Flaviana Matata achoshwa na comments za mitandaoni kuhusu mwili wake

Flaviana matata ni mmoja kati ya wanamitindo  waliotajwa kwenye gazeti la forbes kuwa ni mwanamitindo anaeingizaa ela nyingi Africa,Mwanamitindo huyo  maarufu wa kitanzani anaefanya kazi zake nje ya nchi na mwenye makazi yake marekani ambae pia ni mfanyabiasha wa rangi za kuchwa yenye  brand  ya Lavy  ameamua kufunguka katika ukurasa wake wa instagram na kuonyeshwa kukerwa na comments za watu wanaojifanya kumshauri kuhusu jinsi ya kuuweka mwili wake huku wengine wakionekana kukerwa na yeye kuwa mwembamba sana .

Kwa Flaviana Matata kuwa mwembamba ni moja ya vitu anatakiwa kumaintain kutokana na kazi yake ya modelling anayoifanya, ambapo urefu na kuwa mwembamba ni siafa za kuwa mwanamitindo bora ingawa zipo sifa zingine nyingi ndani yake,katika post hiyo Flavy ameonekana kukasirishwa na watu ambaowamekuwa wakiweka maoni yao kwenye picha zake  kuwa yeye ni mwembamba ivyo ajitaidi kuongeza kula.Flaviana amejibu katika ukurasa wake wa instagram kuwa anakerwa na tabia za watu kuwa wanamfatiliana na wanapaswa kufatilia mambo yao,” Honestly people need to learn to mind their business and be concerned with more important stuff. I am tired of unsolicited advice “YOU NEED TO EAT” comments….who told you I don’t eat??!!”

Flaviana anaongezea na kusema kuwa yeye ameridhika na mwili wake hivyo watu wasimpangie kuhusu mwili wake “am happy and proud of my and that’s all matters ” alimalizia.

Flaviana Matata amekuwa ni mmoja kati ya wanamitindo maarufu sana ndani na nje ya nchi na makampuni mengi kumtumia katika kazi za modelling  pengine labda ni kwa sabbau ya huo mwili mwembamaba ambao watu wanausema ndio unaomfanya yeye afanikiwe, pengine labda hiyo ndio lifestyle yake aliyoichagua  ya kuuweka mwili wake , anaupenda mwili wake na inawezekana pia labda  ni kwasababu anaamini ivyo ndivyo yeye alivyo.

Lakini pia Flaviana Matata alifunga ndoa mwaka jana na mtanzania mwenzie lakini wanaishi marekani hivyohivyo  pia  yeye ndie  mwanzilishi wa flaviana matata foundation.

Mh.Nape akanusha kushindwa kuwapatanisha Diamond na Alikiba

Aliyekuwa waziri wa habari na michezo ambae pia ni mbunge wa Mtama kupitia chama cha CCM mh.Nape Nnauye amefunguka kuhusu jitihaada zake za kutaka kuwapatanisha wasanii wakubwa nchini Diamond na Alikiba kipindi cha uongozi wake katika sekta hiyo ya michezo,mh. nnauye anasema kuwa sio kweli kuwa alishindwa kuwapatanisha ila jitihada hizo zilikwama kutokana na uongozi wake kukoma ghafla, kwa sababu ambayo iko wazi.

Mh.nape alipokuwa waziri wa habari na michezo alikuwa ameunda kamati iliyowashirikisha wasanii hao ili kuchangia vijana wa mpira wa miguu,kamati iyo ilikuwa na lengo la  kuwakutanisha diamond pamoja na alikiba pamoja ili kufanya kampeni za kuhamasisha wananchi kuchangia kusaidia timu ya Taifa ya Serengeti boys under 17 ambao walikuwa wanaenda kucheza nje ya nchi,Mh. nape anasema kuwa lengo kubwa  ilikuwa ni kuweka historia ya kuwafanya Diamond na alikiba kuwa na wimbo ulioimbwa pamoja hata kama hawatakutana sehemu moja yaan katika wimbo huo kila mtu awe na verse yake katiaka wimbo huo,katika kuwaunganisha huko walishatengeneza na beat ,ilikuwa ni  swala la muda wa kuwakutanisha tu ili kutengeneza wimbo.

