Hivi ndivyo Hamisa Mobetto alivyosheherekea siku ya kuzaliwa ya mwanae

Hamisa Mobetto hajulikana tu kwa sababu ya urembo wake lakini kwa moyo wake mkunjufu na mtu ambae hana neno na mtu yeyote. Ameweza kuiweka maisha yake off mitandaoni na mara moja moja huweza kuposti picha za mwanae ambaye anampenda sana, kulingana na anavyomuongelea kwenye mitandao yake ya kijamii.

Hivi leo mtoto huyo, Fansy amefikisha miaka mitatu tangu azaliwe na kama kawaida Hamisa Mobetto aliziposti picha kadhaa kumsheherekea mwanae kupitia account yake ya instagram. Aliandika kusema…

Happy birthday my Baby nakupenda @misfansy .

Model huyu aliposti picha kadhaa ambazo zimewaacha mashabiki wake wakitamani anavyomlea mwanake. Ata hivyo tazama picha hizo hapa.

Huyu ndiye msanii wa Kenya ambaye Harmorapa anataka collabo naye

Harmorapa anamipango ya kutamba nchini Kenya na kwa sababu hii amemtaja msanii ambaye amekuwa akitaka kufanya kazi naye kwa muda sasa.

Akizungumza na Bongo 5 msanii huyu ambaye anafanya vyema nchini Tanzania alisema kuwa anamkubali Prezzo na anaipenda kazi yake. Aliweza kueleza kwa sasa msanii ambaye angependa kufanya at least project moja na yeye nchi za Afrika Mashariki ni Prezzo peke yake.

Prezzo
Prezzo

“Prezzo namkubali sana toka kitambo, tokea niko chini shule ya msingi. Nilikuwa namkubali sana swagga zake na rap zake zilikuwa zinanifurahisha sana na zinanifurahisha mpaka kesho kiukweli.”

Aliendelea kusema iwapo atapata nafasi, Afrika mashariki itaweza kuona collabo yake na Prezzo. Lakini kwa sasa anangoja nafasi hii ikitokeze na kwa kiukweli ataweza kuifanya Tanzania proud.

“So kwahiyo natamani sana one day nifanye naye collabo kwahiyo kama nikipata nafasi kufanya naye itakuwa very good nitashukuru Mungu,”

Picha: Hivyo ndivyo mamake Kanumba na wengine walivyoadhimisha miaka 5 baada ya Steve Kanumba kufariki dunia

Hivi leo 7th Aprili mamake Kanumba na waliokuwa marafiki wake wakairibu walivyoadhimisha miaka mitano baada ya muigizaji huyo kufariki. Wote waliojitokeza walikutana kwenye makaburi ya kinondoni jijini Dar es salaam kufanya ibada kabla ya kumuwekea marehemu maua.

Ingawa sio wengi waliojitokeza, mama Kanumba aliwashukuru wote waliomsidikiza kwenye maadhimisho hayo. Alisema,

“Kiukweli nawashukuru wote waliojitokeza kwenye shughuri hii ya leo kwani sikuwa nimeandaa kitu kikubwa ila nashukuru mungu kuniwezesha,”

Johari ambaye ni staa wa filamu bongo pia aliwasihi wasanii kupendana na kupeana support kwa kila kitu. Na kulingana na alichosema, muigizaji huyu alikuwa na mengi ambayo yangewafaidi mastaa wa bongo kwa hivi sasa. Johari amesema:

Kila mwaka lazima nimkumbuke Steven Kanumba kwani ndiye alikuwa akinitia faraja na nguvu ya kutokata tamaa katika jambo unaloliamini. Kanumba hakupenda kushindwa kwa kile alichokiamini, hakika pengo lake halitazibika, namwombea huko aliko alale mahali pema peponi, alipigania tasnia ya filamu, sema ndiyo hivyo hakuweza kufikia malengo yake, siwezi kumsahau, nitamkumbuka kwa mengi aliyoniachia.

Rayvanny afunguka kuhusu collabo yake na Bahati

Collabo ya Rayvanny na Bahati imeweza kupata umaarufu kwa siku chache baada ya kuachiliwa na Wasafi records. Wimbo huu ambao ni wa Injili umempa Bahati uwezo wa kupenya Tanzania na Kenya pia na kulingana na alichosema sema Diamond Platnumz wawili hawa wanaenda mbali kimuziki.

