Kifesi Adai Diamond Amepoteza Kitu Cha Thamani Maishani Kwa Kumpoteza Zari

Aliyekuwa mpiga picha wa staa wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz, Kifesi amevunja ukimya na kufunguka kuhusu kuvunjika kwa Penzi la Diamond na Zari.

Kifesi aliacha kazi WCB Miezi michache iliyopita lakini ilisemekana kuwa amefukuzwa kazi na Diamond baada ya kuingilia kati Penzi la Diamond na Zari.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Kifesi amefunguka na kuweka wazi kuwa Diamond amefanya makosa kuachana na Zari kwa sababu ni mwanamke anayejielewa sana.

Mimi naamini Diamond amefanya makosa sana kuachana na Zari kwa sababu Mwanaume yoyote mwenye akili na Basara atamuona Zari kama aina ya mwanamke ambaye anatamani awe naye kujenga maisha na kujenga familia.

Kwaiyo Diamond atakuwa ni wa ajabu kama akisema eti hajapoteza kitu cha thamani kwa kumpoteza Zari nitamshangaa halafu hata yeye anaelewa umuhimu wake ukilinganisha na wanawake ambao ameshawahi kuwa nao na hata alionao huwezi ukawalinganisha na Zari”.

Kifesi pia amekiri kuwa hana mawasiliano yoyote na Diamond tangu aache kazi WCB Miezi michache iliyopita lakini bado ana ukaribu na urafiki na Zari na anaongea naye kila siku.

Zari Ampa Pole Hamisa Baada Ya Kukanwa na Diamond Hadharani

Zarinah Hassan ‘Zari’ amerudi Kwenye headlines tena baada ya kumuandikia ujumbe adui yake namba moja Hamisa Mobetto baada ya kukanwa na Diamond hadharani.

Sakata hilo lilianza siku ya leo baada ya Diamond kuachia video yake mpya ya wimbo wake wa ‘Baila’ ambapo aliposti Kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika kuwa hajapata mwanamke wa kuwa naye lakini siku akimpata atamsikilizisha Baila:

Kwa machache niliyojifunza Kwenye Mahusiano nilisema siku nikikutana na mwanamke mpya nitakayetaka kuwa naye kabla ya kuianza Safari sitamwambia neno bali nitamuwekea huu wimbo wa Baila”.

Baada ya Diamond kuweka wazi kuwa hayupo kwenye mahusiano moja kwa moja Zari alianza kumnanga Hamisa na kumpa pole baada ya kukataliwa na mwanaume ambaye amekuwa akijitangaza kuwa Kwenye Mahusiano naye.

Kwenye ukurasa wake wa Snapchat Zari aliandika maneno ambayo directly alikuwa anampiga vijembe Hamisa na kumcheka kuwa amekaa Kwenye Mahusiano na mwanaume kwa miaka kumi lakini bado anamkana hadharani kuwa hana uhusiano naye:

Bifu la Zari na Hamisa lilianza baada ya Diamond kuchepuka Kwenye Mahusiano Yake na Zari na kuzaa mtoto na Hamisa Mobetto tangia hapo Zari na Mobetto hawaivi chungu kimoja ni majungu kwenda mbele na kujibizana mitandaoni.

Zari Ajitapa Kuwa na Pesa Chafu Asisitiza Hawezi Kujibizana na Watu Mtandaoni

Zarinah Hassan au maarufu kama Zari The Bosslady amefunguka na kuweka wazi kuwa ana pesa nyingi kupita kiasi na kusema hawezi kujibizana na Watu mtandaoni.

Siku chache zilizopita Zari aliandika Mtandaoni kuwa yeye ni bilionea na kuwaita watoto wake matajiri, kauli iliyoibua maneno mengi mtandaoni ambapo watu wengi walimnanga na kudai hana pesa.

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers Zari amesema anawashangaa watu wanamnanga na kuamua kuweka wazi mali zake na kutaja biashara zake anazofanya Afrika ya Kusini:

Kuna watu wengi sana hawajui maisha halisi ya Zari, wanakisia tu mitandaoni, Ninaandaa shoo yangu ya TV, ambayo inazungumzia maisha yangu halisi, nadhani wengi watamjua Zari halisi. Nina mambo mengi wasiyoyajua.

Hawajui hapa Afrika Kusini nimewekeza kiasi gani? Ivan aliacha mali kiasi gani? Haya natakiwa kuyaendeleza kwa ajili ya watoto wake. Yapo magari yake ya kifahari hata mimi siyaendeshi.

Tuna shule hapa Afrika Kusini, kampuni ya ulinzi, nimeajiri wafanyakai 360, kila mwisho wa mwezi nalipa mishahara yao. Siwezi kujibizana na mtu mitandaoni”.

