Dully Sykes atoa siri yake ya muziki wake kufanya vyema

Msanii wa Bongo Dully Sykes ni mmoja wa wasanii ambao wanaendelea kufanya vizuri kwenye muziki ilhali ya wasanii wengi wenye sauti nzuri kujitokeza.

Dully Sykes ameweza kuachia nyimbo kwa miaka mingi sasa na bado nyota yake inang’aa. Akizungumza kwenye mahojiano na Bongo5 katika tamasha la Heshima ya Bongo Flava, Dully alifunguka kusema huyo kuwa yeye kuwepo katika mzuki kipindi hiki chote hicho ni kwa sababu anawaelewa wanachotaka mashabiki na pia yeye kujitambua kama msanii….alisema,

“Mimi najitunza najielewa kama msanii, kutengeneza status yako na kujitambua, wasanii wengi hawajitambui. Mimi ninajitambua na ninajua mimi ni nani,”

Mkali huyu ‘Yono’ anaendelea kutisha kupitia nyimbo zake na collabos anazozifanya na wasanii wakubwa kama Harmonize na wengine Bongo.

Tazama interview yake hapa:

Z Anto kumshirikisha mwanawe wa umri wa mwaka 1 kwenye kazi yake mpya

Msanii Z Anto ambaye amekuwa kimya kwa muda sasa ameweza kufunguka kuhusu project yake mpya ambayo ataiwachia hivi karibuni.

Z Anto akizungumza na Bongo5 wakati wa show ya Hweshima ya Bongo Flava, iliyoandaliwa na EATV, alisema kuwa kwa hivi sasa anajitayarisha kuachai nyimbo mpya ambayo amemshirikisha mwane mwenye umri wa mwaka mmoja.

Hata hivyo kwa mara ya kwanza Z Anto alisema kuwa yeye hategemei mziki kupata hela kwani ananjia zingine anazozitumia kupata mkwanja. Z Anto aliambia Bongo 5,

“Sikuwa nategemea sana muziki katika maisha yangu. Hizi ni biashara za familia yangu ndio maana. Hata hivyo sio kiki kuwa hizo fremu ni zangu.”

Tazama interview hiyo hapa:

Mwana FA aeleza sababu hatafuti collabo na wasanii kutoka nje

Mwana FA ambaye ni mmoja wa wasanii ambao wanatamba sana Afrika Mashariki amedai kuwa yeye hana haja ya kufanya mziki na wasanii kutoka nje kwa sababu market yake iko bongo.

Akizungumza kwenye interview Mwana FA alisema kuwa muziki wake huwalenga Watanzania wife na hii ni kwa sababu anatakuwa burudisha. Aliendelea kwa kusema pia anaimba kwa lugha ambaye yeye mwenyewe anajua wataelewa maudhui.

“Aina yangu ya muziki ni kuuza maneno na lugha yangu ni kuwafikia watu wote  wale waliopo ofisini na tai zao hadi mama Tatu aliyeko Tandika na sinia lake la vitumbua, sina mahali ambapo ninaacha lakini ni hapa hapa nyumbani kwa sababu nachokiimba kina-relate na maisha yetu ya kila siku kwa upande wangu naona soko langu halipo nje ya nchi.”

Aliendelea kwa kusema,

“Wale ambao wameshafanya kazi na watu wa nje hawajakosea kwani naamini watakuwa wamejiongezea mashabiki wa nchi zingine, Good Luck to them  lakini pia wanaendelea kujitengenezea ‘Cv’ nzuri…. Lakini kwa upande wangu sijawahi kufikiria au kuweka nguvu yoyote ya kuweza kuwapata wasanii wa kimataifa, kwani hapa ndani wasanii wapo wengi na sidhani kana nitaweza kuwamaliza”

Saida Karoli afunguka kuhusu kazi yake na Diamond Platnumz

Muimbaji mkongwe Saida Karoli amefunguka kukiri kuwa ameweza kufanya vizuri na wimbo wake mpya, Urugambo.

