na mpenzi wa jinsia moja.

Mpenzi mpya wa Wolper, Brown

Ingawa hakuna dhibitisho tosha kuhusu picha hiyo, wengi bado wajiuliza maswali kwani Brown na huyo mwanaume huyo wanaonekana wakiwa katika pozi kitandani.

Hata hivyo Brown na Wolper hawajazungumzia jambo hili…lakini tunatarajia kuyasikia maoni yao. Tazama picha hiyo hapa;

” Avril hana talanta ya kuimba!” Msanii wa bongo AT amchana Avril

Msanii wa muziki kutoka bongo anayefanya muziki wa miondoko ya mduara nchini, AT hivi karibuni alidai kuwa mrembo Avril kutoka Kenya hapaswi kuwa akifanya muziki kwa sababu hana talanta.

Avril

Muimbaji huyo anayetoka zanzibar alisema hayo kupitia cloudsfm huku akisema wengi wanamsifia Avril ilhali yeye huimba vibaya. AT alidai kuwa ashawai kufanya kazi na mrembo huyo lakini ilibidi amfute kwenye wimbo wake baada ya kuimba vibaya. Alisema,

 “Nilishaenda ogopa Dj kufanya wimbo na Avril lakini Avril aliimba utumbo mtupu mimi nilimtoa. Avril sio msanii sio kabisa yani sio msanii ambaye unategemea kumsikia halafu unamkuta kama vile alivyo Linah…no yani she very fake kabisa yani mpaka nimeshangaa nilikuwa najua jina lake ni kubwa anauwezo mkubwa lakini nimeenda kufanya nae wimbo aisee ni shughuli mpaka nimemtoa nimemuweka Alice wa THT na ngoma imekuwa kali lakini sijaitoa”

Aliendelea kwa kusema kuwa anachotambua kwenye muziki ni sauti ila sio ukubwa wa jina la msanii.

Ujumbe wa Jaydee kwa profesa Jay baada ya kufunga ndoa

Jaydee ambaye ni msanii wa zamani katika industry ya Bongo amemsifia Profesa Jay baada ya kufunga ndoa ya kifahari na mpenzi wake anayejulikana kama Grace.

Harusi hiyo iliyofanyika katika kanisa la koliki la Joseph, Dar Es Salam na baadae sherehe karika Mlimani city hall – huku wasanii wengi wakijitokeza kumpa support Profesa Jay.

Jaydee ambaye alikuwa miongoni mwa marafiki waliojitokeza alimpa pongezi Profesa Jay na mkewe hivi karibuni akizungumza na Planet Bongo ya EA Radio. Jaydee alisema,

“Kwanza nimpongeze Prof Jay kwa hatua aliyochukua, ni hatua nzuri katika maisha kwa sababu kwanza ni kuzaliwa, pili ni kuoa au kuolewa na ya tatu ni kufa, kwa hiyo hii ni harusi ya pili katika maisha yake nimpongeze sana kwa uamuzi alioufikia.”

Msanii huyu aliendelea kwa kusema,

“Nimtakie kila la kheri katika maisha yake ya ndoa yenye furaha na mafanikio. Professor kama kaka yangu na kama rafiki yangu ni mambo mengi tumepitia pamoja, tumeweza kusapotiana katika kazi na mambo mengine, kwa hiyo ni furaha kwangu, si kama msanii mwenzake bali kama mwanafamilia,”

Pongezi mingi kwa wapenzi hawa kutoka Ghafla Tanzania.

Wolper adhibitisha kuwa kijana huyu ndiye mpenzi wake mpya! (Picha)

Baada ya kutemana na Harmonize, Wolper anaonekana ashapata mpenzi mpya na kulingana na ubuyu….mrembo huyu anatoka na kijana mdogo na pia ni mrembo kumliko Harmonize.

Hata hivyo Wolper amedhibitisha kuwa kwa sasa anatoka kimapenzi na mwanaume anayetambulika kama Brown. Akizungumza na Wikendi ya Global publishers. Mazungumzo yao yalienda hivi;

Wikienda: Kwa hiyo ni kweli Brown ndiye mpenzi wako kwa sasa?
Wolper: Ndiyo. Kwani kuna sababu gani ya kuficha? Awali hakuna mtu aliyejua lakini kwa sasa tuna muda kama miezi miwili, naona watu ndiyo wanajua sasa hivi.

Wikienda: Je, kweli kwamba unafanya hivyo kumkomoa Harmonize kwa vile inasemekana naye ana mwanamke mjamzito wa Kizungu?
Wolper: Aaah! Wapi! Ili iweje sasa? Kila mtu ana maisha yake jamani.

Wikienda: Je, huyo Brown ni nani au ana wasifu gani?
Wolper: Ndiyo kwanza watu wanaanza kumfahamu, wasijali watamjua tu.

