Zari Athibitisha Kuwa Hajarudiana na Diamond

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari The Bosslady amethibitisha taarifa kuwa yeye na Diamond hawajarudiana bali wameelewana kwa ajili ya kulea watoto wao.

Tangu wiki iliyopita kulikuwa na tetesi zilizodai kuwa Diamond na  Zari wamerudiana baada ya wawili hao kuonekana pamoja nchini South Africa na watoto wao.

Zari amefungukia tetesi hizo na kusema yeye na Diamond hawajarudiana kuwa wapenzi bali wameamua kuelewana kwa ajili ya kulea watoto wao.

Zari amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Snapchat ambapo aliandika:

 

Tetesi za Diamond na Zari kurudiana zilianza baada ya wawili hao kukutana nchini South Africa baada ya kutoanana kwa miezi minne baada ya kuachana.

Zari na Diamond Waibua Tetesi za Kurudisha Penzi Lao

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz na mama watoto wake Zarinah Hassan wamerudi tena Kwenye headlines za kurudiana.

Zari na Diamond waliachana mapema mwaka huu baada ya Zari kumwaga Diamond Kupitia post yake ya Instagram katika siku ya wapendanao.

Tangu waachane Zari amekuwa muwazi kuhusu Mahusiano hayo huku akiweka wazi kuwa aliumizwa na vitendo vya kudhalilishwa na Diamond baada ya kutuhumiwa kuwa Kwenye Mahusiano na warembo kibao huku Diamond amekuwa mgumu kuongelea uhusiano huo.

Lakini sasa kuna Tetesi zinazoendelea kuvuma Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Zari ameamua Kurudisha majeshi kwa Baby dady wake baada ya Meneja wa Diamond Babu Tale kusafiri kwenda South Africa kwa ajili ya kuwapatanisha.

Siku ya jana kuna clip ilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha Diamond akitua nchini South Africa lakini haijajulikana kama alifikia nyumbani kwa Zari au hotelini lakini Zari aliposti picha ya zawadi alinunuliwa na ‘Baba Nee’ ambaye anaweza kuwa Baba Nillan (Diamond).

Ingawa wawili hao hawajathibitisha taarifa za kurudiana lakini Dada wa Diamond Esma amedokeza hilo na kumposti Zari huku akidai yule ndio wifi yake wa ukweli.

 

Zari Amshauri Diamond Atumie Kinga

Mfanyabiashara maarufu kutoka Uganda Zarinah Hassan Zari The Bosslady ambaye pia ni mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, amemtaka Ex wake huyo kutumia kinga.

Zari alishaweka wazi siku za nyuma kuwa alimshindwa Diamond kwa sababu ya Michepuko yake na kupelekea kumtosa siku ya wapendanao Miezi michache iliyopita.

Kupitia Citizen TV, Zari alitumia nafasi hiyo kutuma ujumbe kwa wanaume wote wasaliti kutumia kinga ili kutowahatarishia maisha wapenzi wao. Zari alisema hayo wakati akijibu swali aliloulizwa la sababu hasa iliyomfanya kutangaza kummwaga Diamond.

Zari alieleza kwamba, mwanamke hawezi kumzuia mwanaume kusaliti, lakini kama mwanaume ameshindwa kujizuia na anapaswa au ameamua kufanya hivyo, basi angalau atumie kondomu katika tendo la ndoa.

Kwa wanaume, sisemi kwamba wawe wasaliti kadiri wawezavyo, hapana, lakini kama wanataka kufanya hivyo, wajaribu kutumia kondomu kwa sababu siyo kwamba watapata watoto wasiotarajiwa tu, lakini pia wataishia kupata HIV na magonjwa mengine ya kuambukiza (STD’s).“Siyo hayo tu, lakini pia wasipotumia kondomu watawapelekea magonjwa wengine (wapenzi wao) wanaowasubiria nyumbani”.

Zari alikazia mkazi sana kwenye suala la kutumia kinga unapoenda kuchepuka kwa sababu Diamond hakutumia kinga yoyote ambayo ilisababisha kumpa mimba Hamisa wakati yupo na Zari.

