Juma Nature afunguka baada ya Harmorapa kudai kuwa alikuwa anamdai baada ya collabo yao

Imemchukua Juma Nature wakati kuzungumza kuhusu maneno ambayo Harmorapa aliyosema hivi karibuni akiwa kwenye interview na kipindi cha E News cha EATV. Kulingana na ripoti zinazoenea kwenye mitandao jamii Harmorapa anadai kuwa Juma Nature anamdai pesa ya mavazi aliyovaa kwenye wimbo wake mpya ‘Kiboko Ya Mabishoo’.

Harmorapa
Harmorapa

Harmorapa alisikika akisema,

“Haipo sawa kwa wasanii wakubwa kutudai sisi ‘underground’ pesa ya kufanyia collabo wakati wanajua bado hata hatuanza kufaidika na muziki wenyewe.”

Akizungumza kwenye Kipindi cha E news Juma nature pia alikanusha madai haya akisema kuwa Harmorapa hana pesa za kumlipa ata angekuwa anamdai rapa huyo hawezi kumlipa.

“Nikisema nimemlipisha Harmorapa pesa kwa ajili ya kolabo nitakuwa nakosea. Mimi ni mtu mzima nilikubali kufanya wimbo na msanii yule kwa sababu ni mkali na anajua muziki pia na imani atafika mbali. Hawezi kunilipa mimi, ana hela gani?

Huu ndio ujumbe Alikiba aliomwandikia binti yake kusheherekea siku yake ya kuzaliwa

Alikiba ameonekana kuwa baba aliyenafuraha baada ya binti yake kusheherekea siku yake ya kuzaliwa hivi juzi. Baba huyu ambaye amekuwa akiwaeka watoto wake kipaumbele hakusita kuzipost picha za mwanae huku akimuandika ujumbe wa kupendeza.

Ingawa ni star mkubwa Tanzania, Alikiba huwa anapenda kuwaeka watoto wake off social media na anapowapost yeye huwa akisheherekea siku zake za kuzaliwa.

Mwaka huu inaonekana akumfanyie binti yake birthday kubwa kama ya mwaka uliopita. Hata hivyo haimaniishi kuwa upendo wake kwake umepungua. Muimbaji huyu siku hizi anaonekana kuwa mtu anayeshughuli mingi na career yake ambayo inaonyesha matumaini ya kugrow.

Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram, king Kiba aliandika kusema…

Happy Birthday My Princess ? nitakupenda siku zote ❤️ @Amiyakiba #SupportedByKiba #KingKiba

Binti ya Alikiba
Binti ya Alikiba

Ni kama mapacha: Vanessa Mdee aonyesha picha ya mamake akiwa msichana mdogo

Muimbaji wa Tanzania Vanessa Mdee ameacha mashabiki wake wakimfananisha na mamake baada ya kupost picha ya kitambo ya mamake mzazi.

Kupitia mtandao wake wa kijamii Vanessa Mdee alipost picha hiyo huku akumsifu mamake kwa urembo aliowapa watoto wake (Vanessa na madada zake). Aliandika caption kusema,

Hi Mommy ? Circa 1976 #MothersDay is everyday ? #SophiasDaughter #ChokerAndAll

Ata hivyo pia aliweza kuajulisha mashabiki wake jina la mamake na kwa mara ya kwanza muimbaji huyu aliweza kushare picha ya mzazi wake kitu ambacho yeye hupenda aukiweka kama private kwa kuwa ni personal life.

Ikiwa umekuwa ukijiuliza mrembo huyu alitoa wake umbo lake na uzuri wake basi tazama picha hii ya mamake akiwa mchanga.

Vanessa Mdee na mamake
mamake Vanessa Mdee

Nape Moses aandika ujumbe huu baada ya Nay wa Mitego kuachiliwa

Nay Wa Mitego sasa hivi yuko huru baada ya kuachiliwa siku kadhaa baada ya kushikwa na serikali ya Magufuli. Mashabiki wake walikuwa mkondo wa kwanza kumkaribisha msanii huyu na pia alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses naye pia aliandika ujumbe wake kupitia account yake ya Twitter.

Nape Moses aliandika ujumbe wenye ulisihi viongozi kutumia busara na siyo nguvu katika kufanya maamuzi wakati wanapomuona mtu amefanya kosa ilikurahisisha kumkosoa.