Wikienda: Inasemekana umemzidi umri kama ilivyokuwa kwa Harmonize, je, ni kweli unapenda vijana wadogo?
Wolper: Nani kasema mdogo? Hebu watu waniache nitulize mawazo miye!

Tazama picha hiyo hapa;

Harmorapa amsifia Alikiba kwa kusema haya

Harmorapa ni msanii ambaye anaitambua kazi ya Alikiba na ingawa wawili hawa hawajapata nafasi ya kukutana…hii haimaniishi kuwa Harmorapa hatamani kufanya kazi na King Kiba.

Katika interview aliyoifanya hivi karibuni, Harmorapa alidai kuwa Alikiba ni msanii mwenye bidii na watanzania wanapaswa kuitilia kazi yake maanani kwa sababu Kiba anabusara kuwashinda wengi Wa kisasa. Harmorapa alisema,

Katika vitu ambavyo tunatakiwa kujivunia ni kuwa na wasanii ambao wanatangaza taifa letu mbele na kujivunia juhudi zao. Naimani heshima, busara na juhudi ndiyo nyenzo pekee wazungu kumwaga wino na kumkaribisha Alikiba meza moja na kumkabidhi kampuni kubwa ya Rockstar4000 kuwa mmiliki mmoja wapo na Director.

Rapa huyu wa Tanzania aliendelea kusisitiza kuwa wasanii wanafaa kujifunza na kujivunia uwepo wa Alikiba kwa kuwa muziki wa bongofleva ulitambulika zaidi baada ya Alikiba kuachia nyimbo zake za kwanza.

Wasanii wa Tanzania inabidi tujifunze na kujisifu kwa kuwa na King Alikiba maana anautendea haki mziki wetu wa bongo fleva, hongera zangu zizidi kutiririka kwa King wewe uliokosa mfano hapa bongo.

Wema Sepetu afika Mahakamani kusikiza kesi yake ya kosa la kukamatwa na bangi

Mrembo Wema Sepetu ambaye alikamatwa miezi kadhaa baada ya kupatikana na misokoto ya bangi nyumbani kwake alifika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisuta mapema leo kuisikiza kesi yake.

Wema Sepetu alifika na mama yake, Mariam Sepetu na watuhumiwa wenzake wawili kuisikiza kesi na kulingana na ripoti mitandaoni, Wema Sepetu anasemekana kuwa amekana mashataka hayo na hivyo kesi yake kusogezwa mpaka tarehe 1 mwezi wa nane ambapo itaanza kusikilizwa.

Wema Sepetu (courtesy of Millard Ayo)

Kesi hii hata hivyo imekuwa ikisogezwa tangu miezi ya kwanza ya huu mwaka na bado Mahakama inadai kuwa wanamchunguza mrembo huyu huku wakiwapa mashabiki kiwewe kwani wanaona kuwa kesi hii imevutwa sana.

Wema atafikia mahakamani mwezi ujao kujua kitachotokea sasa.

Nandy afunguka kueleza msanii anayetamani sana kufanya kazi naye!

Nandy ambaye anafanya vizuri kwenye Bongo music kwa hivi sasa anawatisha wasanii wengi. Sio tu kwa urembo wake lakini kwa Sauti yake nzuri ambaye imeipa wimbo wake “one day” uwezo wa kutamba Afrika Mashariki.

Hata hivyo yeye Kama msanii wa kisasa anatamani sana kufanya kazi na wasanii wakubwa. Akizungumza kwenye interview na Clouds FM Top 20 Nandy alimtaja Rayvanny msanii ambaye anatamani kufanya kazi na yeye. Nandy alisema;

 

“Nawaelewa wote lakini kwa haraka haraka nikipewa chance kwa mtu wa WCB kufanya nae ngoma nitafanya na Rayvanny. Nahisi kama tuna chemistry ile ambayo tunaweza tukaendana, yaani ukiwasikiliza mashairi yao wewe ndio unajua unafiti wapi, kwa hiyo mimi naona kwa Rayvanny nafiti.”

Aliendelea kwa kudai kuwa anatamani sana kufanya remix ya wimbo wa Saida Karoli Wa hapo zamani…Iwapo hawezi kupata kufanya kazi na mkongwe wa muziki, Saida Karoli. Nandy alisema,

“natamani sana hata anipe ngoma yake ya zamani niifanyie remix na sijui ni ipi kwa sababu kafumua!, sijui nitaimbaje. Natamani anipe nifanye verse na kama alifanya chorus ibaki pale pale, halafu mimi nirudie zile verse, I hope atakubali.”

Hata hivyo kwa sasa Nandy anatamba na kufanya vizuri na wimbo wake mpya unaojiita ‘Wasikudanganye’.

Harmonize aachia picha mpya na mpenzi wake mpya, lakini hana ujauzito!