Hata hivyo aliendelea kusema kuwa katika album yake mpya amemshirikisha Bella 9 na Diamond Platnumz. Akizungumza kwenye interview Saida Karoli alisema kuwa hizi projects zake ambazo zitawatoa mashabiki jasho.

“Urugambo nimetoa kama zawadi kwa Watanzania, niliona nijitambulishe kama chai ya asubuhi, lakini watarajie mambo makubwa kwani hivi karibuni mimi na Belle 9 tutatoa kazi ambayo itawatoa jasho mashabiki wa muziki,”

Muimbaji aliendelea kudai kuwa kwa hivi sasa anapanga kuachia nyimbo nyingi kali ili kuwakumbusha mashabiki wake alivyokuwa hapo mbeleni. Pia anapanga nyimbo kufanya vizuri kwa sababu kwa hivi sasa Kuna wasanii wa Kisasa ambao anapaswa kuwafikia kimziki.

Hamisa Mobetto aandika ujumbe ambao umewaacha wengi wakijiuliza Kama mtoto anayemtarajia ni wa Diamond Platnumz

Hamisa Mobetto ameonyesha kuwa yeye hamuogopi mtoto yeyote ata Zari Hassan ambaye ni ‘mke’ wa Diamond Platnumz na mama ya watoto wake wawili.

Hii ni baada ya mrembo huyu kuandika ujumbe ambao umewaacha wengi wakijiuliza ikiwa mtoto anaye mtarajia ni wa Diamond Platnumz. Mrembo huyu aliandika kusema,

Mama Daa…? Mama dee…? Mama dii..? Mama doo..? Mama duh..?

Kulingana na mashabiki wa mrembo huyu, kuna unawezo kuwa Hamisa Mobetto alikasirishwa na video ambazo Zari aliwachia Jana kwenye Instagram yake – huku akionekana akitabasamu Diamond akimchezea gitaa wakiwa wawili huko Afrika Mashariki.

Hata hivyo hii sio mara ya kwanza ya Mobetto kufanya jambo kama hili kwenye mitandao yake ya Instagram. Ingawa hapo awali Diamond Platnumz alikuwa ameilana mimba hiyo….kwa hivi sasa hakuna uhakika nani anasema ukweli.

Tazama post hiyo hapa;

Hii ndio sababu mama mzazi wa Young D ajitolea kumlea mjukuu wake

Kuna fununu kuwa aliyekuwa mpenzi na mama ya mtoto wa Young D ameamua kumuacha mtoto wao wa miezi 7 na mama mzazi wa Young D.

Mamisar anasemekana kuwa amemuacha Tamar na mamake Young D baada ya kuondoka ilikujishighulisha na maisha yake. Akizungumza kwenye interview….Mamisar alikiri kuwa maneno haya ni ya Kweli na hata hivyo, mrembo huyu alisema kuwa kwa sasa amerudi kazini na ndio maana aliamua kufanya hivi.

Akizungumza kwenye interview, Mamisar alisema…

Mapenzi hakuna tena kati yangu na Young D, ndiyo maana familia yake iliamua kumchukua Tamar ili kumlea kwani nisingeweza kumlea kwa sababu ninafanya kazi. Nikitaka kwenda kumuona ninakwenda kama kawaida na hata nikitaka kulala huko wiki moja, ninalala.

Hizi ndizo pesa mwanaume yeyote anayetaka kumuoa Sanchi anapaswa kutoka

Model na video vixen Sanchi amewaacha wengi kama wamechanganikiwa baada ya kutaja kiwango cha pesa atakacho itisha mwanaume yeyote anayetamani kufunga ndoa na yeye.

Akizungumza kwenye interview Sanchi alisema kuwa inabidi mwanaume akijikaze ili alipe mahari. Kwa hivyo yeye kuitisha millioni 10 inamaanisha kuwa lazima mwanaume huyo awe na uwezo wa kumuangalia.

