Dogo Janja amkana Muna Love baada ya tetesi kuwa wawili hao ni wapenzi

Dogo Janja amefunguka kuhusu uhusiano wake na muigizaji wa filamu Muna Love. Akizungumza kwenye interview hivi karibuni Dogo Janja alisema kuwa yeye na mrembo huyo hawana uhusiano wowote wa kimapenzi Kama wengi wanavyodhania.

Muna Love

Msanii huyo wa Bongo alidai kuwa tetesi hizi ni za uongo. Aliendelea kwa kusema kuwa uvumi huu umemuumiza na pia familia yake. Dogo alisema,

“Hakuna kitu kibaya kama utandawazi, yaani kila mtu ana simu na bando lake kwa hiyo akiamka asubuhi anajisikia kufanya chochote au kutunga vitu kama hivyo lakini siyo kitu kizuri, maana yananiumiza mimi na familia yangu, Uongozi wangu lakini pia vinamuumiza mpenzi wangu kwa sababu tuna malengo makubwa hivyo haya yanapoendelea yanazidi kumuumiza au kumchanganya”,

Aliendelea kwamba,

“Mimi siyo mtu wa kuonesha maisha yangu binafsi kwenye mitandao ndio maana hata mpenzi wangu sijawahi kumuweka mitandaoni, maisha yangu binafsi ni ya kwangu na siyo ya kila mtu hata huyo dada wa watu anaumizwa na hili na anafamilia pia kwa hioyo hizi habari zinazidi kumuweka pabaya.

Ni kweli Video vixen Tunda anamtarajia mtoto wake wa kwanza?

Ingawa tetesi zinazosambaa mitandaoni Ni kweli, basi Tunda anamtarajia mtoto na alikuwa mpenzi wake wa zamani, Young Dee.

Hapo awali mrembo huyu alikuwa amekanusha taarifa kuwa alikuwa mjamzito. Hata hivyo hivi karibuni aliweka picha ya Utrasound akionyesha mtoto mdogo anayeendelea kuwa kumaanisha kuwa anatarajia kupata mtoto.

Hata hivyo, hakuandika ujumbe unaodhibitosha kuwa anamtarajia mtoto lakini mashabiki wake waliacha ujumbe wa kumpa pombe mrembo huyu pamoja na Younge Dee.

Tazama picha hiyo hapa;

Young Killer amjibu Nay Wa Mtego baada ya kumdiss

Nay Wa Mtego ni msanii ambaye anajulikana kuwachana wasanii wenzake kupitia mziki wake. Hapo mbeleni ameskika akiwachana akina Wema Sepetu, Ommy Dimpoz na wengi kupitia nyimbo zake.

Nay wa Mitego

Hivi karibuni aliachia wimbo mpya ‘moto’ ambapo aliskika akimwambia Young Killer “Young Killer chali, safari ya Mwanza inanukia, usiwadharau waliokufanya ukatoba” kitu ambacho kimemfanya Killer kumjibu Nay.

Kupitia mtandao wa Instagram Young Killer aliandika, “Nasikia kuna mtu kanidiss” kuonyesha kuwa alikuwa ameupokea ujumbe wa Nay. Hata hivyo jambo hili halikumshtua rapper huyu kwani alimjibu Young Killer kwa kuandika ” #Ney True Boya,” kupitia mtandao wake wa Instagram.

Hata hivyo, hakuna anayejua kinachoendelea kati ya wawili hawa.

 

Amber Lulu aeleza sababu hawezi toka kimapenzi na wanamuziki wa Bongo

Amber Lulu anaonekana kuwa anazifuata nyayo za Gigy Money kwani pia yeye anajitambulisha kama muimbaji. Video vixen huyo kutoka Tanzania hata hivyo amefunguka kueleza sababu yeye Kama mwanamke hawezi taka kutoka kimapenzi na wasanii wa Bongo.