Zari alijizolea umaarufu Bongo baada ya kuanzisha Mahusiano ya Kimapenzi na kuzaa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Zari: Diamond Ameniomba Sana Msamaha Baada Ya Kuchepuka

Zarinah Hassan maarufu kama Zari The Bosslady amefunguka na kuweka wazi kuwa mzazi mwenzake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz alimuomba sana msamaha baada ya kuchepuka.

Katika Interview yake na Global Publishers, Zari amekiri kuwa tangu Diamond amsaliti na kuzaa na Hamisa Mobetto mwaka jana amemuomba sana msamaha na hata Babu Tale kuenda South Africa juzi juzi ilikuwa ni kuomba radhi.

Babu Tale alikuja Pretoria, alitaka turudiane na Diamond kwa ajili ya watoto, sikuona ubaya katika hilo, lakini mambo ya mapenzi hapana tena, watu haohao wa karibu walipaswa kumuonya Diamond wakati anafanya mambo yake kwa sababu anaamini walifahamu kila kitu.

Wangemwambia Diamond aache mambo aliyokuwa anayafanya. Kufufua penzi kwa sasa ni vigumu sana, wameshachelewa. Mimi nawaheshimu sana, na ndiyo maana hata Babu Tale alipokuja nilimkaribisha vizuri. Sina ubaya na mtu yeyote, hata ndugu zake Diamond“.

Lakini Zari amesisitiza kuwa taarifa zilizoenea kuwa wawili hao walirudiana Diamond alipoenda Sauzi sio za kweli kwani hawakulala hata chumba kimoja:

Diamond alikuja kuwaona wanawe. Alilala chumba kingine na mimi nikalala chumbani kwangu. Tuliongea kuhusu kuwa karibu lakini ni kwa ajili ya watoto tu. Kwa sasa sina uhusiano wowote.  Nimeyaweka kando mambo hayo, nachoangalia ni kulea watoto wangu”.

 

Diamond- Mtoto Wa Hamisa ni Mtoto Wangu Kama Walivyo Watoto Wa Zari

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amemwaga povu zito kwa mashabiki waliokuwa wanamnanga mtoto mmoja ale aliyezaa na Hamisa wakidai sio mtoto wake.

Siku ya jana Diamond aliachia trailer mpya ya shoo yake ya ‘The real Life of Wasafi’ itakayoonyesha maisha halisi ya familia ya Diamond itakayorushwa Kwenye Wasafi Tv.

Kwenye trailer hiyo kuna kipande kinachomuonyesha Diamond akiwataka anazungumzia watoto wake lakini watoto wanaoonekana ni wawili tu ambao amezaa na Zari huku mtoto wake aliyezaa na Hamisa hakuonekana.

Kuona hivyo mashabiki wa Zari wakaanza kumnanga mtoto wa Hamisa kuwa sio mtoto wa Diamond ndio maaan hajaonekana kwenye trailer ya shoo ile na hapendwi kama watoto wa Zari wanavyopendwa.

Baada ya maneno mengi sana Diamond alishindwa kujizuia na kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa Dylan ni mtoto wake kama walivyo watoto aliozaa na Zari walionekana kwenye trailer ile sababu pekee ambayo ilisababisha mpaka Dyalan hakuonekana ni kwa sababu hakuwa na clip yake:

 

Zari Achaguliwa Kuwa Jaji Wa Mashindano Ya Ulimbwende

Zari The Bosslady amelamba shavu lingine baada ya kutangaza siku ya jana kuwa anatarajia kwenda kuwa ajaji wa mashindano ya ulimbwende nchini Uganda.

Zari amezidi kuthibitisha kuwa yeye ni mfanyabiashara na bosi kwani amekuwa akifanya kila jitihada ya kuingiza mkwanja.

Zari anategemewa kuwa jaji mkuu wa shindano hilo litakalofanyika rasmi tarehe kumi mwezi wa nane mwaka huu katika hoteli ya Sheraton Kampala nchini Uganda.

Kupitia mtandao wa Instagram, waandaaji wa shindano hilo wamethibitisha hilo kwa kuandika,

The Miss Uganda beauty pageant is proud to announce its first patron and judge for #Missug18 @zarithebosslady ??. Miss Uganda is a celebration of beauty with a purpose to inspire young women to succeed in life.”

We are also pleased to announce that she will also be a guest speaker at a CSR (corporate social responsibility) activity targeted to young girls organised by the #MissUgandaFoundation. The Miss Uganda pageant is happening on the 10th of August 2018”.