Zari Adai Hawezi Kudate Mtanzania Tena, Adai Mwanaye Sio wa Tandale

Mfanyabiashara maarufu na baby mama wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari The Bosslady ameibuka na kuapa kuwa hataweza kutembea na mwanaume wa Kitanzania tena.

Zari ameyasema hayo baada ya Kupitia kipindi Kigumu na Ex wake Diamond ambaye alichepuka sana kipindi cha Mahusiano yao ya miaka minne hadi kufikia hatua ya kuzaa nje.

Zari alimwaga Diamond mapema mwaka huu siku ya wapendanao baada ya kuchoshwa na tabia zake za kupenda michepuko.

Lakini pia Zari ameibuka na kudai kuwa mtoto wake  Tiffah sio wa Tandale hii iliyokea siku chache zilizopita wakati Zari na marafiki zake walipokuwa Kwenye Instagram live.

Zari alifunguka na kusema mtoto wake Tiffah anashindwa kutofautisha kati ya R na L tabia ambayo ameirithi kutoka kwa Upande wa Baba yake kwani Watanzania wengi hawawezi kutofautisha R na L na wengi wao wanamuita Zali badala ya zari.

Ndipo mmoja kati ya marafiki wa Zari alisema Tiffah ni wa Tandale Lakini mara moja Zari alikataa na kusema mwanaye sio wa Tandale.

Tandale ndipo Diamond na familia yake walipokulia na hajawahi hata mara moja kukataa asili yake na hata albamu yake inaitwa ‘A boy From Tandale’.

Harmonize Amefungukia Kuvunjika Kwa Mahusiano Ya Zari na Diamond

Mwanamuziki wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Harmonize kwa mara ya kwanza amefungukia suala la kuvunjika kwa Mahusiano ya Zari na Diamond Platnumz.

Miezi miwili iliyopita siku ya wapendanao Zari alitumia ukursa wake wa Instagram kumwaga aliyekuwa mpenzi wake Diamond baada ya kuzidisha michepuko ingawa suala hilo lilitokea muda mrefu uliopita lakini mpaka leo linatrend.

Harmonize mbali ya kuwa msanii wa Diamond lakini pia ni mtu wa karibu ambaye pia alikuwa na ukaribu na Zari kwaiyo alipoulizwa anachukuliaje wawili hao kuachana alisema anaheshimu maamuzi ya Zari.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Funiko Base ya Radio Five, Harmonize amefunguka na kusema kuwa yeye binafsi anaheshimu maamuzi ya Zari kwa sababu ana maamuzi yake binafsi.

Mimi naheshimu sana maamuzi ya mtu siwezi kuongea kama ni vibaya au ni vizuri Kwanza muda wa kumshauri mtu kuhusu Mahusiano Yake ndio sina”.

Lakini pia Harmonize alisisitiza kuwa hawezi kumuongelea sana Zari na kuorodhesha mambo ambayo alimsaidia kwani unaweza ukaonekana mnafki.

Wema Kaja na Hili Jipya Kuchombeza Kuwa Karudisha Majeshi Kwa Diamond

Diamond Platnumz ameachana na Zari mwezi uliopita na tangu hapo Kumekuwa na fununu za wanawake kadhaa kuchukua nafasi yake lakini Wema amerudi kwenye nafasi ya kwanza.

Kumekuwa na tetesi nyingi za kuwa Diamond amerudiana na aliyekuwa mpenzi wake miaka michache iliyopita, Wema Sepetu.

Siku ya leo ni kama Wema amezidi Kutia petroleum kwenye tetesi za yeye kurudisha penzi kwa Diamond kwani ndo zinazidi kuwaka moto.

Siku ya jana Wema alitajwa na watu kadhaa kutoka WCB kuwa kama African beauty na moja ya watu hao ni Harmonize ambaye alimtag Wema kama African beauty wake na Wema alijibu Mapigo kwa posti  hii aliyotupia kwenye ukurasa wake wa Instagram:

Lakini pia Wema hakuishia hapo kama utakumbuka Zari alivyompiga Diamond kibuti siku ya Wapendanao alitumia Ua la rangi nyeusi kuashiria penzi lililokufa lakini leo Wema kaposti Ua la rangi nyekundu kuashiria penzi lilohai na tamu.

