Linah aonyesha muonekano wa kitanda cha mwanae anayemtarijia hivi karibuni

Linah bado hajataja jinsia ya mtoto wake mtarajiwa ila anaonekana ameanza kujipanga mapema kwani amebakisha wiki kadhaa ajifungue.

Muimbaji huyo wa Bongo amekuwa akiposti picha kuonyesha ujauzito wake huku akiwa na furaha ya kuwa mama kwa mara ya kwanza maishani yake. Hata hivyo hajamtambulisha baba ya mtoto anayemtarajia lakini hapo mbeleni aliweza kufunguka kwa kusema kuwa ni mtu wa dini ya Kislamu.

Hata hivyo amebakisha wiki kadhaa ajifungue na kulingana na mtandao wake wa Instagram, Linah ameanza kujipanga kwa kumnunulia mwanae kitanda na doli kadhaa alizoziweka mtandaoni wake.

Tazama picha aliyoiweka hivi karibuni.

Nay wa Mitego amjibu Skyner Ally baada ya kudai ameshindwa kuwa baba bora kwa mtoto wake

Mwanamuziki wa Tanzania Nay wa Mitego hivi karibuni aliiabishwa na muigizaji wa filamu Bongo, Skyner Ally baada ya kumchana kwa kumwambia kuwa hajakuwa akimtunza mtoto wao kama anavyostahili.

Skyner na Nay wakona mtoto wa kike pamoja lakini muigizaji huyo wa filamu amedai kuwa Nay hajakuwa akimsaidia mwanae. Hii ilikuja baada ya Nay alipoweka picha ya mtoto wao mtandaoni wa Instagram huku akimsifu kwa uzuri wake.

Hata hivyo Skyner hakupendelea kwani Nay hajakuwa akihusika na mambo ya mwanae kwa muda mrefu sasa. Kilicho muuma zaidi ni kwamba Nay alikuwa anawadanganya mashabiki wake kuwa anawatunza wanawe vyema ilhali alikuwa ameshindwa kuwa baba bora kwa mtoto wa Skyner ambaye alizaa na yeye.

Inaonekana kuwa Nay aliweza kuiona post ya Skyner na kupitia mtandao wake wa Instagram, Nay aliandika kusema…

“Si kwa kichambo kile jamaniiiiii huh??! Jamani inatosha basiii Povuuu. Nitapeleka Matumiziiiii???. Nawapenda sana awa Watoto Wanguu?. Wasiopeleka Matumizi ya Watoto?? #Wapo,”

Haya basi, wacha tutazame watakacho kifanya hawa wawili sasa.

Skyner amchanwa na Nay baada ya kuposti picha ya binti yao

Skyner aliyekuwa mpenzi wa msanii wa muziki wa Hip Hop, Nay wa Mitego, hivi karibuni aliamuaibisha baada ya kuweka picha ya binti yao mitandaoni huku akijisifu kwa uzuri wa mwanae.

Hata hivyo Nay wa Mitego hakukipata alichotarajia kutoka kwa Skyner ambaye alimchana kupitia Instagram huku akifunguka kuwa Nay hajakuwa baba kwa manae kwa miaka ilhali anawadanganya watu mitandaoni.

Ujumbe na Nay wa Mitego ulisema,

Skyner ambaye alikasirishwa na ujumbe huu aliandika ujumbe akimshangaa Nay ambaye anasemekana kuwa hataki kutoa huduma kwaajili ya mtoto. Aliandika kusema,

“Thats face you make when you see your ‘daddy jina’ anakufanyia promotions na kudanganya Watanzania kama Oooh my Twin sijui nanunua pisto, hata chupi unayovaa hajui thamani yake maskini. Nimevumilia sana it’s 5 Years now nimejiskia kutapika na nimetapikaa. Am done Mungu wa mbinguni nakuomba unijaalie maisha marefu uwezo nizidishie riziki….. uzima wa afya nikuleee mwanangu aje akuone baadae Inshallah umekuja kuwa Waziri wa nchi & Raisi wa nchi then alete pua yake”

Aliendelea kwa kusema…

“Endelea na drama zako ila please shobo na mwanangu sitaki…Please unapost picha za mtoto wangu za nini…shobo dundo zanini? Sitaki shobo na mwanangu koma kama ulivyo komaaa…Je, Wababa anaojisifu kama wanapenda watoto wao then hata hawajui mtoto anakula nini anasoma wapi anavaaa nini Wapooooooo? Drama nyingi sana mtandaoni halafu i love You Nyingi Hana Analofanya Wapooooooooo ??? Am done”