Amber Lulu alibainisha haya alipokuwa akizungumza na Bongo Dot Home ya Time Fm akisema kuwa wasanii wengi wa Bongo hues hawana msimamo na kwa sababu ya jambo Kama hilo, yeye hatamani kupata mpenzi anayefanya mziki wala mtu maarufu. Amber Lulu alisema,

” Mastaa wengi bongo ni wasumbufu sana, mimi huko nyuma niliwahi kuwa katika mahusianio na hao mastaa nikaona aah basi bora niachane nao, naona walivyo kwa sasa na najua wanavyoishi ndio mana sina mpango nao.”

Aliendelea kwa kusema,

“Wastaa wengi hawako serious sana na hata kwenye maisha yao hawako serious, mie naona mastaa naoshindanao naona kabisa hata akiwa na mpenzi kuna kitu kinamiss , unakuta mtu anakaa na watu hata watano yani.”

 

Mrembo kweli kweli; Wema Sepetu atisha kwa picha mpya

Ingawa Wema Sepetu amekawia Kabla ya kuachia picha zozote mpya mrembo huyo hivi Leo amewaacha picha mpya ambayo imewazingua wengi.

Wema Sepetu aliwekaa picha hiyo Instagram na kulingana na maoni ya mashabiki wake, mrembo huyu kweli ameumbwa akaumbika.

Kwenye picha hiyo Wema aliandika kusema,

I am speechless laviemakeup… you killed with this look. They don’t just call you Ms Forbes for nothing… my dada your hands are magical. Yaani nikimaanisha zimetengenezwa kwa magic… you know there are good pictures and then once in a while you get stunning pictures and then in while you get stunning pictures, Jamani this is a stunning picture…Hata usipokubali basi hata kimoyo tu.

Tazama picha hiyo hapa;

Gigy Money kuwachia wimbo mpya – papa

 

Gigy Money ambaye ni video vixen amefunguka kudai kuwa anamipango ya kuachia wimbo wake wa pili unaoitwa ‘Nampa Papa’. Hii inakuja mwaka mmoja baada ya kuachia wimbo wake wa ‘Supu’ uliompa umaarufu Tanzania.

Mrembo huyu aliambia Bongo 5 kuwa wimbo huu ulitayarishwa na procuder Kimambo Touches. Aliendelea kwa kusema kuwa wimbo huu unasifia urembo wa wanawake na kuwa wengi wataufurahia.

“Nampa Papa ni wimbo fulani kama nyimbo zangu zilizopita, ni kama Supu nilikuwa najivunia maumbile yangu. Kwahiyo kwenye ‘Nampa Papa’ ni wimbo fulani ambao bila shaka kila mtu ataufurahia,”

 

Aliongeza,

“Kwahiyo mabibi na mabwana tukae mkao wakula Gigy kaleta balaa jingine jipya tuoneshe ushirikiano na thamini vya nyumbani. Pia wimbo huu sijaandika mwenyewe nimeandikiwa na mwanangu mmoja anaitwa Marioo,”

Amber Lulu ataja sababu amazomtamani Diamond Platnumz

Amber Lulu ambaye anatamba sasa kwa kutokea kwenye video za mziki za Bongo ni mrembo ambaye anatisha.

Kwa hivi sasa anafanya vyema kwenye career yake na ingawa bado yeye ni mdogo. Hata hivyo, hivi karibuni alifunguka kumuongelea Diamond Platnumz huku akisema kuwa ni mmoja wa wasanii ambao anatamaniwa na warembo wengi.

Lulu alisema kuwa Diamond Platnumz anaonekana Kama mwanaume kwenye bidii na ikiwa hangekuwa na familia pia yeye angejaribu bahati yake, akiongea na Times FM, Lulu alisema…

 

“Kibongo Bongo sijaona mwanaume zaidi ya Diamond kwanza ana ni inspire na maisha yake yaani anajiweka kazi na kila kitu na sio kwamba na wish ku’date nae tuu bali kufanya nae kazi pia,”

Aliendelea kwa kusema,

“Kama ikitokea kutembea nae is ok….sio mimi peke yangu kila mwanamke anawish kuwa nae…kila mtu mimi naamini wachache sana ambao hawamuhitaji.”