Aliambatanisha picha ya Nay wa mitego alipoandika ujumbe huo kuonyesha kuwa hakufurahishwa na kitendo ambacho walichomfanyia mwanamziki huyu.

Ata hivyo wanamziki wengi walisita kuandika kitu chochote kupitia mitandao yao ya kijamii huku wakihofia kukamatwa. Huu umekuwa kama mtindo ambao serekali ya Magufuli imeanza kuiga na wengi wanonelea kuwa wamekosa busara na kuwafanya wengi kuogopa.

Mashabiki wamponda Diamond Platnumz baada ya kuonyesha cheni zake za mamilioni

Ni kweli kuwa Diamond Platnumz anapesa nyingi hadi imembidi kununua cheni na pete ambazo alilipia Tsh 158 millioni. Alipost picha hizi kupitia mtandao wake wa Instagram hata hivyo si mashabiki wengi walifurahia kitendo hiki na kuacha comments ambazo zilimfanya Diamond Kuwajibu.

Mashabiki hawa walionelea kuwa Diaomond Platnumz angetumia pesa hizo kuwasaidia maskini ambao hawana hata nyumba za kuishi wala chakula cha kula. Diamond na yeye pia aliwajibu kwa kuwatajia mambo ambayo ameweza kufanya kuisaidia jamii ili kuwajulisha kuwa hakuwa mtu selfish.

Aliandika kusema…

Nimejenga nyumba 5 mwaka janaIringa, Misikiti miwili mmoja Morogoro pia nyingine Mtwara na Madrasa tegeta na nyumba ya Imamu mbili na sadaka mbali mbali sasa unataka nitoe ela zote sadaka nami nisifurahishe nasfi? Hebu niombe radhi kwa hilo.

Comment yake ata hivyo haikuwafurahisha mashabiki hao waliondelea kumponda na kumwambia kuwa amekuwa mtu mwenye kiburi na kuwa amesahau alikotoka. Je wewe waonaje?

Ben Pol amsifu mwanae wa kiume baada ya kutimiza mwaka mmoja mwezi huu

Ben Pol amezipost picha mpya akiwa na mwanae wa kiume, Mali aliyetimiza mwaka mmoja mwezi huu na kulingana na maoni ya mashabiki wake wa Instagram mtoto huyu anapendeza sana kama babake.

Ben Pol na mwanae, Mali
Ben Pol na mwanae, Mali

Picha hizi zimekuwa zikiwakosesha wengi usingizi kwa kuwa wengi bado hawajatosheka kumtamani mtoto huyu. Ata hivyo Ben Pol ameweza kufunguka kumhusu na huku akizungumza na Bongo 5 alisema kuwa mwanae ameonyesha kuwa anavipaji vingi kama anapenda kucheza na mpira na pia anapenda sana kuimba na mamake nyimbo za kitoto.

Ukimpa mpira anapenda kucheza sana kwa mikono, anapenda kudundadunda sana mpira.Lakini vile vile pia mama yake anaimbaga naye mara nyingi sana, nyimbo za kitoto. Mama yake akiwa anaimba anamfuatisha sijui sauti ya pili, sijui anaimba sauti ya ngapi. Kwahiyo anaonekana anapenda kuimba, anapenda mpira, kwahiyo sijui itakuwaje, sijui atakuwa mcheza mpira sijui atakuwa muimbaji, lakini all in all nashukuru Mungu anakua vizuri.

Ben Pol na mwanae
Ben Pol na mwanae

Ben Pol aliongeza kwa kusema kuwa bado wanaendelea kumuangalia ili waweze kujua kipaji chake lakini kwa hivi sasa yeye na mamake mtoto hawana haraka.

Ila kiukweli kwenye kipaji hapo bado tunaendelea kuangalia sababu kiukweli anatuchanganya, atakuwa Shaquille O’Neal au atakuwa R.Kelly, hapo ndio au atakuwa Ben Pol au atakuwa Hasheem Thabeet.

