Juma Jux afunguka kuhusu suala la kujiunga na Wasafi Records

Jux  ambaye ni msanii mkubwa bongo anaonekana kufanya vyema na wimbo wake mpya utaniua.

Hatah ivyo akizungumza na Planet Bongo ya EA Radio msanii huyo alisema kuwa Wasafi record ni label nzuri lakini hajawahi kufikirikia kujiunga na label hiyo.

Ni kitu kizuri sio kibaya kwa sababu ile ni record label, hiyo nafasi ikipatika sio mbaya lakini kwa mimi sikuwahi kufikiria kwa hapa Tanzania au kwa Africa kwa kweli.

Hata hivyo yeye binafsi hana shida yoyote ya kujiunga na label hiyo iwapo watazingatia mkataba wake kwa sababu hafanyi muziki peke yake.

Iwe ni kampuni au sehemu ambayo itanichukua mimi kama kunimeneji pale nilipokuwa wafanye vitu extra zaidi. Sawa wanaweza ikawa wanaweza kwa mkataba kama watakuja na mkataba ambao nitautaka na vitu vyangu ambavyo navihitaji naweza nikasaini kwa sababu mimi ni mfanyabiashara lakini kwa sasa hivi hatukuwahi kuongea au kufikiria.

Msanii maarufu wa bongo aweka picha ambayo imezua utata mitandoni kusheherekea siku ya kuzaliwa ya Rayvanny

Diamond Platnumz amekuwa mada ya wiki huu baada ya Hamisa Mobetto kufunua jina la mtoto wake, Abdul Naseeb.

Kwa kufanya hivi, Diamond Platnumz alimbumburushia Mobetto matusi huku akimuita ‘bitch’ na kuwafanya mashabiki wake kumponda kwa kitendo hiki.

Hata hivyo, Diamond Platnumz ameonekana kuendelea kumponda Hamisa kwa kumuwekea picha za kuudhi mitandaoni. Akimsheherekea Rayvanny Leo, Mkali huyo wa Wasafi aliweka picha huku akionekana akimbusu Zari na Vanny akioneka kwenye background.

Kwenye picha hiyo, Simba aliandika;

Jus wanted to wish the guy at the back happy birthday…please tag him!!!

Lakini, mashabiki wake wameonyesha kutoridhika.

Rayvanny akamilisha kazi yake mpya na Jason Derulo

Mkali wa Wasafi Records Rayvanny hatimaye aliweza kukutana na Jason Derulo marekani ambapo wawili hao waliweza kukamilisha kazi yao mpya itakoyoachiliwa hivi karibuni.

Rayvanny alijumuika na Jason Derulo siku kadhaa baada ya kushinda Tuzo lake la kwanza la BET. Kupitia mtandao wake wa Instagram Rayvanny aliweka picha yake na Jason Derulo huku wakionekana wakiwa kwenye studio session.

Aliandika kusema,

“God bless you my brother @jasonderulo its amaizing opportunity,am so grateful for that……… Toka Saa 8 Usiku amekaa na mimi hadi Asubui… Studio kulikua na Watoto wakaaaaaliiiii lakini kawacha waondoke sababu walichoka kukaa studio yeye kabaki na sisi tu. Naamini kilichofanyika Mtakipenda. Thanks boss @afrikidd @babutale.”

Tazama picha hiyo Hapa;

Lava Lava awatetea wasanii wa Wasafi records baada ya wengi kudai kuwa wanamuiga Diamond Platnumz

Lava Lava ambaye ni msanii mpya wa Wasafi records kwa hivi sasa anatamba kwa wimbo wake mpya ‘bora tuachane’ ambao umempa mashabiki wengi kwa muda wa wiki moja.

Baada ya kuingia Wasafi msanii huyu amepata interview kadhaa kwa redio na hivi karibuni tunatarajia kumuona kwenye televisheni.

Lava Lava
Lava Lava

Hata hivyo kama wasanii wenzake, msanii huyu ameweza kupata changamoto ambazo zinaweza kuiletea career yake shida. Hivi karibuni akizungumza kwenye interview na Bongo 5 msanii huyu alikana kuwa hakuna msanii yoyote kutoka Wasafi Records anayemuiga Diamond Platnumz. Kulingana na yeye kila mtu ananjia tofauti ya kuimba na iwapo saa zingine wengi wanaona kuwa wanaimba kama mkubwa wao…hii sio ukweli.

Alisema,

“Naona watu wanazungumza lakini watu wawe na masikio ya kusikiliza kitu. Sio watu wote wanaweza kufanana ya Diamond japokuwa kuna vitu tunaweza kufanana kwa sababu ni watu ambao tunakaa pamoja kwa muda mrefu. Pia watu wakiwa wanaishi muda mrefu pamoja huwa wanafanana, kwa hiyo kuna muda mkikaa pamoja kuna vitu mnaanza kushare lakini ukichunguza ndani yake kila mtu ana kitu chake,”

Lizer amtaja msanii ambaye anafurahia kufanya kazi naye Wasafi

Muziki wowote wa Wasafi ukianza mara mingi utamsikia mwanadada akisema ‘ayo Lizer’ lakini wengine hawafahamu kuwa yeye ndiye mtayarishaji wa muziki kutoka studio ya Wasafi Records.