Kiongozi huyo anasema kuwa bifu la Diamond na alikiba ni zuri endapo msuguano wao utakuwa mzuri kama utakuwa na manufaa ya kukuza muziki nchini  , kama mmoja anatoa wimbo huu na mwingine akatoa huu ni vizuri pia kama ilivyo sasa mmoja ametoa seduce me mwingine katoa zilipendwa, anaongezea kwa kutoa mfano wa uwepo wa wasanii wa zamani wa taarabu kama khadija kopa na Nasma Kidogo  ambao  walikuwa wanapigana vijembe lakini walikuwa wananogesha sana muziki wa taarabu kutokana na ushindani wao katika muziki huo .

Mh. Nape  alifananisha bifu la diamond na alikiba kama  ushindani wa simba na yanga ‘leo ukitaka mpira ufe basi ua bifu la simba na yanga  , ukishaliua tu na mpira unakufa ,  hivyo ndio burudani ilivyo ‘ anaongezea kuwa kama  bifu liwepo ila tu lisivuke mipaka ya kujenga chuki na kutaka kuumizana.

 

“Labda nina mimba ya Wizkid” Gigy Money asema

Msanii na mrembo wa video Gigy Money amekuwa akisingiziwa kuwa anamimba kitu ambacho aliweza kufunguka kuhusu hivi karibuni.

Akizungumza na FNL ya EATV Gigy Money aligusia kuhusu wimbo wake mpya ‘Papa’, alafu baadae akaongeza kwa kana taarifa zinazodai kuwa anamimba huku akisema kuwa ameiambia FNL ya EATV kuwa anatamani sana kutoka kimapenzi na msanii Wizkid ambaye anaweza kumzalia.

“Kipindi cha sasa hivi na Papa ndio nimetoa?, hapana, ujue mpaka yananishtua maneno haya, you know sina mimba lakini labda nina mimba ya Wizkid unajua mimi natamani ikaenda ikashuka tu.”

Akamalizia kwa kusema;

“Yeah namkubali, unajua dream sio wote wanatimiza ndoto zao, mimi nimetimiza ndoto yangu, nilisema Tekno moyoni siumeona huyu hapa akajaa,”

Rich Mavoko afunguka kuelezea mambo yanavyofanywa katika WCB

Rich Mavoko ambaye ni mmoja wa wasanii kutoka Wasafi records hivi sasa anaonekana kuwa career yake ya mziki inafanya vizuri kushinda hapo mbeleni. Kwa sasa ameachia nyimbo kadhaa ambazo zimemuweka kupata umaarufu Afrika.

Hivi karibuni alifunguka kuzungumzia mambo yanavyofanyika katika familia ya wasafi records. Kulingana na yeye familia hii inautaratibu wa kfuatilia mambo. Rich Mavoko aliendelea kwa kusema kuwa lebo hiyo inamipaka ambayo kila mmoja anapaswa kuiheshimu.

Mavoko amesema kuwa katika WCB inamaanisha kuwa wanaishi kama watoto na wazazi wao na ni lazima kufuata utaratibu. Alisema,

“Mtu kama Tale, Sallam na Mkubwa Fella, useme tu kitu fulani na uamue wewe, huo ni uongo. Ni wakubwa kwangu, so hata kama tunaongea kuna mipaka lazima niwe naheshimu, ukisema sauti yangu ndio isikilizwe tu kwa desturi yetu na mila utakuwa unakosea.”