Harmonize afafanua script ya video yake mpya kwa mashabiki wasioilewa

Imebidi Harmonize kuwaeleza mashabiki wake uhusiano wa video yake mpya na wimbo wake niambie unaowachanganya wengi. Muimbaji huyu wa Wasafi records amekuwa akiona malalamishi ya mashabiki wake wanoaamini kuwa alikuwa off script kwenye video yake mpya.

Harmonize akiwa na Wolper
Harmonize akiwa na Wolper

Kulingana na lyrics zake za Niambie, Harmonize anaonekana kuwa mtu ambaye hana pesa wala kwake ilhali video ya wimbo huo anaonekana akiishi kwa nyumba ya kifahari na maisha yake kuwa ni ya tajiri kitu ambacho hakiambatani na anachoimba.

Hata hivyo Harmonize alichukua fursa ya kuwafafanulia mashabiki wake alipokuwa kuwa kwenye interview na Prince Ramalove kupitia Kings Fm. Harmonize alielezea maana ya script ya hiyo video kwa kusema…

“Sina mtonyo lakini naishi kwake,sasa nikiishi kwake na yeye ana hela,ntafanyaje?”

Kwa ufupi muuimbaji huyo alikuwa akimanisha kuwa nyumba na magari zinazooonekana kwenye vdeo ni mali za Wolper kwa mujibu wa script.

Mchumba wa Aunty Ezekiel aeleza mbona hawezi kuwa muimbaji wa Wasafi records

Moses Iyobo ambaye ni dancer maarufu wa Diamond Platnumz amefunguka kwa nini hawezi kuwa muimbaji ataiwapo angepewa fursa hiyo.

Akiongea na gazeti maarufu la Dimba, Mose alisema kuwa hana mipango ya kuingia katika muziki na kuwa kwa hivi sasa lengo lake ni kuwa dancer ambayo ni kazi anayoifanya kwa hivi sasa.

Mose Iyobo na Aunty Ezekiel
Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Kiluingana na yeye, kuwa muimbaji inatakiwa mtu kuwa na kipaji ambacho yeye mwenyewe hana kwa hivyo si kitu ambacho anaweza kufanya na kufanikiwa. Alisema,

“Unajua kuimba kunahitaji akili nyingi ili ufanikiwe, sasa kwa upande wangu sitaweza ni bora nibaki huku huku ndio pananifaa zaidi,”

Ata hivyo Mose Iyobo alisema kuwa angependa kuwa mwalimu wa kuwafindisha vijana kuwa dancer kama yeye. Kuna watoto ambao wangependa kuwa dancers wakiwa wakubwa kwa hivyo ni heri yeye kuanzisha shule ambayo atawafundisha ili hapo mbeleni waweze kutambulika kama yeye.

Diamond Platnumz awaonyesha mashabiki wake Pete na cheni mpya alizozinunua Tsh 158 million

Kweli Diamond Platnumz sio mtu wa mchezo. Mwimbaji huyo wa Tanzania ameaacha mashabiki wake kama wameduwaa baada ya kuonyesha pete na cheni zake mpya alizozinunua millioni 158 pesa za Tanzania.

Ata hivyo hii sio mara ya kwanza ya huyo muimbaji kuaonyesha baadhi ya vitu anavyovimiliki vya thamani ya juu. Kupitia mtandao wake wa Instagram aliandika kusema…

Thanks God for my new GOLD & DIAMONDS collection…i never thought i would be able to hang 50,000$ on my neck

Aliendelea kumshukuru mungu akisema kuwa kila siku anapata baraka amabazo ata yeye mwenyewe haamini kuwa angepata. Kwenye picha nyingine aliandika kusema…

“Thanks God for your daily blessings never thought i would be able to walk with 22,000 $ on my Hand!!!… jus get inspired @sallam_sk don’t hate.”

Tazama hizi cheni na pete hapa chini.

Msanii mwingine kutoka kenya azuru WCB baada ya Willy Paul

Inaonekana kuwa Willy Paul sio msanii pekee kutoka Kenya ambaye anajulikana na Diamond Platnumz. Siku chache baada ya kuzuru Tanzanian kupromote wimbo wake I Do aliyomshirikisha mrembo kutoka Jamaica, Alaine… msanii mwingine anayejulikana kama Chikuzee kutoka pwani pia alikuwa kwenye ofisi za WCB hivi leo.