Sanchi alisema,

“Unajua mwanaume wa kweli unampima kwenye vitu vidogo kama hivyo, mimi mahari nataka iwe ya heshima kabisa na kama mtu hana milioni hiyo 10 basi hana sifa ya kuwa mkewe na kunimiliki,”

Kajala afunguka kueleza kilichomfanya kujihusisha na utumiaji wa bangi

Kajala ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa Wema Sepetu na pia muigizaji wa movie za bongo amefunguka kueleza sababu zilizofanya aanze kutumia dawa za kulevya Kama bangi na pombe.

Akizungumza na global publishers Kajala alisema kuwa marafiki wake wa hapo zamani ndio waliofanya aanze kuvuta bangi. Aliendelea kusema kuwa pia maisha yake ya wakati huo yalikuwa ya shida, na hii ilimfanya kutumia Madawa ili apunguze mawazo.

Unajua inafika mahali sisi kama vioo vya jamii inatupasa kuzungumza ukweli wa maisha yetu hasaa ya nyuma, ili kama ni watu kujifunza iwe hivyo, binafsi nimewahi kupitia maisha ambayo naweza kuyaita ya mpito, kipindi ambacho kila mtu hupitia katika harakati za ukuaji, kwamba nilijiingiza kwenye kampani za marafiki ambao ni watumiaji wa bangi.

Kulingana na Kajala anamshukuru mungu kwani hakupotelea kwenye maisha nayo. Hata hivyo alisema yeye hajawai kutumia cocaine, heroine wala kujidunga masindano

Hivyo, walinishawishi na kujikuta nikijiingiza kwenye ulevi huo, kidogo nipotee ila namshukuru sana Mungu kwani sikuwahi kuvuta madawa mengine kama cocaine, heroine sijui kujidunga masindano na mambo mengine ya kufanana na hayo, lakini ukweli kabisa huwa najuta sana kwa kuvuta bangi,” alisema Kajala na kuongeza; Ni muhimu wazazi kuwa makini na watoto katika kipindi cha kuingia kwenye utu uzima, kwa maana ya balehe ya kuvunja ungo, ndicho kipindi kibaya sana maishani kwa binadamu katika makuzi, vishawishi ni vingi sana.

Joh Makini aeleza umuhimu wa kuachia audio kali badala ya kutumia hela mingi kwenye video

Imefika wakati ambapo Watanzania wameanza kurudi kisikiza audio badala ya kuangalia video za muziki kulingana na alichosema Joh Makini ambaye ni rapa mkali kutoka Tanzania.

Msanii huyu alisisitiza kuwa kuna umuhimu w kuachia audio kali atakama video yake haitakuwa imefika kiwango cha kuridhisha. Msanii huyu aliambia E-Newz ya EATV kuwa muziki ni audio na ikiwa mtu anapanga kufanya vizuri inabidi ajikaze kwenye mistari yake.

Msanii huyu alipeana mfano wa hapo zamani ambapo wasanii wengi hawakuwa wakitengeneza video kali ilhali audio zao zilikuwa zinafanya vyema, Joh alisema,

“Baadae ilipoanza mambo ya video ikawa hata mtu akitoa wimbo na video kali wimbo unakuwa mkubwa. Baadae Watanzania walipoacha kushangaa picha, imekuja wakati ukipiga video kali kama wimbo ni wa kawaida hautoki, kwa hiyo cycle ni ile ile, wimbo ni audio kwanza haijalishi video kubwa au ndogo kwa hiyo ngoma kama ni kali kwenye audio inafanya chochote.”

Mzee Yusuf afunguka kuhusu kuoa tena baada ya mke wake kufariki

Alhaj Mzee Yusuf hivi karibuni alimpoteza
mke wake ambaye alikuwa akijifungua mtoto wao. Kifo chake kilibadilisha maisha ya Mzee Yusuf na wanawe lakini wamejifunza kuishi hadi watakopo kutana tena.