Aliongeza. kwa kusema,

“Lazima uongee katika njia nzuri na wakuelewe, si semi nikiongea ndio litakuwa limepita kwa sababu mwisho wa siku umempa mtu nafasi ya kukusimamia maana yake umemuamini, pia anajua anachokifanya. Kwa hiyo unaleta mawazo nimeona hiki na hiki nataka nifanye, wao wanakaa na wanajadili kama kipo sawa mnafanya,” a

Nandy afutilia mbali fununu kuwa amekosana na Dully Sykes

Nandy ambaye ni msanii mpya kutoka Bongo ameanza kuwapa wengi wasiwasi kwani anaonekana kuwa anatalanta ambayo itampa umaarufu Afrika Mashariki.

Hata hivyo hapo awali ilikuwa inasemakana kuwa Nandy na Dully Sykes hawakuwa wanasikizana lakini akizungumza hivi karibuni kupitia Planet Bongo ya EA Radio Nandy alisema,

Nandy
Nandy

“Yupo sana proud na mimi kila tukikutana huwa ananisisitiza kuwa na heshima, kusikiliza wakubwa walionitangulia, kufanya kazi kwa bidii kwa sababu hustling yangu aliiona toka way back na ndoto zangu anazijua nyingi sana,”

Aliendelea kwa kuzungumzia issue ambayo mashabiki wengi wanadai kuwa anajaribu kuwa Kama Ruby ingawa alisema,

“Kwa hiyo kaniambia ndoto zako zimetimia, so usiachia hiyo chance kwako kwa kufanya lolote baya.”

Hizi ndizo pesa Harmonize anapata kupitia YouTube

Harmonize ambaye ni msanii kutoka Bongo amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu pesa ambazo yeye hupata kupitia mtandao wa Youtube kwa Mwezi. Muimbaji huyu ambaye anafanya na Wasafi records alikuwa akiongea na Clouds FM alipotaja pesa mbazo kwa hivi sasa anapata.

Kulingana na yeye anapata kiwango cha Dola 3,500 ambazo zimeweza kuchangia kwa maisha yake ya kifahari. Harmonize alisemakuwa pesa hizi ndiyo zimemuwezesha kutembelea magari ya kifahari ambazo mashabiki hushindwa katoa wapi.

Msanii huyu alisema,

“Namshukuru Mwenyezi Mungu Kupitia muziki umenikutanisha na watu wengi,Umenipa Dili napata riziki kwenye njia tofauti tofauti,sio tu kwenye show,licha ya kufanya show nauza nyimbo zangu kwenye Platform,Mimi akaunti yangu ya Youtube kila mwezi nalipwa Dola 3,500.”

Hata hivyo sio siri kuwa muimbaji huyu amejikaza kimziki na ndio maana maisha yake yamebadilika.

Linah aonyesha muonekano wa kitanda cha mwanae anayemtarijia hivi karibuni

Linah bado hajataja jinsia ya mtoto wake mtarajiwa ila anaonekana ameanza kujipanga mapema kwani amebakisha wiki kadhaa ajifungue.

Muimbaji huyo wa Bongo amekuwa akiposti picha kuonyesha ujauzito wake huku akiwa na furaha ya kuwa mama kwa mara ya kwanza maishani yake. Hata hivyo hajamtambulisha baba ya mtoto anayemtarajia lakini hapo mbeleni aliweza kufunguka kwa kusema kuwa ni mtu wa dini ya Kislamu.

Hata hivyo amebakisha wiki kadhaa ajifungue na kulingana na mtandao wake wa Instagram, Linah ameanza kujipanga kwa kumnunulia mwanae kitanda na doli kadhaa alizoziweka mtandaoni wake.

Tazama picha aliyoiweka hivi karibuni.

Reality TV star wa Kenya Mishi Dorah adai kuwa Rayvanny alitaka kumpa mimba

Kilichotokea kati ya Mishi Dorah na Rayvanny hakiwezi julikana kwa kiukweli kwani wawili hao walikutana wakati ambapo hakuna yeyote alijua kuwa wana ‘mahusiano.’