Msanii huyu anayejulikana sana pande za Mombasa Chikuzee aka Zee la Mavuvuzela ni alishare picha zake kupitia mitandao yake ya kijamii alipotembelea WCB.

Kwa hivi sasa kuna tetesi kuwa kuna kitu kiko jikoni baina yake na Rayvanny. Mashabiki wake kupitia kwa comments walitaka kujua kama alienda pale kutia sahihi mkataba wa kuwezesha ngoma zake kuwekwa kwenye wasafi.com ama kama walikuwa wanatengeza projects mpya.

Ata hivyo msanii huyu hajafunguka kueleza alikchokuwa akifanya ofisini mwa Diamond Platnumz lakini kuna uwezekano kuwa kuna jambo kubwa wawili hawa wanataka kuachia.

Msanii wa Bongo Fleva Linex adai kuwa kiki inaua muziki

Linex, msanii maarufu wa bongo amefunguka na kusema kuwa mtindo wa kupa mziki kiki unapoteza ladha na focus ya mziki nchini Tanzania.

Akiongea na waandishi wa global punlishers Tz nyumbani kwake Mbezi Beach Dar es Salaam, Linex amesema kuwa imekuwa kama trend ya wasanii wa Bongo kutokea na skendo wakati wanpotaka kuachilia mziki siku hizi. Kulingana na yeye vitendo kama hivi havina maana kama msanii anaamini kazi yake ni nzuri.

Msanii huyu aliendelea kusema kuwa mashabiki ndio wanaoamua kama projects za wasanii ni za kuvutia au la. Linex alisema,

“Nachoweza kusema turudi kushabikia muziki mzuri, tuache kushabikia skendo. Nachokiona hapa muziki unapotea kabisa”

Ata hivyo hit maker huyo wa Kiherehere aliwasihi mashabiki kuwa makini na kufuatilia muziki wa maana badala ya kushabikia skendo za watu maarufu.

“Naona amepanga kunichafua” Rayvanny amkana Mishi Dorah anayemdai kimapenzi

Rayvanny aliyekuwa nchini Kenya hivi majuzi amekana Mishi Dorah amabaye ni mwanake wa makamo na bado anamtaka Vanyny boy kimapenzi.

Staa huyu wa tanzanian amefunguka kwa kusema kuwa amekataa ofa za Mishi Dorah ambaye anaonekana kumharibia jina nchini Kenya na sasa pia Tanzania. Mishi ambaye ni mwigizaji wa reality show amekuwa akitangaza kuwa ashawai kuwa na Rayvanny kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii, wiki iliyopita. Aliskika akisema,

“Ninampenda Rayvanny, nitamtafuta kwa udi na uvumba nimtunuku penzi ili roho yangu itulie, nampenda sana kwa kweli,”

Mishi Dorah

Ata hivyo Rayvanny sasa amefenguka huku akisema kuwa amekuwa akiona anachosema Mishi Dorah, lakini hatakai mambo ya mwanamke huyu kwani anahofia nyumba yake kuvunjika na pia brand yake kuharibika. Akizungumza Rayvanny alisema,

“Yaani sitaki kumuongelea kabisa huyo mwanamke, maana naona amepanga kunichafua kwani nilienda Kenya wakati f’lani nikakuta habari zake, huku nyumbani Bongo ndiyo hivi tena, sina cha kuongea maana mtu akiamua kukuchafua huwezi kuongea kitu.”

Mpenzi wa Rayvanny aonyesha tumbo lake likiwa uchi wiki kidhaa kabla ya kuzaa

Rayvanny na mpenzi wake fahyma wanamtarajia mtoto wao wa kwanza hivi karibuni kulingana na wanachoandika mitandaoni yao ya kijamii.

wawili hawa wanasemekana kuwa walianza mahusiano yao mwaka uliopita na kwa hivi sasa wanatajia familia yao kuongeza kwa sababu Fahyma ana mimba na kulingana na picha anazoziposti kwenye Instagram msichana huyu amebakisha wiki kadhaa kabla kuzaa mtoto wake wa kwanza.

Ingawa wawili hawa hujaribu kuweka mahusiano yao chini ya maji, Fahyma na rafiki wake wa Karibu ambaye alisemekana kuwa mpenzi wa Diamond Platnumz, Official Lynn, wameweza kushare picha mpya za Fahyma akioneshana tumbo lake huku kama amevaa overall ya kinyasa na crop top.