Posti hiyo inazidi kuibua tetesi kuwa inawezekana Wema anamrusha roho adui yake namba moja Zari baada ya kurudiana na Diamond.

 

Queen Darleen- Bado Nampenda Zari

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva kutoka label ya WCB Queen Darleen ambaye pia amejipatia umaarufu kwa kuwa dada wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, amefunguka na kusema bado anampenda aliyekuwa wifi yake Zari.

Zari alimwaga aliyekuwa mpenzi wake Diamond Platnumz mwezi uliopita lakini mpaka leo bado wanatengeneza headlines kwenye mitandao ya kijamii kwa kuongelewa.

Queen Darleen amefunguka kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers ambapo aliulizwa kuhusu mawifi zake kwa Diamond hasa kwa sababu Amekuwa hatabiriki yupo upande gani maana bado ana urafiki na Penny ambaye alikuwa mpenzi wa zamani wa kaka yake.

Queen Darleen ameongelea mapenzi yake kwa Zari huku akikiri kuwa bado anampenda sana wifi yake huyo:

Kwanza kabisa watu wajue mimi nampenda sana Zari Tena sanaa lakini kiukweli huko nyuma nilimpenda Wema kwa sababu ndiye alikuwa ni wifi kwa kipindi hiko lakini Penny amebaki kuwa rafiki yangu hadi sasa”.

Lakini pia Queen Darleen alifunguka kuhusu Hamisa ambapo amedai yeye na Hamisa hawana mazoea sana anachojua yeye yule ni mama wa mtoto wao Abdul na walikuwa wanaonana kwenye masherehe tu huko nyuma.

Queen Darleen amekiri kuwa hapendi sana kumfuatilia Diamond na maisha yake binafsi kwani yeye hajawahi kumfuatilia hata siku moja.

“Unajiona Mzuri na Mdogo Lakini Huwezi Kupata Mwanaume Wako” Zari Amrushia Hamisa Dongo

Mfanyabiashara na mzazi mwenza wa msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari’ amerudi tena kwenye headlines baada ya kumua kufumua bifu lake na baby mama mwingine wa Diamond, Hamisa Mobetto.

Inaelekea bifu la wazazi wenza wa Diamond  limerudi upyaaa kwani Zari kaamua kulianzisha tena baada ya kimya kirefu juu ya suala hilo na tofauti tulivyodhani kuwa huenda wamemaliza tofauti zao kama ambavyo Diamond na Hamisa walivyomaliza mahakamani.

Siku ya jana Zari kutumia mtandao wa SnapChat alimrushia Hamisa madongo upya kama ilivyokuwa siku za nyuma ambapo ameongelea kuhusu suala la Hamisa kuzaa na Diamond na pia taarifa za Hamisa kuchumbiwa na Diamond.

Siku za nyumba Hamisa ameshawahi kudokeza kuwa aliwahi kuchumbiwa au kuvalishwa Pete ya uchumba na Diamond na hata kuna taarifa zilienea kuwa huenda Diamond na Hamisa walifunga ndoa habari ambazo hazijawahi kuthibitishwa.

Mzuri, Mdogo lakini pamoja na hayo yote huwezi kupata mwanaume wa peke yako…..Eti amekuvalisha pete ya uchumba lakini hajawahi kukubali wala kukukubali hadharani! Dada jiangalie sana ….Anafanya Interview redioni eti mwenye mimba atoke blah blah”.

 

Lakini ni pia Zari ametangaza ujio wa kipindi chake kitakachoonyesha maisha yake halisia (reality show)  kitakachoitwa Life of Zarithebosslady ambacho mashabiki wake watapata kuona kila kitu kuhusu maisha yake.

 

Msanii Aliyejitolea Kumuoa Zari Ajitamba Kuwa Ana Pesa Kuliko Diamond

Msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya anayejulikana kama Alex Apoko ‘Ringtone’ ameibuka tena na kudai ana pesa nyingi kuliko msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Ringtone amezidi kumtaja Zari akubali kuolewa naye kwani amemhakikishia kwa pesa nyingi alizokuwa nazo atamtunza vizuri sana kuliko hata Diamond ambavyo angeweza.