Alikiba asheherekea siku ya kuzaliwa ya mwana wake na ujumbe huu

Alikiba hivi karibuni alisheherekea miaka 7 tangu mtoto wake wa kwanza kuzaliwa. Msanii huyu wa Bongo aliziweka picha kadhaa akimtakia Kiba junior miaka mingi duniani anapoendelea kukua.

Kama wasanii wenzake Alikiba alimwandika Prince Sameer ujumbe wa kuvutia huku akimtakia mwanae kila laheri kupitia mtandao wake wa Instagram. Kiba aliandika,

“Haya kibaba Miaka 7 sasa @kiba_junior mwenyezi mungu akupe umri mrefu wenye faida kwake na kwako InshALLAH

Tazama picha kutoka sherehe hiyo hapa;

 

Snura awajibu mashabiki wanaodhani anatumia dawa za kulevya Kabla ya kujibwaga jukwani

Kama ushawahi kumuona Snura akitumbuiza kwenye jukwaa, basi unaelewa kuwa yeye ni msanii ambaye huwaacha mashabiki wake kama wameridhika.

Lakini, kuna tetesi kuwa yeye hutumia pombe ili kutoa aibu ya kuwatumbuiza mashabiki wake. Hata hivyo hivi karibuni alifunguka kukana maneno haya.

Kulingana na yeye, hatumii pombe wala sigara jumps nguvu ya kutumbuiza. Alikiambia kipindi cha E-Newz ya EATV,

“Mimi napanda kwenye stage situmii kinywaji cha aina yoyote Mungu wangu aliyekamili ni shahidi. Sinywi pombe, sivuti na ninapanda kwenye stage ninahamsha kiasi kwamba unaweza kuhisi kuna kitu nimetumia kichwani, akili yangu nimeijenga hii ni kazi, huwezi kuona aibu kwa sababu ndio kazi uliyoichagua,”

Aliongeza,

“Kwa hiyo napenda nipande kwenye stage nikiwa mzima timamu nione kwa sababu hii ni kazi yangu naifanya, pia nafanya research kujua style gani nikicheza watu wananishangilia, wimbo gani nikiimba watu wanapenda,”

Abdu Kiba akana tetesi za kumuiga Ali Kiba

Abdu Kiba ambaye ni mdogo wa Alikiba hivi karibuni alifunguka kuelezea kilichotokea baada ya mtandao wake wa Instagram kuibiwa na mtu asiyejulikana.

Msanii huyu ambae amekawia bila kuachia nyimbo mpya alisema kuwa baada ya kurudisha Instagram yake alipata kuwa amewafollow watu ambao yeye hawajui na jambo hili likamfanya kuunfollow kila mtu kama anavyofanya Alikiba.

Alisema haya kukana tetesi zinazodai kuwa anamuiga ndugu yake mkubwa. Alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

“Nikizungumzia akauti nakumbuka mwezi mmoja nyuma nikiwa Marekani akaunti yangu walihack kwa hiyo nilikaa karibia wiki tatu siko kwenye mtandao wa instagram, nilipoweza kuirudisha akauti yangu ndipo nilipoamua nisimfollow mtu yeyote kwa sababu watu niliowakuta mule sio watu wangu.”

Aliendelea kwa kusema,

“Kwa hiyo niliwa-unfollow nikabakia siwezi kumfollow mtu tena. Sijafuta utaratibu wake bali ni maamuzi yangu, wategemee any day naweza nikamfollow mtu yeyote,”

Ben Pol aeleza sababu mahusiano yake huwa hayadumu

Msanii mkali wa Bongo Ben Pol ni mmoja wa wanaume ambao mashabiki hutamani. Yeye ni mwanaume ambaye anajitambua ila kulingana na yeye mahusiano yake huwa hayadumu.