Aliendelea kwa kuonyesha binti yake alivyokuwa muhimu katika maisha yake alivyoandika kusema…

“Hakuna anayejua thamani yako zaidi yangu hata huyo anayejita baba’ko hana analolijua kuhusu wewe, si shule, malazi wala chakula kutwa kucha kukupost na kuongopea jamii kama anakujali, ninayehangaika nimie nakuhakikishia na kumuomba Mola wangu anijaalie uhai nguvu uwezo riziki nizidi kukulea kwa nguvu zangu Inshallah nakuonea gere sana umepata mama bora na sio bora mama uko mikono salama mwanangu wa uchungu. Happy Birthday My Happiness,” alisema Skyner.

Hata hivyo rapa huyo bado hajazungumza chochote kuhusu sakata hilo, Bongo5 bado inafanya jitihada za mtafuta.

Baada ya kutangaza anamrudia mungu Sabby Angel aonekana kwenye kumbi za starehe akila bata

Msanii anayefanya muziki na filamu Bongo, Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ alifunguka hivi karibuni na kutangaza kuwa anamipango ya kustaafu kwani alikuwa anahisi kuwa imefika wakati ambao anafaa kumrudia mungu.

Sabby Angel aliwashangaza wengi kwa tangazo hilo wengi na mashabiki wake huku wakiwa na hofu kuwa msanii huyu angepotea kabisa kama wengi ambao waliacha kutumbuiza hapo zamani.

Sabby Angel
Sabby Angel

Lakini inaonekana kuwa Sabby Angel bado hajaamua anachotaka kwa kweli. Hivi karibuni alionekana akijivinjari kwenye klabu wiki kadhaa baada ya kusema kuwa anapanga kumrudia mungu.

Hata hivyo alivyohojiwa na global Publishers msanii huyu alisema…

“Mmh! Sina hata la kujitetea, ukweli nimeamua nimrudie Mungu, lakini haya mambo ya starehe najitahidi kuacha kidogokidogo, hadi pale nitakapoweza kuacha kabisa kwenda klabu na upuuzi mwingine.”

Muigizaji wa Bongo Zuberi Mohammed adai Wema Sepetu, Uwoya na wengine hawafikii uzuri wa mke wake

Mwanaume ni kujiamini na muigizaji wa Bongo Zuberi Mohammed anaejulikana kama Niva amefunguka kwa kusema kuwa mke wake anauzuri ambao Uwoya, Wema na Kajala hawana.

Wema Sepetu

Akiongea katika interview, muigizaji huyu hakuogopa kwa kuwachana warembo hawa ambao wamekuwa kwenye sekta ya burudani kwa muda sasa. Kulingana na yeye, alibarikiwa na mwanamke ambaye anauzuri ambao bado hajauona katika mwanamke mwingine.

“Nakuambia ukweli kabisa hakuna mwanamke mzuri Bongo Muvi zaidi ya mke wangu Maisala, wewe muamshe usingizini Uwoya, Wema, Kajala halafu muamshe na mke wangu uone nani anavutia zaidi, hakuna kama mke wangu,”

Uwoya
Uwoya

Jibu hili lake lilikuwa la kuwapasha watu ambao wamekuwa wanaosema eti anauwezo wa kumsaliti mkewe kwani kila wakati anaonekana akitembea na wasanii wa Bongo Muvi wakati alifunguka ndoa na nia ya kutulia na kuanza familia.

Mahakama yatoa amri Agnes Masogange akamatwe tena

Video vixen wa bongo Agnes Gerald amejipata mashakani tena baada ya mahakama kutoa amri akamatwe kwa mara ya pili baada ya kutofika mahakamani kwa mara ya pili kesi.

Agnes ambaye hapo mbeleni alikosa kufika mahakamani wakati kesi yake ilikuwa ikitajwa amerudia kosa hili kwa mara ya pili baada ya kutofika mahakamani alipopangwa kutajiwa kesi yake.

Agnes
Agnes

Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam ametoa amri hiyo baada ya Masogange na wakili wake kukosa kuwasili. Kwa kosa hili sasa hivi Agnes Masogange atakamatwa kwa kutofika mahakamani na kutotoa taarifa ya kilichofanya kutofika.