Hata hivyo Rayvanny hivi karibuni alifunguka kuhusu collabo hii na kulingana na alivyoongea, kijana huyu hana majuto yoyote kumchagua Bahati kama msanii ambaye angefanya project na yeye

Akiongea katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM Jumanne hii, Rayvanny alisema kuwa kabla ya kuanza kuimba alianza kuimba kwaya kanisani.

“Kwanza mimi nimekuwa nikimfuatilia Bahati kwa muda mrefu na nilikuwa nikifikiria nikikutana naye nitaimba wimbo wa aina gani na mimi niliwa narap huko nyuma lakini nimejua kuimba kwa kupitia kanisani. Kwa hiyo haikuwa ngumu kwangu kufanya kwa sababu ni wimbo wakijamii zaidi ndio maana wimbo hauonyeshi kama ni wa Injili au wakidunia,”

Sasa hivi wimbo wao wa nikumbuke umeweza kupata airplay mzuri katika nchi zote mbili.

Mke wa Roma aeleza alivyozunguka vituo vyote vya polisi kumtafuta mumewe ambaye hajulikani aliko

Mke wa Roma, Nancy amezungumza kwa mara ya kwanza baada ya mumewe, Roma kupotea. Kulingana na stori mitandaoni kuna fununu kuwa Roma na rafiki yake walichukuliwa na polisi wakiwa studio za Tongwe Record Masaki jijini Dar es Salaam.

Kama Watanzania wenzake Nancy hafahamu alipo mumewe ambaye ni baba ya mtoto wake, Ivan. Akizungumza na wanahabari, Nancy ameeleza kuwa amemtafuta mume wake katika vituo vya polisi lakini kila andako hakuna anayerecords za Roma Kutiwa mbaroni. Alisema,

Mimi kama mke wa Roma mara ya mwisho niliwasiliana na mume wangu jana saa kumi na mbili jioni, akaniambia anaelekea Tongwe Records kwajili ya kazi zake za kila siku. Baada ya hapo sikuwa nampata tena kwenye simu lakini nikachukulia ni kawaida tu simu imezima, nimekuja kuamka saa 7 nikapokea simu kutoka kwa rafiki yake akaniambia uko na Roma nikamwambia hapana alikuwa Tongwe, akaniambia kuna taarifa kwenye mitandanao na mimi nikaingia nikakuta hizo taarifa kama walizopata watu wengine. Baada ya hapo nikaanza kutafuta watu wa kunisaidia, baadhi ya ndugu zangu wameangaika vituo vyote vya polisi Roma hayupo, hadi sasa hivi sifahamu yuko wapi, kwa ufupi sina ninachokijua wala ninachokifahamu. Jitihada zangu za kutafuta kwenye vituo vyote vya polisi nimemaliza.

Hivi sasa watanzania kwa ujumla wameungana mikono katika jitihada za kumtafuta Roma ambaye mpaka sasa hajulikani aliko.

Huu ndio ujumbe Diamond Platnumz aliowaandikia watoto wake

Diamond Platnumz hivi karibuni aliwaandikia watoto wake ujumbe kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram kuwatania kwani wanamidomo ambayo inafanana na yake.

Hii sio mara ya kwanza kusikia muimbaji huyu akikiri kuwa wanae wanamfanana hasaa kwenye area ya mdomo. Na Kwa mara ya kwanza aliwaandikia ujumbe kuwasihi watumie midomo yao vizuri, kama alivyofanya yeye. Aliandika kusema,

Prince & Princess Lion!!!.. Midomo mkaitumie vizuri hiyo watoto….

Diamond aliambatanisha ujumbe huu na picha ya wawili hao kuonyesha wanavyofanana kisura. Kulingana na comments zilizoandikwa na mashabiki, wengi wao walipata wakati mgumu kuwatofautisha.

Hata hivyo ni kweli kuwa genes za Diamond na Zari zinatoa watoto warembo na picha hii aliyoipost inaonyesha kuwa ni ukweli.

Tiffah na Nillan
Tiffah na Nillan

Linah adai wazazi wake walimkataa mpenzi wake kwa sababu ya dini

Linah ambaye ni muimbaji maarufu Tanzania amefunguka mara ya kwanza kuhusu mchumba wake na baba ya mtoto anayemtarajia hivi karibuni.