Ben Pol alifunguka kwa mara ya kwanza kudai kuwa mahusiano yake ambayo yalidumu sana ni pale ambapo alikaa na mwanamke kwa miezi 9 lakini wakaachana.

Kulingana na yeye warembo wengi huja na matarajio ambayo yeye hawezi fikia. Ben Pol ameiambia Choice FM.

“Miezi tisa ndio longest relationship kwa sababu unajua yaani nimekutana na watu wa aina tofauti, watu ambao wanaokuwa na expectation kubwa zaidi kuhusu mtu flani, kwa hiyo akiingia kwenye maisha yako anakuwa ana vitu tayari ali-picture kwamba Ben Pol tutakuwa tunakula bata every weekend, tunakula bata milioni, tunaenda huku na kule. Kwa hiyo mtu anaingia kwenye maisha yako anakuta si mtu wa hivyo ni staa ndio lakini we don’t go to club mara kwa mara, we don’t do this, we don’t do that, kwa hiyo mtu anakuwa disappointed anatoka kwenye mahusiano ndio hicho nime-experience zaidi kwenye mahusiano yangu yaliyopita,”

Baby Madaha aendelea kumchana Vanessa Mdee

Muimbaji Baby Madaha ameonekana kuwa na uchungu na mwenzake, Vanessa Mdee. Hivi karibuni alisema kuwa Vmoney hana kipaji chat kuwa msanii ambaye anatajwa kuwania tuzo zozote za muziki.

Baby J
Baby Madaha

Hata hivyo Baby Madaha haonekani kujuta kwa kusema maneno haya. Hivi karibuni akiongea na Bongo 5 Baby Madaha alidai kuwa kuna wasanii wakali kumshinda mrembo huyu wa Jux . Kulingana na Madaha, Vmoney bado hajafikia kitengo cha kuwania tuzo za kimataifa Kama anavyofanya kwa sasa. Madaha alisema,

“Mimi si shabiki wa Vanessa hata muziki wake, hata nyimbo zake sizisikilizi kabasa,”

Aliendelea kusema kuwa yeye anawatambua wasanii Kama Lady Jaydee na wengi even ambao wameonyesha talanta zao za kuimba kupitia mziki mzuri ambao wameachana. Aliongeza,

“Kuna wasanii wakali hawapewi tu nafasi, mimi ni shabiki wa Lady Jaydee, akina Mwasiti kuna wasanii wengi wanafanya muziki nzuri,”

Hata hivyo alisema kuwa yeye hana wivu kwa Vanessa Mdee ila tu ni maoni yake.

Baada ya kuacha matumizi ya madawa za kulevya, Chidi Benz apanga kuachia muziki

Kunauwezekano wa kuziskiza nyimbo za Chidi Benz tena ikiwa ni kweli ambacho walichosema wao hizi wake wapya walisema katika interview yao.

Kulingana na Bongo 5 ambao walinena na uongozi wake mpya, ni kweli kuwa Chidi Benz ameungana na Q Chief kuachia wimbo mpya ambao uataachiwa hivi karibuni.

Nyimbo hii imeandaliwa katika studio za Kill Record chini ya producer Mbezi.

“Wiki ijayo Chidi Benz anarudi upya kwenye game, ngoma ni kali sana bila shaka mashabiki walikuwa wanamsubiria Chidi yule wazamani,” alisema meneja huyo aitwae Shabaha. Mimi binafsi nje ya umeneja Chidi ni msanii ambaye namkubali sana toka kitambo, nilivyosikiliza hii kazi yake mpya akiwa amemshirikisha Chidi Benz nimeona kabisa hapa kuna kitu kipya. Unajua ngoma nyingi za Chidi ambazo amekuwa akizitoa hivi karibuni sio level zake, lakini alivyonisikilizisha huu wimbo nimeona kuna kitu cha ziada kipo. Kwahiyo mashabiki wakae mkao wa kula kuna jiwe linakuja,”

Gigy Money aeleza sababu hampendi Shilole

Mrembo kutoka Bongo Gigy money ambaye ni star wa video za mziki amefunguka kudai kuwa yeye si shabiki wa nyimbo za Shilole wala hampendi.