Mashabiki wa Fahyma walimsifu huku wakimpongeza kwa mtoto anayemtarajia hivi karibuni. Ikiwa bado hujaziona picha hizi basi ziangalie hapa chini.

Fahyma
Fahyma
Fahyma na rafiki yake official Lyyn
Fahyma na rafiki yake official Lyyn

“Wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,” Harmorapa ambia watu wanaomuongela vibaya

Staa na rapa wa Tanzania, Harmorapa hivi majuzi aliweza kufunguka kuhusu watu ambao wanamtusi na kumuongelea vibaya tangu awe maarufu.

Rapper huyo ambaye amekuwa akifanya vizuri Tanzania na Afrika Mashariki kupitia nyimbo zake hivi sasa ndiye anayepata kiki kubwa Bongo na anavyoonekana, Harmorapa atakuwa na umaarufu kama wa Diamond Platnumz iwapo ataendelea kurelease projects ambazo watu watapenda.

Hata hivyo, akizungumza na Bongo 5 rapa huyu alisema kuwa habebwi na kiki na kuwa kazi yake ndiyo inafanya awemaarufu kwa hivyo wanomchukia wanafanya kazi bure na kuwa ataendelea kuachilia nyimbo zake kama kawaida.

“Watu ambao wanahisi Harmorapa hatodumu kwenye game kwanza wanakosea halafu pia naweza nikasema kwamba wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,”

Aliendelea kwa kusema kuwa…

“Kama mimi binafsi nimejipanga sana vya kutosha. Unajua kwamba maneno yao mimi hayanivinjii chochote ni ile sawa na kumpiga chura teke na kumwongezea mwendo. Wanavyoniongea mimi ndo wananipa power na wananipa maujuzi na wananipa kuweza. Ni wao wananiweza mimi kuweza na kukaza ilmradi niweze kufanya kazi nzuri.”

Harmorapa  pia amehaidi mashabiki wake projects kubwa ambazo ataachilia mwaka huu.

Agnes Masogange apewa onyo na Hakimu Mkuu baada ya kuchelewa kuwasili Mahakamani wakati unaotakiwa

Agnes Masogange ni mmoja wa Video vixen ambao wanajulikana sana Afrika Mashariki. Ameweza kufeature katika video kadhaa nchini Tanzania lakini hivi sasa yuko matatani na Mahakama baada ya kudaiwa kuwa mmoja wa watu maarafu anayetumia madawa ya kulevya.

Mwezi Februari aliweza kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo aliposomewa mashitaka yake kwa mara ya kwanza na kama wengi alikana na mahakama ikabidi kuhairisha kesi yake hadi, March 21, ili kuwapa polisi mda wa kutosha kufanya upelelezi wao.

Video vixen huyu anakabiliwa na mashitaka ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Hata hivyo Jumanne hii mrembo huyu hakuwa mahakamani kuskiza kesi yake baada ya kuchelewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilibidi kutaja kesi hiyo ingawa hakuwa.

Wakili wa Masogange, Nictogen Itege, aliweza kumtetea Masogange huku akisema kuwa yuko njiani. Masogange alipowasili Hakimu Mashauri alimtaka mshitakiwa kutii sheria anazopewa na Mahakama huku kesi yake ikihairishwa hadi Aprili 20, mwaka huu kwa kutajwa.

Huzuni tele baada ya Tanzania kujumuishwa kwenye list ya nchi zisizokuwa na furaha duniani

List ya Nchi zilizo na furaha na huzuni duniani ilitolewa leo,March 20,2017 na Tanzania ilitokea kwenye hiyo list.

Na sio kwa nchi zenye furaha sana lakini nchi zenye huzuni sana. Iko nambari mia moja hamsini na tatu mbele ya nch mbile pekee; Burundi na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Imejumuishwa na nchi zingine za Afrika kama Rwanda na Togo na Guinea.

Kwa mujibu wa ripoti ya BBC imetoa list ya viwango vya furaha kwenye nchi zote duniani na hapa nimekuwekea hapa nchi 20 zenye watu wenye furaha na wasio na furaha duniani:

Tanzania