Mishi Dorah

Hata hivyo, Rayvanny amekuwa akimkana mwanamke huyu kwa kusema kuwa anataka kumuharibia nyumba na jina lake. Lakini baada ya Ghafla kumhoji mwigizaji huyo wa Nairobi Diaries, Mishi Dorah alisema kuwa ni kweli aliweza kupatana na Rayvanny kimapenzi.

Mishi Dorah aliendelea kwa kusema kuwa hajapata hedhi zake kwa mwezi mmoja kuonyesha kuwa kunauwezekano wa mwanamke huyu kuwa na mimba ya Rayvanny kutokana na alivyosema. Kulingana na Mishi, Rayvanny alikuwa anataka sana wawili hao wapate mtoto wao wa kwanza kitu ambacho alihisi hawezi kuharikisha kwani hakutaka kuiharibu figure yake.

Lakini swali bado ni…Kati ya mwanamke huyu na Rayvanny nani anasema ukweli? Ebu itazame interview yake hapa.

https://youtu.be/wN6ppPh-TEI

Wema Sepetu amsifu Martin Kadinda katika ujumbe alioamwandikia kusheherekea siku yake ya kuzaliwa

Aliyekuwa manager wa Wema Sepetu, Martin Kadinda hivi leo amesherekea siku yake ya kuzaliwa na kama kawaida marafiki wake wa dhati wamekuwa wakimpost kwenye Instagram huku wakimsherekea leo.

Wema Sepetu ni mmoja wa marafiki waliompost Martin Kadinda. Katika ujumbe wake, Wema Sepetu alimsifu Martin na kumfungulia roho katika ujumbe wake uliowaacha mashabiki na tabasamu. Aliandika kusema,

Wema sepetu akiwa na Martin Kadinda

The World Knows How I feel about You… I have nothing more to add to dat… I love you more everyday than yesterday… (Mi nakupenda Leo kuliko Jana, ?) Happy Birthday wa kwangu mimi apa…. Wa Sunny, Wa Sunshine, Kaka manager wa kwanza kabisa duniani… Yaani hapa natafuta maneno mapya mapya ambayo sijawahi kukwambia ila najikuta nakosa maana yote nishamalizaga… Basi wacha niache kutype….

Wawili hawa wamekuwa marafiki kwa miaka mingi na ata baada ya Martin kuanza biashara zake, bado wako pamoja kama ndugu na dada.

Msanii mwingine kutoka kenya azuru WCB baada ya Willy Paul

Inaonekana kuwa Willy Paul sio msanii pekee kutoka Kenya ambaye anajulikana na Diamond Platnumz. Siku chache baada ya kuzuru Tanzanian kupromote wimbo wake I Do aliyomshirikisha mrembo kutoka Jamaica, Alaine… msanii mwingine anayejulikana kama Chikuzee kutoka pwani pia alikuwa kwenye ofisi za WCB hivi leo.

Msanii huyu anayejulikana sana pande za Mombasa Chikuzee aka Zee la Mavuvuzela ni alishare picha zake kupitia mitandao yake ya kijamii alipotembelea WCB.

Kwa hivi sasa kuna tetesi kuwa kuna kitu kiko jikoni baina yake na Rayvanny. Mashabiki wake kupitia kwa comments walitaka kujua kama alienda pale kutia sahihi mkataba wa kuwezesha ngoma zake kuwekwa kwenye wasafi.com ama kama walikuwa wanatengeza projects mpya.

Ata hivyo msanii huyu hajafunguka kueleza alikchokuwa akifanya ofisini mwa Diamond Platnumz lakini kuna uwezekano kuwa kuna jambo kubwa wawili hawa wanataka kuachia.