Hivi karibuni Mzee Yusuf kwa mara ya kwanza alifunguka kuzungumzia ikiwa anapanga kupata mke mwingine. Hata hivyo Mzee Yusuf akili ambao Gazeti la Risasi kuwa suala hilo ni la Allah na akipata bibi basi ataoa lakini kwa sasa ameamua kupumzika na kutulia.

“Suala la kuoa tena ni la Allah, nitamuomba kama akiamua mimi nioe nitaoa, kama pengine amenipunguzia ili nitulie basi nitatulia maana hili jambo linatakiwa subira kwa kila kitu, hutakiwi kukurupuka, nikikurupuka nitajikuta nashindwa mtihani huu ambao Allah amenipa,”

Mzee Yusuf aeleza watoto wanavyomuulizia marehemu mama yao atarudi lini

Siku kumi zilizopita Mzee Yusuf ambaye alikuwa muimbaji wa nyimbo za Taarabu alimpoteza bibi yake mdogo Chiku Khamis akijifungua mtoto wake wa tatu.

Hata hivyo wanawe ambao ni wadogo bado hawajafahamu kilichotokea kwenye familia yao. Mzee Yusuf amefunguka kusema kuwa sasa hivi watoto hawa wamekuwa wakimuulizia mama yao. Mzee Yusuf aliambia Gazeti la Risasi Mchanganyiko kuwa watoto hao wamekuwa wakimlilia mama yao sana huku wakiuliza alipo.

Aliendelea kusema kuwa alilazimika kuwapeleka kwa ndugu wa mama yao, ili kupunguza machungu yao.

Ninapata taarifa kuwa watoto hawaishi kuuliza alipo mama yao na kila wakikumbuka wanalia, hili ni jaribio kubwa ambalo atalazimika kupigana ili kuhakikisha linaisha salama.

Hata hivyo kwa hivi sasa anataka kuwarudisha nyumbani kwake. Aliendelea kwa kusema,

Nadhani huu muda ambao wamekaa kwa ndugu wa mama zao hao unatosha, hivyo nakwenda kuwachukua ili nikae nao mwenyewe, nianze nao maisha mapya ya bila mama yao kwa sababu nahisi ndiyo faraja yangu kwa sasa. Sijawa na maisha, bado nimechanganyikiwa, hivyo naamini nikienda kuwachukua watakuwa faraja yangu maana nikiwa nao naona niko salama zaidi, watoto wangu nitakaa nao mwenyewe maana mimi ndiye baba yao, watakaa na nani tena kama siyo mimi?

Barakah the prince afunguka kuhusu kufeli kwa wimbo wake mpya

Baada ya kuachaia wimbo wake mpya ‘acha niende’ msanii wa bongo Barakah the Prince almefunguka kudai kuwa amegundua kuna vitu kadhaa ambazo zimefanya wimbo wake kutofanya vizuri Kama nyimbo zake za hapo awali.

Akizungumza na kipindi cha Enewz cha EATV Barakah the Prince alisema kuwa aliwachia wimbo wake wakati kulikuwa na mambo mengi yanaendelea. Msanii huyo alisema,

Barakah The Prince
Barakah The Prince

Hali ni ngumu kweli kwa wasanii, nyimbo nyingi ambazo zimetoka hivi karibuni zimeshindwa kufanya kusema kweli hata wimbo wangu haujafikia kwenye malengo ambayo nilijiwekea wakati natoa ai hata nikilinganisha na nyimbo zangu zilizopita.

Hata hivyo amejipa moyo wa kufanya nyimbo zingine hivi karibuni.

Wolper amepata mchumba mwingine baada ya Harmonize?

Muigizaji wa filamu Wolper Stylish anaonekana kuwa amepata mchumba mpya baada kuachana na Harmonize ambaye anatarajia mtoto wake wa kwanza na mrembo wake mpya wa kizungu.

Wolper Stylish
Wolper Stylish

Kuachana kwa wawili hawa kuliwashtua mashabiki wao ambao walikuwa wakitarajia harusi kulingana na walivyokuwa wakipendana. Hata hivyo Harmonize alidhibitisha kuwa uhusiano wao ulikuwa umeisha na sasa alikuwa na mchumba mpya.