Akizungumza na kipindi cha XXL cha Clouds Fm alisema kuwa dini iliwafanya wazazi wake kumkataa mchumba wake mara ya kwanza. Muimbaji huyo alisema kuwa amelelewa katika misingi ya dini ya kikristo na alipopata mimba ya mwanaume wa dini nyingine iliwafanya wazazi wake kuwa na ugumu wa kumkubali mwanaume huyo.

“Mwanzoni wazazi wangu walimkataa mpenzi wangu kisa ni dini tofauti na mimi, lakini sasa hawana pingamizi. Tumeunganisha damu na kwenye mahusiano naamini upendo, nisingependa mtu anipangie, lakini jambo la wazazi kwa familia za kiafrika ni tofauti.”

Aliendelea kusema kuwa hajuti kubeba mimba hiyo kwani aliipata at the right time.

Nimebeba ujauzito katika right time kwangu na mwenzangu yupo tayari. Mashabiki wategemee ndoa kabisa muda wowote.

Reality TV star wa Kenya Mishi Dorah adai kuwa Rayvanny alitaka kumpa mimba

Kilichotokea kati ya Mishi Dorah na Rayvanny hakiwezi julikana kwa kiukweli kwani wawili hao walikutana wakati ambapo hakuna yeyote alijua kuwa wana ‘mahusiano.’

Mishi Dorah

Hata hivyo, Rayvanny amekuwa akimkana mwanamke huyu kwa kusema kuwa anataka kumuharibia nyumba na jina lake. Lakini baada ya Ghafla kumhoji mwigizaji huyo wa Nairobi Diaries, Mishi Dorah alisema kuwa ni kweli aliweza kupatana na Rayvanny kimapenzi.

Mishi Dorah aliendelea kwa kusema kuwa hajapata hedhi zake kwa mwezi mmoja kuonyesha kuwa kunauwezekano wa mwanamke huyu kuwa na mimba ya Rayvanny kutokana na alivyosema. Kulingana na Mishi, Rayvanny alikuwa anataka sana wawili hao wapate mtoto wao wa kwanza kitu ambacho alihisi hawezi kuharikisha kwani hakutaka kuiharibu figure yake.

Lakini swali bado ni…Kati ya mwanamke huyu na Rayvanny nani anasema ukweli? Ebu itazame interview yake hapa.

https://youtu.be/wN6ppPh-TEI

Mwigizaji wa filamu Batuli afunguka kuhusu beef yake na Irene Uwoya

Yobnesh Yusuph anayejulikana kwa umaarufu kama ‘Batuli’ amedai kuwa yeye hana beef yoyote na mwigizaji wa kibongo, Irene Uwoya. Mwigizaji huyo aliendelea kusema kuwa Uwoya ndiye anapaswa kueleza beef yao inatokana na nini kwani yeye ndiye anayesambaza maneno haya.

Batuli
Batuli

Batuli aliendelea kusema kuwa hana muda wa kuanzisha ugomvi na mtu yoyote haswa Uwoya. Kulingana na yeye amewazibia watu macho na maskio wanoeneza stori hizi mitandaoni. Batuli alisema,

“Sina muda wa kugombana na Uwoya, kama kuna tatizo aulizwe yeye siwezi kuusemea moyo wake.”

Uwoya
Uwoya

Uwoya alipotafutwa kupitia simu yake Mwigizaji huyu hakushika wala kujibu SMS kuhusu beef hii yake na Batuli. Kwani kuna nini?

Mabishoo wamtupia chupa Harmorapa akitumbuiza Maisha Basement

Harmo rappa alinusurika kifo usiku wa Jumapili 02 April 2017, baada ya kupigwa chupa na shabiki mmoja akiwa stejini. Msanii huyo alikuwa na show ya ‘USIKU WA KOMELA’ na kama kawaida mashabiki walijitokoza kwa wingi kumuona star huyu akiwatumbuiza.

 

Harmo rappa atupiwa chupa stejini
Harmo rappa atupiwa chupa stejini (photo credits)

Hata hivyo, Harmo rapper alipopanda jukuani kuperform wimbo wake mpya ‘Kiboko ya mabisho’ alishtukia akirushiwa chupa iliyokuwa na bia na mmoja ya mashabiki aliyekuwa ukumbuni mwa mashabiki wenzake.