Msanii wa Bongo Fleva Linex adai kuwa kiki inaua muziki

Linex, msanii maarufu wa bongo amefunguka na kusema kuwa mtindo wa kupa mziki kiki unapoteza ladha na focus ya mziki nchini Tanzania.

Akiongea na waandishi wa global punlishers Tz nyumbani kwake Mbezi Beach Dar es Salaam, Linex amesema kuwa imekuwa kama trend ya wasanii wa Bongo kutokea na skendo wakati wanpotaka kuachilia mziki siku hizi. Kulingana na yeye vitendo kama hivi havina maana kama msanii anaamini kazi yake ni nzuri.

Msanii huyu aliendelea kusema kuwa mashabiki ndio wanaoamua kama projects za wasanii ni za kuvutia au la. Linex alisema,

“Nachoweza kusema turudi kushabikia muziki mzuri, tuache kushabikia skendo. Nachokiona hapa muziki unapotea kabisa”

Ata hivyo hit maker huyo wa Kiherehere aliwasihi mashabiki kuwa makini na kufuatilia muziki wa maana badala ya kushabikia skendo za watu maarufu.

Harmorapa awataja mastaa ambao waliompa jina analolitumia sasa

Rapper wa Tanzania, Harmorapa, kwa sasa hivi ni mmoja wa watu maarufu Afrika Mashariki. hii ni kwa sababu ya jina lake na pia nyimbo anazoziachilia.

Kabla ya kuwa staa mkubwa rapper huyo hakuwa anatumia jina hilo lakini baada ya kujitokeza na alikutana na mastaa kadhaa waliomshauri kutumia jina analotumia sasa.

Akizungumza katika show ya Bongo Dot Home cha Times FM, Harmorapper alisema kuwa Roma na Mr T-Touch ni watu ambao walimsihi kutumia jiona la Harmorapa na pia kwa sababu anafanana na mwimbaji wa Wasafi records, Harmonize

“Baadhi ya mastaa wakubwa katika muziki wa hapa Bongo nao walinishauri nijiite hivi, akiwemo brother Roma Mkatoliki na Mt T-Touch,”

Hapo mbeleni rapper huyu wa Tanzania alikuwa akifahamika kama Jembe la Kusini, jina ambalo ata mimi kama shabiki wake naona halingeweza kumake kwa hii industry.

“Wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,” Harmorapa ambia watu wanaomuongela vibaya

Staa na rapa wa Tanzania, Harmorapa hivi majuzi aliweza kufunguka kuhusu watu ambao wanamtusi na kumuongelea vibaya tangu awe maarufu.

Rapper huyo ambaye amekuwa akifanya vizuri Tanzania na Afrika Mashariki kupitia nyimbo zake hivi sasa ndiye anayepata kiki kubwa Bongo na anavyoonekana, Harmorapa atakuwa na umaarufu kama wa Diamond Platnumz iwapo ataendelea kurelease projects ambazo watu watapenda.

Hata hivyo, akizungumza na Bongo 5 rapa huyu alisema kuwa habebwi na kiki na kuwa kazi yake ndiyo inafanya awemaarufu kwa hivyo wanomchukia wanafanya kazi bure na kuwa ataendelea kuachilia nyimbo zake kama kawaida.

“Watu ambao wanahisi Harmorapa hatodumu kwenye game kwanza wanakosea halafu pia naweza nikasema kwamba wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,”

Aliendelea kwa kusema kuwa…

“Kama mimi binafsi nimejipanga sana vya kutosha. Unajua kwamba maneno yao mimi hayanivinjii chochote ni ile sawa na kumpiga chura teke na kumwongezea mwendo. Wanavyoniongea mimi ndo wananipa power na wananipa maujuzi na wananipa kuweza. Ni wao wananiweza mimi kuweza na kukaza ilmradi niweze kufanya kazi nzuri.”

Harmorapa  pia amehaidi mashabiki wake projects kubwa ambazo ataachilia mwaka huu.