Muigizaji huyu ana mashtaka mawili ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Aslay amefunguka sababu iliyomfanya ahame kutoka nyumba ya Mkubwa na Wanawe

Aslay amekubali kuwa alihama kutoka nyumba ya Mkubwa na Wanawe, ambapo akiishi na Waimbaji wenzake wa Yamoto band.

Akizungumza katika kipindi cha ‘On The Eight’ cha TVE Aslay alieleza kuwa hakuwa na tatizo yoyote na mtu na kilichomsababisha kuhama ni kwa sababu ya familia yake.

Aslay

Kulingana na yeye, amekaa muda mrefu mbali na familia yake na ndio maana aliamua kuwafuata . Anahofia akiendelea kukaa mbali nao hataweza kuwa karibu nao kama zamani.

Hata hivyo amekana maneno ambayo yanasambazwa mitandaoni. Hata hivyo, kwa hivi sasa amepanga kujibrand yeye mwenyewe na kuachia nyimbo zake mwenyewe.

Shamsa Ford apasuliwa uso baada ya kupigwa ngumi

Shamsa Ford ‘Chausiku’, amepata jeraha usoni baada ya mwanaume ambaye hajulikani alimpiga ngumi huku akimuacha kama amepasuka na kuvuja damu. Kupitia Instagram Shamsa aliposti picha na kuonyesha mashabiki wake alivyofanywa na mtu huyo.

Jeraha lake limewaacha wengi wakisema kuwa litabaki maisha. Shamsa naye aliandika ujumbe kwa mashabiki zake kuwa alipigwa akiwa anaamua ugomvi. Inasemekana kuwa jamaa aliyempasua uso alikuwa akimtongoza mfanyikazi wa Shamsa kwa nguvu na ndipo muigizaji huyu aliingilia kumsaidia msichana wa wenyewe.

Shamsa Ford
Shamsa Ford

Hata hivyo inaonekana jamaa huyo alikuwa amejaa hasira baada msichana huyo kumkataa na baada ya Shamsa kuingilia, akamtolea hasira kwa kumpiga ngumi ya uso.

Ingawa Shamsa alikuwa akilalamika maumivu makali kichwani, hivi sasa anaendelea vizuri.

Ni nini kinachoendelea kati ya Alikiba na Ruby?

Ubuyu mtaani ni kuwa Alikiba na Ruby kuwa wamekuwa watu wa karibu sana na kuzua maswali mitandaoni ya kijamii.

Habari hii imevuma mda mchache baada ya Alikiba alisemekana kuwa alimvisha pete ya uchumba mwandani wake aitwaye Amina kutoka nchini Kenya.

Ruby
Ruby

Hata hivyo baada ya kuonekana na Ruby sana wengi wanaamini kuwa wawili hao wanauwezekano wa kuwa wapenzi ikiwa hawafanyi wimbo mpya pamoja.

Ruby ambaye aliweza kuzungumzia jambo hili aliwasihi watu hataki kuulizwa kuhusu mahusiano yake…. Ruby alisema,

“Sorry, sitaki kuulizwa kuhusiana na hayo mambo, naomba niulizwe kuhusu kazi zangu tu!”

Alikiba naye hajazungumzia jambo hili kwa sasa hata hivyo kuna uwezakano kuwa yeye na Ruby wanapanga kuachia wimbo mpya hivi karibuni.

Babake mzazi na Belle 9 afariki dunia baada ya kugongwa na boda boda

Mzazi na Bella 9 wamem[poteza baba yao baada ya kugongwa na boda boda kama ilivyoripotiwa kupitia mitandao ya kijamii.

Mzee Damian anasemekana kuwa aligogwa na boda boda iliyomuacha akiwa hali mahututi. Hata hivyo mzee huyu alifariki dunia usiku wa kuamkia leo kulingana na alichosema Jah Zamba ambaye ni meneja wa Mzazi.

Ajali hii ilitokea mjini Morogoro alikokuwa akiishi. Kulingana na Bongo 5 mzee Damian alivunja mguu mmoja na kuumia vibaya baada ya ajali hiyo.

Ata baada ya kupelekwa hospitali madaktari hawakuwa na njia yoyote ya kumsaidia. Alipelekwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi lakini hawakuwa na dawa zilizokuwa zinahitajika kumtibu mzee huyu. Hata hivyo dereva wa boda boda hiyo pia aliumia vibaya baada ya taya kuvunjika na kumjeri kichwa.