Kulingana na ripoti shabiki huyo alitupa chupa hiyo baada ya Harmo rappa kuimba mstari mfupi wa wimbo wake, tulikuwa WASAFI kabla ya WCB, maneno yao machafu hayaniharibii CV…. ulio mkasirisha shabiki huyu mkubwa wa wasafi.

Shabiki aliyemtupia Harmo rappa chupa stejini
Shabiki aliyemtupia Harmo rappa chupa stejini

Hata hivyo chupa hiyo ya bia haikumfikia Harmo rappa kwani alikwepa na kuitoraka. Baada ya tukio hilo, klabu ya Maisha Basement wasiwasi lakini bouncers waliweza kumtoa rappa huyu stejini kabla ya kumtafuta kijana aliyesababisha fujo hizo.

Baada ya muda jamaa huyo alipatikana na bouncers waliomhoji kujua kilichomsababisha kufanya kitu kama hicho. kuwa ameshachakazwa na wananchi wenye hasira kali. Kulingana na alichosema, inaonekana huyo hakuwa shabiki wa Harmo rapper. Hata hivyo alikamtwa na kupelekwa polisi na sasa hivi anangoja kupelekwa kotini.

 

Nay Wa Mitego anahofia maisha yake Sasa

Rapper Nay Wa Mitego ameewacha wengi wakimhofia maisha yake baada ya ujumbe aliouandika kwenye mtandao wake wa Instagram. Ujumbe huu umekuja wiki moja baada ya rapper huyo aliwekwa ndani na jeshi la polisi baada ya kuachia wimbo wake mpya ‘Wapo’.

Kulingana na ubuyu mitandaoni, wimbo huu ukikuwa ukichana serikali ya Magufuli hata hivyo Rais wa Tanzania Magufuli alitoa amri msanii huyo kuachiwa kwa kwa kusema wimbo wake haukuwa na matatizo yoyote.

Hata hivyo, Nay wa Mitego sasa hivi anasema kuwa anahofia maisha yake kwani anahisi kwamba kuna watu wanaotaka kumpoteza. Kupitia Instagram aliandika kusema

“Usalama wa maisha yangu umekua mdogo kwasasa, Wanapanga kunipoteza ikibidi nisiwepo kabisa kwenye hii dunia. Nipo tayari kwa chochote wanacho panga kufanya Coz sijajipanga kupambana nao, Mimi ni mwana muziki si vingine. Kwa chochote kitachotokea familia yangu itakua na chakuongea. Siwezi kuhama nchi wala kukimbia nitafia hapa hapa. Na siko tayari kupindisha chochote.! nyie Ndo mtanilinda. Sina Mlinzi na sitarajii kua na mlinzi. OnlyGod??#Wapo,”

Haijulikani ni nini kilichomfanya kuhisi hivyo, lakini tunafuatilia kusikia atachokisema hivi karibuni.

Snura akana kupangiwa nyumba na mwanaume wa Kiarabu

Inasemekana kuwa mwanamziki Snura amepangiwa nyumba mpya na mwanaume wa Kiarabua ambaye anaweza kuwa mpenzi wake hivi sasa.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa Global Publishers amabao walimtembelea katika nyumba yake huko maeneo ya Tabata, Dar Snura alikana kwa kusema kuwa hana mawanume wa kiarabu ambaye amempangia nyumba.

Aliendelea kusema kuwa alihamia sehemu hiyo ili mwanae awache kuchoka akienda shule. Hivi ndivyo mazungumzo yao yalikuwa.

Snura
Snura

Wikienda: Snura mambo vipi? Mbona kimya sana kimuziki? Au ndiyo mambo ya ubuyu unaosemwa?

Snura: Yapi tena? Mimi mbona nipo najiandaa kutoa kazi? Siyo kila siku kusikika bila mpango. Mimi huwa nasikika kwa kazi ninayoitoa ninyi subirini mtanisikia.

Wikienda: Hata hivyo, tuna ubuyu hapa kuwa nyumba hii umepangishiwa na mwanaume wa Kiarabu ambaye amekuhamisha Mwananyamala kwa sababu alikuwa hapapendi, unalizungumziaje hilo?

Snura: Hahahahaha, mmenichekesha kweli, watu wanajua kuongea sana, mimi nimehama nyumba kwa sababu ya mtoto. Shule anayosoma mwanangu ipo huku Tabata. Mwananyamala ilikuwa ni mbali sana. Mwanangu alikuwa anachoka sana. Hayo mengine ya mwanaume wa Kiarabu ndiyo kwanza nayasikia kwenu.