Mtoto kapendeza! Zari Hassan amnyoa Nillan mara ya kwanza tangu azaliwe

Mtoto wa pili wa Zari Hassan na Diamond Platnumz , Prince Nillan ameachwa akifanana na babake baada ya kunyolewa na mama make hivi leo.

Kupitia mtandao wake wa Instagram Zari aliweza kupost picha hizi mpya za Nillan huku akimsifu alivyopendeza baada ya kumnyoa nywele zake.

Ni kweli kuwa Mtoto huyu ambaye ni mmoja wa mastar awachanga Tanzania anafanana sana na babake Chibu Dangote na Tiffah.

Wengi wa mashabiki wake wamekuwa wakimfananisha na dadake Tiffah na kusema ukweli hawa wawili wanakaa mapacha ingawa Tiffah atafikisha miaka miwili mwezi wa Agosti.

Ikiwa hujaziona picha mpya za Nillan, basi ziangalia hapa chini.

 

Picha ya Hamisa Mobetto akiwa amevaa suruali ya Diamond Platnumz

Kuna riporti zimekuwa zikianaa mitandaoni kuwa Diamond Platnumz ashawai kuwa na mahusiano ya ndani na Hamisa Mobetto, video vixen ambaye alishirikisha kwenye video yake ya Salome.

Hivi majuzi kuna picha iliyoebuka mitandaoni ikimuonesha Hamisa Mobetto kama amevaa suruali ya Diamond Platnumz.

Picha hii imewawacha mashabiki wakiamini kuwa wawili hawa washiakuwa pamoja na hivi ndivyo Hamisa aliweza kuipata suruali hii.

Ingawa hakuna kitu kinachodhibitisha kuwa Hamisa alitoa trouser hii kwa Diamond Platnumz, wengi bado wanaamini kuwa uvumi uliokuwa ukiwafuata Diamond na Hamisa Mobetto ni wa ukweli.

Pia Wengi wanadai kuwa hii ndio maana Zari Hassan and Mobetto hawajaweza kupatana kwa muda sasa.

Hamisa Mobetto hajazungumzia kuhusu picha hii inayoenea mitandaoni lakini mashabiki wa team Diamond Platnumz wamekuwa wakimtag mrembo huyu kwa hiyo picha kuona kama ataweza kusema kitu kuihusu.

Hata hivyo, Tazama hiyo picha hapa chini.

Hamisa na Diamond Platnumz kavaa suruali zinazo fanana
Hamisa na Diamond Platnumz kavaa suruali zinazo fanana

New Video: Harmonize aachia video yake mpya aliyomshirikisha mpenzi wake kama video vixen

Msanii wa Tanzania Harmonize ameachia mpya video ya wimbo wake mpya Niambie aliofanya miezi 6 baada ya Matatizo.

Harmonize ambaye anafanya kazi chini ya uongozi wa Wasafi records amefurahisha washabiki kwa wimbo huu uonawagusa kidani maana ameimba kuhusus mapenzi, kitu ambacho mashabiki wa bongo hupenda.

Katika video yake, Harmonize alimshirikisha mpenzi wake wa dhati, Jacqueline Wolper. Kwa kufanya hivi, mashabiki wengi wameachwa wakifikiria kuwa mapenzi yake na Wolper ni ya kiki.

Hata hivyo, alifutilia maneno haya mbali alipokiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM Jumatano hii, kuwa kuna wakati alipogombana na mpenzi wake lakini sasa wamesuluhisha kila kitu.

“Kuna vitu vilitokea tukajikuta hatuko sawa, lakini Mungu ndio mwenye kheri tukawa tupo pamoja tukajua kabisa kuwa hiki kitu Jack hakipendi au mimi. Sasa hivi kila kitu kinaenda sawa na mapenzi yetu sio ya kiki, nafasi yetu kwenye jamii imefanya ionekane kuwa ni kiki,”

Hata hivyo, tazama video yake mpya hapa.