Muigizaji Elizabeth Michael akana taarifa za ndoa yake na Majay

Elizabeth Michael hivi karibuni alikuwa anasemekana kuwa anatarajia kufunga ndoa na mpenzi wake Majay ambaye pia ni bosi wa EFM na TVE. Taarifa hii ilienea baada ya magazeti kadhaa ya Tanzania yalioandika kusema kuwa walifanya mahojiano na mrembo huyo.

Hata hivyo Elizabeth Micheal anaejulikana kama Lulu amekana taarifa hizi kupitia mtandao wa Twitter baada ya kuandika ujumbe uliosema…

“Hivi kwa Akili yenu Ndoa inatangazwaga Kwenye Magazeti!??Muwege mnajiongeza kabla ya kuparamia Story…!.”

Hii inakuja baada ya gazeti la Mtanzania lilikiri kwa kumnukuu muigizaji huyo…

“Siku zinakaribia na karibu tarehe ya ndoa yangu itatangazwa kwa uwezo wa Mungu. Hapo ndipo waliotamani tuachane wataziba midomo, maana natarajiwa kuwa mke halali hivi karibuni.”

Kwa hivi sasa inaonekana kuwa Lulu hana mipango ya kuolewa.

Harmorapa aeleza sababu za kutomiliki bastola kama wasanii wenzake

Ni kweli kuwa Harmorapa anatisha wasanii wenzake ambao amewaonyesha kivumbi muda mfupi baada ya kuwa staa maarufu Tanzania.

Sasa hivi anapesa zake na anamiliki gari kubwa lakini bado hajafikiria kumiliki bastola yake kwa kuwa ana ulinzi wa kutosha. Alizungimza katika kipindi cha Dj Show cha Radio One, Harmorapa alieleza kuwa bado hajafikiria kuwa na bastola kwakuwa ana personal bodyguard ambaya hutembea na yeye kila mahali aendapo.

“Sasa hivi nina pesa nyingi, nina gari nini. Lakini sijawaza au kufikiri siku nije kumiliki bastola kwa sababu eti nina pesa sijawaza kwa muda huu ila sijajua huko mbeleni iatkuwaje,”

Aliendelea kwa kusema kuwa ulinzi alionao hauwezi kubali mtu amkaribie. Kulingana na yeye bodyguard wake ameshiba tosha na ndio maana haoni haja ya bastola.

“Nikisema kwaajili ya kujilinda unajua sasa hivi mimi nina bodyguard wangu ameshiba na ameenda hewani. Hata ninapokaa kwenyewe nina ulinzi mpaka umfikie Harmorapa kuna kazi kubwa sana na unaweza usionane naye,” ameongeza.

Kuna nini? Rich Mavoko na Nay wa Mitego wakijibizana mitandaoni

Kuna dalili za Rich Mavoko na Nay Wa Mitego kuanza beef baada ya majibizano yao mitandaoni ya kijamii hivi karibuni.

Hii ilianza baada ya Mavoko kuposti picha na maneno ya kuwajulisha mashabiki wake kuwa anatarajia kuachia nyimbo mpya hivi karibuni kwa kuandika.

Haya Mkimaliza Mambo Zenu Za Siasa Mtupe Tarehe Na Sisi Tufumue Hiii ? #Showme

Lakini baada ya masaa kadha Nay wa Mitego alirepost picha hiyo ya Mavoko na kumchana kwa kumwambia kuwa ngoma yake mpya WAPO ndio inapaswa kutiliwa maanani na wananchi. Aliandika kusema,

Haya Mkimaliza Mambo Zenu Za Siasa Mtupe Tarehe Na Sisi Tufumue Hiii ? #ShowmeNAOMBA MUENDELEE KUSUBILI, MAY BE MPAKA MWAKANI 2018, NDO MTAANZA KUJISHUGHULISHA NA MASWALA YA KUWAIMBIA WANA NCHI. MWAMBIENI NA BABA YENU PIA AWE MPOLE KWASASA ALEE WATOTO. KAZI TULIYO NAYO IKIENDA SAWA TUTA WARUHUSU MUENDELEE KUBURUDISHA WANA NCHI. TUNATAKA MAMBO YAENDA SAWA KWANZA✊?.
Wimbo wetu wa TAIFA ni #Wapo LINK ON MY BIO☝?️

Askofu Gwajima aachiliwa huru na Mahakama

Askofu Gwajima sasa hivi yuko huru baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumuachia baada ya upande wa mashitaka ushadi kukosa ushahidi wa kutosha baada ya kupelekwa kotini na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinari Pengo.