Zari amethibitisha habari hizo kwa kuweka posti hii Kwenye ukurasa wake wa Instagram:

 

 

“Mimi ni Bilionea” Zari Amwagia Povu Mange Kimambi

Zarinah Hassan au maarufu kama Zari The Bosslady ambaye ni mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, amemwagia povu zito Mange Kimambi.

Mange na Zari wamerudi tena vitani huku safari hii Zari akiweka wazi kuwa yeye ni bilionea hivyo asimchukulie Poa.

Sakata hilo lilianza siku ya jana baada ya Zari kumwagia sifa marehemu Ivan za kuwa baba bora na sio mzazi mwenzake Diamond ambapo Mange alimjia juu na kumtaka amshukuru Diamond kwa sababu yeye na watoto wake wanaishi kwenye nyumba ya Diamond.

Baada ya Kuambiwa hivyo Zari alimwaga povu zito na kudai Mange ndio anaishi Kwenye makazi yasiyoeleweka nchini Marekani lakini yeye anaishi Kwenye nyumba ya Diamond kwa sababu ameamu.

Zari aliendelea kumwaga povu na kudai kuwa akiamia kuhaama anaweza kwa sababu Ivan ameacha nyumba tatu na yeye pia anamiliki nyumba moja na kusisitiza kuwa yeye ni bilionea.

Kama utakumbuka Mwanzoni mwa mapenzi yao Diamond alimnunulia Zari bonge la mjumba Nchini South Africa ambapo ndipo anaishi na Watoto wake.

Zari Awaonya Wasafi Tv Kuwa “ Endapo Mtaendekeza Kiki za Kijinga Mtapotea”.

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz Zarinah Hassan ‘Zari’ amekitolea uvivu kituo cha Wasafi Tv.

Bila kujaribu kuwa mmiliki wa kituo hicho cha habari ni Diamond, Zari amewajia juu akiwataka kuripoti Habari za maana kuhusu mambo yanayoendelea nchini.

Zari alitoa povu hilo baada ya Wasafi Tv kuposti clip ya kipindi cha Refresh kinachorushwa na kituo hiko kikionyesha mahojiano waliyofanya na video Queen maarufu Irene Au Lynn.

Kwenye mahojiano hayo Irene aliulizwa endapo anamfahamu Zari ambapo alijibu kuwa hamjui Zari wa hajawahi kumsikia ambapo alisikika akisema ‘Zari Who?’.

Baada ya clip hiyo kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii Zari alienda kwenye ukurasa wa kituo hicho na kuwataka waripoti mambo ya maaan yanayoendelea Kwenye jamii badala ya kukazania mambo ya kijinga.

 

Zari Athibitisha Kuwa Hajarudiana na Diamond

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari The Bosslady amethibitisha taarifa kuwa yeye na Diamond hawajarudiana bali wameelewana kwa ajili ya kulea watoto wao.

Tangu wiki iliyopita kulikuwa na tetesi zilizodai kuwa Diamond na  Zari wamerudiana baada ya wawili hao kuonekana pamoja nchini South Africa na watoto wao.

Zari amefungukia tetesi hizo na kusema yeye na Diamond hawajarudiana kuwa wapenzi bali wameamua kuelewana kwa ajili ya kulea watoto wao.

Zari amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Snapchat ambapo aliandika:

 

Tetesi za Diamond na Zari kurudiana zilianza baada ya wawili hao kukutana nchini South Africa baada ya kutoanana kwa miezi minne baada ya kuachana.

Zari Amwaga Povu Kuhusu Suala la Umri Kwenye Mapenzi

Mfanyabiashara maarufu na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zari The Bosslady amemwaga povu kwa watu walio na mtazamo hadi juu ya Mahusiano kati ya mwanamke mkubwa na kijana mdogo.

Zari amefunguka na kuonyeshwa kushangwa na jinsi ambavyo jamii ilivyokuwa na haraka ya kumuhukumu mwanamke mwenye umri mkubwa kutoka kimapenzi na mwanaume mdogo kuliko kiumri.

Zari amemwaga povu hilo kupitia ukurasa wake wa Snapchat ambapo amesema lakini anashangazwa na Utayari wa jamii kuona msichana mdogo akiwa Kwenye Mahusiano na mwanaume mkubwa kiumri tena vibabu kabisa.

Sitting here and thinking. Society is so quick to judge an older woman dating a young guy, but not a 40+ guy dating a 19 yr old. so typical! Watu na vibabu vyenu”.

Zari amewahi kuwa Kwenye uhusiano wa Kimapenzi na Diamond ambaye inasemekana kuwa amemzidi zaidi ya miaka kumi.