Hata hivyo Wolper alikaa kimya hadi Jana alipoandika ujumbe ambao umewaacha wengi wakisema kuwa kunauwezekano kuwa amepata mwanaume ambaye ameituliza roho yake sasa.

Hawa ndio wasanii wa Bongo ambao Lulu Diva anawakubali

Lulu Diva ambaye anajulikana kupitia mziki wake hivi karibuni aliwataja warembo wawili kutoka Tanzania ambao yeye anazitambua kazi zao.

Akizungumza kwenye interview, Lulu Diva alisema kuwa Vanessa Mdee na Lady Jaydee ni wasanii ambao wameweka bidii kwenye kazi zao. Aliendelea kuwasifu kuwa wawili hao wameipa Tanzania sifa kutokana na kazi zao za kuridhisha.

Lulu Diva pia alimtaja Beyoncé na Celine Dion Kama wanawake ambao anafurahia kazi zao za kimziki. Akiongea katika interview Lulu alisema,

“Kimataifa namuangalia sana Beyonce na Celine Dion. Nikimuangali Beyonce naangalia hadi life style yake anayoishi, nikimuangalia Celine namuangalia hata the way anavyoimba, anavyoweza ku-control sauti yake. Beyonce kuanzia swagger anavyoimba, anavyocheza jukwaani, anavyocheza mwenyewe kwenye video zake, mavazi hata life style yake akiimba nakubali sana.”

Rayvanny akamilisha kazi yake mpya na Jason Derulo

Mkali wa Wasafi Records Rayvanny hatimaye aliweza kukutana na Jason Derulo marekani ambapo wawili hao waliweza kukamilisha kazi yao mpya itakoyoachiliwa hivi karibuni.

Rayvanny alijumuika na Jason Derulo siku kadhaa baada ya kushinda Tuzo lake la kwanza la BET. Kupitia mtandao wake wa Instagram Rayvanny aliweka picha yake na Jason Derulo huku wakionekana wakiwa kwenye studio session.

Aliandika kusema,

“God bless you my brother @jasonderulo its amaizing opportunity,am so grateful for that……… Toka Saa 8 Usiku amekaa na mimi hadi Asubui… Studio kulikua na Watoto wakaaaaaliiiii lakini kawacha waondoke sababu walichoka kukaa studio yeye kabaki na sisi tu. Naamini kilichofanyika Mtakipenda. Thanks boss @afrikidd @babutale.”

Tazama picha hiyo Hapa;

Roma aweka wazi kuwa amewasamehea na kuwasahau waliohusika na kutekwa kwani

Roma ambaye ni msanii wa hiphop bongo alitekwa miezi kadhaa iliyopita lakini akapatikana baada ya siku kadhaa kitu ambacho yeye Kama mwanadamu hajaweza kusahau.

Hivi karibuni akizungumza na Times FM, Roma alifunguka kudai kuwa tangu awachiliwe serikali ya Tanzania haikumsaidia kwa njia yoyote. Msanii huyu alisema kuwa familia, marafiki na mashabiki ndio walisimama na yeye hadi kupona kwake. Alipoulizwa ikiwa Serikali ilimjulia hali wala kumshughulikia alijibu kwa kusema,

“Lahashaa! Hapana juu kwa juu tuu polisi, polisi Mwananyamala PF3 sijui nini ile, baada ya pale nikajiongoza mimi mwenyewe na familia yangu,so ikawa hivyo tuu“

Hata hivyo Roma alisema kuwa ameshawasamehe na amewasahau wote waliohusika na kutekwa kwake.

“Yaliyopita yamepita tunasamehe,tunasahau waliohusika Mungu atawahukumu na mkono wake na Mungu atupe neema uvumilivu na neema ya kuwasamehe…Lakini usidanganyike na mtu anakwambia sijui alikuja akatoa bugana lake au sijui akatoa hela ya panadol, Lahashaa!“