Muimbaji kutoka Wasafi records Harmonize amewaacha wengi wakijiuliza mimba ya mpenzi wake iko wapi. Hii ni baada ya kuachia picha mpya ambapo anaonekana akistahereka na mrembo huyo.

Hata hivyo Harmonize aliamua kuzima comment section yake ilimashabiki wake wasimchane kwa maneno. Katika picha hizi muimbaji huyo anaonekana akiwa na mrembo wake huyo akicheza pool table mbele ya nyumba ya kifahari inayosemekana wawili hao wanaishi.

Katika moja ya picha hizo msanii huyo aliweka wazi uwanja wa kutuma komenti lakini mashabiki wengi walionekana kuacha komenti mbaya kwa mpenzi wake na kwa hivyo akafunga komenti kwenye picha hizo zingine.

Tazama picha hizo hapa;

Chini Bees amjibu Chid Benz baada ya kumchana

Baada ya Chid Benz kumwambia msanii mwenzake Chin Bees awembunifu na kutafuta jina lingine…. Chin Bees ameamua kumjibu mwenzake.

Wawili hawa ambao wanaonekana kuwa na beef kutokana na kufanana kwa majina yao, uenda wakakosana baada ya Chin Bees kusema kuwa hawezi kubadilisha jina ili kumkwepa Chid Benz.

 

Akizungumza kwenye mahojiano na E-News ya EATV, Chin Bees ambaye ni mmoja wa wasanii wanaotamba kupiti nyimbo zake za bongo Fleva aliweka wazi kuwa hana mipango ya kubadilisha jina kwa kuwa hata yafanani. Chin Bees alisema,

“Mimi siwezi kubadilisha jina kwa sababu ya Chid Benz kwa sababu halifananini, very different. Mimi nafanya muziki wangu, siwezi nikakaa nipiganie jina, hivyo bro kama anahitaji jina dah!, sidhani kama jina langu linaendana na lake  me am do my thing.”

Haya basi tutazame tuone watakachafanya sasa!

Nuh Mziwanda afanyiwa upasuaji wa shingo

Msanii wa Bongo Nuh Mziwanda ameandika ujumbe kuwashukuru madaktari wa hospitali ya Mwananyala kwa kumfanyia upasuaji wa shingo baada ya kupata maumivu makali shingoni.

Nuh Mziwanda anayejulikana kwa hit song yake ya Jike Shupa, aliweka picha huku akionekana na bandage shingoni na tabasamu usoni kwa upasuaji salama.

Ingawa bado hajafunguka kusema kilichotokea, Nuh aliandika ujumbe kusema,

“Thanks Jesus….thanks MY SUPER DR KIWALE BINGWA kabisa wa upasuaji ‘Na MWANANYAMARA HOSPITAL kwa surgery (Upasuaji)uliokua chini ya shingo yangu’ bila kusahau MAMA yangu na ndugu zangu waliokua pamoja na mimi.naomba Maombi yenu Mashabiki wangu nirudi katika hali yangu na Kazi ziendelee.Love you.”

Mbunge na msanii wa hip hop Profesa Jay kufunga ndoa na mpenzi wake

Profesa Jay ambaye anajulikana na wengi kutokana na nyimbo zake za hiphop amekuwa kimya kwa muda sasa tangu kuwa mbuge wa Jimbo la Mikumi kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Hata hivyo bado anatamba kwa wimbo wake aliouachia mwaka jana akimshirikisha Sholo Mwamba.

Sasa hivi msanii huyo yuko kwenye maandalizi ya ndoa yake na mpenzi wake anayefahamika kama Grace Mgonjo. Profesa alitangaza haya kupitia mtandao wake wa Instagram alipoandika kuonyesha send off yake ilivyofanyika akina na marafika zake.

Tazama ujumbe wake;

Mke wa Roma amchana mrembo aliyemkalia Roma akitumbuiza jukuwaani hivi karibuni

Kuolewa na msanii ni kitu ngumu sana kwani unapaswa kuwa na subra ya kuelewa kuwa hiyo pia ni kazi. Hata hivyo mke wa Roma ameonyesha kukerwa na mwanamke aliyemkalia Roma wakati alipokuwa akipiga show yake ya kwanza tangu tokeo lake la kutekwa miezi kadhaa iliyopita.