Hivi karibuni Lizer alimtaja msanii wa WCB ambaye yeye hufurai kufanya kazi naye. Akizungumza kwenye interview Lizer alisema kuwa Rayvanny ni msanii ambaye ameweza kufanya kazi naye bila matatizo yoyote.

Aliendelea kwa kusema,
“Msanii yoyote anayejua mimi nina enjoy sana kufanya naye kazi, ukimuelekeza fuata hiki anafuata. Lakini naweza kusema kwa kuwa Raymond ndiye msanii aliyegundua kitu kilichopo ndani ya Lizer huwa nina enjoy naye zaidi kwasababu ndiye msanii ambaye nilitoka naye.”

Diamond Platnumz aeleza kwanini vijana wanashindwa kuingia Wasafi Records

Ni wengi ambao wanatamani kujiunga na label ya Wasafi Records. Hata hivyo kulingana na sheria ambazo Diamond Platnumz ameziweka wasanii wachache ndio tu wamehitimu

Akizungumza kwenye kipindi cha XXL cha Clouds Fm Diamond Platnumz alisema kuwa yeye hutaka wasanii ambao wanaubunifu wa kujiandikia nyimbo kwa sababu hii inasaidia kuangalia maudhui na uzuri wa wimbo.

“Kwanza Rich Mavoko ndiye mgumu kwenye kupitisha nyimbo, ikitoka hapo Ravvanny aipitishe, Queen Darleen aipitishe, ikitoka hapo niipitishe mimi, iende kwa Mkubwa Fella na Babu Tale waipitishe na Sallam aipitishe, ukitoka hapo wewe ni mwanaume haswa.”

Diamond aliendelea kwa kusema,

“Kwa hiyo wengi wanakuwa na uwezo mkubwa. Labda unaweza ukaja ukasikia kitu kidogo, ukasema ukiweka hapa kitu flani itakuwa poa zaidi, yaani ukiandika unaandika haswa.”

Lakini kwa sasa Diamond Platnumz amemsign Lava Lava ambaye amenonekana kuwa mkali baada ya kuachia wimbo wake mpya.

Baada ya kuachia nyimbo mpya, Rich Mavoko afunguka kuhusu kitu anachokifanya kwa sasa

Rich Mavoko ambaye anafanya muziki chini ya Wasafi records hivi sasa anajipanga kuachia album mpya hivi karibuni baada ya collabo yake ya Show me na Harmonize.

Ingawa umaarufu wake sio kama wa Rayvanny na Harmonize muimbaji huyu anajikaza kufikia kiwango ambacho wasanii wote wa Wasafi records wako.

Akizungumza kupitia kipindi cha Top 20 cha Clouds FM kuwa, Rich Mavoko alisema kuwa yeye mwenyewe hufika saa 12 jioni studio ilikufanya kazi hadi saa 12 asubuhi kwa sababu hivi sasa anamipango ya kuachia album ambayo itakuwa yake ya kwanza. Alisema,

“Hii itakuwa albam yangu ya kwanza kubwa kufanya, nilishawahi kutengeneza na watu wangu wa mwanzo ila haikufanikiwa kutoka.”

Hata hivyo kuna matumaini kwamba Rich Mavoko ataendelea kuwavutia mashabiki kwa wingi baada ya project hii yake mpya.

Mchumba wa Aunty Ezekiel aeleza mbona hawezi kuwa muimbaji wa Wasafi records

Moses Iyobo ambaye ni dancer maarufu wa Diamond Platnumz amefunguka kwa nini hawezi kuwa muimbaji ataiwapo angepewa fursa hiyo.

Akiongea na gazeti maarufu la Dimba, Mose alisema kuwa hana mipango ya kuingia katika muziki na kuwa kwa hivi sasa lengo lake ni kuwa dancer ambayo ni kazi anayoifanya kwa hivi sasa.

Mose Iyobo na Aunty Ezekiel
Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Kiluingana na yeye, kuwa muimbaji inatakiwa mtu kuwa na kipaji ambacho yeye mwenyewe hana kwa hivyo si kitu ambacho anaweza kufanya na kufanikiwa. Alisema,

“Unajua kuimba kunahitaji akili nyingi ili ufanikiwe, sasa kwa upande wangu sitaweza ni bora nibaki huku huku ndio pananifaa zaidi,”

Ata hivyo Mose Iyobo alisema kuwa angependa kuwa mwalimu wa kuwafindisha vijana kuwa dancer kama yeye. Kuna watoto ambao wangependa kuwa dancers wakiwa wakubwa kwa hivyo ni heri yeye kuanzisha shule ambayo atawafundisha ili hapo mbeleni waweze kutambulika kama yeye.