Wikienda: Nasikia amekununulia na gari la kutembelea maana tunaliona hapa, tunasikia ana mpango wa kukupiga stop kuimba, je, ni kweli?

Snura: Gari nimenunua mwenyewe kwa jasho langu nikimaanisha kazi yangu, huyo Mwarabu mnayemkazania kama yupo hakuna la kufi cha kwani mwisho wa yote atajulikana tu na ataonekana, lakini nahisi labda wanayemzungumzia ni baba mtoto wangu, hahaha…

Msanii wa muziki wa hip hop Bongo,‘Tammy The Baddest’ aeleza kwanini anapenda nguo fupi fupi

Kama mnamjua Tamara Ally ‘Tammy The Baddest’ basi unaelewa mavazi ambayo yeye huyavaa kwenye video zake. Si siri kuwa anapenda vitu fupi ambazo humuacha akikaa ni kama yuko uchi, lakini hiki ni kitu cha kawaida kwake.

Katika interview na Global Publishers msanii huyu alisema kuwa yeye amezoea mavazi ya aina hii na hata akiwa nyumbani kwao na wazazi wake yeye huvaa hivi kwani wamemzoea nahata hivyo si ajabu kitu cha ajabu.

Tammy
Tammy

Aliendelea kusema kuwa kukaa nusu utupu anajichukulia poa kwani ni kawaida mwanamke kujiachia na lifestyle yake.

“Mchumba utupu mara kwa mara kuwa ni mazoea.kukaa nusu utupu wangu mwenyewe ananichukulia poa kwani ni kawaida mwanamke kujiachia just life style tu, hata kwenye video yangu (Mtoto wa Kike) nimeonesha hadi nguo ya ndani mbona ni vitu vya kawaida tu jamani.”

Sasa hivi anapepea na nyimbo yake mpya ya Mtoto wa Kike ambayo yeye pia anaonekana kuwa nusu uchi.

Picha Hizi ni Ishara tosha kuwa Wema Sepetu ni Binti Mrembo Zaidi Tanzania

Ingawa ni mwanamke ambaye amekuwa na scandals mingi, ni kweli kuwa Wema Sepetu ni binti ambaye ameumbwa kama malkia na ambaye anatambulika Afrika Mashariki na wengi.

Alipoanza career yake kama model sio wengi walidhania kwamba binti huyu angeleta mabadiliko mengi katika burudani ya Bongo. Wema Sepetu si model tu bali mwigizaji na kwa hivi mwanasiasa.

Hata hivyo, yeye ni fashion killa na mwanamke ambaye anajitambua. Akitembea mitaani watu wengi huduwaa kutokana na urembo alionao.

Nimeweza kupata picha kadhaa kama mfano kuonyesha mbona Binti huyu anaurembo watu wengi hutamani. Ingawa hukubaliani na mimi, pia ni sawa kila mtu ana maoni yake. Tazama picha hizi hapa.

 

Baada ya kufanya collabo na King Kiba, Barakah The Prince aeleza changamoto alizopitia

Mwimbaji wa Tanzania Barakah the Prince ameeleza baadhi ya changamoto alizopitia baada ya kutoa colabo ya wimbo wake Nisamehe aliyomshirikisha King kiba. Hii ni kufuatia tofauti zilizopo kati ya team Kiba na team Diamond Platnumz.

Akizungumza katika interview na kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha Salama Jabir, Barakah alisema kuwa ilikuwa vigumu kupata support kutoka team Diamond ambao hawampi support Kiba.

Ujue Alikiba ni brand kubwa na ni brand ambayo ina mvutano na vitu vingi, kwahiyo unavyofavya collabo na Alikiba kuna mawili hapo, kuna nyimbo kufanya vizuri na kuna nyimbo kufanya vizuri wastani, wa kawaida kwasababu ya ule mvutano wa kibiashara ambao upo kati yake na timu nyingine

Ingawa halalamika kuwa jambo hili liliadhiri wimbo wake, muimbaji huyu amekiri kuwa timu hizi mbili zinangumvu ya kuaffect career ya muimbaji bongo. Kwa hivi sasa anaendelea kuzipush nyimbu zake kabla atoe project nyingine mwaka huu.