Kulingana na malalamishi ya Askofu Mwadhama inasemekana kuwa Gwajima alitumia lugha chafu na kuharibu jina la Mwadhama. Hata hivyo kesi hii imetupiliwa mbali baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuleta mashidi kwa muda wa miezi 14.

Hata hivyo wakili wa Serikali, Joseph Maugo aliomba mahakama kuhairisha kesi hiyo ili kuwapa muda tosha wa kupata mashahidi katika kesi badala ya kesi hiyo kufutwa.

Gwajima anasemekana kuwa aliluita Askofu Mwadhama Polycarp ; Ni mpuuzi mmoja mjinga mmoja asiyefaa mmoja anaitwa Askofu Pengo aliropoka sijui amekula nini mimi naitwa Gwajima namwita mpuuzi yule mjinga yule na kuonesha Pengo ni mtoto mpuuzi na mwenye akili ndogo na kwamba maneno hayo yangeweza kuleta uvunjifu wa amani

Dadake mdogo Vanessa Mdee asimulia changamoto alizopitia kabla ya kuwa maarufu

Mimi Mars ambaye ni dadake mdogo Vanessa Mdee hivi karibuni aliweza kufunguka kuhusu changamoto alizopitia kabla ya kuwa muimbaji maarufu bongo. Kama wasanii wenzake alitafuta njia za kuiingia kwenye movie za bongo lakini hakuwa na uwezo.

Akizungumza kwenye kipindi cha Bongo Dot Home cha Times FM, Mimi alisema kuwa dadake mkubwa Vanessa aliweza kumsaidia awezavyo na ata kutafuta usadizi kutoka kwa Lulu na Wema Sepetu kumpa shavu dadake lakini waliambulia patupu.

Hata hivyo Mimi Mars hana kinyongo na wasanii hawa kwani anaamini kuwa wakati wake haukuwa umefika. Katika interview yake Mimi alisema kuwa sasa hivi yeye na akina Wema ni marafiki wakubwa na ingawa hawakuwepo alipokuwa akiwahitaji, bado anawachukulia kama marafiki wa dhati.

“Nilishawahi kumuomba Lulu, Elizabeth Michael nakumbuka tuliwahi kuongea naye hata akina Wema kuomba kuingiza kwenye bongo movie lakini, Vanessa ndio alikuwa ananisaidia kuongea nao lakini kama walinipiga chini fulani hivi but it’s okay,”

Hivi sasa Mimi Mars anafanya vyema na wimbo wake na akona matumaini ya kwenda mbali kama dadake. Tazama interview yake hapa chini.

Mashabiki wa King Kiba wamtolea Barakah the Prince hasira baada ya kumpost Chibu

Ingawa Baraka the Prince alifanya wimbo na King Kiba Nisamehe haamanishi kuwa hawezi msupport Diamond Platnumz. Hata hivyo hivi sivyo mashabiki wa Kiba wanavyofikiria. Hivi Karibuni muimbaji huyu wa Bongo, Baraka the Prince aliupost wimbo mpya wa Diamond Platnumz na kilichofuatia ni matusi kutoka team Kiba.

Soma: Baada ya kufanya collabo na King Kiba, Barakah The Prince aeleza changamoto alizopitia

Barakah The Prince
Barakah The Prince

Mashabiki wengi ambao wamekuwa wakicomment kwa picha hii wanashangazwa na Baraka kupost wimbo huu kwa sababu wengi wanajua Baraka yuko kwenye lebel moja na Alikiba.

Kama mnavyoelewa Kiba na Diamond wamekuwa na beef kwa muda sasa kwa hivyo Baraka asingeweza kupost chochote kuhusu Diamond Platnumz, wengine wamecomment kwa kutopendezwa na post hiyo wengine wamepost kumpongeza.

Kupitia Instagram Barakah the prince aliandika kusema…

Chanzo cha kutengenezewa maden na makaka poa..ila mama alinifunza kukaa kimya..eeehh mungu niokoe vita