Mrembo huyu alifunguka kuhusu tekeo hilo kupitia mtandao wake wa Instagram huku akisema kuwa alitamani sana kupanda jukwaani kumshusha yule binti….aliandika kusema,

 

Kuwa Na Mume Msanii Wakati Mwingine Ni #Stress Nyie Acheni Tu Jamani!!!
.
.
Aaaf kuna vibinti ndiyo kama vinafanya makusudi

Kama Huyu!!!
Nilitamani Nipande Jukwaani Nikamshushe.
Sijui Hata alivyombeba alimpeleka wapi!!!!
.
.
Aaaah Ntafanyaje Mie Na Ndiyo Kazi Inayonifanya Niende Saloon!! .
.
By the way uliua…Show nzuri kama kawaida yako
Cc @usimsahau_mchizi_roma@usimsahau_mchizi_roma

Hata hivyo mashabiki wengi walimuunga mkono huku wengine wakimwambia kuwa mambo Kama hayo hutendeka lakini ikiwa Roma ni wake hakuna mwanamke yeyote anaweza kumchukua.

Tazama video hiyo hapa;

https://youtu.be/VA66Muo5-KE

Chege awashirikisha Ray C na Sanaipei kwenye wimbo wake mpya-Najiuliza

Chege ameamua kuwachia nyimbo mpya ambayo inawazingua mashabiki wake baada ya kuwashirikisha warembo, Ray C na Sanaipei Tande kutoka Kenya.

Watatu hao wamejiunga kwenye wimbo unaozungumzia mapenzi huku Ray C na Sanaipei wakiomuomba Chege achungue mrembo anayemtaka.

Wimbo huu unalenga mambo ambayo wanaume na wanawaka wengi hupitia. Video hiyo imetengenezwa na Kwetu Studio. Itazame hapa

“Naachia ngoma moto” Shilole awahaidi mashabiki

Zuwena Mohammed anayetambulika sana kama Shilole anafuraha mingi baada ya kukamilika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Hii inamtia msanii huyu furaha kwa sababu sasa anauwezo wa kuachia kazi zake mpya, kitu ambacho hangekifanya hapo awali kwa sababu ya kuhufadhi sheria za dini yake.

Akizungumza kwenye mahojiano,Shilole alisema kuwa ilimbidi kukaa kimya lakini kwa sasa akona mipango ya kuiachia kazi kubwa kubwa hivi karibuni, hivyo akiwaonya wanamuziki wenzake kujipanga.

Shilole alisema…

“Wanamuziki wajipange maana nina ngoma kali itakayotoka hivi karibuni, ikiwa ni baada ya kukaa kimya kwa muda kutokana na mwezi mtukufu, lakini kwa sasa umeisha hivyo nakuja kwa kasi ya ajabu.”

Hii ndiyo sababu ya Chid Benz kumchana Chin Bees

Chid Benz ambaye ni mmoja wa wasanii wa hip hop walioanza kuachia nyimbo zao kitambo ameonelea kumkanya Chin Bees ambaye anatumia jina linalokaribiana na staa huyu.

Sababu za Chidi Benz kumwambia Chin Bees atafute jina lingine ni kwa sababu majina hayo yanafanana na kunauwezekano wa kuwakanganya mashabiki wake.

Ingawa wawili hawa wanafanya nyimbo tofauti Chid Benz anamtaka Chin kuwa mbunifu na kutafuta jina ambalo halifanani na lake. Msanii huyo alisema,

“Siku moja nimeona Shetta anamuangalia Instagram nikamuuliza huyo ni nini?, akaniambia ni Chin Bees, nikamuuliza anafanya muziki gani, akaniambia Bongo Fleva!. Sisemi kwa ubaya ila sikuelewa ile style anayofanya yeye ni tofauti sana na mimi mtu mzima mwenye hit kama 32 najua nikiingia kwenye stage nachapa tu,”

Akipiga stori na Planet Bongo ya EA Radio aliendelea kusema;

“Huyo Chin Bees ana single hata saba kweli?, atafute jina lingine,”

“Nilikuwa nakunywa pombe sana” Saida Karoli

Kama wasanii wengi Saida Karoli ambaye ni muimbaji na pia mama hivi karibuni alifunguka kueleza baadhi ya vitu ambazo zilimfanya kuteleza kutoka kwa muziki akizungumza kwenye mahojiano na Clouds FM.

Saida ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya wa ‘Orugambo’, alisema kuwa alijipata ameanza kutumia pombe lakini baada ya kugundua kuwa haikuwa na faida basi aliwacha na tangu 2006 hajagusa ata bia… Saida alisema,

“Vitu vingi nilipitia ila namshukuru Mwenyenzi Mungu sikufikia hatua ya kusema najiuza, na mpaka mtu anafikia anaona yeye sio kitu anaenda kujiuza barabarani, kuuza mwili wake lakini mimi sikufanya hivyo,”

Msanii huyu aliendelea kusema,

“Nilikuwa nakunywa pombe sana lakini kutokana na kushuka kwangu nikaona na pombe niache tangu mwaka 2006, situmii bia, situmii Sigara namshukuru Mwenyenzi Mungu amenipa ustahimilivu nimesimama wima hatimae nimerudi Saida yule yule.”

Hata hivyo kwa sasa amejiandaa kuwachia album yake hivi karibuni.