Ringtone alifunguka hivi karibuni kwenye mahojiano aliyofanya na Citizen Tv ambapo alijitapa kuwa kama mjasiriamali alitengeza milioni moja yake akiwa mwanafunzi alipoanza kuuza cd zake za muziki lakini pia amejitapa kuwa ana biashara zake kwenye sekta ya afya na nyinginezo.

Msanii huyo amejitapa ana pesa za kutosha za kuweza kumlea Zari pamoja na watoto wake wote na pia Zari ni mwanamke mzuri na wa gharama ndio maana Diamond ameshindwa kumuhudumia alijaribu kwa miaka mitatu lakini ameshindwa kuendelea lakini yeye yupo tayari.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ringtone alimuwekea Zari ujumbe huu:

Dear Zari Jesus loves you so much na amenitumia mimi leo kukwambia ana mipango poa na wewe. Mimi alinitoa from the streets mahala sikuwa na family, nyumba hata lishe buy now na magari, hela na magari ninavyo tele. Don’t waste time you never know tomorrow. I love you tha same way God loves you”.

 

Zari: Wema Amevuruga Penzi langu na Diamond

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Zarinah Hasssan ‘Zari the Bosslady’ amerudi tena kwenye headlines mwishoni mwa wiki hii baada kufanya Interview kwa mara ya kwanza baada ya kutangaza kumuacha Diamond rasmi.

Siku ya Valentine’s Zari aliushangaza uma wa watu baada ya kutangaza kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa ameamua kumuacha mpenzi wake na Baba watoto wake kwa kile alichodai ni michepuko imesababisha.

Lakini Zari ametaja sababu kubwa ambayo imepelekea yeye kuachana na Diamond ni mpenzi wake wa zamani (Ex wake) Wema Sepetu.

Wiki chache zilizopita video na picha zilizomuonyesha Wema na Diamond wakikumbatiana na kushikana hadharani kwenye party ya WCB.

Zari amefunguka mengi Kwenye mahojiano aliyofanya na BBC Swahili nchini Uingereza, London ambapo ameweka wazi alifikia uamuzi wa kumuacha Diamond baada ya kuona picha na video akiwa anakumbatiana na Wema Sepetu kusambaa kila kona Kwenye mitandao ya kijamii:

Kwanza hakuwa ametegemea mimi kuposti vile Instagram kutangaza kumuacha kwa sababu nilikaa mwenyewe muda mrefu nikafikiria mwishowe nikaamua tuishie hivyo”.

Zari amezidi kufunguka na kueleza kuwa walikuwa katika jitihada za kuuweka uhusiano wao kwenye mstari ulionyooka baada ya usaliti aliomfanyia uliompelekea kuzaa na Hamisa lakini alimuumiza zaidi alivyoona video akiwa anakumbatiana na Wema kwenye mitandao ya kijamii.

Unakaa leo unasikia hiki kesho unasikia kile kukumbatiana na ma-EX kwenye public kufanya vitu vya kunidhalilisha mimi na watoto wangu na unaona kabisa sio sawa na mtu ukiamua kuwa na familia unatakiwa vitu vingine unataka kama nimeshakukubali kuwa wewe ni msanii kutakuwa kuna vitu vingine unafanya lakini kuna vitu unatakiwa uweke stop ili kuiheshimu familia yako”.

Zari amefunguka na kusema baada ya kuona Diamond anapiga picha anakumbatiana na Wema kwenye social media aliamua kumblock kila sehemu hivyo alikuwa hana mawasiliano naye ya aina yoyote kuanzia hapo mpaka siku ya Valentines alipoamua kumuacha.

Zari amefunguka na kusema tangu amuache Diamond Kwenye Instagram hajawahi kuongea naye Tena wala kuwasiliana naye wala hajawaona watoto wao.

Amber lulu- Nillan ni Mtoto wa Ivan sio Diamond

Msanii wa mziki wa Bongo fleva, Amber lulu amejikuta akivamiwa na kupewa vichambo vya maana na Team Zari baada ya kusema mtoto wa Zari Nillan sio mtoto wa Diamond.

Siku ya jana Hamisa aliweka picha za mtoto wake aliyezaa na Diamond Instagram na moja kwa moja zilizua gumzo huku kila mmoja akiibuka na kusema lake.