“Hamisa Hata Akitaka Kuzaa Watoto Kumi na Diamond Azae Tu”-Zari

Mfanyabiashara maarufu na mama watoto wa Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan amemwaga povu na kusema Hamisa hata akitaka kumzalia watoto kumi Diamond yeye kwake ruksa.

Kauli hiyo ili Jina siku ya jana baada ya Zari kuweka posti yake aliyokuwa anasherehekea kufikisha followers milioni 4 Kwenye mtandao wa Instagram ambapo shabiki alimtahadharisha kuwa kuna tetesi Hamisa ana ujauzito mwingine.

Shabiki huyo aliandika maneno haya:

Zari kuwa makini kuna tetesi huku mtaani kwetu kuwa Hamisa kashanasa mimba nyingine ila lisemwalo lipo kama halipo laja”.

Baada ya kupewa maneno hayo Zari alimjibu hata wangezaa watoto kumi yeye hana habari kwani hayumo.

Zari alijibu kwa kuandika:

Azae hata kumi mimi simo!”.

Huu ni muendelezo tu wa drama iliyoanza mwaka jana baada ya Hamisa kuanika ana ujauzito wa Diamond kwa wakati huo alikuwa mpenzi wa Zari.

Kumekuwa na tetesi tu kuwa Diamond amerudisha majeshi kwa mama watoto wake Zari baada ya kutoonana kwa muda wa Miezi minne.

Ringtone Amchana Zari Baada Ya Tetesi Za Kurudiana na Diamond

Mwanamuziki wa nyimbo za Injili kutoka 254 Kenya Ringtone Apoko amemjia juu Zari baada ya kuanza kusikika kwa tetesi kuwa amerudiana na Diamond.

Ringtone alishika headlines mwezi uliopita baada ya kukiri kumzimia Zari na kudai yupo tayari kumuoa na hata kumnunulia gari aina ya Range Rover mpya ambayo Zari aliikataa.

Lakini sasa Ringtone amerudi kumhoji Zari kuhusu Tetesi za yeye kurudiana man Diamond Ikiwa alishatangaza kuwa wameachana na hawezi kurudi kwake Tena.

Siku ya jana kuna Tetesi zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Zari na Baby dady wake staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz wamerudiana baada ya kutengana kwa takribani Miezi minne.

Ringtone amemtolea povu Zari kwa uamuzi wake wa kuamua kupasha kiporo na Diamond ambapo amempa maneno haya kupitia ukurasa wake wa Instagram:

Mpendwa Zari huwezi ukaendelea kusoma kurasa za kitabu kile kile kila siku ilihali unajua kitakavyoishia, ulioandoka Misri ukaenda Kanani itasikitisha kama utarudi tena.

Nini kitatokea kwa wasichana kibao uliowaambia sasa unamjenga Zari? Ushauri wangu ni kuwa hivi sasa mtafute Mungu kwa kufunga na maombi ili Mwenyezi Mungu akupe mwelekeo.

Lakini hivi sasa hatuna wasiwasi maana wote tunajua huwezi kurudiana na Diamond”.

 

 

 

Nay wa Mitego: Babu Tale Kaiba Wazo Langu La Kuwapatanisha Diamond na Zari

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nay Wa Mitego amemjia juu Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale huku akidai yeye ndio aliyetoa wazo la kuwapatanisha Diamond na Zari.

Mwanzoni mwa wiki hii Babu Tale alifunga Safari kwenda nchini South Africa kwa ajili ya kuwapatanisha Diamond na Zari kitendo ambao Nay amekiri kuwa ni kizuri lakini amehoji kwa nini amesubiri mpaka yeye atoe wazo hilo alafu ndio na yeye aende.

Babu Tale Alipoenda South Africa kumuombea Diamond msamaha

Kwenye na mahojiano na Risas Mchanganyiko, Nay wa Mitego amemtolea povu hilo Babu Tale:

Suala la Babu Tale kwenda kumuombea msamaha Diamond ni zuri lakini alitakiwa afanye hivyo muda mrefu na siyo asubiri mpaka nizungumze mimi kwamba nitawapatanisha. “Nashukuru wazo langu limekubalika na kila mtu na yeye mwenyewe kuliona linafaa na kufanyia kazi.

Diamond ni mshikaji wangu wa muda mrefu sana, japo mapenzi hayaingiliwi lakini kwa upande wangu namkubali sana mama Tee (Zari) maana akiwa naye mambo yake yanakuwa kwenye mstari kwani anakuwa mtu wa kazi sana tofauti na akiwa na hawa wanawake wengine.