Gigy alisema haya baada akisititiza kuwa yeye binafsi ni fan wa hip hop na kwa hilo jambo, yeye anamsupport Rosa Ree. Aliendelea kwa kusema yeye angepata mtu wa kumuandikia mistari, panda kufanya muziki ambao ungewavutia mashabiki wengi. Mrembo huyu alisema,

shilole
shilole

“Sina hata mpango wala sitaki, sio fun wake (Shilole), labda Rosa Ree, tatizo la watu walio up wanasumbua, so hip hop its better, mimi ningepata mtu wa kuniandikia niwe nachana ningependa, I don’t love this kind of music ambayo nafanya, nafanya ili nipate hela, mimi napenda hip hop,”

Hata hivyo Gigy anaonekana kuwa na ‘beef’ na mastaa wa kike kutoka Tanzania.

Tundaman asema hili ndilo jambo ambalo hajawahi kumfanyia Mke tangu waoane

Tundaman ni mmoja wa Wasanii ambao wameweza kutamba Afrika Mashariki kupitia muziki wao. Hata hivyo yeye pia ni mume wa mtu na yeye analiheshimu jambo hili.

Tangu afunge ndoa na mpenzi wake Tundaman anadai kuwa hajawai kumpiga mke wake ata wanapokuwa na shida kwenye ndoa yake. Msanii huyu alifunguka kunena maneno haya akiwa kwenye kipindi cha XXL kwenye U-Heard na kueleza kuwa,

“Mie sijawahi kumpia mke wangu we muulize kama nimewahi kumpiga mimi labda huyo ni Tunda mwingine sio mimi.”

Tundaman na mpenzi wake walifunga nikaha mwaka uliopita na bado anaendelea kuachia project zake mpya kila wakati.

Aliyekuwa mpenzi wa Nandy afunguka kuhusu uhusiano wao wa sasa

Nandy kwa kweli ni mwanamke ambaye ameumbwa akaumbika. Kwa sababu hii ni wengi ambao wanatamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na yeye ila kwa hivi sasa mrembo huyo ametulia na kufocus kwenye muziki wake.

Hata hivyo aliyekuwa mpenzi wake hapo mbeleni Emmanuel Mathias ambaye anajulikana Kama MC Pilipili alifunguka kuelezea uhusiano wao wa sasa ni wa aina gani.

Akizungumza na Bongo 5 mchekeshaji huyo alidai kuwa bado anawasiliana na Nandy kuonyesha kuwa ingawa wameachana, bado wawili hao ni marafiki. Alisema,

“Mimi na Nandy bado tuna wasiliana vizuri tu, nimerudi kutoka Marekani nimemletea zawadi ya Perfume, hata hivyo yeye yupo Kenya amenicheki kunijulisha kuwa yupo huko na ninaona picha anazopost akiwa huko, unajua mimi na Nandy tumeachana sio kwa ubaya, ila tulifanya hivyo kwa sababu Nandy alikuwa anataka afanye kazi zake kwa uhuru zaidi,”

Aliongeza kuwa

” Kuachana na Nandy hapakuwa na kosa, sikutaka kumpa stress (mawazo)ni makubaliano yetu yalikuwa ni hayo, sio kwa ubaya ni kwa wema kabisa. Sikutaka kuzima ndoto zake kwani ningeshindwa kuwa mume wake ningekuwa nimezima ndoto zake za kufika hapo alipo.”