Amber lulu ambaye anajulikana wazi kuwa ni rafiki wa Hamisa aliweka picha ya Nillan huku ikisindikizwa na maneno haya:

Toto Dee raha ya mtoto afanane na na Baba yake kwa kweli maana unaambiwa wako hujafanana naye hata kidole nasubiri wa shoga yangu Gigy Money najua Baba Candy sio mtu wa mchezo mchezo ila hongera mzaa chema”.

Lakini baada ya kuweka posti hiyo kwenye ukurasa wake wa Instagram kuna mtu akamuuliza Yule mwingine kafanana akimaanisha Nillan, Amber Lulu alionekana kajibu Kafanana na Baba yake Ivan mi sipo.

 

Kwa muda mrefu watu wamekuwa wakimfananisha na kudai mtoto wa Zari Nillan hafanani na Diamond na kuunganisha picha huku wakidai Nillan ni mtoto wa Marehemu Ivan jambo ambalo Zari amekwisha kataa na kusema sio kweli na hata Diamond alisema ameshakubali yule ni mtoto wake.

Tunda Akiri Kuogopa Kumuongelea Tena Zari

Mrembo Tunda Sebastian ambaye ni Video queen maarufu amefunguka na kusema hatokaa kumuongela Zari wala kuvunjika kwa penzi la Diamond na Wema.

Tunda amedai amefikia uamuzi huo baada ya kukiri kuoga mvua ya matusi kila mara akifungua mdomo wake kuongelea jambo lolote linalomuhusu Zari amekuwa akiishia kuoga mvua ya matusi kutoka kwa Watanzania.

Tunda alipata umaarufu zaidi mwezi uliopita baada ya kupatwa na skendo ya kutoka kimapenzi na Diamond ambaye kwa kipindi hiko alikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mzazi mwenzake Zari the Bosslady.

Kwenye Interview aliyofanya na Global Publishers Tunda alifunguka na kusema kuwa amefikia uamuzi wa kutokaa na kumzungumzia tena Zari kwani chochote kile anachokizungumza watu wataanza kumshushia mvua ya matusi na familia yake haipendi kuoana anatukanwa vile.

Kwenye mahojiano hayo Tunda ameongea haya:

Mimi kuhusu Zari au sijui ishu zao za kuachana kwao na Diamond au kitu chochote kinachohusiana na mambo yao sitaki kabisa kuzungumzia maana wengine sisi Damu zetu ni kama za kunguni nikisungumza chochote itakuwa ni shida tupo”.

 

Zari ‘Amtosa’ Diamond na familia Yake Yote Mtandaoni

Mfanyabiashara maarufu Zarinah Hassan ‘ Zari’ ambaye ni maarufu Tanzania kwa kuzaa na uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz ameamua kumtosa Diamond na familia yake yote huko kwenye mitandao ya kijamii.

Wiki hizi chache zimekuwa zikimhusisha mrembo Zari na mpenzi wake Diamond kwenye vichwa vya habari kila siku huku kila uchao ni stori mpya na mwanamke mwingine huku wiki hii ni Tunda ndiye anatawala headlines.

Kumekuwa na stori kwenye mitandao ya kijamii kuwa Tunda anatoka na Diamond lakini pia kikubwa ni kwamba ni baba wa mtoto wa Tunda aliye tumboni.

Piano kumekuwa na video clip inayomuonyesha msichana anayeitwa Mia ambaye ana undugu na Tunda huyu alipata umaarufu juzi juzi baada ya video yake kusambaa akiwa Nyumbani kwa Diamond Madale lakini baadae time ya Diamond ilidai msichana yule alikuwa demu wa dancer wa Diamond ingawa baadae alikuja sema kuwa alilala naye.

Lakini pia Diamond ana skendo nyingine kubwa ni kuwa yeye na mpenzi wake wa zamani, Wema Sepetu wamerudiana hiyo imeonekana mwishoni mwa wiki iliyopita pale Wema na Diamond walipoanza kushikana shikana na kukumbatiana ukumbini halo iliyozua tafrani.

Baada ya skendo zote hizi kumfikia Zari ambaye hivi sasa yupo nchini South Africa ameamua kuwa-unfollow kwenye mtandao wa Instagram familia nzima ya Diamond kuanzia Diamond mwenyewe, Mama Diamond, Esma, Rommy Jones mpaka mameneja wote wa Diamond na Time nzima ya WCB.

Mara ya mwisho Diamond kuhojiwa nchini Rwanda alidai kuwa hana msichana mwingine zaidi ya Zari na bado wako wote hadi hivi sasa lakini Zari hajaongelea lolote kuhusu status ya relationship yao mpaka hivi sasa.

Zari Ndio Mwanamke Wa Mwisho Kumtongoza- Diamond

Mwanamuziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz Amefunguka na kudai kuwa mwanamke wa mwisho aliyemtongoza alikuwa ni mzazi mwenzie Zarinah Hassan ‘Zari the Bosslady’.

Diamond alifunguka hayo alipokuwa nchini Rwanda wiki hii ambapo ameenda nchini humo kwa ajili ya kuzindua bidhaa zake ambazo ni Diamond karanga na Chibu perfume.

Katika kipindi cha wiki hizi chache kumekuwa na maneno maneno ya chini chini ambayo yanadai kuwa Diamond wamechepuka na Tunda na kumsaliti mpenzi wake Zari lakini pia inadaiwa Diamond amempa mimba mrembo huyo.

Diamond ameweka wazi kuwa tangu amtongozee mpenzi wake Zari mwaka 2014 ndio ilikuwa mara yake ya mwisho kufanya hivyo hahawahi tena kutongoza mwanamke yoyote lakini pia amedai sababu ya kutomtongoza mwanamke mwingine ni kwa sababu yuko na Zari tofauti na kipindi cha nyuma kabla hajawa maarufu.

Diamond alifunguka hayo kwenye mahojiano aliyofanya na kituo cha Kiss FM cha nchini Rwanda, ambapo katika utaratibu wa maswali na majibu Diamond aliulizwa Kama alishawahi kukataliwa na mwanamke kabla ya umaarufu wake? Diamond alijibu “Ndio wengi tuu kwanini isitokee?”.

Lakini pia Diamond alihojiwa na kuulizwa kama ni lini alikataliwa na mwanamke au kusikia neno hapana kutoka kwa mwanamke?Diamond alijibu “Tangu nimtongoze Zari hadi sasa sijawahi kumtongoza mwanamke mwingine”.

 

Zari Afunguka Mazito Baada ya Diamond Kushusha Bonge la Mjengo

Mwanamuziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amezidi kujidhihirisha kuwa yeye ni mkali baada ya Jana kuonyesha bonge la mjengo ambao utatumika kama makao makuu ya WCB.

Diamond ambaye ni mmiliki wa studio za Wasafi Classic Co. ambayo ilianza kama label ya muziki inayosimamia wasanii wakubwa wa Bongo fleva nchini kama Rayvanny, Harmonize, Lavalava, Rich Mavoko, Queen Darleen, Mbosso.

Wiki chache zilizopita kwa mara ya kwanza meneja wa Diamond, Babu Tale alidokeza kuwa kuna mpango wa kufungua stesheni ya redio na kituo cha televisheni ambavyo vitamilikiwa na Diamond. Lakini pia siku chache zilizopita alipokuwa nchini Kenya kwenye interview na kituo kimoja Diamond alithibitisha mipango hiyo ya kufungua television station na radio station hivi karibuni.

Siku ya Jana maneno hayo yalitimia kwani kwa mara ya kwwnza Diamond rasmi katambulisha mjengo mpya ambao utatumika kama makao makuu ya WCB na studio za redio na televisheni.

Baada ya habari hiyo njema na watu mbali mbali  kumpongeza sana mzazi mwenza wa Diamond na mpenzi wake Zari the Boss lady alifunguka maneno mazito mtandaoni na kuandika mambo yafuatayo kwa Diamond:

Hongera Diamond sanaa kwa bidii na juhudi uliyonayo Allah akujaalie kwa mengine mazuri zaidi. Siku zote umekuwa mpiganaji wa kazi zako kwa kuwa njia pekee ya kuijenga familia ni kupiga kazi najua malengo yako Alhamdulilah!”.