Kutokana na kuliona hilo ndiyo maana niliona nimpe ushauri kupitia ukurasa wangu wa Instagram na kuahidi kuwarudisha pamoja, lakini kabla sijafanya hivyo, Babu Tale akalifanyia kazi, siyo vibaya nimefurahi sana kwa kweli”.

Siku video ya wimbo wa Iyena ulipotoka Nay alimshauri Diamond aachane na Hamisa na arudiane na Zari na hata kumuhaidi atasaidia kumuombea msamaha na kuwapatanisha.

Nay wa Mitego: Babu Tale Kaiba Wazo Langu La Kuwapatanisha Diamond na Zari

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nay Wa Mitego amemjia juu Meneja wa Diamond Platnumz, Babu Tale huku akidai yeye ndio aliyetoa wazo la kuwapatanisha Diamond na Zari.

Mwanzoni mwa wiki hii Babu Tale alifunga Safari kwenda nchini South Africa kwa ajili ya kuwapatanisha Diamond na Zari kitendo ambao Nay amekiri kuwa ni kizuri lakini amehoji kwa nini amesubiri mpaka yeye atoe wazo hilo alafu ndio na yeye aende.

Babu Tale Alipoenda South Africa kumuombea Diamond msamaha

Kwenye na mahojiano na Risas Mchanganyiko, Nay wa Mitego amemtolea povu hilo Babu Tale:

Suala la Babu Tale kwenda kumuombea msamaha Diamond ni zuri lakini alitakiwa afanye hivyo muda mrefu na siyo asubiri mpaka nizungumze mimi kwamba nitawapatanisha. “Nashukuru wazo langu limekubalika na kila mtu na yeye mwenyewe kuliona linafaa na kufanyia kazi.

Diamond ni mshikaji wangu wa muda mrefu sana, japo mapenzi hayaingiliwi lakini kwa upande wangu namkubali sana mama Tee (Zari) maana akiwa naye mambo yake yanakuwa kwenye mstari kwani anakuwa mtu wa kazi sana tofauti na akiwa na hawa wanawake wengine.

Kutokana na kuliona hilo ndiyo maana niliona nimpe ushauri kupitia ukurasa wangu wa Instagram na kuahidi kuwarudisha pamoja, lakini kabla sijafanya hivyo, Babu Tale akalifanyia kazi, siyo vibaya nimefurahi sana kwa kweli”.

Siku video ya wimbo wa Iyena ulipotoka Nay alimshauri Diamond aachane na Hamisa na arudiane na Zari na hata kumuhaidi atasaidia kumuombea msamaha na kuwapatanisha.

Mafanikio Hayaambukizwi Kwa Njia Ya Kujaamina- Zari

Mwanamama mfanyabiashara maarufu Zarinah Hassan ‘Zari The Bosslady’ amewatolea povu zito wasichana ambao amedai ni wadangaji na kuwaambia mafanikio hayapatikani kwa njia ya kujaamiana.

Zari alitoa povu hilo siku chache zilizopita alipokuwa anamkumbuka Ex wake Ivan Semwanga aliyefariki dunia mwaka jana kutokana na maradhi ya ugonjwa wa moyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari aliandika ujumbe huo:

Pale unaposikia pesa za urithi…apo vipi Mafanikio hayaambukizwa kwa njia ya kujaamiana. .Endeleeni kudanga mkafikiri mwanaume tajiri atatokea man kukupa utajiri wa ghafla, na hata kama akiweza wewe utakuwa kama pambo ambalo anaweza akalitupa akinunua jipya lakini mimi sio rahisi kunitupa kwa maana mimi ni msingi na sio paa”.

Zari alitoa povu hilo baada ya kudaiwa pesa alizonazo ni za  Marehemu Ivan na sio Mali yake lakini Zari alianika picha zake za zamani na Ivan na kuwajulisha  watu wakati anaanza uhusiano na Ivan alikuwa hana hizo Mali hivyo walichuma wote.

Zari Amkumbuka Ivan Katika Kumbukumbu Ya Kifo Chake

Zarinah Hassan maarufu kama Zari The Bosslady amezidi kumkumbuka aliyekuwa mume wake Ivan Semwanga aliyeaga dunia mwaka jana tarehe 25 mwezi wa tano.

Ivan ametimiza mwaka mmoja Tangu alipofariki mwaka jana nchini Afrika ya Kusini kutokana na maradhi ya moyo.

Zari alijaliwa kupata watoto watatu wa kiume na marehemu Ivan na walikuwa katika Mahusiano kwa miaka mingi sana.

Zari alianza kumuenzi Marehemu Ivan tangu jana ambapo aliandika ujumbe huu Kwenye ukurasa wake wa Instagram: